IGP - Mtandao huu ni hatari - Part I

police jamii

Fanyia kazi kichwa cha hbr!
Ina maana mdau amekurupuka tu na akaja kama alivyoanguka hapo juu,hakika ameona kitu kama alivyokwisha kusema!

Freemason siyo mchezo we jane 000
nakwambia hawa washikaji wakikupitia na wakukute hauna msimamo nakwambia wanazama na mtu!
Achana nao kbs!
Fanyia kichwa cha hbr kazi!
 
maswali ya msingi ya kujiuliza...........
1.hii taarifa ni nzito na inasikitisha kama ni kweli.
2.mbona mleta mada hajataja hata mtu mmoja katika hizo ofisi ambazo zinashiriana na hawa watu?mfano amtaje askari flani au afisa ardhi flani ili taarifa yake iwe na kitovu ie pahali pa kuanzia.
3.taarifa ni ya jumla mno kiasi kwamba inaelea,haina pakushika.
4.taja hata mwananchi mmoja alienyang'anywa ardhi/kiwanja chake ili asaidie hata kuwatafuta hao maafisa wa serikali wanaotumia ofisi zao kinyume na taratibu.
 
Nadhani hili swala si kama tunavyochangia kimasiara wakuu, mtoa mada umefanya vizuri sana na ukweli ni kwamba hili swala lipo na wahusika ni hao wanaojiita mapedeshee wa mjini, kamanda IGP na wengine wanaopita humu lichukueni hili mlifanyie kazi maana litakuwa janga la taifa soon, watu watakufa kwa hili na sisi wenye uchunga na wanaoonewa hatutakaa kimya!
 
Mada nzuri sawa lakini na sisi lazima tutafakari...hebu mleta thread angalau ungesema ni viwanja vipi vimedhulumiwa (fafanua).Maelezo yako yamekuwa ya jumla mno.ukiongezea na neno FREE MASON ni kama unavuta hisia za watu ili "waone uonevu" unaousema,na kwa kadri navyofahamu eneo hilo la mbezi wamiliki wake ni watu wa kujiweza sana - hawawezi kukaa kimya - kuona mfumo huu mpya wa uonevu ukifanyika.

Najua inaweza kutolewa hoja hapa kwamba kuna watu wa kipato cha chini wanamiliki viwanja...sawa lakini si wengi siku hizi,na waliopo si rahisi kuwaondoa wamekuwapo miaka mingi hawajadhulumiwa.

Nachofikiri kwa hakika ni hali iliyokuwapo muda wote ya kununua ama kuuziwa kiwanja ambacho ni mali ya mtu mwingine na hayo yanatokea kwa watu wenye kipato kizuri tu na kesi zipo mahakamani.Mpaka hapo utakapoleta part 2 ikanishawishi..otherwise ni ugomvi wa wakubwa ndio naouona.
 
maswali ya msingi ya kujiuliza...........
1.hii taarifa ni nzito na inasikitisha kama ni kweli.
2.mbona mleta mada hajataja hata mtu mmoja katika hizo ofisi ambazo zinashiriana na hawa watu?mfano amtaje askari flani au afisa ardhi flani ili taarifa yake iwe na kitovu ie pahali pa kuanzia.
3.taarifa ni ya jumla mno kiasi kwamba inaelea,haina pakushika.
4.taja hata mwananchi mmoja alienyang'anywa ardhi/kiwanja chake ili asaidie hata kuwatafuta hao maafisa wa serikali wanaotumia ofisi zao kinyume na taratibu.
Natumia simu but thanx umetoa point zako msingi
 
narudi tena mleta mada labda kachukuliwa demu wake na hao watu hakuna usibitisho hata moja tuamini vipi toa ***** wako
 
polisi wapewe kipaumbele bajeti ijayo, hawa madaktari wanaweza kufikiriwa bajeti ya 2013/14, napendekeza mishahara ya polisi kima cha chini kiwe 700,000/= labda itaondoa tatizo kama si kupunguza maana matendo yao kwakweli mh.. inafika kipindi mtu kabla ya kwenda kituoni unapitia kwanza bank au kwenda kukopa kwa jamaa
 
Sasa ushahidi si msearch hayo majina. Hebu nenda kwenye google usearch papa msofe au kama humfahamu kwa sura bofya hapa the eastafrica: PAPAA MSOFE ATUHUMIWA KUVAMIA KIWANJA MBEZI BEACH!

Pia Papa Msofe akamtapeli Mama Mjane na ITV walimuhoji Kamanda Kenyela RPC wa Kinondoni na huyo Tapeli na Kenyela akamtetea na kusema msofe sio tapeli ni mfanyabiashara. Baadae jamii forum na ITV wakaripoti kwamba huyu Papa Msofe ambaye RPC amemtetea kwenye vyombo vya habari ni tapeli na kwamba Wanaharakati wakiongozwa na mpiganaji Mama Ananelia Nkya walilisimamia kidedea mpaka Waziri Mkuu akingilia kati na kuamuru swala hili lishughulikiwe mara moja. Cha ajabu kuona hivyo tunaambiwa Polisi walimpa huyu tapeli siku saba kurudisha kiwanja na tapeli huyu hakuchukuliwa hatua yoyote. Nadhani ukisearch papa msofe au papaa msofe utapata skendo lukuki za huyu jamaa. Tunaambia polisi wanalipwa mshahara na huyu jamaa.

Mwingine ni Mr Mushi ambaye alikuwa ardhi. Naye ni hatari na anatetewa na maafisa wa Ardhi na Polisi.

Nasikia kweli ukienda Polisi ukataja jina la mtu wanayemfahamu na kusema amevamia kiwanja chako ndio umewaletea mtaji, kwanza wanakwambia hawahusiki nenda kapigane nae mwenyewe au nenda mahakamani na baada ya hapo wanampigia simu huyo jamaa wanamwambia Mkubwa naona umefanya kazi lete pesa yakulinda huku na jamaa fasta anawafikishia fungu lao.

HUU NI UKWELI SION MAJUNGU. hakuna mtu Tanzania anaweza kumdhulumu mtu Ardhi bila kushirikiana na Polisi - HAKUNA!
 
Habari hii ni kweli kabisa. Wiki tatu nyuma walivamia kiwanja Mbezi beach maeneo ya Five Star na kuzungusha ukuta na kuleta walinzi. Nina habari mwenye kiwanja hakupata ushirikiano kabisa na polisi ya Wazo zilipo ofisi za OCD hivyo kwa msaada wa ofisi ya mwanasheria wake waliweza kupata amri ya kusimamisha ujenzi iliyotolewa na mahakama ya Ardhi na kesi itaanza karibuni. Katika uvamizi huo walitumia risasi za moto kumtisha the legal owner na majirani na hata baada ya ku report polisi hawakuchukua hatua yeyote. Habari ni kuwa tapeli mmoja papaa mfadhili wa bendi ndie kiongozi wa kundi lakini anawatumia wasaidizi wake kuongoza uhalifu huu kwa kuwa ameshaonywa karibuni na baadhi ya viongozi wa Polisi na hajatii alichoonywa. Naomba ifahamike kabisa hutapata msaada polisi hawa jamaa wakivamia kiwanja chako na hii ni kwa sababu ya wanalindwa na baadhi ya viongozi wa polisi. Nadhani huu ni uonevu uliokithiri na swala hili lingefuatiliwa na usalama wa Taifa kwani linakua kwa kasi. Nawakilisha wakuu

Inaonekana hawa watu unawajua ila hutaki kuwataja, lakini labda nikupe siri ni kuwa hawa matapeli huwa wanatafuta kiwanja au kuonyeshwa na maafisa ardhi then wanaenda wizarani wanaiba faili zima na kubadilisha nyaraka zote wakishamaliza ndio wanakuja kuvamia by the time unaanza kufuatilia mambo ya kisheria unakuwa umeshachelewa kwani mahakama ya ardhi ikiitisha faili toka wizarani unakuta documents si zako tena, huyo predeshee unayesema alionywa na waziri ni Papaa Msofe alivamia kiwanja cha mama mmoja mbazi beach. Majina yao tunayo ila ninahofu security system ya JF kwa usalama wetu kwani jamaa ni mafia na wanaweza kuua kwani hilo si tabu kwao
 
ndoleha Unaweza kukutana na mimi kesho njoo makumbusho unipe data naweza kufanyia kazi kama kweli unayoyasema na ushahidi unao sitaki mambo ya udaku au umepata viroba

