ntamaholo
JF-Expert Member
- Aug 30, 2011
- 12,906
- 6,909
Wadau salamuni.
Tarehe 14.11.2011, IJP Mwema aliongea na vyombo vya habari na kutoa alichokiita PRESS RELEASE kama tahadhari lakini pia katika kuutumikia umma wa watanzania kama kazi yake ilivyo. Waraka huu, sijauona hapa JF pamoja na kuwa ulitolewa kwa wanahabari, labda wengi hawahudhurii humu ndani au wameuupuuza.
Nimefanikiwa kuupata waraka huu, ambao pia unapatikana katika web ya jeshi la polisi ili tuweze kuujadili. Kwani malengo ya afande ni kuusambaza waraka huu hadi ngazi ya vijiji ili wananchi wafundishwe kuendelea kuvumilia na wajiepushe katika michakato ya kutafuta haki mbalimbali.
Tunapoelekea katika mchakato wa kudai katiba mpya ambayo pia tutahakikisha inamwajibisha hata yeye mwenyewe kwa umma na sio kwa serikali kama ilivyo sasa.
Nawasilisha taarifa hiyo kwa kuijadili.
Tarehe 14.11.2011, IJP Mwema aliongea na vyombo vya habari na kutoa alichokiita PRESS RELEASE kama tahadhari lakini pia katika kuutumikia umma wa watanzania kama kazi yake ilivyo. Waraka huu, sijauona hapa JF pamoja na kuwa ulitolewa kwa wanahabari, labda wengi hawahudhurii humu ndani au wameuupuuza.
Nimefanikiwa kuupata waraka huu, ambao pia unapatikana katika web ya jeshi la polisi ili tuweze kuujadili. Kwani malengo ya afande ni kuusambaza waraka huu hadi ngazi ya vijiji ili wananchi wafundishwe kuendelea kuvumilia na wajiepushe katika michakato ya kutafuta haki mbalimbali.
Tunapoelekea katika mchakato wa kudai katiba mpya ambayo pia tutahakikisha inamwajibisha hata yeye mwenyewe kwa umma na sio kwa serikali kama ilivyo sasa.
Nawasilisha taarifa hiyo kwa kuijadili.
IJP MWEMA said:
TAARIFA YA INSPEKTA JENERALI WA POLISI SAID A. MWEMA ALIYOTOA KWA VYOMBO VYA HABARI TAREHE 14 NOVEMBA, 2011, KUHUSU VITENDO VYA VURUGU NA FUJO VILIVYOJITOKEZA KATIKA MAENEO MBALIMBALI HAPA NCHINI
Ndugu Wananchi,
1. Nimelazimika nizungumze nanyi kuhusu matukio ya vurugu na fujo yaliyojitokeza katika maeneo mbalimbali hapa nchini. Matukio haya ya wananchi kushindwa kupata suluhu ya matatizo yao kwa kufuata sheria, kanuni na taratibu yamejitokeza katika mikoa ya Arusha, Mbeya, na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Matukio haya yamesababisha hasara kubwa kwa raia wema na hata kurudisha nyuma juhudi za maendeleo ya nchi. Naomba nitumie fursa hii ili kuwasiliana na wananchi wenzangu katika kuhakikisha kwamba amani, usalama na utulivu vinadumishwa hapa nchini.
2. Kama mnavyofahamu, moja ya jukumu la Polisi popote duniani ni kuhakikisha usalama na amani pamoja na kulinda maisha ya raia na mali zao. Ili Jeshi la Polisi lifanikishe jukumu lake hili ni muhimu sana kwa raia /wananchi kuenzi amani na usalama uliopo nchini. Sababu ya msingi ya raia kuenzi amani, usalama na utulivu uliopo nchini ni rahisi kuona kwani; Amani ya nchi ikiharibika ni kama mfano wa chombo kinachozama baharini, hakuna anayepona wote wanakwenda na maji. Ikiwepo bahati ni wachache tu wanaonusurika. Kwa mantiki hiyo, fujo na vurugu zilizojitokeza hivi karibuni katika baadhi ya maeneo hapa nchini si dalili nzuri na zinaashiria uvunjifu wa amani na utulivu ambazo ni nyenzo muhimu katika kuleta maendeleo nchini. Fujo, vurugu na vitendo vingine vya ukiukwaji wa sheria visipodhibitiwa haraka vinaweza kufikisha nchi pabaya.
3. Ili tusifike huko, na wakati tukisubiri matokeo ya uchunguzi wa matukio hayo, nimeona nizungumzie mustakabali wa amani na usalama wa nchi yetu kwa kutazama baadhi ya mambo yafuatayo:-
(i) Kuhamasisha kufanya fujo, vurugu kama vile kwenda kubomoa Benki, kuvamia na kuharibu vituo vya polisi, kuharibu mali za watu na kuharibu miundombinu mbalimbali iliyojengwa kwa kodi ya umma kwa kisingizio cha siasa ama jazba; ni kuvunja sheria. Kwa sasa yako mazoea ya kutaka huruma itokane na shinikizo la kisiasa. Ikumbukwe Tanzania ni yetu wote na sote lazima tuheshimu sheria tulizojiwekea. Itakuwa sio hekima kwa nchi yetu kuona sheria inavunjwa na watu wachache kwa kisingizio cha siasa ama jazba bila kuchukuliwa hatua. Shughuli za siasa ni kitu kimoja na fujo ama vurugu za jazba ni kitu kingine. Upo umuhimu wa kutenganisha mambo hayo mawili na hapana budi mamlaka za kisheria ziheshimiwe na watu wote bila kujali itikadi zao kisiasa au kijamii.
(ii) Waheshimiwa Wabunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, walipitisha sheria ya Vyama Vya Siasa na Sheria ya Jeshi la Polisi, sheria hizo zimeweka utaratibu na miongozo ya kufuata katika kuratibu mikusanyiko mbalimbali ikiwemo maandamano na mikutano ya hadhara. Haki na utaratibu wa kufuatwa na Vyama Vya Siasa pamoja na Jeshi la Polisi kupewa taarifa ya mikusanyiko imefafanuliwa pia katika sheria hizo. Kwa hali hiyo ifahamike wazi kwamba Jeshi la Polisi halina nia mbaya ya kuzuia mikusanyiko ama maandamano. Hata hivyo, katika utekelezaji wa sheria na kanuni hizo, pale Jeshi la Polisi linapopata taarifa ya mkusanyiko au maandamano, hulazimika kuzingatia mambo mengine muhimu kabla ya kuruhusu mkusanyiko ama maandamano kama vile: haki ya raia wengine ambao hawatahusika na mikusanyiko hiyo kwa mfano njia ya kupita na mahala pa mkutano, kuepusha migongano, kusaidia watu wengine kuendelea na shughuli zingine za kujitafutia maisha, watoto kwenda shule, au wagonjwa kwenda hospitali. Kwa hiyo ikitokea Polisi kuzuia mkusanyiko isihesabike kwamba wanaonea wanasiasa ama kundi fulani la watu. Sheria tajwa zinatoa pia fursa ya kukata rufaa kwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi na hata kwenda Mahakamani ikibidi kudai haki iliyozuiwa. Vilevile hakuna kipengele cha sheria kinaruhusu kufanya fujo na kujichukulia sheria mkononi kwa sababu za zuio la Polisi. Taratibu hizi ziko pia katika nchi nyingine nyingi zilizokomaa kidemokrasia kwa miaka mingi kama vile Marekani, Uingereza na Ujerumani.
(iii) Katika kutekeleza jukumu la kuhakikisha amani na usalama unakuwepo wakati wote nchini, Polisi wanawajibika kisheria kudhibiti vitendo vyote vya uvunjifu wa amani. Wakati mwingine, kulingana na mazingira ya vurugu na fujo, polisi hulazimika kutumia nguvu za kiasi kulinda maisha na mali za raia pamoja na kukamata wahalifu. Wakati wa matumizi ya nguvu za kadri polisi hufanya mchakato ili kupima ni nguvu za aina gani zitumike kulingana na changamoto zilizopo kwa wakati huo. Kutoa tafsiri ya fikra ya nguvu kubwa ni nini na nguvu ndogo ni nini na ni matukio gani yaliyokuwa yanatendeka wakati nguvu inatumika, matendo na mazingira ya mapambano ndio yanayolazimisha Polisi kutumia nguvu kumkabili yule anayelazimisha nguvu itumike ili kumzuia mtu ama kikundi cha watu wanaovunja sheria.
(iv) Ndugu wananchi, mbali na vurugu hizo za kisiasa na kijamii, nchi yetu inakabiliwa pia na matishio mengine ya kiusalama kama vile: Ugaidi, Uharamia, Uhamiaji haramu, Ujambazi, Mapigano na vurugu zinazoendelea katika nchi za jirani. Naomba kutumia fursa hii kutoa wito kwa wananchi kuendelea kutoa taarifa kuhusu wale wote wanaowashuku kuhusika na uhalifu wa aina yoyote ili kudumisha amani na utulivu nchini hususan katika kipindi hiki tunachoelekea mwisho wa mwaka na maadhimisho ya miaka hamsini tangu tupate uhuru wetu.
(v) Pia, navishukuru vyombo vya habari kwani nyinyi ni sehemu ya Watanzania. Naamini kwa taaluma zenu mnayo fursa kubwa ya kuelimisha jamii kuhusu madhara ya fujo kwa maana vurugu zitawagusa na nyinyi pia. Usalama ni bidhaa muhimu na adimu ambayo inahitajiwa na kila mtu. Usalama ninaozungumzia hapa sio wa chama tawala au vyama vya upinzani tu, ni usalama wa Watanzania wote (watoto, vijana, wazee, wanawake kwa wanaume). Kwa hiyo ni lazima sote tushiriki kuhakikisha hakuna mtu anayepata nafasi ya kuvunja amani na utulivu wa nchi yetu. Ni muhimu kila mtu atii sheria bila shuruti, kwa wale wanaokaidi hatuna budi kuwashurutisha watii sheria, jambo ambalo limekuwa na gharama kubwa kwa kodi za wananchi. Polisi kama chombo cha dola hatutakuwa na ajizi kwa yeyote atakayevunja sheria za nchi na kila mtu atawajibika peke yake kwa kosa alilolitenda.
(vi) Natoa rai kwa watanzania wote kuelewa kuwa Polisi ni Jeshi lao; askari ni watoto wenu ama ndugu zenu. Pia ni watumishi wenu mliowaajiri kulinda usalama. Tutafakari ni kwanini mtu mwenye busara au kikundi cha watu wanaotakiwa kutii sheria wanamua kufanya fujo, vurugu na hata kupigana na Polisi, ni kwa nini tulazimishe nguvu itumike? Historia inaonyesha fujo na vurugu haziwezi kutatua kero na malalamiko yoyote bali zinarudisha nyuma maendeleo kiusalama, kiuchumi, kijamii na kidemokrasia (Kisiasa). Nawasihi wananchi kufuata taratibu katika kuwasilisha kero kwa mamlaka husika. Pia, nawashukuru wananchi wote ambao wamekuwa wakitupa ushirikiano kwa kutii sheria bila kushurutishwa. Niwaombe waendelea kuwa watulivu kwa kutokukubali kushawishiwa na mtu yeyote au kikundi cha watu wanojihusisha na vitendo vinavyoweza kuhatarisha usalama wa maisha ya raia na mali zao.
AHSANTENI KWA KUNISIKILIZA