Huyu ndiye Prof. Abdulrahman Mohamed Babu!

mwankuga

JF-Expert Member
Aug 30, 2010
334
120
JE,UNAMFAHAMU PROF.ABDULRAHAMAN MOHAMED BABU?

Leo nimejikuta namkumbuka sana Mwalimu wangu Prof.Haroub Othaman Miraji.Prof.Haroub Othaman alifariki tarehe 28/06/2009,moja kati ya vifo vilivyowahi kunigusa sana katika maisha yangu.Huyu kwangu alikuwa zaidi ya Mwalimu,msomi,mwanaharakati,mnyenyekevu,asiyependa makuu,mwenye busara na mjamaa wa kweli.

Prof.Haroub ndiye aliyenifanya nimfahamu japo kiasi Komradi Prof.Abdulrahaman Mohamed Babu.Kuna vitu vingi sana ambavyo watu hawa wanafanana,lakini ni Prof.Haroub ambaye alikuwa inspired na Prof.Mohamed Babu,hasa ikizingatiwa kwamba Prof Babu alikuwa mkubwa kwa Haroub kwa zaidi ya miaka 18.Prof.Haroub ameandika mambo mengi sana kuhusu Prof.Babu kwenye kitabu kiitwacho “WHEN I SAW BABU”.

Si rahisi sana kuandika mengi kwa huyu Babu.Lakini historia ni mwalimu mzuri sana,lakini kwa bahati mbaya sana,katika historia ya taifa letu (Tanganyika na Zanzibar) kuna watu watu ambao wamesahaulika sana kwa bahati mbaya au kwa makusudi.Kwa mfano,Oscar Kambona (alifukuzwa uanachama wa TANU mwaka 1968,na hivyo muda mwingi aliishi uahamishoni Uingereza),historia yake inapotoshwa sana ,na taswira waliyonayo watu wengi ni kwamba alikuwa ni muasi,kwa sababu tu walikuwa na mitazamo tofauti na Mwalimu Nyerere.Pengine hicho ndicho kilimkuta Prof.Mohamed Babu huko Zanzibar kwa kutofautiana na Sheikh Abeid Karume kwa upande mmoja na Mwalimu Nyerere kwa upande wa pili.

Prof.Mohamed Babu alizaliwa mwaka 1924 huko Unguja,Zanzibar,kati ya wasomi wa aina yake katika historia ya Zanzibar.Si tu kwamba Babu alikuwa ,Msomi,bali alikuwa mwanamapinduzi,mwanasiasa,mchumi na mjamaa wa kweli.

Prof.Babu alishiriki hasa katika harakati za ukombozi wa Taifa la Zanzibar.Ni moja kati ya wanzilishi wa chama cha ZNP ambacho kilikuwa kinaendesha harakati za kuikomboa Zanzibar katika mikono ya Sultan na Utawala wa Kiingereza.

Akiwa kama Katibu wa ZNP,inasemekana Babu alisaidia sana kukijenga chama hicho,japo hakikuwa na support kubwa kama ya chama cha ASP.Harakati zake pamoja na wenzake zilisaidia sana kupatikana uhuru wa Zanzibar (tarehe 10 Desemba,1963,hivyo sasa ni miaka 48 ya uhuru wa Zanzibar).Hata hivyo uhuru huo haukudumu sana,na baadae ndipo yalitokea Mapinduzi ya Mwaka 1964.

Aidha,inasemekana chama cha Umma (Umma Party) kilichoanzishwa na Prof.Babu na wenzake,kilichangia sana katika mapinduzi hayo (Japo Prof.Shivji katika kitabu chake cha Pan- Africanism or Pragmatism?,Lessons for Tanganyika and Zanzibar Union hakubaliani na hilo).Wanachama wa Umma Party wengi wao walikuwa wamepata mafunzo ya kijeshi katika nchi ya Cuba,hivyo ndio waliokuwa wanaendesha mafunzo ya kutumia bunduki na namna ya kuipindua serikali ya Shamte na Sultan kwa wenzao wa ASP.Pamoja na kwamba John Okello anasemwa kuwa kiongozi wa mapinduzi hayo,lakini wanachama wa umma party walishiriki sana,ndio maana hata kwenye Baraza la Kwanza la Mapinduzi,wanachama kadhaa wa Umma Party walikuwemo,akiwemo Prof.Abdulrahaman Mohamed Babu.

Inasemekana Chama cha Umma,kikiongozwa na Prof.Mohamed Babu kilisaidia sana katika harakati za kuunganisha Tanganyika na Zanzibar,ambayo leo tunaita Tanzania.Wakati huo Zanzibar ilianza kuyatisha mataifa ya Magharibi na Marekani,hasa kwa uhusiano wake na Cuba na Uchina (umma party ndio waliokuwa na mahusiano na nchi hizo,na sio ASP),mataifa ambayo yalikuwa ya kijamaa.
Kwa hiyo uhusiano wa Babu (socialist) na mataifa ya Uchina na Cuba,yalifanya mataifa ya Magharibi na Marekani kumtumia sana Mwalimu Nyerere ili aikomboe Zanzibar isiwe mikononi mwa Cuba na China.

Lakini kwa bahati mbaya sana,Karume alikuwa anaiendesha Zanzibar kibabe na kama taasisi binafsi bila kuzingatia utawala wa sheria.Na kwa kuwa lengo lake lilikuwa kuwatawala milele,hivyo hakujali tofauti zilizokuwepo kati ya yeye na Babu pamoja na wenzake.Hivyo Karume alikuwa katika tishio la kuangushwa,hivyo ili aweze kujinusuru,aliweka uhusiano usio rasmu na Tanganyika hasa Nyerere.Na ikumbukwe kwamba ,Zanzibar kulikuwa na zaidi ya wanajeshi 300 wa Tanganyika ili kulinda amani.

Kutokana na pressure ya Mataifa ya Magharibi na Marekani kuidhibiti Zanzibar na siasa za ujamaa,na kutokana na tishio la Karume kupinduliwa,ndipo Muungano wa Tanganyika na Zanzibar uliwezekana.Muungano ulimsaidia sana Karume (kuliko wazanzibari) kujiimarisha zaidi na ndio maana Karume alikuwa anauita Muungano kuwa ni kama koti,likikubana unalivua.

Kilichotea baada ya Muungano,wale wote ambao walikuwa na Mlengo wa kushoto (hasa wa umma party) na ambao walikuwa tishio kwa utawala wa Karume na Mataifa ya Ulaya na Marekani,waliteuliwa kushika madaraka katika serikali ya Muungano chini ya Rais Mwalimu Nyerere ambae alionekana anaweza kuishi nao na kuwadhibiti tofauti na Karume.Hicho ndicho kilichotokea kwa Mohamed Babu kuwa waziri wa mambo ya nje katika serikali ya Muungano na baadae kuwa waziri wa mipango.

Katika jambo la kushangaza Prof.Babu,pamoja na usomi wake,hakuweza kupata nafasi ya kutumia mawazo yake/taaluma yake katika kuisaidia Tanzania kiuchumi.Nafasi aliyopewa ilikuwa ya kisiasa zaidi,na kifupi alikuwa anapingana na sera ya kiujamaa ambazo Mwalimu Nyerere alikuwa ameiga Uchina.

Mchango mkubwa wa Prof.Babu ilikuwa ni kuanzishwa kwa Reli ya TAZARA.Ikumbukwe kwamba Wachina walikuwa na imani sana na Babu kuliko hata Mwalimu Nyerere ambaye alikuwa mjamaa lakini pia alikuwa na uhusiano mkubwa sana na Waingereza (wabebari).Babu alipofanya ziara ya kwanza kabisa huko China,inasemwa ndipo alipowaomba Wachina kusaidia katika ujenzi wa reli hiyo.Mwaka 1972,Babu alipokuwa katika mkutano wa Mawaziri wa OAU (sasa AU),huko Adis Ababa,huku nyuma,Mwalimu Nyerere alimwondoa katika nafasi ya uwaziri.

Baada ya kifo cha Sheikh Abeid Karume,ambaye aliuwawa kwa kupigwa risasi mwaka 1972,Prof.Babu na wenzake hasa wale wanzilishi wa chama cha umma party walikamatwa na kuwekwa ndani kwa kuhusishwa na kifo cha Karume.Hivyo Mohamed Babu alikaa kizuizini kutoka mwaka 1972 hadi mwaka 1978 ambapo aliachiwa na Mwalimu Nyerere katika kuadhimisha miaka 14 ya Tanganyika na Zanzibar.

Prof.Babu alikaa uhamishoni Uingereza ambapo aliendeleza shughuli za kitaaluma hadi mwaka 1995 aliporejea nyumbani,na safari hii aliibukia kwenye chama cha NCCR-MAGEUZI,ambapo aliteuliwa kuwa mgombea mwenza wa Augustino Mrema ambaye alikuwa anagombea urais,lakini tume ya uchaguzi ilimwondoa kwa kile kilichoitwa kukosa sifa,hasa kutokana na historia ya nyuma.

Hatimaye Prof.Abdulrahaman Mohamed Babu alifariki dunia tarehe 5 Agosti,1996 huko Uingereza na kuzikwa nyumbani kwao Unguja.Swali ambalo najiuliza,ni kwa nini Mwalimu Nyerere alishindwa kuishi na watu aliokuwa anatofautina nao kimawazo na itikadi? Kwa ufupi hivyo ndivyo ninavyomfahamu Prof.Abdulrahman Babu.Je,wewe unasemaje?
 
Hata JK naye kashindwa kuishi na waliotofautiana naye kimawazo:
1. Wapinzani wanafunguliwa mashtaka kwa kigezo feki cha tishio la Al Shabaab!
2. Mzee Babu Seya anaozea gerezani kwa kula "chakula cha mzee!"
3....
Kwa kifupi, nyuma ya tabasamu la Bwana Mkubwa kuna visasi kibao!
 
Hata JK naye kashindwa kuishi na waliotofautiana naye kimawazo:
1. Wapinzani wanafunguliwa mashtaka kwa kigezo feki cha tishio la Al Shabaab!
2. Mzee Babu Seya anaozea gerezani kwa kula "chakula cha mzee!"
3....
Kwa kifupi, nyuma ya tabasamu la Bwana Mkubwa kuna visasi kibao!
Maandishi yako yanatoa picha kuwa na ww nawe umeshindwa kuishi na unaotofautiana nao kimawazo. Chuki binafsi eeenh? Kwa taarifa yako, Sio wapinzani tu, hata wasio wapinzani, kama hawataki kutambua na kuheshimu Mamlaka zilizopo, wataendelea kukiona cha moto.
 
Babu was great akiwa uhamishoni tu, lakini akiwa Kiongozi wa Taifa hakuwa na nia njema rohoni mwake na hili taifa na Mwalimu alimjua mapema sana. - William
 
Maandishi yako yanatoa picha kuwa na ww nawe umeshindwa kuishi na unaotofautiana nao kimawazo. Chuki binafsi eeenh? Kwa taarifa yako, Sio wapinzani tu, hata wasio wapinzani, kama hawataki kutambua na kuheshimu Mamlaka zilizopo, wataendelea kukiona cha moto.

Haaaa haaaa! Sina chuki mkubwa ila sikulaumu kutetea kitumbua chako. Vipi mafisadi mbona wanaendelea kutamba kama hawana akili nzuri? Au kwa kuwa wao wanakula na vipofu?
 
Hata JK naye kashindwa kuishi na waliotofautiana naye kimawazo:
1. Wapinzani wanafunguliwa mashtaka kwa kigezo feki cha tishio la Al Shabaab!
2. Mzee Babu Seya anaozea gerezani kwa kula "chakula cha mzee!"
3....
Kwa kifupi, nyuma ya tabasamu la Bwana Mkubwa kuna visasi kibao!

Kuhusu hilo la babu seya ni uongo...hayo mengine siyajui,namjua babu seya na familia yake yote,na miongoni mwa watu ambao tumeendelea kuwa rafiki zake hata kipindi hiki kigumu akiwa gerezani ni mimi,mara kadhaa nakwenda kumtembelea na kumjulia hali,na kwa taarifa yako huyo jakaya ndio alijitahidi sana ku fight awasaidie tatizo issue yao ni nzito na ilishikiwa bango na nchi za magharibi kwa msaada wa kina ANANILEA NKYA ambao ndio waliishikia bango kinoma kesi yao huku wakipita kila nchi kuonyesha ushahidi wa walichokifanya kina babu seya!tuache kuzungumza mambo kwa hisia kwa kutumia he said she said drama tujikite kuongea kwa facts!
 
je,unamfahamu prof.abdulrahaman mohamed babu?

Leo nimejikuta namkumbuka sana mwalimu wangu prof.haroub othaman miraji.prof.haroub othaman alifariki tarehe 28/06/2009,moja kati ya vifo vilivyowahi kunigusa sana katika maisha yangu.huyu kwangu alikuwa zaidi ya mwalimu,msomi,mwanaharakati,mnyenyekevu,asiyependa makuu,mwenye busara na mjamaa wa kweli.

Prof.haroub ndiye aliyenifanya nimfahamu japo kiasi komradi prof.abdulrahaman mohamed babu.kuna vitu vingi sana ambavyo watu hawa wanafanana,lakini ni prof.haroub ambaye alikuwa inspired na prof.mohamed babu,hasa ikizingatiwa kwamba prof babu alikuwa mkubwa kwa haroub kwa zaidi ya miaka 18.prof.haroub ameandika mambo mengi sana kuhusu prof.babu kwenye kitabu kiitwacho "when i saw babu".

Si rahisi sana kuandika mengi kwa huyu babu.lakini historia ni mwalimu mzuri sana,lakini kwa bahati mbaya sana,katika historia ya taifa letu (tanganyika na zanzibar) kuna watu watu ambao wamesahaulika sana kwa bahati mbaya au kwa makusudi.kwa mfano,oscar kambona (alifukuzwa uanachama wa tanu mwaka 1968,na hivyo muda mwingi aliishi uahamishoni uingereza),historia yake inapotoshwa sana ,na taswira waliyonayo watu wengi ni kwamba alikuwa ni muasi,kwa sababu tu walikuwa na mitazamo tofauti na mwalimu nyerere.pengine hicho ndicho kilimkuta prof.mohamed babu huko zanzibar kwa kutofautiana na sheikh abeid karume kwa upande mmoja na mwalimu nyerere kwa upande wa pili.

Prof.mohamed babu alizaliwa mwaka 1924 huko unguja,zanzibar,kati ya wasomi wa aina yake katika historia ya zanzibar.si tu kwamba babu alikuwa ,msomi,bali alikuwa mwanamapinduzi,mwanasiasa,mchumi na mjamaa wa kweli.

Prof.babu alishiriki hasa katika harakati za ukombozi wa taifa la zanzibar.ni moja kati ya wanzilishi wa chama cha znp ambacho kilikuwa kinaendesha harakati za kuikomboa zanzibar katika mikono ya sultan na utawala wa kiingereza.

Akiwa kama katibu wa znp,inasemekana babu alisaidia sana kukijenga chama hicho,japo hakikuwa na support kubwa kama ya chama cha asp.harakati zake pamoja na wenzake zilisaidia sana kupatikana uhuru wa zanzibar (tarehe 10 desemba,1963,hivyo sasa ni miaka 48 ya uhuru wa zanzibar).hata hivyo uhuru huo haukudumu sana,na baadae ndipo yalitokea mapinduzi ya mwaka 1964.

Aidha,inasemekana chama cha umma (umma party) kilichoanzishwa na prof.babu na wenzake,kilichangia sana katika mapinduzi hayo (japo prof.shivji katika kitabu chake cha pan- africanism or pragmatism?,lessons for tanganyika and zanzibar union hakubaliani na hilo).wanachama wa umma party wengi wao walikuwa wamepata mafunzo ya kijeshi katika nchi ya cuba,hivyo ndio waliokuwa wanaendesha mafunzo ya kutumia bunduki na namna ya kuipindua serikali ya shamte na sultan kwa wenzao wa asp.pamoja na kwamba john okello anasemwa kuwa kiongozi wa mapinduzi hayo,lakini wanachama wa umma party walishiriki sana,ndio maana hata kwenye baraza la kwanza la mapinduzi,wanachama kadhaa wa umma party walikuwemo,akiwemo prof.abdulrahaman mohamed babu.

Inasemekana chama cha umma,kikiongozwa na prof.mohamed babu kilisaidia sana katika harakati za kuunganisha tanganyika na zanzibar,ambayo leo tunaita tanzania.wakati huo zanzibar ilianza kuyatisha mataifa ya magharibi na marekani,hasa kwa uhusiano wake na cuba na uchina (umma party ndio waliokuwa na mahusiano na nchi hizo,na sio asp),mataifa ambayo yalikuwa ya kijamaa.
Kwa hiyo uhusiano wa babu (socialist) na mataifa ya uchina na cuba,yalifanya mataifa ya magharibi na marekani kumtumia sana mwalimu nyerere ili aikomboe zanzibar isiwe mikononi mwa cuba na china.

