EasyFit
JF-Expert Member
- Jul 4, 2011
- 1,269
- 1,082
Aliyekuwa mgombea wa jimbo la Igunga kupitia tiketi ya CUF, Lucas Mahona, amesema wameanza kuwalipa posho mawakala wote 522 waliosimamia uchaguzi mkuu uliopita, amesema mawakala hao walikuwa wanawadai hivyo wameamua kuwalipa Sh4,000 kila mmoja hivi sasa na kwamba walichelewa kuwalipa kwa sababu hawakuwa na fedha.
"Ni kweli tunaendelea kuwalipa mawakala wetu na hiyo si rushwa kwa vile ni haki yao. Mafungu yalichelewa kutufikia ndio maana tunawapa posho zao na si kwa sababu ya uchaguzi mdogo, tunaomba mtuelewe," alisema.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Sera na Utafiti wa Chadema, Mwikabe Mwita Waitara ambaye yuko Igunga, amedai CUF wamekuwa wakipita vijijini huku wakigawa fedha katika mazingira ya rushwa wakijidai kulipa madeni ya mawakala wao katika Uchaguzi Mkuu uliopita kiasa cha Sh5,000 na nyongeza ya Sh4,000 kama fidia na usumbufu.
Source: Mwananchi
"Ni kweli tunaendelea kuwalipa mawakala wetu na hiyo si rushwa kwa vile ni haki yao. Mafungu yalichelewa kutufikia ndio maana tunawapa posho zao na si kwa sababu ya uchaguzi mdogo, tunaomba mtuelewe," alisema.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Sera na Utafiti wa Chadema, Mwikabe Mwita Waitara ambaye yuko Igunga, amedai CUF wamekuwa wakipita vijijini huku wakigawa fedha katika mazingira ya rushwa wakijidai kulipa madeni ya mawakala wao katika Uchaguzi Mkuu uliopita kiasa cha Sh5,000 na nyongeza ya Sh4,000 kama fidia na usumbufu.
Source: Mwananchi