Ibara ya 15:1 na 2

Mkuu Lunyungu,

Na wewe usijiangushe bure kujifanya hujui maana sahihi ya hicho kipengere.

Mambo kama haya ndio yanatisha Watanzania wengine. Ukiwa na watu kama akina mwanakijiji serikalini, wanaweza kuwa wabaya (last time you said Hatari!) kuliko akina Rweyemamu.

Take your shots all you want.. my argument still stand.

Na unaweza kujaribu tafsiri za kichina, kijerumani, kizaramo na kindegereko ili kuondoa ukweli ambao uko wazi katika lugha ya Kiswahili. Jukumu la "kwanza" la mwanaCCM ni kwa CCM, unaweza kujaribu kuchambua unavyoweza lakini kwa mwana CCM hili halina mjadala.

Kunapotokea mgongano kati ya maslahi ya CCM na ya Taifa mwana CCM achague lipi anapoangalia Katiba yake..? Kwangu hakuna utata lakini kwa mwana CCM kijijini?

Juzi, mtu mmoja alivamiwa na kuwashika wabaya wake na aliwapeleka wapi Polisi? hapana kwa "mwenyekiti wa CCM".
 
Hongereni kwa ku-spin mambo!!! Hivi kujiunga CCM si hiari!!! Kama hukubaliani, si unakuwa nje kama mimi, sasa kuna haja gani ya Ku-spin.

Kila siku zinavyoenda hizi spinning strategy zinaendelea kuweka wazi kwamba kumbe CCM wako fiti zaidi.

Sasa ma-think tank wa Upinzani badala ya kuja na mambo yao... kueneza siasa zao wanapata shida na wanaCCM ambao wanabadilisha katiba yao kwa vikao... wanatoa matamko kwa vikao...

Kasheshe,

Yaani wewe unataka kusema kuwa kuuza migodi ya madini kwa bei ya karanga na spin? Unataka kusema kuwa wizi wa BoT ni spin? Kweli unaona kuwa mikataba kama Richmonduli ni spin?

CCM inajimaliza yenyewe na wala sio spinning! kama yote haya wewe huyaoni na bado unasema kuwa ccm wako fit zaidi, basi nina kila sababu ya kusema kuwa neno fit unalotumia hapa lina maana nyingine... oopppss hii nayo inaweza kuwa spin!

Huwezi kuamini vile mimi huwa nasubiria hapa kwa hamu kuona ccm wakifanya mambo mazuri ili wasifiwe. Nilianza kufanya hivyo in advance kabla ya kikao cha juzi lakini nini nilichopata in return?

CCM ibadilike, kama Bush amebadili sera zake hapa US pamoja na kiburi chake itakuwaje ccm wasibadilike?
 
CCM ibadilike, kama Bush amebadili sera zake hapa US pamoja na kiburi chake itakuwaje ccm wasibadilike?

Dear.. wanachotakiwa kuanza kubadilika ni kukipangua hicho kifungu chao cha 15 na kuweka wazi kuwa Jukumu la mwana CCM kwanza ni kwa nchi yake na maslahi ya Taifa lake.. wakiendelea kuwa na mawazo kuwa jukumu lao ni kulinda na kuendeleza CCM hawaendi kokote na hasa inapotokea kuwa watu wanakubaliana na mawazo hayo.
 
Mwanakijiji,

Lets not quibble over semantics, I will rather put effort and energy on other useful discussions than this. Its a wastage of time.

Mwanakijiji, hili nimekuachia endelea!
 
Q.M
hahaaha ndugu yangu naona umespin kinyumenyume..

a. Tunaishi katika nchi inaitwa Tanzania, na nchi hii ndio lengo, nia, kusudio, la shughuli zote za Mtanzania (no pun intended). Hivyo, maslahi ya chama, taasisi n.k ni katika kuhakikisha ustawi wa nchi hii iitwayo Tanzania na ustawi wa watu wake.

b. Hivyo basi, Polisi anapokula kiapo hali kiapo cha kulinda Jeshi la Polisi ili ailinde Tanzania, au Askari wa JWTZ hali kiapo cha kulinda mipaka ya JWTZ ili aweze kuilinda mipaka ya Tanzania. Polisi na Jeshi siyo lengo la Tanzania.

c. Chama cha siasa ni chombo cha kutekeleza makusudio ya kuitumikia Tanzania na kuistawisha. Unapokigeuza chama kuwa ndiyo lengo na hatima ya shughuli za wanachama unakuwa umepindua wazo zima la "nitaitumikia nchi yangu saa yoyote,siku yoyote, na mahali popote nitakapoamriwa".

d. Jaribu tena kusikiliza maelezo ya Msekwa akizungumza kwenye NEC utaona kuwa maazimio yote yamezunguka CCM na si Tanzania;

e. Kosa kubwa ambalo naamini lipo ni mawazo kuwa CCM na Tanzania ni synonymous, kuwa Ukiitumikia Tanzania unatumikia CCM na ukitumikia Tanzania unatumikia CCM. Mfano; waliochangia CCM mara wamechangia amani Tanzania, aliposhinda Richard kwenye BB, imeshinda Tanzania na CCM.

Hivyo utaona basi, tatizo siyo kuwepo kwa kipengele hicho kwani ni haki ya CCM kuwa nacho, tatizo ni kusema kuwa huo ndio "wajibu wa kwanza" wa mwanaCCM. Je ina maana gani?

Well, inawezekana natumia jicho la kengeza kusoma, lakini bado ninaamini kuwa hicho kipenele kiko sawa. CCM ni organization. Na kama organization zingine zote, ina "Mission Statement" ambayo memba wake wanapaswa kuitekeleza kwanza. Ni hiyo "Mission Statement" ya CCM ndiyo inatengeneza dira na mwelekeo wa kuliongoza taifa la Tz.

Kwa mujibu wa hicho kipengele, mwanaCCM asiyetimiza wajibu wa CCM kwanza, hafai kuwa mwanaCCM, hence hawezi kulitumikia taifa la Tanzania. Ni ulimwengu wa CCM....that's all.

Nje ya hapo, inawezekana kwa mtanzania mwingine yeyote kuweza kuitumikia Tz...just hatakuwa mwanaCCM.


Endapo chama cha mapinduzi kinajiandaa na uchaguzi na kinaweza kushinda na mwana CCM yuko kwenye nafasi serikali ambayo inaweza ikasaidia kupata fedha za "ziada" na anajua jinsi ya kufanya hivyo, je akisaidie chama chake na kudhuru serikali - Jibu ni ndiyo!

Je, mwana CCM anapoona kuwa tume ya uchaguzi inaboronga na inatishia chama chake kupoteza viti au hata ushindi na yeye ana nafasi ya kufanya mazingaombwe je akisaidie chama chake? - Jibu ni ndiyo!

Yes, atakuwa ametimiza kipengele cha wajibu wa CCM kwanza. Na hapo ndipo CCM inapokuwa challenged na utumishi wa CCM kwa taifa la Tz. Lakini kipengele chake kiko sahihi. Tatizo liko kwenye uadilifu wa CCM kama chama kwa taifa la Tz. Na hapa ndipo kwenye matatizo makubwa.

Je, MwanaCCM anaposikia kuwa kuna watu wamekwama Mererani na yeye ana kikao muhimu Butiama ambacho kinaendelea, je wakatishe na kutoa pole kwa wahanga na kuagiza mara moja waendelee hata kuchelewesha kikao kumalizika je afanye hivyo? Jibu ni hapana, lazima aendelee na kikao na kwenda Mererani Jumatatu jioni baada ya kikao cha NEC..

Je, mwana CCM anapoona kuwa chama cha CUF kinaweza kuingizwa madarakani na hivyo kushirikiana katika kutawala visiwa vya Zanzibar na hivyo kuondoa ujiko wa chama kimoja je akubali kuungana na CUF? Je atumie mbinu za kuchelewesha maamuzi hayo ili asiondolee CCM ukiritimba wake wa kisiasa visiwani hata kama suala hilo linaweza kuzua mgogoro usio wa lazima? jibu ni ndiyo!

kwanini basi mwana CCM aitetee CCM bila kujali matokeo ya utetezi huo kwa Taifa? Jibu ni soma Ibara ya 15.

Same thing....tatizo ni uadilifu wa CCM kwa taifa la Tz.

Kama CCM ingekuwa inafanya vizuri, basi hiki kipengele kisingekuwa kinaonekana kama tatizo. Tatizo linakuja kwa sababu, wanachama wake wanatimiza wajibu wa CCM, na CCM imeoza.
 
Well, inawezekana natumia jicho la kengeza kusoma, lakini bado ninaamini kuwa hicho kipenele kiko sawa. CCM ni organization. Na kama organization zingine zote, ina "Mission Statement" ambayo memba wake wanapaswa kuitekeleza kwanza. Ni hiyo "Mission Statement" ya CCM ndiyo inatengeneza dira na mwelekeo wa kuliongoza taifa la Tz.

wrong analogy. Mission ya CCM iko kwenye "madhumubi, nia, na malengo ya Chama" na pia kwenye "Imani ya chama". Ibara hiyo inahusu "Majukumu ya MwanaCCM". Na jukumu lake la kwanza ni kwa CCM. Sijui kwanini hili ni gumu kuonekana?


Kwa mujibu wa hicho kipengele, mwanaCCM asiyetimiza wajibu wa CCM kwanza, hafai kuwa mwanaCCM, hence hawezi kulitumikia taifa la Tanzania. Ni ulimwengu wa CCM....that's all.

That is exactly my point! Kwamba mwana CCM ambaye anaweza kusimamia maslahi ya Taifa ambayo yanagongana na ya CCM basi hawezi kulitumikia taifa. Mfano, CCM iliamua kufuta haki ya mtu kugombea bila kulazimika kuwa na chama, ilikuwa ni kwa maslahi ya CCM. Hakuna mwana CCM ambaye amepinga uamuzi huo licha ya kuitwa ni wa "kipumbavu".

Sababu ni kuwa CCM iko sawa na mwanaCCM anawajibu kwa CCM (kwa kufuata ibara ya 15) hivyo hawezi kupingana na uamuzi wa CCM.


Nje ya hapo, inawezekana kwa mtanzania mwingine yeyote kuweza kuitumikia Tz...just hatakuwa mwanaCCM.

Inaonesha pia tatizo hilo hilo kuwa Mtanzania ambaye anaweza kuona maslahi ya Taifa ambayo yanatishia ya CCM hawezi kujiunga na CCM. Nimetumia mfano ya Tume ya Uchaguzi. Tume ya uchaguzi ambayo ni huru kabisa haiwezekani nchini kwa sababu inatishia maslahi ya CCM. Sasa kama kuna mwanaCCM anaona haja ya kuwa na tume huru na anapenda mambo mengine ya CCM afanye nini?


Yes, atakuwa ametimiza kipengele cha wajibu wa CCM kwanza. Na hapo ndipo CCM inapokuwa challenged na utumishi wa CCM kwa taifa la Tz. Lakini kipengele chake kiko sahihi. Tatizo liko kwenye uadilifu wa CCM kama chama kwa taifa la Tz. Na hapa ndipo kwenye matatizo makubwa.

Nadhani unamiss kitu bado, sijasema kipengele hakiko sahihi nimesema kimeweka CCM juu ya wajibu wa mwanaCCM kwa nchi.



Same thing....tatizo ni uadilifu wa CCM kwa taifa la Tz.

Kama CCM ingekuwa inafanya vizuri, basi hiki kipengele kisingekuwa kinaonekana kama tatizo. Tatizo linakuja kwa sababu, wanachama wake wanatimiza wajibu wa CCM, na CCM imeoza.

Wanatimiza wajibu wao kwa sababu CCM imeoza au CCM imeoza kwa sababu wanatimiza wajibu wao? Kama CCM wangekuwa wanafanya mambo kwa maslahi ya Taifa basi ni wazi usingetokea mgongano lakini mgongano upo kwa sababu wanatimiza wajibu wao wa kwanza zaidi kuliko kitu kingine.
 
Katiba ya CCM ina matatizo. Bado nadhani ni ile ile ya wakati wa chama kimoja (chama dola).

Ukitaka kujua katiba yao ni bomu, jaribu kufikiria scenario where they will no longer be the rulling party (yaani wao ndiyo wawe opposition). Hiyo katiba (na hususan hicho kipengele) itakuwa very redundant!
 
Hivi kwa nini wanadhani 'fikra' zao ziko 'sahihi'? Hivi hapa duniani kuna fikra zilizo 'sahihi' kweli?

Hiyo lugha ya 'sahihi' mimi sijaipenda kabisa!!!
 
Katiba ya CCM ina matatizo. Bado nadhani ni ile ile ya wakati wa chama kimoja (chama dola).

Ukitaka kujua katiba yao ni bomu, jaribu kufikiria scenario where they will no longer be the rulling party (yaani wao ndiyo wawe opposition). Hiyo katiba (na hususan hicho kipengele) itakuwa very redundant!

nurujamii, unafikiri kuna wakato wowote wamewahi kufikiria wao kama opposition? sidhani..
 
wrong analogy. Mission ya CCM iko kwenye "madhumubi, nia, na malengo ya Chama" na pia kwenye "Imani ya chama". Ibara hiyo inahusu "Majukumu ya MwanaCCM". Na jukumu lake la kwanza ni kwa CCM. Sijui kwanini hili ni gumu kuonekana?

That is exactly my point! Kwamba mwana CCM ambaye anaweza kusimamia maslahi ya Taifa ambayo yanagongana na ya CCM basi hawezi kulitumikia taifa. Mfano, CCM iliamua kufuta haki ya mtu kugombea bila kulazimika kuwa na chama, ilikuwa ni kwa maslahi ya CCM. Hakuna mwana CCM ambaye amepinga uamuzi huo licha ya kuitwa ni wa "kipumbavu".

Sababu ni kuwa CCM iko sawa na mwanaCCM anawajibu kwa CCM (kwa kufuata ibara ya 15) hivyo hawezi kupingana na uamuzi wa CCM.

Inaonesha pia tatizo hilo hilo kuwa Mtanzania ambaye anaweza kuona maslahi ya Taifa ambayo yanatishia ya CCM hawezi kujiunga na CCM. Nimetumia mfano ya Tume ya Uchaguzi. Tume ya uchaguzi ambayo ni huru kabisa haiwezekani nchini kwa sababu inatishia maslahi ya CCM. Sasa kama kuna mwanaCCM anaona haja ya kuwa na tume huru na anapenda mambo mengine ya CCM afanye nini?

Nadhani unamiss kitu bado, sijasema kipengele hakiko sahihi nimesema kimeweka CCM juu ya wajibu wa mwanaCCM kwa nchi.

Wanatimiza wajibu wao kwa sababu CCM imeoza au CCM imeoza kwa sababu wanatimiza wajibu wao? Kama CCM wangekuwa wanafanya mambo kwa maslahi ya Taifa basi ni wazi usingetokea mgongano lakini mgongano upo kwa sababu wanatimiza wajibu wao wa kwanza zaidi kuliko kitu kingine.

Mkjj
Duh...kweli nimeingia kwenye 18 zako.

Haya kaka, this one is yours.
 
Mwanakijiji,

Lets not quibble over semantics, I will rather put effort and energy on other useful discussions than this. Its a wastage of time.

Mwanakijiji, hili nimekuachia endelea!


Mtanzania, hoja hazilazimishwi na nguvu ya hoja haitokani na majina unayoweza kumuita mtu au sifa unazoweza kumpamba nazo. Kama hoja yangu kuhusu Ibara 15 ni mbovu na haina msingi tumia mantiki na mifano au uwezo wako kunishawishi, lakini kuamua kuniita "nitakuwa mbaya" mara "hatari zaidi" siyo tu kulazimisha hoja bali ni a mediocre attempt of character assassination..

Nimezoea watu kunishambulia kama hawakubaliani na mimi, lakini inapotokea watu ambao I hold dear to use those cheap shots its not only disheartening but also puzzling.

Tunaweza kutofautiana katika mambo mbalimbali lakini haya kuanza kuitana hatari mbaya kuliko sidhani kama yanasaidia kufanya hoja iwe na nguvu. Unaweza kuona hoja yangu kuwa ni radical au ufafanuzi wangu umekosewa na ukijitahidi unaweza kunishawishi.

Lakini kama na wewe umeamua kujiunga katika msululu wa waitao majina. well, whatever pleases you. I have learned to live with that reality.
 
Mmhhhh...na wewe naona sasa umeshalewa na sifa ya kujiona una hoja bora kuliko wenzako....

Sikuiti jina...bali na observe tu. Nisamehe kama observation yangu si 'sahihi'...
 
Mmhhhh...na wewe naona sasa umeshalewa na sifa ya kujiona una hoja bora kuliko wenzako....

Sikuiti jina...bali na observe tu. Nisamehe kama observation yangu si 'sahihi'...

Nyani, ni kusaliti dhamira ya mtu kukaa kimya kama unajua uko sawa na hivyo kuacha uongo uenee kwa hofu ya kuonekana bora au kuhofiwa kuwa unajiona bora. Kama watu watakuwa wanakaa kimya ili wasionekane "bora" au "wanajua" sana basi ndio utakuwa mwisho wa mawazo huru katika ulimwengu wa fikra maana mawazo yatakayotolewa ni yale ya kumfanya mtu aonekana "wa kawaida" na asiwe "outstanding".

Lakini kama hiyo ndiyo impression uliyonayo juu yangu, niwie radhi for I can't help it. Siwezi kukaa kimya nikiamini kuwa mawazo fulani siyo sahihi na siogopi kuoneshwa mawazo yangu kuwa hayako sahihi. Hili nalifanya siyo kwa ajili ya kushinda hoja au mjadala bali kwa ajili ya kuhakikisha hoja zinazoshinda out there zimepitia kwenye tanuru la moto.

Je, ulitaka niseme hewala kuwa nimekosea tafsiri yangu ya Ibara ya 15 ili nisionekane najiona bora? Nikae kimya na nisitoe mawazo kwa sababu nitaonekana najifanya kujua sana? Well, I wish I could, but I can't. Don't ask me why.

Ila inanikumbusha wachezai LeBron na Kobe, kuna wakati wanakuwa katika zone ya kucheza hadi hata wachezaji wenzao wanawashangaa kwa sababu wanaonesha so much talend hadi unaweza kujisikia wako "unstoppable". Sasa kwa mwelekeo wako basi hawa jamaa wasicheze vizuri zaidi au kuonesha uhodari wao kwa sababu watakuwa wanaonesha vipaji vyao kuliko watu wengine na kwa kufanya hivyo wanaonekana wanajiona bora. Hivyo wapunguze makali kidogo na wacheze kikawaida tu ili wasiwakwaze watu wengine.

Wakifanya hivyo, maadui zao watawashindwa na watu watauliza timu yenu si ina kina Kobe au LeBron?
 
katiba.JPG

Mimi nadhani hii katiba hata JK hajawahi kuisoma hata siku moja,au kuna katiba nyingine jamani,mbona hii ibara peke yake kama ccm wangeielewa vizuri basi nadhani huko Butiama kimsingi kwa watu ambao wako serious na nchi yao MOTO UNGEWAKA.Nasema hivyo kwa sababu ndani ya ccm kunaubinafsi mwingi sana na usultani unaweza kurudi tena tusipoangalia.Labda niseme TOTALY CCM YOU ARE AGAINST THIS ARTICLE which is very impotant.

CCm huko butiama mlikwenda kutalii,kula posho,kuchangisha pesa za ccm,ulikua ni unafiki,mbona hamueleweki mlichokwenda kufanya wajameni?
 
Chief wa kijijini,

Nashukuru kwa kutuletea hii nakala...imefungua macho ya wengi kwani pengine huu ufisadi, ubabe na uonevu mwingine tulidhani ni wa kina EL, BWM na wengineo kumbe kuna maelekezo! Nashukuru wakuu wengine waliojumuika nawe katika kukokotoa kipengele namba moja.

