IFM wamegoma

Fidel80

JF-Expert Member
May 3, 2008
21,947
4,444
Habari nilizo zipata hivi punde wanafunzi wa IFM wamegoma.
Wanasema wamegomea ratiba ya mitihani wanadai wengine wana mitihani 2-3 kwa siku wameanza kugoma kuanzia saa 12 asubuhi kwa hiyo FFU wapo pale kuangalia amani.
 
Suala la ratiba ya mitihani ni la utawala wa Chuo, FFU wamefuata nini hapo
 
Kugoma kwa sababu ya ratiba ni sababu finyu sana.Kwani mwanafunzi hajui kuwa kuna mtihani mwisho wa siku? Sioni ubaya kufanya mitihani 2-3 kwa siku.
KUGOMA KWA SABABU HII NI UTOVU WA NIDHAMU.
 
Jamani hata ratiba ya mitihani nayo ni ya kugomea?
Sasa kila kitu hata kisicho maana wagome tu? Migomo sasa wanaitumia isivyo.
 
Kama wanagomea ratiba ya mitihani naona kuna tatizo! But ni ngumu sisi tulio nje ya pale kujua kwa undani.Swala hili lingewezekana kumalizwa na chuo! Labda kuna wanachogomea ambacho hawajakiweka hadharani au walikuwa na ratiba ya mgomo leo wameamua kuitimiza!
 
Mitihani 2-3 si kitu kigeni hasa kutokana na wingi wa wanafunzi na uchache wa miundombinu ambao vyuo vingi vimepata toka yebo yebo. UD kuna wanofanya mitihani 4 kwa siku toka alfajiri mpaka usiku sana. Hii huwakumba zaidi wanafunzi waliochanganya uchaguzi wa kozi, tena huwa wanafungiwa baada ya mtihani mmoja ili wafanye mwingine.
Kuna mitihani inafanyika Jumamosi na Jumapili kutokana na uamuzi wa wanafunzi wenyewe maana ratiba haipangiki. Suluhisho la kufanya mtihani mmoja kwa siku lipo ila ni uchaguzi binafsi unawalazimisha ili wasirudi kufanya mtihani semester nyingine. Utaratibu wa mitihani na ratiba nadhani uko wazi kwa vyuo vingi.
Kugoma kwa sababu ya ratiba ya mtihani bado sijaelewa... any info please?
 
Suala la ratiba ya mitihani ni la utawala wa Chuo, FFU wamefuata nini hapo

Ninavyofahamu mimi ni kuwa kazi ya FFU ni kutuliza fujo.Uwepo wao ni mahali penye fujo.Kazi ya polisi wa kawaida ni kulinda usalama wa raia na mali zao.Case ya IFM haikuhitaji FFU kukaa pale.Haku uvunjifu wa amani hata kidogo.Kiutaratibu ni polisi wanatakiwa kulinda mali za chuo na usalama wa watu wote.Kupeleka FFU pale ni sawa na ku-provoke wanachuo kuanzisha vurugu.

Naamini huu ni utaratibu wa kisiasa na siyo wa kiusalama.
 
Tunahitaji kuwa na macho ya ndani kabla hatuja comment hapa........! mlioko jirani na IFM mtafuteni Rais wao athibitishe uwepo wa mgomo pili aeleze sababu za mgomo huo, kama kweli upo! Ratiba tu...haiwezi sababisha wanafunzi kugoma...is admin issue which can be easily rectified!
 
Unajua ratiba ya Mitihani kwa ufahamu wangu huwa inapangwa na utawala wa chuo kwa kushirikiana na Serikali ya wanafunzi. Ndio maana huwa kunakuwa na 'draft' ya kwanza ya ratiba, kisha cmarekedbisho yanapita kupata final draft. Sasa kama inatokea hivi sidhani kama kuna sababu ya msingi ya kugoma katika hili, ila nadhani kuna sababu nyengine vkubwa zaidi ya mitihani!
 
Suala la ratiba ya mitihani ni la utawala wa Chuo, FFU wamefuata nini hapo

Wakuu wanahisi hao jamaa kuna wanachogomea zaidi ya mitihani! Labda walikuwa na agenda ya wenzao waliotangulia, sasa mkuu wa kaya na wasaidizi wake wameshatoa tamko! kwa hiyo wanapogoma, wakuu wanajua uzi ule ule,wanataka kutumia nguvu kama kawaida yao!
 
Katika ratiba ya sasa, hii mitihani imekuwa squeezed ndani ya working hours, i.e ratiba ya hairuhusu mitihani kufanyika jioni na week-end kama ilivyokuwa hapo nyuma. Kuna taarifa kwamba walimu wao wanainfluence mgomo ili ratiba itawanywe hadi masaa ya nje ya kazi (jioni) na week-end ili invigilators (ambao ni walimu) waweze kujipatia vihela vya overtime !!! Kwa hiyo you can see how hela zinavyotafutwa hadi hatua ya kuviolate ufanyikaji wa mitihani !! Na wanafunzi nao wamekubali kwani kwa upande wao watajiandaa na mitihani michache per day, ingawa ni weak reason!
 
sasa watu wanagomea ratiba the ffu wanaletwa?
What crap is these my God?
 
I suspect there is more to it than a mere exam. timetablle. Hawa jamaa si juzi tu walimkwida Gray Mgonja pale hazina wakilalamika kupunjwa fdedha zao; inawezekana hilo ndilo chimbuko la mgomo wao kama kweli wamegoma.
 
kwa kugoma kufanya hizo test, wanfunzi wamefunga milango ya madarasa yote kwa kugandisha milango na super glue. hii ni kuzuia wote wasiingie madarasani. sasa hii ndio nini jameni!!!

macinkus
 
Ninavyofahamu mimi ni kuwa kazi ya FFU ni kutuliza fujo.Uwepo wao ni mahali penye fujo.Kazi ya polisi wa kawaida ni kulinda usalama wa raia na mali zao.Case ya IFM haikuhitaji FFU kukaa pale.Haku uvunjifu wa amani hata kidogo.Kiutaratibu ni polisi wanatakiwa kulinda mali za chuo na usalama wa watu wote.Kupeleka FFU pale ni sawa na ku-provoke wanachuo kuanzisha vurugu.

Naamini huu ni utaratibu wa kisiasa na siyo wa kiusalama.

Nafikiri kama wazee wa kazi wamepelekwa pale kwa lengo la kulinda amani hakuna tatizo, Ila tatizo litakuwa pale watakapo anza kuwapiga virungu hao vijana au vijana watakapoanza kuharibu mali ya chuo. Ila kama ni mgomo wa kimya kimya hakuna sababu ya kuwaogopa Hao wazee wa kazi.
 
kwa kugoma kufanya hizo test, wanfunzi wamefunga milango ya madarasa yote kwa kugandisha milango na super glue. hii ni kuzuia wote wasiingie madarasani. sasa hii ndio nini jameni!!!

macinkus

Hii ni uhuni na uharibifu wa mali, kwa nini watumie superglue ku-seal milango?, nafikiri hapo sasa ndipo wanapo-waprovoke FFU. Hawa ni watu wachache ambao hawaja jiandaa vema kwa mitihani, ila walitakiwa kutumia hoja ili kuwashawishi wenzao na si kuwazuia kuingia madarasani. Mwisho wa siku watajikuta wanatajwa na wao pekee kuwa kafara. Hapa ilitakiwa "solidarity forever"
 
Sasa hii imezidi mi nilidhani wanagomea final exam ,kumbe test ama kweli ndivyo tulivyo
 
Back
Top Bottom