I got to say it; watawala wana matatizo kichwani!?

macho nimefunguka Waberoya, naninaamini sakata la muro litaibua mengi mazuri aidha kisheria ama kijamii, maaana nimeanza kujua matumizi mwanana wa pingu katika mahaba, hii imenipa hamasa ya mimi kuitafuta ili nikidhi haja....
nataraji jambo moja rate ya wanunuaji wa bidhaa hiyo itaongezeka.

Mkuu hayo matumizi nami nimeyafurahia yanaweza yakawa solution kwa matatizo fulani fulani ya Ndoa.
Hili sakata la muro natamani niuushuhudie mwisho wake kwa kauli thabiti kutika kwa viongozi wetu....lakini nahofia mambo yatakuwa kama stori zingine za EPA,Meremeta n.k
 
Nilitegemea wangesema labda risiti sio halali wangeanzia hapo..
Walipoanzisha Duka lao walitegemea wateja wawe nani Polisi na Magereza pekee?
 
HIVI NI KIPI KIGUMU ENYI watawala WETU?! Kumuuzia raia bunduki na risasi za moto au kumuuzia pingu? Kama mmepitisha sheria inayokubali raia kununua bunduki na risasi kwenye duka la serikali inakuwaje jambo la kushangaza kununua pingu KWENYE duka hilo hilo?
?

MM,
umenichekesha sana Kaka,ila me kwa upande mwingine namuunga mkono huyo mjeda ingawa of cpurse point zako zina mashiko, ni vigumu kwa Raia kujilinda kwa kutumia pingu,haiwezekani kabisa wewe MM ,majambazi wamekuvamia afu ukawatisha na pingu..MM umenisoma!!!!
Ila bunduki,Raia wa kawaida anaweza akaitumia kujilinda nayo,au sio MM..
ila nijuavyo mimi,hakuna kifungu cha sheria kinachosema ni marufuku raia kumiliki pingu, hivyo si kosa kuwa nayo coz sheria iko silence on that..wanasheria watanisaidia katika hili..
Mwisho kabisa et nimesikia fununu kuwa MM Muungwana anataka ugombee ubunge mwaka huu,kakuahid Uminista....Natania MM
 
Taanzania Tanzaniaaa nilukupenda nchi yangu!!!
KUNA MWENZAKO alikosea,penye "Tanzania" akaweka jina la shemeji, na penye "nchi" akaweka mpenzi...weeeeee
hebu jaribu na wewe dada..
Natania Dadaaangu.
Av a gud day
 
macho nimefunguka Waberoya, naninaamini sakata la muro litaibua mengi mazuri aidha kisheria ama kijamii, maaana nimeanza kujua matumizi mwanana wa pingu katika mahaba, hii imenipa hamasa ya mimi kuitafuta ili nikidhi haja....
nataraji jambo moja rate ya wanunuaji wa bidhaa hiyo itaongezeka.

we! sikukuambia ufungue macho ukanunue pingu! ila uangalie kuwa swala la Muro la kununua pingu inaonekana ni common kwa baadhi ya raia kwenye lile duka!

ukinunua mimi simo! usiisahau tu kwenye gari! LOL!
 
Sisemi kwa maana ya kuwatukana lakini kutokana na uzoefu wangu katika mambo ya afya ya akili (mental health) naweza kusema pasipo shaka kabisa kuwa kuna watu wanahitaji kupimwa na kupatiwa matibabu ya haraka kwani wana matatizo katika uwezo wao wa kutumia chembechembe za ubongo kufikiri na kujenga hoja.

Soma sehemu hii ya habari iliyoko kwenye gazeti la mwananchi kuhusu mambo ya Muro:



wengi wamekuwa wakihoji mtu kukutwa na pingu ati ni raia; na sasa duka linasema wanashangaa inakuwaje raia kuuziwa pingu! Sikutaka kusema lakini sina budi kusema.

HIVI NI KIPI KIGUMU ENYI watawala WETU?! Kumuuzia raia bunduki na risasi za moto au kumuuzia pingu? Kama mmepitisha sheria inayokubali raia kununua bunduki na risasi kwenye duka la serikali inakuwaje jambo la kushangaza kununua pingu KWENYE duka hilo hilo?

Yaani mnachofanya ni sawasawa mnashangaa imekuwaje mtu kanunua baskeli wakati yeye ni raia ilhali duka lenu linauza magari!? Kama raia anaweza kununua gari kusafiria na akakuta mnauza, piki piki na baskeli, akiamua kununua gari na baskeli ni kipi kinaweza kudhuru zaidi barabarani!?

Naheshimu sana michango yako ambayo imejaa nguvu za hoja... lakini angalia safari hii isije ikawa wewe ndiye mwenye stahili ya kupimwa akili...
Kwanini?
1. Mwenye duka hakusema raia kumiliki pingu ni uvunjivu wa sheria bali amesema raia wa kawaida hawaruhusiwi kununua pingu.
2. Bunduki/risasi za moto vs pingu ni vitu viwili tofauti... na vinatumika kwa kazi mbili tofauti.
AND... Raia wa kawaida hawauziwi pingu kama wasivyouziwa mavazi ya jeshi/polisi..... kwa sababu wanaweza ku-mis-use kazi zake i.. e. wakatumia kwa utapeli kama alivyofanya Muro
 
Naheshimu sana michango yako ambayo imejaa nguvu za hoja... lakini angalia safari hii isije ikawa wewe ndiye mwenye stahili ya kupimwa akili...
Kwanini?
1. Mwenye duka hakusema raia kumiliki pingu ni uvunjivu wa sheria bali amesema raia wa kawaida hawaruhusiwi kununua pingu.
2. Bunduki/risasi za moto vs pingu ni vitu viwili tofauti... na vinatumika kwa kazi mbili tofauti.


Hakuna kitu kama "raia wa kawaida".

AND... Raia wa kawaida hawauziwi pingu kama wasivyouziwa mavazi ya jeshi/polisi..... kwa sababu wanaweza ku-mis-use kazi zake i.. e. wakatumia kwa utapeli kama alivyofanya Muro

Muro ameitumia vipi pingu kitapeli? alimfunga nayo nani na wapi?
 
Hakuna kitu kama "raia wa kawaida".



Muro ameitumia vipi pingu kitapeli? alimfunga nayo nani na wapi?


OPSS... ni kweli hakuna kitu kama raia wa kawaida (theoretically) lakini hoja yangu inabaki palepale.... raia...

Hii ya Muro ameitumia vipi... tusubiri tafadhali... kesi iii mahakamani... utajua tu aliitumia vipi...
 
Mkuu hayo matumizi nami nimeyafurahia yanaweza yakawa solution kwa matatizo fulani fulani ya Ndoa.
Hili sakata la muro natamani niuushuhudie mwisho wake kwa kauli thabiti kutika kwa viongozi wetu....lakini nahofia mambo yatakuwa kama stori zingine za EPA,Meremeta n.k

Dinho halafu inaonekana ni very romantic! Mimi baada ya MMKJ kuweka ule ushairi kule basi nikasema wacha tutafute lakini tatizo Mzinga watakuwa wanajishtukia kuuza kwa sasa
 
Hii ya Muro ameitumia vipi... tusubiri tafadhali... kesi iii mahakamani... utajua tu aliitumia vipi...

kwanini tusubiri tena mahakamani wakati tayari umeshahitimisha kuwa aliitumia kitapeli? Umesema hivi:


... sababu wanaweza ku-mis-use kazi zake i.. e. wakatumia kwa utapeli kama alivyofanya Muro

inaonekana hukutaka kusubiri mahakamani kwani tayari umeshajua kuwa Muro ametumia pingu kitapeli? umejuaje?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom