Elections 2010 Igunga: Kikwete amnadi Rostam (picha)

Harakati za kujipatia ushindi wa kishindo zimeendelea leo baada ya mgombea urais kwa tiketi ya chama cha mapinduzi kumnadi mgombea ubunge huko igunga kwa tiketi ya ccm mh. Rostam Aziz, asema ni mtu safi anasingiziwa!

kikwete_rostam1.jpg

kikwete_rostam2.jpg

rostam_election.jpg

Lini Kikwete amekuwa hakimu mpaka aseme fisadi huyu anasingiziwa? kama alijua anasingiziwa mbona hakumfikisha mahakamani ili kujibu tuhuma dhidi yake na kuacha sheria ifuate mkondo wake? Mafisadi wote alikuwa anawaogopa akina Chenge, Yule aliyekuwa MD wa tanesco, Karamagi, Lowassa, Mkono na wengineo. Kama alikuwa anajua kuna ushahidi wa kuwaweza kushinda kesi zao basi angeruhusu wapandishwe kizimbani, vinginevyo kauli zake hazina mvuto wowote na zinathibitisha kwa mara nyingine kwamba Kikwete ni mtetezi wa mafisadi.
 
Kikwete amtakasa Rostam

ASEMA NI MTU SAFI ALIYEENEA KAMA TIMU YA MPIRA Send to a friend

Ibrahim Bakari, Igunga

MGOMBEA urais kwa tiketi ya CCM, Jakaya Kikwete amemsifu mweka hazina wa zamani wa chama hicho, Rostam Aziz kuwa ni mtu safi na aliyeenea kila sehemu.Kikwete alisemna hayo wakati akimtambulisha Rostam, ambaye anatetea kiti chake kwenye Jimbo la Igunga ambako amekuwa mbunge tangu mwaka 1995.

Kikwete alitua Igunga baada ya kukamilisha mikutano ya kampeni katika Jimbo la Igalula na Tabora Kaskazini katika mkoa wa Tabora.

Akimnadi Rostam mbele ya halaiki kwenye mkutano uliofanyika Igunga Mjini, Kikwete alisema kuwa Rostam 'ameenea' na anaweza, hivyo wananchi wa Igunga hawana sababu ya kuacha kumpa kura.

"Rostam ni kama timu iliyoenea, timu iliyokamilika kila idara, sasa mnataka nini tena...mnamfahamu, anawasaidia ni mtu wa watu, anawapenda," alisema Kikwete na kushangiliwa na wafuasi wa chama hicho waliofurika kwenye mkutano huo.

Kikwete alisema pia kuwa angeshangaa kama wanachama wa CCM wasingempa nafasi ya kuwa mbunge wa chama hicho.

Kwa upande wake Rostam alimsifu Kikwete kwa uongozi safi na kueleza kuwa yuko tayari kuwatumikia wananchi wa Igunga katika kipindi kingine cha miaka mitano na kwamba Kikwete asisumbuke kuwaza kura za Igunga kwani zipo asilimia 99.99.

"Nimepita katika kata zote 26 za Igunga, wananchi wamenihakikishia kuwa kura zote ni za CCM, usiwe na wasiwasi... usihofie porojo za majukwaani," alisema Rostam huku akishangiliwa.

Pia Rostam aliahidi kusaidia ujenzi wa daraja la Mbuto linalounganishanisha Wilaya ya Igunga na Shinyanga.

Awali katika mkutano wa kwanza kwenye Jimbo la Igalula pamoja na Tabora Mashariki, Kikwete aliwataka wananchi kutochagua vyama alivyoviita vya wanung'unikaji na wanaohubiri kumwaga damu.

"Wenye vyama hivi hawana sera, wao ni wadandiaji sera na wanung'unikaji tu, hawana kipya wakati mwingine wanahubiri kumwaga damu. Sasa hakuna damu itakayomwagika kwa mtu wa kawaida na hata hao wanaohubiri," alisema.

Akizungumza hali za wakulima, Kikwete alisema kuwa serikali itabeba madeni yote ya vyama vya ushirika na kuwapa fedha ili kuwapa nguvu wakulima waweze kuuza mazao yao kwa kuwa vyama vya ushirika sasa vimeshapata uwezo na vinakopesheka.

Kwa upande mwingine, Kikwete alisema kuwa serikali imetoa ruzuku ya mbolea ya Sh40 milioni kwa wakulima wa tumbaku na mazao mengine. Hata hivyo alitoa ahadi mbalimbali za maji na barabara.

Akiwa njiani kwenda Kiomboi mkoni Singida, Kikwete alisimama katika Kijiji cha Makomelo na kuelezwa shida ya maji inayowakabili wananchi wa kijiji hicho.

"Haya nielezeni matatizo yenu, mnataka tuwafanyie nini," alisema Kikwete na baadaye akampatia kipaza sauti mama mmoja na kusema: "Sisi hapa kama unavyotuona, tunataabika kwa maji... tunaomba sana utupatie maji."

Kikwete alisema: "Nimeyasikia, sasa nachukua 'notebook' yangu na kalamu, ninaandika na matatizo yenu nitayashughulikia."

Kata ya Shelui, Kikwete alisimama tena na mwenyekiti wa Kijiji cha Mselebwe, Said Tunu alipewa nafasi azungumze matatizo yao na kuyataja kuwa ni pamoja na ukosefu wa maji katika vijiji sita, barabara na zahanati.

Hata hivyo, Kikwete alisema kuwa atakachofanya ni kuwasaidia kujenga kituo cha afya na kuwataka wananchi kukaa na halmashauri yao kwa ajili ya ujenzi huo wa zahanati. Leo atakuwa Singida mjini.

Chanzo: Mwananchi
 
Hii inaweza kuwa-cost CCM na hasa JK mwenyewe sana vote-wise hasa ikizingatiwa kuwa Rostam kamwe siyo kipenzi cha Watz wengi, hata ndani ya CCM. Wanaonufaika naye labda ni watu wa Igunga na mafisadi wenzake -- you know birds of a feather....

Ninaamini kabisa ninachokisema kwani. Chadema ikilitumia vizuri tukio hili inaweza kumharibia JK.
 
Kukosa matumaini kwenye jamii ndiko kulikofanya ndugu zetu huko mashariki ya kati kujilipua kila siku. Rostam anajulikana kwa uovu wake, kiongozi wa nchi anaposimama jukwaani na kututolea kufuru kama alizotoa huko Igunga natamani ningekuwa karibu nilipuke naye.
 
Haya maisha ya double standards...ndiyo nature ya watu wanaofanya kazi za u spy? Siwaelewi kabisa wana siasa. Huku wanasema hivi kule wanasema tofauti na mwanzo. What a compromise of values!!!
 
Lenye mwanzo halikosi mwisho na mwisho wa ccm ni 31st october.

Chagua mabadiliko chagua chadema
 
Inashangaza na kutia aibu Watanzania kwenda kujikusanga na kupiga makofi kwenye shughuli
hizo. Hii ni usaliti kwa umma unaotaka kujinasua katika mikono ya mabaradhuli hao.
 
The voters will speak 0n 10/31/2010!!

Wewe ni mwizi unaewatetea wezi wenzio, lakini ujue your days are numbered!! Kiwete amefikia kiburi cha hata kuuma mkono ule unaomlisha!! Ufisadi wa Rostam umewaua waTanzania mamia kwa maelfu na ati leo Jakaya anamsifia kuwa mtu safi anayesingiziwa?
 
Kichwa cha habari Kingepaswa kuwa:

JK AWAUMBUA AKINA KILANGO, MWAKYEMBE, SITA NA WENZAKE


-ADAI ROSTMA NI MTU SAFI

-ALISINGIZIWA

-AWATAKA WANANCHI KUWAPUUZA WALE WOTE WANAOMPINGA ROSTAM
 
Sijui nani aliwaruhusu hawa wafanyabiashara waingie kwenye ulingo wa siasa ........................tungewapiga stop kufanya siasa na kuwaruhusu tu kuendelea na biashara zao halali...............hivi watz tutatawaliwa mpaka lini?............kikwete hapo alipo hawezi kuongoza kwa sababu lazima aangalie kwanza masilahi yake na ya rostam na lowasa..................
 
Hapa ndio CCM walipochanganyikiwa kabisa!! JK anajiaribia kuwapigia debe RA,EL, Mramba na Chenge. CCM wamelewa madaraka duh!!
 
Sikio la kufa halisikii dawa..this will cost CCM dearly. Kwa RA,EL, Basil na Chenge angemwacha Dk Bilal aende. Hapa anaonyesha yeye ndio tatizo kubwa kwenye uongozi CCM...I can't believe he has gone this low
 
Sasa nimeamini malipo ni hapahapa duniani! yaliyomkuta Mr.Bush yakupigwa na kiatu natumaini yatawakuta na hawa jamaa shem on you two guys! kweli na ndio maana hata wale viongozi wakongwe waliomaliza muda wao wameona hakuna haja yakumpa suport huyu jamaa kwenye kampeni zake za kutaka kukalia kiti cha uraisi kwa mara ya mwisho, walijua kabisa hii ni aibu! We angalia Mkapa/Cleopa
Msuya/Warioba/Salmini/Ahamed Salim na wengine wengi wenye heshima zao wameona kumpa huyu anayejiita hendsome boy tuff ni noma!! Sasa angalia aibu anayotuonyesha watanzania kweli iko siku kizazi kinachokuja kitawahukumu! Inauma roho sana kutudanganya kwakutuambia wale mafisadi wote lazima utawaaibisha kwakuwachukulia hatua leo unawanyanyua mikono juu nakusema walisingiziwa Loooo!!! Kweli Jakaya unafaa kucheza picha na kina Kanumba hii ni kali! Hadanganyiki mtu watanzania wa sasa sio wale wazamani.
 
Embu tukumbushane mnamtetea vipi Marando kwa ajli ya kutetea mafisadi mahakamani?

Halafu kabla ya kutumia neno mnafiki, jaribuni kutafuta maana halisi ya neno hilo halafu muangalie je nyinyi mnapomtetea Marando kutetea mafisadi ni sawa kumsema JK kumfisia RA? :tonguez:
 
Kikwete amtakasa Rostam

ASEMA NI MTU SAFI ALIYEENEA KAMA TIMU YA MPIRA Send to a friend

Ibrahim Bakari, Igunga

MGOMBEA urais kwa tiketi ya CCM, Jakaya Kikwete amemsifu mweka hazina wa zamani wa chama hicho, Rostam Aziz kuwa ni mtu safi na aliyeenea kila sehemu.Kikwete alisemna hayo wakati akimtambulisha Rostam, ambaye anatetea kiti chake kwenye Jimbo la Igunga ambako amekuwa mbunge tangu mwaka 1995.

Kikwete alitua Igunga baada ya kukamilisha mikutano ya kampeni katika Jimbo la Igalula na Tabora Kaskazini katika mkoa wa Tabora.

Akimnadi Rostam mbele ya halaiki kwenye mkutano uliofanyika Igunga Mjini, Kikwete alisema kuwa Rostam 'ameenea' na anaweza, hivyo wananchi wa Igunga hawana sababu ya kuacha kumpa kura.

"Rostam ni kama timu iliyoenea, timu iliyokamilika kila idara, sasa mnataka nini tena...mnamfahamu, anawasaidia ni mtu wa watu, anawapenda," alisema Kikwete na kushangiliwa na wafuasi wa chama hicho waliofurika kwenye mkutano huo.

Kikwete alisema pia kuwa angeshangaa kama wanachama wa CCM wasingempa nafasi ya kuwa mbunge wa chama hicho.

