Ijue CPU ya Kompyuta

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Feb 3, 2009
42,319
33,125
Watu wengi wamekuwa wakitumia neno CPU wakimaanisha Kompyuta,ila leo tutaona tofauti iliyopo kati ya CPU na Kompyuta,na kwanini watu wanapenda kutumia neno CPU wakimaanisha Kompyuta.Pia tutaitazama CPU kwa ukaribu zaidi kuona ina nini ndani yake na infanya vipi kazi.
Neno CPU kwa kirefu ni Central Processing Unit pia inajulikana kama Microprocessor Unit.Ila watu wengi upenda kutumia neno CPU au Processor.Yote ni kitu kile kile.CPU ni kichwa cha kompyuta,wengine upenda kusema CPU ni moyo wa kompyuta.Hii ina maana kwamba CPU ni kiungo muhimu sana kwenye Kompyuta kama vilivyo Moyo na Kichwa kwenye mwili wa binadamu.Kutokana na umuhimu huu wa CPU kwenye Kompyuta ndo maana watu wengi wanatumia neno CPU wakimaanisha kompyuta.

Ufahamu wa CPU utakusaidia kujua unahitajika kutumia softwares gani,hardwares gani,Operating Systems gani,pia Kompyuta yako ina nguvu kiasi gani bila kusahau bei ya Kompyuta inategemea sana CPU iliyotumika kwenye Kompyuta hiyo.
CPU zina matoleo mengi sana na mpaka sasa makampuni yanayoongoza kwa uzalishaji wa CPU za desktop na laptop computers ni Intel na AMD.
CPU ina umuhimu gani?
CPU ni kikokotoo(calculator) chenye nguvu sana. Inafanya hesabu za kujumlisha,kutoa,kuzidisha na kugawanya kwa haraka sana.Kwa maana nyingine mambo yote au kazi zote unazozifanya kwenye Kompyuta yako kupitia softwares au Operating System,zinabadilishwa kwenda kwenye binary(1 au 0).Baada ya kubadilishwa kwenda kwenye binary basi CPU inazifanyia hizo binary mahesabu ya kujumlisha,kutoa,kuzidisha na kugawanya kwa haraka sana na kukupa jibu au kitendo unachotarajia.Sio uchawi ni hesabu tu za kujumlisha,kutoa,kuzidisha na kugawanya.
Kwenye ufanyaji kazi CPU lazima iwe na mawasiliano na Memory(RAM),pia mawasiliano na Motherboard kupitia kwenye waya mahususi.
Michoro hapo chini inaonyesha uhusiano uliopo kati ya mtumiaji wa kompyuta pamoja na CPU na hardware nyingine za Kompyuta.


Sehemu muhimu za CPU
CPU inasehemu muhimu zifuatazo Control Unit,Arithmetic and Logic Unit(ALU) na Registers.

Control Unit(Instruction Fetcher and Decoder) hii inafanya kazi ya ku-control mambo yote yanayoendelea ndani ya CPU,pia ku-control Input na Output devices za kompyuta.Input devices ni kama keyboard na mouse.Output devices ni kama monitor na speakers.Pia inafanya kazi ya kuchukua maelekezo(instructions) kutoka kwenye programu ambazo zipo kwenye Main Memory(RAM) na kuzitafsri kwenda kwenye machine language na baadae kutoa ishara ambazo zitapelekea sehemu husika kuyafanyia kazi maelekezo hayo.
Arithmetic and Logic Unit(ALU) hii sehemu inachukua data kutoka kwenye Memory na kuzifanyia mahesabu na ufananishaji.Arithemetic unit ya ALU inafanya mahesabu ya kujumlisha,kutoa,kuzidisha na kugawanya.Logic unit ya ALU inafanya ufananishaji wa data,kwa kuangalia data moja na nyingine kama ni ndogo kuliko,sawa sawa au kubwa kuliko.
Registers ni kama memory ndogo ndani ya CPU.Zinahifadhi data na maelekezo kwa mda wakati ALU inapokuwa inafanya kazi.Pia inahifadhi data na maelekezo kutoka kwenye Main memory(RAM) wakati yakisubiri kufanyiwa kazi na ALU.
Matoleo ya CPU
CPU zipo kwenye makundi makuu mawili,CPU kwa ajili ya Laptop na CPU kwa ajili ya Desktop Kompyuta.CPU kwa ajili ya Desktop zina nguvu zaidi kulinganisha na CPU kwa ajili ya Laptop ata kama jina la toleo zinafanana.Na hii ni kwasababu ya kwamba Laptops zinahitaji kutumia umeme mdogo,pia zinatakiwa zisiwe za moto sana kutokana na nafasi ndogo ya hardware.Kwahiyo hivi vitu vyote vitahitaji CPU ambayo inatumia power kidogo,kwa maana nyingine utendaji wa CPU inabidi kupunguzwa kidogo ili kufikiana na hayo matakwa.
Kama nlivyosema mwanzoni watengenezaji wakubwa wa CPU kwa ajili ya Laptop na Desktop ni Intel na AMD.Hawa wanamatoleo mengi sana,ambayo yanaweza kukuchanganya uchague lipi uache lipi pale inapofika kwenye ununuzi wa CPU au ununuzi wa Kompyuta kwa ujumla.Maana CPU ni kiungo muhimu sana cha kompyuta.Basi usisite kufwatilia muendelezo wa makala hii.Ntakuchambulia kundani vitu gani vya kuangalia unapofikia sasa swala la kuchagua CPU ya kutumia.
 
safi sana kumbe tunaweza kufundisha IT kwa kiswahili na ikaeleweka zaidi kuliko umombo. tuendelee kuelimishana tutafikatu siku moja na sisi tutakuwa kama ASIA
 
Hii imetulia. weka na nyingine kama hizi mkuu tuendelee kuongeza maarifa.
 
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]Because Kiswahili is spoken both as a first and second language, you may hear different pronunciation. However, there is a set of vowels and consonants that are crucial for your pronunciation.[/FONT]

Vowels

[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]There are five distinct vowel sounds in Kiswahili.[/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]a[/FONT]​
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif] alama ‘sign’ [/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]e[/FONT]​
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif] eleza ‘explain’ [/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]i[/FONT]​
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]ili ‘so that’ [/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]o[/FONT]​
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]okota ‘pick up’ [/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]u[/FONT]​
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]ukuta ‘wall’ [/FONT] Consonants

[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]b[/FONT]​
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]baba ‘father’ [/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]c[/FONT]​
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]chai ‘tea’ [/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]d[/FONT]​
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]dada ‘sister’ [/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]f[/FONT]​
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]fika ‘arrive’ [/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]g[/FONT]​
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]gari ‘motorcar’ [/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]h[/FONT]​
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]habari ‘news’ [/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]j[/FONT]​
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]jana ‘yesterday’ [/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]k[/FONT]​
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]kaka ‘brother’ [/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]l[/FONT]​
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]lala ‘sleep’ [/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]m[/FONT]​
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]mama ‘mother’ [/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]n[/FONT]​
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]nazi ‘coconut’ [/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]p[/FONT]​
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]paka ‘cat’ [/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]r[/FONT]​
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]ramani ‘map’ [/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]s[/FONT]​
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]soko ‘market’ [/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]t[/FONT]​
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]tia ‘put’ [/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]v[/FONT]​
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]vizuri ‘good’ [/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]w[/FONT]​
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]watu ‘people’ [/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]y[/FONT]​
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]yai ‘egg’ [/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]z[/FONT]​
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]zawadi ‘present’ [/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]th[/FONT]​
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]theluji[/FONT] [FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]‘snow’ [/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]dh[/FONT]​
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]dhahabu[/FONT] [FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]‘gold’ [/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]gh[/FONT]​
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]ghasia[/FONT] [FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]‘chaos’ [/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]sh[/FONT]​
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]shimo[/FONT] [FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]‘pit’ [/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif] The following chart represents the nasal consonants and nasal consonant clusters found in this language. [/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]ny[/FONT]​
nyanya [FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]‘[/FONT]grandmother[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]’ [/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]ng'[/FONT]​
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]ng'ombe[/FONT] [FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]‘cow’ [/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]ng[/FONT]​
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]ngoma[/FONT] [FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]‘drum/dance’ [/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]nd[/FONT]​
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]ndege[/FONT] [FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]‘bird’ [/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]mb[/FONT]​
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]mbuzi[/FONT] [FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]‘goat’ [/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]mw[/FONT]​
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]mwalimu[/FONT] [FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]‘teacher’ [/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]mchana[/FONT]​
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]‘[/FONT]day time [FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]’ [/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]mdudu[/FONT]​
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]‘bug’ [/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]mfalme[/FONT]​
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]‘king’ [/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]mganga[/FONT]​
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]‘medicinal healer ’ [/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]mhenga[/FONT]​
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]‘a wise person’ [/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]mji[/FONT]​
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]‘town or city’ [/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]mkia[/FONT]​
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]‘tail’ [/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]mlinzi[/FONT]​
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]‘guard’ [/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]mmea[/FONT]​
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]‘plant’ [/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]mnene[/FONT]​
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]‘fat’ [/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]mpira[/FONT]​
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]‘ball’ [/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]mrefu[/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]‘tall’ [/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]msitu[/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]‘forest’ [/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]mtoto[/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]‘child’ [/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]mvuvi[/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]‘fisherman’ [/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]mzazi[/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]‘parent’ [/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]mbwa[/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]‘dog’ [/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]mchwa[/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]‘termit’ [/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]mnyama[/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]‘animal’ [/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]ncha[/FONT]​
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]‘tip’ [/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]nywele[/FONT]​
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]‘hair’ [/FONT]
 
