mmbangifingi
JF-Expert Member
- Mar 9, 2011
- 2,839
- 559
Mkuu wa Jeshi la Polisi S.A Mwema katika kile kinachoonekana kuendeleza dhana ya polisi jamii sasa ameanzisha post ya "Mkaguzi wa Polisi wa Tarafa". Jumla ya wakaguzi wasaidizi (Assistant Inspectors) 631 waliomaliza mafunzo yao ya promotion CCP hivi karibuni, zaidi ya 550 wamepangiwa katika post hizi mpya (Community Policing Officers) ambapo watafanya kazi katika tarafa wakiripoti kwa OCD wa eneo husika katika kile kinachoelezwa 'kulipeleka Jeshi kwa wananchi". Je,,hii itasaidia kurejesha imani ya wananchi kwa Jeshi hasa baada ya hivi karibuni IGP kuonekana kupoteza uweledi wake na jeshi zima kwa kutumiwa kisiasa zaidi hasa kwa kuibeba ccm? Je itarejesha imani ya wananchi kwa ujumla baada ya kuonyesha kushindwa/kulegalega ktk kukabiliana na tatizo la ajali za barabarani, na uhalifu mwingine?