Idadi ya Mbumbumbu yazidi kuongezeka elimu ya watu wazima

Manyanza

JF-Expert Member
Nov 4, 2010
9,410
14,156
Idadi ya watu wazima wasio jua kusoma na kuandika hapa nchini. inaongezeka kwa wastani wa asilimia mbili kila mwaka, hali inayoiweka Tanzania katika wakati mgumu wa kutimiza malengo ya mkataba wa Elimu Kwa Wote (EFA).
Mkataba huo unataka idadi ya watu wa kundi hilo ipungue hadi kufikia asilimia 50 ifikapo mwaka 2015.
hayo yalisemwa jana na katibu mkuu wa wizara ya Elimu na Mafunzo ya ufundi Profesa Hamisi Dihenga katika hotuba yake ya uzinduzi wa stashahada ya elimu ya watu wazima, itakayokuwa ikitolewa kwa njia ya masafa.
hata hivyo hotuba ya katibu mkuu hiyoo ilisomwa na Mkurugenzi wa elimu ya watu wazima katika wizara ya elimu na mafunzo ya ufundi, Salum Mnjagila.
Profesa Dihenga, alisema kuanzishwa kwa stashada hiyo kutatoa fursa kwa watu wazima hasa walisoma kusoma.
Mkurugenzi wa taasisi ya Elimu ya watu wazima, lamberpha Mahai, alisema lengo la mpango huo ni kuwa na watu wenye elimu ya kutosha ambao watasaidia kutoa mafunzo kwa watu wazima wasiojua kusoma na kuandika.

Haya Challenge nyingine kwa JK, maana enzi za Mkapa watu wazima walihamasika sana kujiendeleza.
 
hali hiyo siyo tu kwa watu wazima! bali ni kwa wote hali ni hiyo si uliona mwenyewe wadogozetu wa kidato cha nne si ni ushahidi tosha kuwa mambumbumbu hata waliohudhuria kidato cha nne nao wameongezeka! kwa kujikumbusha hali ilikuwa hivi

MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2010
DARAJA
WANAFUNZI
%
I
5,363
1.51%
II
9,942
2.81%
III
25,083
7.08%
IV
136,633
38.59%
0
177,021
50.00%
354,042
100.00%
Jumla ya waliofaulu (Daraja la I mpaka III)
11.41%
Jumla ya wenye Daraja la IV na wasio na Daraja: Yaani "ZERO"
88.59%
(source is Wanazuoni forum)



hapa yatupasa kumuomba mungu ili atupe faraja na kutupa amani kwa kuwa tunachangia ujenzi wa sekondari ili tuharibu future za wadogozetu na watoto wetu!.
 
MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2010
DARAJA
WANAFUNZI
%
I
5,363
1.51%
II
9,942
2.81%
III
25,083
7.08%
IV
136,633
38.59%
0
177,021
50.00%
354,042
100.00%
Jumla ya waliofaulu (Daraja la I mpaka III)
11.41%
Jumla ya wenye Daraja la IV na wasio na Daraja: Yaani "ZERO"
88.59%
(source is Wanazuoni forum)
 
Back
Top Bottom