Mimi nimevutiwa na vipengele 2,3 na 4...viongozi wengi wa CCM (sio wote) hususan wenye influence, wamekuwa wakifanya every thing but vipengele 2,3 na 4. Wana ubinafsi, sio wazalendo, hawalipi taifa kipaumbele bali maslahi binafsi. Hivi kwanini wenye uchungu na chama chao mpaka wakakutana Butiama, wanaachia watu kama RA, EL, hata JK mwenyewe (IMMA connection) wakinajisi chama?
 
Nyani, ni kusaliti dhamira ya mtu kukaa kimya kama unajua uko sawa na hivyo kuacha uongo uenee kwa hofu ya kuonekana bora au kuhofiwa kuwa unajiona bora. Kama watu watakuwa wanakaa kimya ili wasionekane "bora" au "wanajua" sana basi ndio utakuwa mwisho wa mawazo huru katika ulimwengu wa fikra maana mawazo yatakayotolewa ni yale ya kumfanya mtu aonekana "wa kawaida" na asiwe "outstanding".

Lakini kama hiyo ndiyo impression uliyonayo juu yangu, niwie radhi for I can't help it. Siwezi kukaa kimya nikiamini kuwa mawazo fulani siyo sahihi na siogopi kuoneshwa mawazo yangu kuwa hayako sahihi. Hili nalifanya siyo kwa ajili ya kushinda hoja au mjadala bali kwa ajili ya kuhakikisha hoja zinazoshinda out there zimepitia kwenye tanuru la moto.

Je, ulitaka niseme hewala kuwa nimekosea tafsiri yangu ya Ibara ya 15 ili nisionekane najiona bora? Nikae kimya na nisitoe mawazo kwa sababu nitaonekana najifanya kujua sana? Well, I wish I could, but I can't. Don't ask me why.

Ila inanikumbusha wachezai LeBron na Kobe, kuna wakati wanakuwa katika zone ya kucheza hadi hata wachezaji wenzao wanawashangaa kwa sababu wanaonesha so much talend hadi unaweza kujisikia wako "unstoppable". Sasa kwa mwelekeo wako basi hawa jamaa wasicheze vizuri zaidi au kuonesha uhodari wao kwa sababu watakuwa wanaonesha vipaji vyao kuliko watu wengine na kwa kufanya hivyo wanaonekana wanajiona bora. Hivyo wapunguze makali kidogo na wacheze kikawaida tu ili wasiwakwaze watu wengine.

Wakifanya hivyo, maadui zao watawashindwa na watu watauliza timu yenu si ina kina Kobe au LeBron?

Kwa hiyo ujengaji wako wa hoja unaulinganisha na uhodari wa Kobe na LeBron kwenye korti ya mpira wa kikapu sio...?
Haya bana umeshinda...
 
Matatizo yetu wa-Tanzania, hayawezi kusingiziwa katiba za vyama, katiba ya CCM au ya Chadema, hazina uhusiano wowote na matatizo yetu kitaifa ya kutotii sheria, na uwezo mdogo wa viongozi wetu wa kufikiri, sasa si ndio haya maneno wamesema sasa watayaeneza zaidi kwani haya maneno ya hiyo katiba ya CCM ni ya nani?
 
Matatizo yetu wa-Tanzania, hayawezi kusingiziwa katiba za vyama, katiba ya CCM au ya Chadema, hazina uhusiano wowote na matatizo yetu kitaifa ya kutotii sheria, na uwezo mdogo wa viongozi wetu wa kufikiri, sasa si ndio haya maneno wamesema sasa watayaeneza zaidi kwani haya maneno ya hiyo katiba ya CCM ni ya nani?

Wasababishaji wa matatizo yetu ni sisi wenyewe...
 
Nionesheni nchi yenye Katiba mbaya na imeendelea na nitawaonesha nchi yenye katiba mbovu na haijaendelea. Huwezi kuwa na Katiba mbovu ukategemea maendeleo, lakini ukitengeneza Katiba nzuri unafungulia msingi wa maendeleo..
 
Back
Top Bottom