MAMMAMIA
JF-Expert Member
- Feb 26, 2008
- 3,811
- 1,603
Sumatra ilisema abiria walikuwa 288 (watu wazima 288+31+9 watoto na mabaharia)
Ikulu Zanzibar ilitaja abiria 290 (sijui wawili walitoka wapi)
Leo Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa DSM imebandika majina ya watu 340 (ziada ya watu 50, 52)
Nani anasema ukweli?
Haya ndio yale yale yaliyotokea mwaka jana katika ajali ya Spice Islanders - Idadi kamili haikupatikana hadi leo.
Makosa yale yale yamekuwa yakijirejea siku hadi siku. Hivi viongozi wetu wana akili za mende kuwa wanasahau kila baada ya sekunde moja?
Nimesoma kwenye gazeti moja Waziri wa Mawasiliano na Uchukuzi anajitetea kuwa "Asilaumiwe mtu kwa kazi ya Mungu".
Kwa nini basi wanajazana mawizarani, wasimwache Mungu aongoze nchi? Abiria wametoa ushahidi kuwa tangu meli ilipozama hadi kufika chombo cha kwanza kuwaokoa yalipita masaa mawili kwa mahali pa masafa ya kutumia dakika 25.
Mungu hauwi, yeye hupokea tu roho zaviumbe wake waliodhulumiwa maisha yao.
Ikulu Zanzibar ilitaja abiria 290 (sijui wawili walitoka wapi)
Leo Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa DSM imebandika majina ya watu 340 (ziada ya watu 50, 52)
Nani anasema ukweli?
Haya ndio yale yale yaliyotokea mwaka jana katika ajali ya Spice Islanders - Idadi kamili haikupatikana hadi leo.
Makosa yale yale yamekuwa yakijirejea siku hadi siku. Hivi viongozi wetu wana akili za mende kuwa wanasahau kila baada ya sekunde moja?
Nimesoma kwenye gazeti moja Waziri wa Mawasiliano na Uchukuzi anajitetea kuwa "Asilaumiwe mtu kwa kazi ya Mungu".
Kwa nini basi wanajazana mawizarani, wasimwache Mungu aongoze nchi? Abiria wametoa ushahidi kuwa tangu meli ilipozama hadi kufika chombo cha kwanza kuwaokoa yalipita masaa mawili kwa mahali pa masafa ya kutumia dakika 25.
Mungu hauwi, yeye hupokea tu roho zaviumbe wake waliodhulumiwa maisha yao.