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]Aspects of Grammar

Noun Classes in Swahili
[/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]m[/FONT]​
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]mtoto mzuri
[/FONT] [FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]A good child[/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]wa[/FONT]​
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]watoto wazuri[/FONT] [FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]Good children[/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]m[/FONT]​
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]mti mzuri[/FONT] [FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]Good tree[/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]mi[/FONT]​
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]miti mizuri[/FONT] [FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]Good trees[/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]-[/FONT]​
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]tunda zuri[/FONT] [FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]Good fruit[/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]ma[/FONT]​
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]matunda mazuri[/FONT] [FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]Good fruits[/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]ki[/FONT]​
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]Kisu kizuri[/FONT] [FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]Good knife[/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]vi[/FONT]​
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]visu vizuri[/FONT] [FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]Good knives[/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]n[/FONT]​
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]nyumba nzuri[/FONT] [FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]Good house[/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]n[/FONT]​
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]nyumba nzuri[/FONT] [FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]Good house[/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]-/n[/FONT]​
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]radio nzuri[/FONT] [FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]Good radio[/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]-/n[/FONT]​
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]radio nzuri[/FONT] [FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]Good radio[/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]u/m[/FONT]​
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]ukuta mzuri[/FONT] [FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]Good wall[/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]-/n[/FONT]​
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]kuta nzuri[/FONT] [FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]Good walls[/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]ku[/FONT]​
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]kucheza kuzuri[/FONT] [FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]Good playing[/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]The Swahili Verb

The Swahili verb contains lot of grammatical information that is signaled by an affix.

For example:
[/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]Mtoto[/FONT] [FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]a [/FONT] [FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]-na [/FONT] [FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]-cheza[/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]child[/FONT] [FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]he/she[/FONT] [FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]is[/FONT] [FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]play[/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]‘The child is playing’[/FONT]​

[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]Mtoto[/FONT] [FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]a [/FONT] [FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]-li [/FONT] [FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]-cheza[/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]child[/FONT] [FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]he/she[/FONT] [FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]was[/FONT] [FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]play[/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]‘The child was playing/played’[/FONT]​

[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]Mtoto[/FONT] [FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]a [/FONT] [FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]-ta [/FONT] [FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]-cheza[/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]child[/FONT] [FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]he/she[/FONT] [FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]will[/FONT] [FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]play[/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]‘The child will play’[/FONT]​
 
AVG 9.0

. AVG Technologies ni kampuni ya kompyuta, na imekuwa inalinda watu dhidi ya virus, spyware na aina nyingine ya matishio kwenye computer toka mwaka 1991, na software yake ya AVG imefikisha toleo la 9.0.

Tofauti na version 8 mpaka 8.5 ambayo wakati unapotaka kuingiza kwenye computer ni lazima ufunge vitu unavyofanya kwenye computer yako kama unaangalia tovuti fulani au kama unatumia programu ya word kusoma au kuchapa kitu kwanza ndio ikubali usipofanya

hivyo basi itazifunga yenyewe, unapokuwa unataka kuinstall version 9.0 hautokuuliza suala la kuzima programu zingine au vile vitu ulivyokuwa unafanya wakati huo ingawa ni muhimu kufanya hivyo ili unapostart settings ziwe tayari intalled.

Nimejaribu kuscan external harddrive yangu yenye data za zaidi ya GB 900 imetumia nusu ya muda wa toleo lililopita la AVG.
Kwa wiki nzima sasa nimekua naitumia Antivirus hii ile free edition ambayo ni bure pamoja na professional edition hii inauzwa pamoja na internet security , kitu kingine nilichoangalia

ni kama inasema uwongo kuhusu baadhi ya tovuti.
Kama kawaida nilivyoinstall kwenye computer nikaenda kwenye search engine nikatafuta tovuti moja hivi ambayo ni haramu kweli AVG ikaniambia tovuti hiyo ni haramu nilipojaribu kuichungulia ikaniambia tovuti ninavyoingilia sio salama chochote kinaweza kutokea kama

naingia basi ni kwa kutaka kwangu mwenyewe , sasa ukiwa na antivirus nyingi ambazo zina matoleo mapya sasa hivi haziwezi kutambua tovuti hiyo kama si salama kwenye avg kuna kitu kinaitwa Link scanner ndio inaweza kufanya hivyo .

Pamoja na hiyo inaweza kuzuia computer yako kudownload programu ambazo hazitakiwi hizi ni pamoja na zile zinazokusanya taarifa binafsi za watu bila ya wao wenyewe kujua na kuzifuta moja kwa moja kwa kukupa taarifa ambayo ina popoup kwenye taskbar . Kitu

ambacho hupati kwenye hii free edition ni firewall ambayo ni kama ukuta wako kuzuia wengine wasiweze kukuona kwenye mitandao ingawa kama unatumia windows basi ina firewall yake ingawa haina ufanisi kama hizi zingine kama unataka firewall nzuri mimi huwa natumia zonealarm pia jua hii imenunuliwa na kampuni moja ya huko Israel sasa watu wa

mashariki ya kati wanaiogopa sana wanahisi kwamba labda inatumika dhidi yao ila ni moja ya firewall nzuri zaidi duniani haijawahi kushuka kimasoko toka imeanzishwa .
Pia huwezi kupata msaada wa bure toka kwa AVG wenyewe ingawa kuna sehemu ya forum ambayo unawezakuungana na watumiaji wa AVG wa sehemumbalimbali duniani kubadilishana nao mawazo na maswali na game mode hii ina weza kukusaidia pale unapocheza game kwa njia ya mtandao kukulinda dhidi ya shambulio lolote kwa njia ya games .

ITAENDELEA SIKU NYINGINE INSHALLAH
 
MziziMkavu:

Pamoja na kutafsiri hii makala - N lazima uwe muungwana kwa kuonyesha makala ya awali iliandikwa na nani - Acknowledge the Author ::: Always!
 
Matoleo ya CPU
CPU zipo kwenye makundi makuu mawili,CPU kwa ajili ya Laptop na CPU kwa ajili ya Desktop Kompyuta.CPU kwa ajili ya Desktop zina nguvu zaidi kulinganisha na CPU kwa ajili ya Laptop ata kama jina la toleo zinafanana.Na hii ni kwasababu ya kwamba Laptops zinahitaji kutumia umeme mdogo,pia zinatakiwa zisiwe za moto sana kutokana na nafasi ndogo ya hardware.Kwahiyo hivi vitu vyote vitahitaji CPU ambayo inatumia power kidogo,kwa maana nyingine utendaji wa CPU inabidi kupunguzwa kidogo ili kufikiana na hayo matakwa.

Kwa hiyo vingine vyote vikiwa sawa (upya, aina ya Operating System, kumbukumbu na chipset zingine) laptop siku zote ina uwezo mdogo kikazi (kasi, ukokotoaji, aina ya kazi inayomudu) kuliko desktop?
 
Kwa hiyo vingine vyote vikiwa sawa (upya, aina ya Operating System, kumbukumbu na chipset zingine) laptop siku zote ina uwezo mdogo kikazi (kasi, ukokotoaji, aina ya kazi inayomudu) kuliko desktop?
Hapo mzee napingana nawe Dr. MziziMkavu. CPU speed in uwezo wa ku process instructions per given time. Sasa kama zina Uwezo sawa wa ku process na kuhifadhi vitu, then ziko sawa. Kuna some aspect Desktop is powerful than Laptop. Mfano sauti ya laptop lazima itakuwa kidogo kwa sababu ukuzaji wa sauti (amplification) unategemea Nguvu ya umeme (Power=VxI).
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom