I hate you Jo burg, I hate O.R Tambo I. A

Feb 15, 2009
99
2
Fikilia waenda nchi au mji ambao wapewa tahadhariya usalama wako na mali zako ata kama ni kasimu ka promoshen kariakoo kila unapotaka kutoka nje upate japo upepo au kuona mandhari ya mji, nawe kwa kuofia usalama wako unatii na kwa hakika kila baada ya dinner rafiki yako ni TV ama kitanda,fikilia wakaa siku kadhaa kwa tahadhari kuu namna hiyo ata wahesabu siku za kurudi bongo tulikozoea shida za umeme na maji ata tumekuwa mapacha alafu yanakuja kukukuta pale ambapo wadhani uko salama.



Nimerejea na SAA lakini kwamaumivu makubwa sana, kwani nimeibiwa Laptop yangu,camera na lens kadhaa kwenye ndege ambapo niliakikishiwa na wausika pale O.R Tambo Internatrional Airport, Johannesburg kuwa kila kitu kitakuwa salama mradi nimefunga begi langu, kumbe ni njia tu ya kunilainisha wanichape.

Kwa hali kama hii kuchwapwa vitendeakazi vyangu je nitaipendaje nchi au mji huo? naanzia wapi hasa?

Na je hawa jamaa ndowanatarajia kupokea wageni wa dunia nzima mwezi wasita kwa ajili ya Kombe la Dunia 2010, kwa mtaji huu wengi watalizwa sana, kifupi S.A itarajie aibu katika hili isipochukua hatua sasa.


Joburg is this the way you prepare to receive the world for 2010 World Cup?
 
Mjomba sauz laptop zabebwa kwenye mabegi ya mgongoni kama waenda shule vile, halafu imekuaje ukaweka kwenye begi kubwa? Inatakiwa uwe nayo ila tu kwenye begi dogo la mgongoni na si vile vibegi spesho vya laptop maana watakujeruhi wachukue. Sauz hata mapolisi ni wezi, walishawahi kunisachi hapo Park-town(jburg city centre).
 
Kwani uligundua laptop yako na vitu vingine vimeibiwa wakati gani? Je, ulitoa taarifa kwa SAA kwamba umeibiwa laptop yako nk. Kama ulifanya hivyo wamechukua hatua gani? Je hiyo begi ulilofunga lilichanwa au kuharibiwa kwa namna yoyote? Kama hukutoa taarifa SAA umewaarifu Polisi na hatua gani inafanyika ili uunganishwe na mali zako?
 
We umekosea kweli!! Yaani laptop na camera lenses umeweka kwenye checked luggage!! Hivyo vitu ni vya carry on always and forever, anyway nadhani hauta rudia kosa.
 
We umekosea kweli!! Yaani laptop na camera lenses umeweka kwenye checked luggage!! Hivyo vitu ni vya carry on always and forever, anyway nadhani hauta rudia kosa.




I was forced by Check In staff at O.R Tambo to check my baggage even after telling her whats inside the bag and she assured me that so long as its locked hakuna tatizo, lakini kufika Dar ni balaa lock zote zimevunjiliwa mbali, na kibaya zaidi nimeenda SAA afisi wanasema vitu hivyo havimo katika mkataba wao wa fidia. This is very very sad, I mean those x-rays are there to let them see what you have na kisha waibe, hii inasikitisha sana wadau, nimeshatumia huduma za ndege nyingine kama KLM, Qatar, BA au zetu sijawai kutana na hili.
 
pole sana. inauma sana na kweli
june 2010 kutakuwa na "vilio" kwa sana
mitaa ya bondeni
 
Nakushauri uandike barua kwa mojawapo ya magazeti maarufu SAF uwasimulie yaliyokupata. Kwa sababu wamo katika maandalizi ya World Cup na hawataki kupata aibu labda watasukumwa kuchukua hatua kuhakikisha wizi huu hautokei tena. Pole sana hata hivyo.
 
I can understand how you are feeling and all I can say is, pole sana. It is a shame kwamba mambo haya yanatokea kila kona Afrika. Nenda msikitini Mwanza mara umeibiwa viatu, it is a shame...
 
Nakushauri uandike barua kwa mojawapo ya magazeti maarufu SAF uwasimulie yaliyokupata. Kwa sababu wamo katika maandalizi ya World Cup na hawataki kupata aibu labda watasukumwa kuchukua hatua kuhakikisha wizi huu hautokei tena. Pole sana hata hivyo.

Nashukuru kwa ushauri wenu wote naomba kama utakuwa na address yao nisadie ndugu yangu au yeyote alokuwa nayo kwani walivyochukuwa ni vitendea kazi vyangu na sasa sina budi kuanza alif kwa kidole.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom