Ndugu wana Jamii, nilikua na waza kidogo ni nani wa kuwajibika hususani mauaji yaliyofanyika Arusha. Nimegundua IGP mwema ndio mtuhumiwa namba moja wa mauaji ya Arusha pamoja na majeruhi. Hii ni kutokana na kuawaagiza polisi kuchukua sheria mkononi na kupiga risasi watu wasio na hatia yeyote. Nguvu aliyotumia ni kubwa sana hasa pale police inapoamua kutumia risasi za moto kumpiga raiya ambaye hana silaha yeyote. Ni wakati muafaka sasa wa kumwomba IGP ajiuzulu kutokana na kashifa ya mauaji na kujeruhi watu wasio na hatia. Wao wameishitaki CHADEMA kwa kuandamana tu, je aliyeua si zaidi ya kuandamana? Kutoa uhai wa mtu?Je wategemezi ya waliokufa au waliopata majeraha na vilema vilivyotokana na fujo? Tunaomba tuungane wote kwa pamoja kufanya haya yafuatayo
1.Kumtaka IGP ajiuzulu wadhifa wake kutokana na kashifa ya mauaji na kujeruhi Arusha na afikishwe mahakamani.
2.Iundwe tume huru ya kuchunguza ili wote wanaohusika wafikishwe mahakamani
3.Kamanda wa Police Arusha nae ajiuzulu na kufikishwa mahakamani pia
Tushirikiane wananchi wote, asasi za kiraiya, tume ya haki za binadamu, NGOs, jumuiya ya kimataifa na vyama vya siasa (CHADEMA, CUF,DP,TLP,NSSR,UDP,PPT n.k) ili wahanga wa majeruhi na mauaji ya Arusha wapate haki zao. Bila hivi ndigu zetu watakua wanauwawa bila sababu na sisi tunanyamaza tu
1.Kumtaka IGP ajiuzulu wadhifa wake kutokana na kashifa ya mauaji na kujeruhi Arusha na afikishwe mahakamani.
2.Iundwe tume huru ya kuchunguza ili wote wanaohusika wafikishwe mahakamani
3.Kamanda wa Police Arusha nae ajiuzulu na kufikishwa mahakamani pia
Tushirikiane wananchi wote, asasi za kiraiya, tume ya haki za binadamu, NGOs, jumuiya ya kimataifa na vyama vya siasa (CHADEMA, CUF,DP,TLP,NSSR,UDP,PPT n.k) ili wahanga wa majeruhi na mauaji ya Arusha wapate haki zao. Bila hivi ndigu zetu watakua wanauwawa bila sababu na sisi tunanyamaza tu