Kwa upande wake Rostam alimsifu Kikwete kwa uongozi safi na kueleza kuwa yuko tayari kuwatumikia wananchi wa Igunga katika kipindi kingine cha miaka mitano na kwamba Kikwete asisumbuke kuwaza kura za Igunga kwani zipo asilimia 99.99.

"Nimepita katika kata zote 26 za Igunga, wananchi wamenihakikishia kuwa kura zote ni za CCM, usiwe na wasiwasi... usihofie porojo za majukwaani," alisema Rostam huku akishangiliwa.

Pia Rostam aliahidi kusaidia ujenzi wa daraja la Mbuto linalounganishanisha Wilaya ya Igunga na Shinyanga.

Awali katika mkutano wa kwanza kwenye Jimbo la Igalula pamoja na Tabora Mashariki, Kikwete aliwataka wananchi kutochagua vyama alivyoviita vya wanung'unikaji na wanaohubiri kumwaga damu.

"Wenye vyama hivi hawana sera, wao ni wadandiaji sera na wanung'unikaji tu, hawana kipya wakati mwingine wanahubiri kumwaga damu. Sasa hakuna damu itakayomwagika kwa mtu wa kawaida na hata hao wanaohubiri," alisema.

Akizungumza hali za wakulima, Kikwete alisema kuwa serikali itabeba madeni yote ya vyama vya ushirika na kuwapa fedha ili kuwapa nguvu wakulima waweze kuuza mazao yao kwa kuwa vyama vya ushirika sasa vimeshapata uwezo na vinakopesheka.

Kwa upande mwingine, Kikwete alisema kuwa serikali imetoa ruzuku ya mbolea ya Sh40 milioni kwa wakulima wa tumbaku na mazao mengine. Hata hivyo alitoa ahadi mbalimbali za maji na barabara.

Akiwa njiani kwenda Kiomboi mkoni Singida, Kikwete alisimama katika Kijiji cha Makomelo na kuelezwa shida ya maji inayowakabili wananchi wa kijiji hicho.

"Haya nielezeni matatizo yenu, mnataka tuwafanyie nini," alisema Kikwete na baadaye akampatia kipaza sauti mama mmoja na kusema: "Sisi hapa kama unavyotuona, tunataabika kwa maji... tunaomba sana utupatie maji."

Kikwete alisema: "Nimeyasikia, sasa nachukua 'notebook' yangu na kalamu, ninaandika na matatizo yenu nitayashughulikia."

Kata ya Shelui, Kikwete alisimama tena na mwenyekiti wa Kijiji cha Mselebwe, Said Tunu alipewa nafasi azungumze matatizo yao na kuyataja kuwa ni pamoja na ukosefu wa maji katika vijiji sita, barabara na zahanati.

Hata hivyo, Kikwete alisema kuwa atakachofanya ni kuwasaidia kujenga kituo cha afya na kuwataka wananchi kukaa na halmashauri yao kwa ajili ya ujenzi huo wa zahanati. Leo atakuwa Singida mjini.

Chanzo: Mwananchi


JK ni balaa, anawafanya wananchi kama watoto!!! Eti haya nachukua notebook naandika, tutayashughulikia matatizo yenu!!! Mhh!!

Mbona anafanya kama tayari ni raisi? Hakuna haja ya kampeni...!!!:hand:
 
Du hapo ndo mimi nachoka kabisaa kwanini anamkumbatia huyu mtu???
Hawezi kuachana nae ningekuwa mwakyembe na eng manyanya ningehama ccm leo hii kwani aibu inamaana walimsingizia na lowasa jamani tunaelekea wapi sasa!??
 
Embu tukumbushane mnamtetea vipi Marando kwa ajli ya kutetea mafisadi mahakamani?

Halafu kabla ya kutumia neno mnafiki, jaribuni kutafuta maana halisi ya neno hilo halafu muangalie je nyinyi mnapomtetea Marando kutetea mafisadi ni sawa kumsema JK kumfisia RA? :tonguez:
marando yupo kwenye kazi aliyosomea wewe ni haki yake!
 
Back
Top Bottom