I got to say it; watawala wana matatizo kichwani!?

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,474
39,987
Sisemi kwa maana ya kuwatukana lakini kutokana na uzoefu wangu katika mambo ya afya ya akili (mental health) naweza kusema pasipo shaka kabisa kuwa kuna watu wanahitaji kupimwa na kupatiwa matibabu ya haraka kwani wana matatizo katika uwezo wao wa kutumia chembechembe za ubongo kufikiri na kujenga hoja.

Soma sehemu hii ya habari iliyoko kwenye gazeti la mwananchi kuhusu mambo ya Muro:

"Sisi wenyewe tumeshangazaa baada ya kuona taarifa ile kwenye vyombo vya habari, lakini tunachojiuliza ni kwamba inakuwaje raia anauziwa pingu wakati hana matumizi nayo,” alisema Kanali Mgawe.

wengi wamekuwa wakihoji mtu kukutwa na pingu ati ni raia; na sasa duka linasema wanashangaa inakuwaje raia kuuziwa pingu! Sikutaka kusema lakini sina budi kusema.

HIVI NI KIPI KIGUMU ENYI watawala WETU?! Kumuuzia raia bunduki na risasi za moto au kumuuzia pingu? Kama mmepitisha sheria inayokubali raia kununua bunduki na risasi kwenye duka la serikali inakuwaje jambo la kushangaza kununua pingu KWENYE duka hilo hilo?

Yaani mnachofanya ni sawasawa mnashangaa imekuwaje mtu kanunua baskeli wakati yeye ni raia ilhali duka lenu linauza magari!? Kama raia anaweza kununua gari kusafiria na akakuta mnauza, piki piki na baskeli, akiamua kununua gari na baskeli ni kipi kinaweza kudhuru zaidi barabarani!?
 
This is only the tip of the iceberg I am afraid.

Sheria zetu za ajabu nyingine hazijabadilishwa tangu zikokotolewe na muingereza kutoka India 1948.
 
Mkjj, unasahau kwamba serikali yetu inapinga shughuli za ukahaba??... hatuchelewi kukuta kwamba sababu kubwa zinazowapelekea 'watawala' wetu kupinga manunuzi ya pingu hizo ni matumizi yake yasiyotarajiwa kwenye mambo ya ukahaba. Wamegundua hivi karibuni ununuzi wa pingu umeshamiri na uchunguzi wao umewajuza kuwa pingu hizi zinatumika kwenye S & M (ngono machachari), jambo ambalo ni kinyume na sheria zetu.
 
Jamani mimi sijapata jibu. Hii kesi inasikilizwa kwenye vyombo vya habari? Hakimu ni nani? Mawakili Je?
 
Mkjj, unasahau kwamba serikali yetu inapinga shughuli za ukahaba??... hatuchelewi kukuta kwamba sababu kubwa zinazowapelekea 'watawala' wetu kupinga manunuzi ya pingu hizo ni matumizi yake yasiyotarajiwa kwenye mambo ya ukahaba. Wamegundua hivi karibuni ununuzi wa pingu umeshamiri na uchunguzi wao umewajuza kuwa pingu hizi zinatumika kwenye S & M (ngono machachari), jambo ambalo ni kinyume na sheria zetu.

Kwa hiyo kama mtu unajiexpress kama "Californication" na mkeo nao pia ni ukahaba?

Au bongo tuna Cultural police kama Saudi Arabia na Iran?
 
Sisemi kwa maana ya kuwatukana lakini kutokana na uzoefu wangu katika mambo ya afya ya akili (mental health) naweza kusema pasipo shaka kabisa kuwa kuna watu wanahitaji kupimwa na kupatiwa matibabu ya haraka kwani wana matatizo katika uwezo wao wa kutumia chembechembe za ubongo kufikiri na kujenga hoja.

Soma sehemu hii ya habari iliyoko kwenye gazeti la mwananchi kuhusu mambo ya Muro:



wengi wamekuwa wakihoji mtu kukutwa na pingu ati ni raia; na sasa duka linasema wanashangaa inakuwaje raia kuuziwa pingu! Sikutaka kusema lakini sina budi kusema.

HIVI NI KIPI KIGUMU ENYI watawala WETU?! Kumuuzia raia bunduki na risasi za moto au kumuuzia pingu? Kama mmepitisha sheria inayokubali raia kununua bunduki na risasi kwenye duka la serikali inakuwaje jambo la kushangaza kununua pingu KWENYE duka hilo hilo?

Yaani mnachofanya ni sawasawa mnashangaa imekuwaje mtu kanunua baskeli wakati yeye ni raia ilhali duka lenu linauza magari!? Kama raia anaweza kununua gari kusafiria na akakuta mnauza, piki piki na baskeli, akiamua kununua gari na baskeli ni kipi kinaweza kudhuru zaidi barabarani!?

Sasa na hilo duka kwa nini linauza bidhaa ambazo raia hawaruhusiwi kumiliki. Si wangehifadhi warehauzi kama ni kwa matumizi ya taasisi maalumu??????
 
Sasa na hilo duka kwa nini linauza bidhaa ambazo raia hawaruhusiwi kumiliki. Si wangehifadhi warehauzi kama ni kwa matumizi ya taasisi maalumu??????


kinachonishangaza Nyambala ni kuwa wanakasirishwa sana na kukutwa pingu ndani ya gari kuliko bunduki!! NIlikuwa najiuliza mara ya mwisho kusikia majambazi yamevamia mitaa na pingu au wamepora benki kwa kutumia pingu ilikuwa lini?
 
kinachonishangaza Nyambala ni kuwa wanakasirishwa sana na kukutwa pingu ndani ya gari kuliko bunduki!! NIlikuwa najiuliza mara ya mwisho kusikia majambazi yamevamia mitaa na pingu au wamepora benki kwa kutumia pingu ilikuwa lini?

...Hii ni kali......Imebidi nicheke sana...You have made my morning!
 
Hivi hawa viongozi wetu wanashindwa nini kabla ya kuongea kuhakikisha kuwa wemepima wanachoongea? Ngumu kweli kwa sasa kujua kuwa mtu amekosea kwa makusudi au hajui aongeacho
 
hili swala naamini likifikishwa mahakamani kuna mengi yaliofichika yatakua wazi, upo upande utaumbuka na utatafuta pakufichia sura zao. nasema haya kwa maana kuna mtafaruku katika kila hatua, hali ambayo inamuacha mtanzania wakawaida asiwe na maoni binafsi yaliyo huru....bado natamani kumuona Jerry Muro akiulizwa swali la matumizi ya pingu yake mahakamani .... maana Kova ameshindwa kumuhoji hilo swali kama Jerry mwenyewe alivyonukuliwa.
sasa baaada ya sakata hili na UMMA kueleweshwa juu ya matumizi ya PINGU bila shaka duka linalouza pingu lijiandae kupokea maombi mengi ya kuhitaji bidhaa hiyo.
 
HUYU KOVA KASEMA PINGU NI ILLEGAL,swali la msingi MTU AKIKUTWA NA GONGO(which is deemed illegal) huwa anaulizwa risiti ya kununulia gongo hiyo?au huwa anakamatwa kwa kumiliki,kunywa gongo?
 
hili swala naamini likifikishwa mahakamani kuna mengi yaliofichika yatakua wazi, upo upande utaumbuka na utatafuta pakufichia sura zao. nasema haya kwa maana kuna mtafaruku katika kila hatua, hali ambayo inamuacha mtanzania wakawaida asiwe na maoni binafsi yaliyo huru....bado natamani kumuona Jerry Muro akiulizwa swali la matumizi ya pingu yake mahakamani .... maana Kova ameshindwa kumuhoji hilo swali kama Jerry mwenyewe alivyonukuliwa.
sasa baaada ya sakata hili na UMMA kueleweshwa juu ya matumizi ya PINGU bila shaka duka linalouza pingu lijiandae kupokea maombi mengi ya kuhitaji bidhaa hiyo.

Unless it is ILLEGAL,matumizi ya Pingu ni Private matter ya mhusika.Walichotakiwa kufanya Polisi ni kumkamata akiitumia red-handed katika matumizi ambayo ni kinyme cha sheria.
 
Mimi nadhani hawa jamaa wala hawapingi wala kukataza watu kumiliki Pingu ila tu kwasababu wana agenda zao kwa Muro ndo maana wanajifanya leo wanashangaa kuona raia wa kawaida akimiliki Pingu wakati huo huo ni wao wenyewe wameruhusu uuzwaji wake na mimi sidhani kama Muro ni mtu wa kwanza kukutwa na pingu mpaka kwake iwe skendo....naamini kabisa Kova na wenzake katika harakati zao za kukuamata wahalifu wameshawahi kukuta Pingu lakini hawakuwahi kuripoti,tumekuwa tukisikia tu,tumekamata risasi na bunduki kadhaa walikuwa haripoti pingu kwasababu it was not a big deal kwanini leo iwe kwa Muro?
 
kinachonishangaza Nyambala ni kuwa wanakasirishwa sana na kukutwa pingu ndani ya gari kuliko bunduki!! NIlikuwa najiuliza mara ya mwisho kusikia majambazi yamevamia mitaa na pingu au wamepora benki kwa kutumia pingu ilikuwa lini?

Duuuuuuuuuuhhhhhhhhh! mkuu hii ni kali kuliko!1 haaaaa heeeeeeeee kwekwekweeeeeeeeeeeeee.
Ntafukuzwa kazi kwa kicheko.
 
kinachonishangaza Nyambala ni kuwa wanakasirishwa sana na kukutwa pingu ndani ya gari kuliko bunduki!! NIlikuwa najiuliza mara ya mwisho kusikia majambazi yamevamia mitaa na pingu au wamepora benki kwa kutumia pingu ilikuwa lini?

Unajua huyo kamanda wa polisi alichofanya ni kujaribu kucheza na minds za watanzania. Ajenda ikiwa ni rushwa, well attempted rushwa.......... Ikaingizwa bunduki na pingu to justfy maelezo ya mtu aliyedai kuombwa rushwa. Sasa Imekuja kuonekana ishu haina mashiko baada ya kutenganisha hizo items:

1. Rushwa - Tunaambiwa CCTV imekamata. Lakini kwa mtu wa stahiki ya Kova angekuwa amesharusha hiyo clip hewani. And he would be one of the most genious cop kusubstantiate ushahidi kisheria kutoka kwenye the alleged CCTV videos.

2. Bunduki - Inamilikiwa kihalali

3. Pingu - Hapa naona Kova ndio aliamua kukandamizia huku akisahau ubatili au uhalali ulitakiwa uthibitishwe kisheria. Sasa kwa sababu, nadhani ni audience aliyoizoea akakurupuka kutamka kwamba hakuna raia anaruhusiwa kuwa na pingu. Na kama eti ni halali aje na risiti...........

Sasa na hawa wengine inaonekana hawajaelewa kwamba polisi wameshafanya fu..up ya namna walivyohandle the whole ishu. Nao wanaanza kwa mtindo ule ule wa kushangaa.......... I would have thought kwa watu smart kama JWTZ wangefanya uchunguzi kwanza kabla ya kuanza kushangaa.

Well nadhani ni staili ya serikali siku hizi kushangazwa, kushtushwa etc.
 
hili swala naamini likifikishwa mahakamani kuna mengi yaliofichika yatakua wazi, upo upande utaumbuka na utatafuta pakufichia sura zao. nasema haya kwa maana kuna mtafaruku katika kila hatua, hali ambayo inamuacha mtanzania wakawaida asiwe na maoni binafsi yaliyo huru....bado natamani kumuona Jerry Muro akiulizwa swali la matumizi ya pingu yake mahakamani .... maana Kova ameshindwa kumuhoji hilo swali kama Jerry mwenyewe alivyonukuliwa.
sasa baaada ya sakata hili na UMMA kueleweshwa juu ya matumizi ya PINGU bila shaka duka linalouza pingu lijiandae kupokea maombi mengi ya kuhitaji bidhaa hiyo.

nguvumali (old or new?), kwani kazi ya pingu ni nini hadi mtu aulizie mahakamani? Kweli tunahitaji mahakama kuuliza kazi ya pingu ni nini?
 
Yuko jamaa yangu mmoja anafanya kazi kwenye nyumba ya mapadre. Alikuta kondomu kwenye moja ya mifuko ya suruale ya Padre. Akashtuka. Akaja kunisimulia. Nikamuuliza kondomu hiyo ilikuwa imeonyesha kutumika? Akaniambia hapana. ilikuwa imefungwa vizuri tu ndani ya kifuko chake. Nikwamwambia Padre wetu Mkatoliki hana kosa. Huenda alikuwa anaitumia kuonya wanaozitumia wakidhani ni kinga ya ukimwi!
Huenda na Muro alikuwa akizitumia pingu kuwaonya wala rushwa.
 
Unless it is ILLEGAL,matumizi ya Pingu ni Private matter ya mhusika.Walichotakiwa kufanya Polisi ni kumkamata akiitumia red-handed katika matumizi ambayo ni kinyme cha sheria.

bingo!!!!!!!!!!! I like you Kimweri.. ndio maana nimesema kwenye ule ukurasa mwingine hakuna jaji wala mahakama inayoweza kumfunga Muro kwa "kosa" la kukutwa na pingu ambazo zilikuwa ndani ya gari (wapi???)! Vinginevyo, itafungua mlango wa watu kufungwa wakikutwa na kamba, mnyororo n.k!
 
bingo!!!!!!!!!!! I like you Kimweri.. ndio maana nimesema kwenye ule ukurasa mwingine hakuna jaji wala mahakama inayoweza kumfunga Muro kwa "kosa" la kukutwa na pingu ambazo zilikuwa ndani ya gari (wapi???)! Vinginevyo, itafungua mlango wa watu kufungwa wakikutwa na kamba, mnyororo n.k!

Tena afadhali piongu maana kamba hutumika kunyongea!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom