Lazaro, unasahau kitu kimoja, hii sii kesi ya madai au ya jinai (not a civil or criminal case) ni kesi ya Kikatiba. Tukirudi hata kwenye kesi ya madai, mahakama inaposema fulani amlipe x kwa kumchafulia jina, yule x halazimiki kuanza kulipa mara moja kama anampango wa kukata rufaa na polisi hawawezi kwenda kukamata mali yake kutekeleza hiyo hukumu. Lakini katika muda uliopo mawakili wake n.k watatoa notice kwa mahakama kuwa wana nia ya kukata rufaa na hivyo hiyo hukumu isitekelezwe pending the appeal process.
hii sii kesi ya madai au ya jinai (not a civil or criminal case) ni kesi ya Kikatiba.
Mwkjj, Hapo juu nakataa. Hii ni kesi ya MADAI, amabyo mlalamikaji (Mtikila) anadai katiba imekosewa/haiko fair na Mahakama baada ya kusikiliza MADAI yake, ikapendekeza/ikaamuru kifungu hicho cha katiba kifutwe/kibadilishwe. Serikani ikakata rufaa kukataa maamuzi ya Mahakama, kesi ipo pending for appeal.
Thanks that we now speak the same language. "Tukirudi hata kwenye kesi ya madai, mahakama inaposema fulani amlipe x kwa kumchafulia jina, yule x halazimiki kuanza kulipa mara moja kama anampango wa kukata rufaa na polisi hawawezi kwenda kukamata mali yake kutekeleza hiyo hukumu". Na ndiyo kitu imetokea kwenye kesi ya Mtikila ambayo ni Madai, Mahakama ikatoa maamuzi na Serikali ikakata rufaa, muda wa rufaa haujaisha, thats why maamuzi ya Judge ya kufuta kile kifungu cha katiba hajajatekelezwa. Mtikila hajashinda hii kesi bado, wait for the appel.
Turudi kwenye kesi ya Kikatiba. Ikitokea kesi ambayo hukumu yake inasema "hukumu ya kifo ni kinyume na Katiba kwa sababu inapingana na kipengele kinachosema Kila mtu ana haki ya kulindwa maisha yake n.k" halafu kesho yake kuna hukumu ya mtu kunyongwa je mtu yule anyongwe wakati mahakama inasema sheria inayohalalisha hukumu ya kifo ni kinyume cha Katiba? Tukiangalia ibara ya 30:5 jibu ni ndiyo, kwa sababu ingawa mahakama imesema sheria hiyo ni kinyume na Katiba, sheria hiyo bado ina nguvu na inapaswa kufuatwa.
'Kila mtu ana haki ya kulindwa maisha yake n.k" lets put this way, Kila mtu ana haki ya KUISHI. Thats means, we dont expect somebody with or without intention to kill another person. But if it happen, what do you think the law should do to them? Say sorry and allow them to live wait for the next person to kill another , and another, and another na wasihukumiwe kunyongwa kwamba sheria itakiukwa? what about them killing wengine? hao walio wauwa hawakuwa na haki ya kuishi ama maisha yao kulindwa?
Mtu yule atanyongwa kwa sababu atakuwa amefall kwenye kesi zenye hukumu hiyo 'kunyongwa', For sure, endapo katiba itasema kama ulivyoweka hapo juu, hiyo hiyo katiba haiwezi sema kesi so and so watu wahukumiwe kunyongwa.
Tatizo lake ni kuwa hukumu ya Kikatiba haina ulazima wa injunction ya kuizuia serikali nk kutii amri ya mahakama (hata kama ni mahakama ya chini) pending appeal. Kwenye kesi ya kifo, je tukiamua kumuua huyu mtu baada ya hukumu kutolewa na kabla ya rufaa kumalizwa, itakapokuja mwishoni (kwenye mahakama ya rufaa) ikakubaliana na mahakama ya chini kuwa kweli sheria ile ni kinyume na Katiba.. tutawezaje kuhalalisha kitendo hicho cha sisi kama jamii kumuua mtu wakati tumeambiwa na mahakama kuwa ni kinyume na Katiba tangu kabla hatujamuua?
Mkjj, Mahakama husika ikitoa hukumu ya mtu kunyongwa, then defence wakakata rufaa, YULE MTU HAWEZI KUNYONGWA HATA SIKU MOJA KABLA RUFAA KUMALIZIKA (kama imeshatokea naomba mfano). Ila, yule mtu ataendelea kukaa JELA na hukumu yake itasomeka Rufani-kunyongwa. Defence wakishinda kesi, then ataachiwa ama kufungwa kutokana na maamuzi ya majudge kusikiliza facts za kesi, ushahidi na uzito wa kesi yenyewe, akishindwa appeal, Appeal court watakubaliana na Maamuzi ya Hakimu aliyotoa hukumu ya kunyongwa. Ni baada ya appeal.
Thanks,
Lizy