IGP Mwema na Polisi Jamii

mmbangifingi

JF-Expert Member
Mar 9, 2011
2,839
559
Mkuu wa Jeshi la Polisi S.A Mwema katika kile kinachoonekana kuendeleza dhana ya polisi jamii sasa ameanzisha post ya "Mkaguzi wa Polisi wa Tarafa". Jumla ya wakaguzi wasaidizi (Assistant Inspectors) 631 waliomaliza mafunzo yao ya promotion CCP hivi karibuni, zaidi ya 550 wamepangiwa katika post hizi mpya (Community Policing Officers) ambapo watafanya kazi katika tarafa wakiripoti kwa OCD wa eneo husika katika kile kinachoelezwa 'kulipeleka Jeshi kwa wananchi". Je,,hii itasaidia kurejesha imani ya wananchi kwa Jeshi hasa baada ya hivi karibuni IGP kuonekana kupoteza uweledi wake na jeshi zima kwa kutumiwa kisiasa zaidi hasa kwa kuibeba ccm? Je itarejesha imani ya wananchi kwa ujumla baada ya kuonyesha kushindwa/kulegalega ktk kukabiliana na tatizo la ajali za barabarani, na uhalifu mwingine?
 
Kama wana nia nzuri itasaidia kupunguza matatizo ya vibaka kwa wananchi. LAkini najua hata hao Polisi wataishi katika mazingira ya namna gani. KAta unazoongelea ni mijini au Maana hebu angalia maisha ya walimu yakoje huko katani vijijini!
 
Good idea,i believe this system will help,in Uk hampshire police wamefanikiwa sana kupambana na uhalifu kw kutumia hii dhana ya Community policing,na customer care!sasa itabidi askari wabadilike ili waweze kwenda na hii kasi..
 
huwezi kuishi vizuri kwenye nyumba yako safi wakati majirani zako mende na panya ni mifugo yao!
 
Mkuu wa Jeshi la Polisi S.A Mwema katika kile kinachoonekana kuendeleza dhana ya polisi jamii sasa ameanzisha post ya "Mkaguzi wa Polisi wa Tarafa". Jumla ya wakaguzi wasaidizi (Assistant Inspectors) 631 waliomaliza mafunzo yao ya promotion CCP hivi karibuni, zaidi ya 550 wamepangiwa katika post hizi mpya (Community Policing Officers) ambapo watafanya kazi katika tarafa wakiripoti kwa OCD wa eneo husika katika kile kinachoelezwa 'kulipeleka Jeshi kwa wananchi". Je,,hii itasaidia kurejesha imani ya wananchi kwa Jeshi hasa baada ya hivi karibuni IGP kuonekana kupoteza uweledi wake na jeshi zima kwa kutumiwa kisiasa zaidi hasa kwa kuibeba ccm? Je itarejesha imani ya wananchi kwa ujumla baada ya kuonyesha kushindwa/kulegalega ktk kukabiliana na tatizo la ajali za barabarani, na uhalifu mwingine?

Kwa mtazamo mwingine inaweza kuwa mojawapo ya mbinu za kuthibiti nguvu ya umma!
 
Tatizo mwema na uongozi wake hajajipanga kwani mapolisi tarafa hao hajawaandalia miundo mbinu yeyote ya kuzungukia tarafa husika.Amepanga askari ktk tarafa lakini hajui watafikaje na kwa ujumla wametelekezwa huku fungu kubwa la polisi jamii na uwezeshaji wake akibaki nalo makao makuu.MI NAona kama utapeli mwingine tu kwa wananchi.
 
Back
Top Bottom