Idadi ya wizara na mawaziri iwe kwenye katiba mpy

Mandown

JF-Expert Member
Apr 8, 2012
1,665
503
... hivi jamani waziri asiye na wizara maalumu anabanwa vipi na bunge! atakuwa akisimamia maswala gani,. mie hichi cheo naona ni cha kifisadi tu!
 
WAZIRI BILA WIZARA NI JANGA LA KITAIFA.

Waziri bila Wizara ni Janga la Kitaifa na kwa mwendo huu tunaumizwa na serikali ya CCM..

Ikumbukwe Waziri asiyekuwa na Wizara ni Wizi mkubwa kwa kuwa:-
1. Atakuwa na ofisi ilipiwayo ilhali haina kazi
2. Atakuwa na wafanyakazi wa ofisi wasiokuwa na kazi; hawa wote watakuwa kama wafanyakazi hewa isipokuwa mfanya usafi ofisini.
3. Waziri bila wizara ni kama Waziri hewa ilhali analipwa mshahara
4. Waziri huyu atakuwa na gari aina ya V8 ambayo ina Piston 8; inatumia mafuta kiasi cha kama pikipiki 8 zikiwa zinatembea.
5. Atakuwa na mlinzi 'Body guard' anayelipwa na serikali ilhali amlindaye hana kazi.
6. Atakuwa na dereva amwendeshaye Waziri asiyekuwa na kazi.
7. Waziri huyu asiyekuwa na kazi ataenda ziara nyingi zisizo za mathumuni kwa Taifa.

Kwa haya na MAPUNJO mengine mengi ni lazima tujiandae kama vijana katika Kundi liitwa BIDII YETU ITAINGIZA CHADEMA MADARAKANI ili ifikapo mwaka 2015; tuondoe huu mchezo wa CCM ambao lengo lao ni kumnyonya mvuja jasho.
Pamoja tunaweza.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom