IGP Mwema, Please, Please, Please, Stop This Police Brutality!. Utampeleka JK The Hague-Part II!

Mkuu IGP, Kamanda Saidi Mwema,

Hebu Shuhudia!.

attachment.php


Hii ndio picha ya mwisho ya mwanahabari, mpiganaji Daudi Mwangosi aliyefia kwenye uwanja wa mapambano!,

1. Ukiangalia kwa makini, utashuhudia hapa, Daudi Mwangosi alikuwa amepigwa mpaka kuangushwa chini, askari hao 6 wenye uniform na mmoja plain clothes mwenye T-shirt ya blue na kofia nyeusi ameshika bastola kwa mkono wake wa kulia, walikuwa wanaendelea kumpigia nini ili hali hana silaha yoyote, haja resist arrest yoyote, why all this police brutality?.

2. Ukimwangalia Mwangosi, amejishika kiunoni kwa huyo OCD mwenye kifimbo, licha ya kipigo alichokipata, kamwe hakuacha zana zake za kazi, mkuno wake wa kulia bado umeshika kamera yake na baada ya kifo, begi lake la laptop ndogo lilikuwa pembeni yake!. Hivi hawa polisi wote sita, wanamshambulia mtu mmoja tena mwenye camera inaonekana wazi, huku kamanda wao akijitahidi kuwazuia kwa kumkinga, lakini bado wakaona haitoshi ndipo unamuona askari huyo akimuelekezea kabisa mtutu wa bomu la machozi!, whay all this police brutality, why?!.

3. Najua Mkuu Kamanda Mwema, inawezekana wewe hupati muda kupita humu jf kwa vile mtandao huu hauna jema la kuisifia serikali yako, na vile vile uko bize sana na shughuli za ulinzi wa raia na mali zao (japo wengine kwa kuwaua kwa makusudi mazima), lakini naamini vijana wako wanapita humu na watakuletea hizi salamu zetu,
tunakuomba sana sana sana, stop this police brutality, utakuja kumponza bure shemeji!.

4. Tanzania tuna uchache sana wa wanasheria, na waliopo wengi hufanya kazi kwa wenye nazo, hivyo tangu huu mlolongo wa mauaji ya polisi, hakuna mwanasheria, shirika, wanaharakati, au chama chochote cha siasa kimelifikisha jeshi la polisi mahakamani, simply because wanaokufa wote ni watu hohehahe, familia zao hazina uwezo wa hata tuu wa kujua haki zao za kudai fidia rasmi serikalini, bali uwezo wa kuajiri mwanasheria kuwatetea mbele ya haki kwa kulishitaki jeshi la polisi!.

5. System ilipoamua kumshuhulikia Imram Kombe kwa kutumia polisi wazembe, angalau familia ile ilikuwa na uwezo wa kuajiri wakili jeshi la polisi likashitakiwa na serikali ikalipa fidia ya kifuta machozi cha mamilioni, japo mlizuga kuwa askari wale walihukumiwa vifungo japo hawakuvitumia lakini familia ile angalau chochote kitu ilipata, milioni 300 kwa miaka hiyo, japo hailingani na uhai wa binadamu, lakini angalau ilikuwa sii haba!, hawa wengine wote, hawakuwa na wa kuwapigania lakini kwa Mwangosi, its a wrong button!.

6. This time, tunataka kuwaona vijana wako behind bars, the soonest posible wakati uchunguzi ukiendelea, hata kama utawashitaki wewe kwa negligence, sisi bado tutakushitaki wewe kwa kesi ya madai, ili familia ya Mwangosi angalau ipate pa kushikilia!.

7. Yote vijana wako waliyoyafanya, watu wamevumilia l;akini kwa hili la Daudi Mwangosi, uvumilivu umetufika mwisho maana ni kifo cha unyama wa ajabu kab isa kupata kushuhudiwa na binadamu alietendewa na binadamu mwingine kwa kisingizio cha line of duty!.

8. Nimekupa angalizo, kama usipochukua hatua madhubuti zenye genuinity kama sura yako inavyoonyesha, unaweza kushindwa kuamini kuwa hata 2015 inaweza kuwa mbali, angalia sana usije kujikuta unamponza shemeji, wewe na yeye na wenzenu, mnaweza kujishtukia mko njia moja kuelekea the Hague bila kuamini!.

9. Watanzania ni watu wapole, wavumilivu na wastahimilivu wa hali ya juu, lakini angalia usiwafikishe mahali, wakaishiwa upole, uvumilivu na usahilivu na kufikia kuamua liwalo na liwe, Hata Ghadafi alijua kuwa anapendwa hivi hivi anavyopendwa shemeji, hata Hosni Mubarak alijua anapendwa hivi hivi anavyopendwa shemeji, hata Wamisri nao walikuwa wapole, wastahimilivu na wavumilivu kama Watanzania, hata Walibya nao walikuwa vivyo hivyo, uvumilivu ulipofika mwisho, matokea sote tunayajua, yakitokea ya kutokea, usije kusema hatukukuonya kabla!.

10. Mwisho kiukweli, to be honest, Kamanda Mwema kama lilivyo jina lalo, unaonekana wewe ni mwema genuinely kwa maneno na matendo, na naamini alishataka kuwachukulia hatua vijana wako siku nyingi, ila ulizuiwa na aliyekuzuia tunamjua na sababu tunazijua!, nakushauri this time, usikubali!, mkatalie na uchukua hatua zile za dhamira yako inazokutuma, vinginevyo 2015, na wewe utajikuta unatafuta nchi ya kuhamia!.

RIP KAMANDA MPIGANAJI DAUDI MWANGOSI, DAMU YAKO HAIKUMWAGIKA BURE!, SOMEONE MUST PAY VERY DEARLY HAPA HAPA DUNIANI! KAMA NI NOMA NA IWE NOMA!, LIWALO NA LIWE!.

PASCO.

NB: Pasco wa JF ni mwanahabari wa kujitegemea aliyesomea fani ya sheria lakini anaendelea kuitumikia fani ya habari kutokana na mapenzi makubwa ya fani hii!. Kufuatia kifo cha Mwangosi kumgusa sana, sasa ameamua kumbe msaada mkubwa kwa Watanzania sio fani ya habari tena, anaanza taratibu za ku wind up, kuachana na ku fani ya habari, na kuelekeza majeshi kuitumikia rasmi fani ya sheria, to stand for the voiceless ambao can't affort to pay for an advocate!.



Mzee Pasco 2015 ni mbali mno! tunatakiwa ku act now and just now, sikumbuki vizuri ni nchi gani lakini kuna story ya kijana mmachinga aliyejipiga kiberiti kwa kupinga unyanyasaji wa askari waliokuwa wanawanyanyasa kama wafanyavyo mgambo wa manispaa za Tz, nakumbuka alivyoibuka kuwa vuguvugu la mapambano ya ana kwa ana yaliyoleta mabadiliko ya kweli kwa wananchi wa nchi hiyo.

Daudi Mwangosi awe ni kichocheo cha mapambano ya vitendo dhidi ya polisi wadharimu wa nchi hii tupambane nao kwa vita ya kutoana roho kama wanavyotufanyia kwa kutumia siraha tulizonunua wenyewe tukawakabidhi wakazitumia kutumaliza! inawezekana raia kuwashinda polisi suala ni kuondoa woga tu.

Jamaa yangu msomi aliwahi kuniambia kuwa ubinafsi ndio ulisababisha mwarabu mmoja mwenye gobole kuongoza watumwa zaidi ya mia eti kwa sababu hakukuwa na wakujitoa muhanga kumkamata mwarabu kabla hajafyatua gobole lililohitaji nusu saa kushindilia baruti kwanza! kila mtumwa alikuwa anaogopa akijitokeza wa kwanza atauawa yeye japokuwa hilo lilikuwa halizuii kuuawa kwao.

Tangu tumewaogopa polisi hatujanusurika kuuawa lakini tunaogopa kuchukua hatua kwa kile tunachodai tutauawa kumbe tunadelay time tu kwani wao ni zilahir wanachukua wanayemtaka kwa wakati wanaotaka! Twaweza kupamabana na kupata haki ya uhuru wa kuishi.
 
Duu.... Ucambuzi umetulia... hivi kumbe mabomu ya machozi yapigwa kwa mtutu..?
duh ulikuwa hujui mkuu? umesoma seminari gani? au chuo gani hicho ambacho hamjawahi kugoma hata siku moja? au hata kwa wamachinga kwenye mahangaiko yao na polisi hujawahi kukatiza ushuhudia mabomu yanavyorushwa toka kwenye mitutu??
 
kumbe kwenye fujo za polisi inafaa uvae vitu tummboni

kama mapolisi ili UTUMBO usije fumuka ee, oo nimejua leo
 
Are you serious? mnamwomba na kumsifia kuwa ni mwema na sura yake inaonesha wema? Watu wanakufa tunamwomba achukue hatua? Hatua ya kwanza kama alizuiwa kuchukua hatua ni yeye kujiuzulu kwanza. Then awe tayari kuwa shahidi mahakamani kama siyo mshtakiwa nambari moja. Mnawaendekeza hawa sana!!!

Well said but hapo kwenye BOLD, ingekuwa vema ukisema TUNAWAENDEKEZA, naamini u r also a real Tanzanian
 
Mkuu Pasco, siamini kabisa kama huo ulikuwa ni mtutu wa bomu la machozi. Mtutu wa bomu la machozi hauwezi hata siku moja kuelezwa kwa staili ile kwa mtu. Mimi nadhani ulikuwa ni mtutu maalum kwa kazi maalum. Halafu jamaa bado hata hajawekwa chini ya ulinzi wahojiwe.

Mkuu, nimsaidie Pasco, huo ndio wenyewe hasa kwa sisi tuliopitia JKT tunaujua vema, natamani nanyi vijana wa leo muende Juni Kumi na Tano (JKT) ili walau mjue haya mambo. Labda useme kuwa huamini kama yule aliyemuelekezea aliulipua pale au aliulipua later, but y can connect dots, marehemu alichanwa sehemu gani, na alichanwa na nini, na hapo kwenye picha kinaonekana nini, from there unaweza kupata ushahidi wa kimazingira wa kilichotokea kwa mujibu wa picha.
 
Baba wa taifa RIP analia kaburini anapoiangalia nchi aliyoiacha akiongozwa na Masultani wasiojali maslahi ya nchi. Analia anapoiona Ikulu ikigeuzwa kuwa pango la matapeli, wapiga dili, walanguzi wa madawa ya kulevya, na watu kuongwa suti. Analia kumuona kikwete akiligawa nchi katika matabaka ya kidini na kikabila.

Rais Nyerere analia akiwaona usalama wa Taifa wakitumiwa kuwauwa raia wasio na hatia. Nyerere analia kukiona chama alichokiacha na nguvu nyingi ikigeuzwa Chama Cha Masultani na chama cha anasa. Chama cha kurithishana madaraka na kuuza rasilimali za nchi

Nyerere analia kumuona Kikwete akikiua chama chake. Wana CCM. Hatuwezi kunyamaza tena. Hatuwezi tena kuendelea kuongea kwenye makundi chini chini. Lazima Tumuondoe huyu nduli Kikwete. Nyerere anatuhimiza sote watanzania kuamka, kuchukua silaha dhidi ya adui Kikwete na Polisi Wake. Pengine hatuna silaha leo, lakini kesho tutakuwa nazo
 
Mkuu Pasco. Siku zote nimekua najua kwamba kazi ya kupambana na kuondoa utawala mkongwe kama wa kwetu ni ngumu sana,lakini sijawahi waza kwamba watawala wetu wangefanya kitu ya aibu kama hii,na badala ya kuwawajibisha wahusika wanaanza kurushiana mpira! Kwa ufupi hatuna serikali,tunatawaliwa na magenge ya wahalifu wa kisiasa! Hakuna aliye salama,kwasababu hata hawa wachovu wanaowatetea watala humu,wanaweza pigwa risasi mitaani wakafa kama mbwa!
 
Huyu kamanda KAMHANDA ameleta balaa!!!watu wamewachukia polisi kupindukia kwasababu yake.akamatwe apelekwe huko THE HAGE akajibu mashitaka.ukitaka watanzania waamke wenye fura wasikie RPC Iringa amekamatwa na yuko jela.
 
Pasco nimechelewa kurudi nyumbani, ndio narudi muda huu, nitachangia hii thread asubuhi, wacha hasira zipunguwe kidogo. I wanna kill right now.
 
Last edited by a moderator:
Leo PASCO umenifurahisha! kumbe hutumiki. Kifo cha Mwanosi kimeninyima raha mpaka leo. kuna wakati machozi yananitoka nahisi hasira kali.nashukuru MUNGU kanipa subira lakini nilitamani niwe karibu na KAMANDA KAMHANDA ndio angejua kuwa kaniudhi kupindukia. ningemuuma kwa meno yangu koo lake mpaka....
 
Tuko wengi tunaosikia hasira mpk unashindwa kutype. Toka j2 nimeshindwa kabisa kuja na kupost chochote. Hivi mapolisi wote wanaroho mbaya kama ya hao sita kwenye picha? Walionyuma ya hii kadhia wanajisikiaje? Je wamejiandaa kisaikolojia na kile kitakachofuata kwao? Nilijua namna Rais atakavyovurunda kazi awamu yake ya mwisho lkn si kwa kiwango hiki. This is highly stupid. Napita picha kwanini biashara ya madawa ya kulevya inashindikana kuisha nchini kumbe ni kwa sababu inafanywa na mapolisi. Mwisho najiuliza hivi Jwtz wako wapi jamani? Kweli hawaguswi kuwafundisha adabu mapolisi? Na hapo bado hajarudi Mh. Marmo maana naskia alipelekwa china kujifunza kazi kama ya hao hapo juu.
 
Nyelele anaria kwa uchungu sana....

Nyelele atafufuka kalibuni na kuinisulu nchi ya jamhuli ya muungano wa Tanzaniya
zomba ...tupange kwenda msoma tukatembelee kabuli la baba wa taifa
 
Last edited by a moderator:
Nyelele aliiacha hii nchi kila mtu tajiri, mwenye kisomo cha chini ana digrii, nyumba nzuri kwa kila Mtanzania, maji safi, mabarabara kote mazuri ya lami. miji misafi, benki zimejaa fedha za kigeni.
 
Nyelele aliiacha hii nchi kila mtu tajiri, mwenye kisomo cha chini ana digrii, nyumba nzuri kwa kila Mtanzania, maji safi, mabarabara kote mazuri ya lami. miji misafi, benki zimejaa fedha za kigeni.

kuhakikisha kila Mtz anapata elimu ya juu ..alijenga vyuo vikuu vingi sana Dar na mikoani kote
 
Hivi karibuni Waziri wa Mambo ya Ndani, Mh. Emmanuel Nchimbi aliunda tume kuchunguza chanzo cha mauaji ya aliyekuwa mwandishi wa habari wa kituo cha televisheni cha Channel Ten, Bw Daudi Mwangosi, anayedaiwa kuuwawa na askari polisi wakati wakiwadhibiti wanachama wa CHADEMA waliokuwa wakiwazuia wasifungue tawi la chama chao ktk Kijiji cha Nyololo, wilayani Mufindi. Kwa upande mwingine, Baraza la Wahariri Tanzania (MCT) nao waliunda tume nyingine kuchunguza chanzo cha kuuliwa kwa mwandishi huyo.

Matokeo yaliyotolewa na kamati hizi mbili yalitofautiana kwa kiasi kikubwa sana. Wakati tume iliyoundwa na MCT ikiwatia hatiani polisi na kuwanyooshea kidole kwa kusababisha mauaji hayo, tume ya Nchimbi iliwasafisha polisi kwa kudai kwamba hawakuhusika na kadhia ya kuuwawa kwa Mwangosi. Ushahidi wa picha za video na mnato zilizopigwa na vyombo mbalimbali vya habari unaonesha kwamba Mwangosi aliuawa kwa bomu lililorushwa na mmoja wa askari polisi waliokuwa wakimchapa bila huruma mwandishi huyo.

Badala ya tume ya Nchimbi kutoa majawabu juu ya nini kilichotokea, ilijitahidi kuficha ukweli kwa kisingizio cha kwamba hilo swala liko mahakamani. Huenda hayo ndiyo majibu waliyoagizwa na bosi wao, Nchimbi, waje wayatoe kwa wananchi, ambao wengi wao hudhaniwa kuwa mbumbumbu na wasiokuwa na uwezo wa kuchambua mambo. Pamoja na umbumbumbu wao, wananchi wengi wamebaki wakijiuliza maswali mengi yasiyokuwa na majibu (ambayo yalipaswa yajibiwe na tume ya Nchimbi).

Mosi, ikiwa polisi hawakuhusika kumchapa na hatimaye kumuua Mwangosi, je, polisi anayeshikiliwa kwa sababu ya mauji yaliyotokea katika hizo vurugu, anashitakiwa kwa kumuua nani, hasa ikizingatiwa kwamba katika hizo vurugu kilitokea kifo cha mtu mmoja pekee ambaye ni marehemu Daudi Mwangosi? Pili, je, zile picha za mnato na za video zinazoonyesha kundi la polisi wasiopungua wanane wakimpiga vibaya marehemu Mwangosi zilipigwa kutoka nchi gani kama sio kutoka Tanzania, mkoani Iringa? Tatu, inasemekana lile kundi la askari lilikwisha kumuua Mwangosi hata kabla yule polisi mmoja hajamlipua kwa bomu. Nne, je, ni kwa nini wale polisi walioshirikiana kumuua wasitiwe hatiani wote na badala yake akamatwe mmoja tu (aliyerusha bomu) ilihali wote walishiriki kufanya mauaji?

Maswali haya, pamoja na mengine mengi, ndiyo yanayohojiwa na wananchi, na ndiyo yanayoifanya ripoti iliyotolewa na tume ya Nchimbi kuwa batili na ya kugushi. Kwa maana nyingine ni kwamba ripoti hiyo haikukata kiu ya wananchi walio wengi ambao walitaka kufahamu, kwa undani, juu ya utata mzima uliokuwa umegubika kisa cha kuuliwa mwandishi huyu wa habari kufuatia kipigo kikali cha polisi, licha ya kwamba marehemu alikuwa akifahamika kwa polisi wa Iringa kwa muda mrefu.

Ni sababu hizo ndizo zinazowashawishi wananchi kuamini kwamba pesa zao za kodi zimetumika vibaya kwa kuunda tume kanyaboya yenye lengo la kuficha ukweli badala ya kuuanika na hatimaye kutoa majawabu muafaka juu ya nini kifanyike ili kutokomeza ukatatili wa polisi kwa raia wasiokuwa na hatia. Ikumbukwe kwamba kabla ya tukio la kuuwawa kwa Mangosi, polisi walikwishaua wananchi kadhaa katika maeneo tofauti ya nchi, wengi wao wakiwa wafuasi wa CHADEMA waliokuwa wakipigwa risasi za moto kiholela, na hayo yamekuwa yakifanyika hadharani na mchana kweupe!

Wakati bado tunatafakari mauaji ya Daud Mwangosi, majuzi tumesikia kwamba mwandishi wa habari wa gazeti la Tanzania Daima, Shaban Matutu, naye kapigwa risasi na polisi na kunusurika kuuawa. Kama ilivyo kawaida, Kamanda wa polisi wa mkoa wa Kinondoni akaibuka na kutetea uovu huo. Watu tumebaki tunajiuliza bila majibu: ‘Ni lini hasa haya mauaji ya kionevu yatakoma?’ Je, tubaki tukiuawa hivi hivi mpaka Yesu atakaporudi? La hasha! Uvumilivu huo unakaribia kufikia kikomo sasa. Kila jambo likizidi kipimo huleta madhara yasiyovumilika, hasa linapokuwa linatendwa kwa makusudi bila kuzingatia weledi na utumiaji wa akili!

Jeshi la polisi, pamoja na wale wanaowatuma kufanya hayo mauaji (kama wapo) wanapaswa kufahamu kwamba mauaji wanayoyafanya ni ya kiuonevu na kishetani, na kwamba risasi wanazotumia kuua zinatokana na kodi za wananchi wanaowaua. Damu ya hawa watu haiwezi kwenda bure. Iko siku wananchi wataishiwa uvumilivu na kuamua kuwa sugu, kisha wachukue sheria mikononi mwao. Hapo ndipo wanasiasa wanaowatumia polisi kufanya mauaji ya kiholela watakapolia na kusaga meno.
 
Ee kweli sasa naelewa ni kwa nini JK anaenda kubembea au kukokotwa kwenye matoroli na farasi. Nchi imemshinda. Shemeji anamwangusha. Washkaji wanashtukiwa na wapinzani kila kukicha. Dr. Slaa anamshinda ujanja. Mtandao kama unavyoona haufichi kitu. Na uraisi kumbe ni zaidi ya raha! Duuu! Ama kweli watanzania twalipuliwa na walinzi wa uhai na mali zetu! Tukimbilie Rwanda au Kongo?
 
Mukajifunze znz bado wadanganyika hamjakuwa na upeo huo. nyinyi kazi yenu humu jf muandike misamiati mizur basi, watu wakijibu unyanyasaji kwa raia kule znz mnasema ni alqaid kumbe watu wanatafuta haki yao, kama mnakwenda mahakaman unakwenda kumshitak nani unajipotezea muda, akiua kwa bunduk na yeye ni kuuliwa tu, dawa hapa ni kukamata na kuchinja askari angalau 5 kwa mwezi heshima itapatikana tanzania nzima kwa na kwa kila mtu
 
Back
Top Bottom