Dada Jane nakupa pole kama unataka kufanyia kazi huu mtandao umeshachelewa kwani hawa wanakula na maboss wako hasa wasaidizi wa mwema kwani ndio wanajua usalama wao jaribu kuongea na wale askari wanaotembea na yale magari yenu watakwambia kwani huwa wanajitahidi kupambana ila wanakutana na vikwazo kutoka kwa maboss wenu. Na watu hawataamini ila kamanda mstaafu Tibaigana anawajua vizuri sana hawa wahalifu
 
maswali ya msingi ya kujiuliza...........
1.hii taarifa ni nzito na inasikitisha kama ni kweli.
2.mbona mleta mada hajataja hata mtu mmoja katika hizo ofisi ambazo zinashiriana na hawa watu?mfano amtaje askari flani au afisa ardhi flani ili taarifa yake iwe na kitovu ie pahali pa kuanzia.
3.taarifa ni ya jumla mno kiasi kwamba inaelea,haina pakushika.
4.taja hata mwananchi mmoja alienyang'anywa ardhi/kiwanja chake ili asaidie hata kuwatafuta hao maafisa wa serikali wanaotumia ofisi zao kinyume na taratibu.

Mkuu nataka nikuhakikishie kuwa hii kazi huwa inafanywa kama teamwork kwa hiyo hutakuja kupata jina moja moja iwe ardhi au polisi bali ni group la watu wengi
 
Sasa ushahidi si msearch hayo majina. Hebu nenda kwenye google usearch papa msofe au kama humfahamu kwa sura bofya hapa the eastafrica: PAPAA MSOFE ATUHUMIWA KUVAMIA KIWANJA MBEZI BEACH!

Pia Papa Msofe akamtapeli Mama Mjane na ITV walimuhoji Kamanda Kenyela RPC wa Kinondoni na huyo Tapeli na Kenyela akamtetea na kusema msofe sio tapeli ni mfanyabiashara. Baadae jamii forum na ITV wakaripoti kwamba huyu Papa Msofe ambaye RPC amemtetea kwenye vyombo vya habari ni tapeli na kwamba Wanaharakati wakiongozwa na mpiganaji Mama Ananelia Nkya walilisimamia kidedea mpaka Waziri Mkuu akingilia kati na kuamuru swala hili lishughulikiwe mara moja. Cha ajabu kuona hivyo tunaambiwa Polisi walimpa huyu tapeli siku saba kurudisha kiwanja na tapeli huyu hakuchukuliwa hatua yoyote. Nadhani ukisearch papa msofe au papaa msofe utapata skendo lukuki za huyu jamaa. Tunaambia polisi wanalipwa mshahara na huyu jamaa.

Mwingine ni Mr Mushi ambaye alikuwa ardhi. Naye ni hatari na anatetewa na maafisa wa Ardhi na Polisi.

Nasikia kweli ukienda Polisi ukataja jina la mtu wanayemfahamu na kusema amevamia kiwanja chako ndio umewaletea mtaji, kwanza wanakwambia hawahusiki nenda kapigane nae mwenyewe au nenda mahakamani na baada ya hapo wanampigia simu huyo jamaa wanamwambia Mkubwa naona umefanya kazi lete pesa yakulinda huku na jamaa fasta anawafikishia fungu lao.

HUU NI UKWELI SION MAJUNGU. hakuna mtu Tanzania anaweza kumdhulumu mtu Ardhi bila kushirikiana na Polisi - HAKUNA!

Mkuu nakushukuru sana kwa kuleta haya majina nataka kuongezea kwa huyu Mushi yeye mkewe bado yuko ardhi na ndio huwa anachezesha mambo yote ya mmewe pale wizarani.
 
narudi tena mleta mada labda kachukuliwa demu wake na hao watu hakuna usibitisho hata moja tuamini vipi toa ***** wako

Hacha kumkejeli mtoa mada nataka nikwambie inawezekana hata wewe uko kwenye mtandao kwani kusema mtu uonane nae makumbusho halafu baadae unaanza kejeli nina wasiwasi kama huwafanyii kazi hawa jamaa kwani aneo lenyewe la makumbusho ndio makutano yao ya mipango kwa hiyo ninawapa tahadhali watu kukupa namba labda wakuwe mawazo ya kufanyia kazi kwa kuanzia tafuta viwanja vinavyolindwa na kampuni ya ulinzi ya kiwango security mbezi beach halafu fuatilia historia za hivyo viwanja
 
Kama unafahamu haki zako huwezi lalamika, namba ya simu ya huyo IGP ipo mpigie mweleze na ushahidi uwe nao
Utakaporudi na hiyo part 2 uje na majina ya hao wahalifu pamoja na hao makamanda

Pima hoja kabla ya kukurupuka na majibu mepesi katika hoja nzito kama hii.......haya ndo huleta machafuko makubwa sana, hata hayo ya mauaji unayoyasikia "Great lakes" yamekuwa na element za land conflict historically. Sasa mtu kaanza kuchukua hatua kwa kuweka in public na kusema kuwa baadhi ya polisi wanashiriki katika mambo hii...

Hujui kuwa public attention is part and parcell ya ku- deal na the so said to be a corrupt system????

Kama unafuatilia habari leo utakuwa umeona DCI katoa maelezo.....ambayo pia yamefuatia baada ya utata uloambatana na sintofahamu ya muda mrefu kwenye public na source ilikuwa public media.

Hizi majibu nyepesi please songa kule MMU huwa tunajadili emotions....hii ni stake ya watu specifically and a nation in its general aspects


They say a mere spark may turn a house into ashes if......................................!!!!!!!!!!
 
Hii ni Issue serious lkn wengine wanaleta utani. Ni vema tukatoa msaada kwa mtoa maada ili malalamiko yaende sehemu sahihi pa1 na ushahidi uliotolewa humu.
 
sinauhakika na mtoa mada nikupe simu ya igp said mwema au ya dci manumba mimi mwenyewe nipo kwenye system kama nikweli na ushahidi unao mimi naweza kusaidia

Hii maneno kwisha chosha sisi jamani

If you are in the system(as per your claims) you took oath........... "to prevent this state, its interest and its people even though the mission will be dangerous or even lethal to yourself".......

Inforamation is information hata kama umeitoa kwenye kipande cha karatasi jalalani........it is forbiden to undermine information or your enemy even if it is just an ant.....etc etc

Sasa wewe mwana system (kwa madai yako) unayeona habari yenye kutishia usalama uloapa kuulinda kwa gharama yoyote badala ya kuchukua hatua unatoa namba za simu ambazo zipo kwa vituo vya polisi zimeandikwa kwenye vibao wazi kweupe????? R U SERIOUS......????????

YOU think hapa unatakiwa kusaidia.....????? an active companion.......!!!!!! This is the routine work sio kusaidia hata siku moja.......wenye kazi zao hii ni task tayari n wapo kazini

Next time be a more little kean on posting madam jane_000
 
Makamanda wa polisi wawe wanachaguliwa na wananchi....

kinachotakiwa ni uadilifu na uzalendo wa dhati siyo kuchaguliwa, wapo viongoz waliopatikana kwa kuchaguliwa lakini ni corrupt kupita maelezo, wengine ni top leaders, unawafahamu!
 
mtoa mada usimtafute mtu mpaka umepata uhakika wa usalama wako isijekuwa wabaya wako bure wanajifanya wanausalama.inasikitisha mtu mdogo kama papaa msofe vyombo vya usalama vinashindwa kumuadhibu!
 
Back
Top Bottom