Lakini kwa bahati mbaya sana,karume alikuwa anaiendesha zanzibar kibabe na kama taasisi binafsi bila kuzingatia utawala wa sheria.na kwa kuwa lengo lake lilikuwa kuwatawala milele,hivyo hakujali tofauti zilizokuwepo kati ya yeye na babu pamoja na wenzake.hivyo karume alikuwa katika tishio la kuangushwa,hivyo ili aweze kujinusuru,aliweka uhusiano usio rasmu na tanganyika hasa nyerere.na ikumbukwe kwamba ,zanzibar kulikuwa na zaidi ya wanajeshi 300 wa tanganyika ili kulinda amani.

Kutokana na pressure ya mataifa ya magharibi na marekani kuidhibiti zanzibar na siasa za ujamaa,na kutokana na tishio la karume kupinduliwa,ndipo muungano wa tanganyika na zanzibar uliwezekana.muungano ulimsaidia sana karume (kuliko wazanzibari) kujiimarisha zaidi na ndio maana karume alikuwa anauita muungano kuwa ni kama koti,likikubana unalivua.

Kilichotea baada ya muungano,wale wote ambao walikuwa na mlengo wa kushoto (hasa wa umma party) na ambao walikuwa tishio kwa utawala wa karume na mataifa ya ulaya na marekani,waliteuliwa kushika madaraka katika serikali ya muungano chini ya rais mwalimu nyerere ambae alionekana anaweza kuishi nao na kuwadhibiti tofauti na karume.hicho ndicho kilichotokea kwa mohamed babu kuwa waziri wa mambo ya nje katika serikali ya muungano na baadae kuwa waziri wa mipango.

Katika jambo la kushangaza prof.babu,pamoja na usomi wake,hakuweza kupata nafasi ya kutumia mawazo yake/taaluma yake katika kuisaidia tanzania kiuchumi.nafasi aliyopewa ilikuwa ya kisiasa zaidi,na kifupi alikuwa anapingana na sera ya kiujamaa ambazo mwalimu nyerere alikuwa ameiga uchina.

Mchango mkubwa wa prof.babu ilikuwa ni kuanzishwa kwa reli ya tazara.ikumbukwe kwamba wachina walikuwa na imani sana na babu kuliko hata mwalimu nyerere ambaye alikuwa mjamaa lakini pia alikuwa na uhusiano mkubwa sana na waingereza (wabebari).babu alipofanya ziara ya kwanza kabisa huko china,inasemwa ndipo alipowaomba wachina kusaidia katika ujenzi wa reli hiyo.mwaka 1972,babu alipokuwa katika mkutano wa mawaziri wa oau (sasa au),huko adis ababa,huku nyuma,mwalimu nyerere alimwondoa katika nafasi ya uwaziri.

Baada ya kifo cha sheikh abeid karume,ambaye aliuwawa kwa kupigwa risasi mwaka 1972,prof.babu na wenzake hasa wale wanzilishi wa chama cha umma party walikamatwa na kuwekwa ndani kwa kuhusishwa na kifo cha karume.hivyo mohamed babu alikaa kizuizini kutoka mwaka 1972 hadi mwaka 1978 ambapo aliachiwa na mwalimu nyerere katika kuadhimisha miaka 14 ya tanganyika na zanzibar.

Prof.babu alikaa uhamishoni uingereza ambapo aliendeleza shughuli za kitaaluma hadi mwaka 1995 aliporejea nyumbani,na safari hii aliibukia kwenye chama cha nccr-mageuzi,ambapo aliteuliwa kuwa mgombea mwenza wa augustino mrema ambaye alikuwa anagombea urais,lakini tume ya uchaguzi ilimwondoa kwa kile kilichoitwa kukosa sifa,hasa kutokana na historia ya nyuma.

Hatimaye prof.abdulrahaman mohamed babu alifariki dunia tarehe 5 agosti,1996 huko uingereza na kuzikwa nyumbani kwao unguja.swali ambalo najiuliza,ni kwa nini mwalimu nyerere alishindwa kuishi na watu aliokuwa anatofautina nao kimawazo na itikadi? Kwa ufupi hivyo ndivyo ninavyomfahamu prof.abdulrahman babu.je,wewe unasemaje?

ulichoandika hakina chembe ya shaka,ni kweli tupu;na hili suala ndio maadui zake salim a salim wamekuwa wakilitumia kumuangamiza kisiasa,kisa idhbu!
 
Kuhusu hilo la babu seya ni uongo...hayo mengine siyajui,namjua babu seya na familia yake yote,na miongoni mwa watu ambao tumeendelea kuwa rafiki zake hata kipindi hiki kigumu akiwa gerezani ni mimi,mara kadhaa nakwenda kumtembelea na kumjulia hali,na kwa taarifa yako huyo jakaya ndio alijitahidi sana ku fight awasaidie tatizo issue yao ni nzito na ilishikiwa bango na nchi za magharibi kwa msaada wa kina ANANILEA NKYA ambao ndio waliishikia bango kinoma kesi yao huku wakipita kila nchi kuonyesha ushahidi wa walichokifanya kina babu seya!tuache kuzungumza mambo kwa hisia kwa kutumia he said she said drama tujikite kuongea kwa facts!

Haya mzee!
 
JE,UNAMFAHAMU PROF.ABDULRAHAMAN MOHAMED BABU?

Leo nimejikuta namkumbuka sana Mwalimu wangu Prof.Haroub Othaman Miraji.Prof.Haroub Othaman alifariki tarehe 28/06/2009,moja kati ya vifo vilivyowahi kunigusa sana katika maisha yangu.Huyu kwangu alikuwa zaidi ya Mwalimu,msomi,mwanaharakati,mnyenyekevu,asiyependa makuu,mwenye busara na mjamaa wa kweli.

Prof.Mohamed Babu alizaliwa mwaka 1924 huko Unguja,Zanzibar,kati ya wasomi wa aina yake katika historia ya Zanzibar.Si tu kwamba Babu alikuwa ,Msomi,bali alikuwa mwanamapinduzi,mwanasiasa,mchumi na mjamaa wa kweli.

Kwa hiyo uhusiano wa Babu (socialist) na mataifa ya Uchina na Cuba,yalifanya mataifa ya Magharibi na Marekani kumtumia sana Mwalimu Nyerere ili aikomboe Zanzibar isiwe mikononi mwa Cuba na China.

Katika jambo la kushangaza Prof.Babu,pamoja na usomi wake,hakuweza kupata nafasi ya kutumia mawazo yake/taaluma yake katika kuisaidia Tanzania kiuchumi.Nafasi aliyopewa ilikuwa ya kisiasa zaidi,na kifupi alikuwa anapingana na sera ya kiujamaa ambazo Mwalimu Nyerere alikuwa ameiga Uchina.

Mchango mkubwa wa Prof.Babu ilikuwa ni kuanzishwa kwa Reli ya TAZARA.Ikumbukwe kwamba Wachina walikuwa na imani sana na Babu kuliko hata Mwalimu Nyerere ambaye alikuwa mjamaa lakini pia alikuwa na uhusiano mkubwa sana na Waingereza (wabebari).Babu alipofanya ziara ya kwanza kabisa huko China,inasemwa ndipo alipowaomba Wachina kusaidia katika ujenzi wa reli hiyo.Mwaka 1972,Babu alipokuwa katika mkutano wa Mawaziri wa OAU (sasa AU),huko Adis Ababa,huku nyuma,Mwalimu Nyerere alimwondoa katika nafasi ya uwaziri.

Hatimaye Prof.Abdulrahaman Mohamed Babu alifariki dunia tarehe 5 Agosti,1996 huko Uingereza na kuzikwa nyumbani kwao Unguja.Swali ambalo najiuliza,ni kwa nini Mwalimu Nyerere alishindwa kuishi na watu aliokuwa anatofautina nao kimawazo na itikadi? Kwa ufupi hivyo ndivyo ninavyomfahamu Prof.Abdulrahman Babu.Je,wewe unasemaje?

In short, namkubali sana Prof Babu kutokana na yale machache sana ninayoyafahamu kuhusu yeye! Nahisi, umeniubulia kiu ya kutaka kumfahamu kwa undani zaidi mzee huyu. Hata hivyo, kuna sehemu umenichanganya pale unaposema Prof Babu alikuwa mjamaa na bado alikuwa hakubaliani na sera za ujamaa za Mwalimu ambazo aliziiga kutoka China! Aidha, umeshaeleza kwamba Babu alikuwa na mafungamano na mataifa ya kijama hususani China na Cuba!!! So, ina maana Babu alikuwa anaikubali China kwa lipi ikiwa alikuwa hakubaliani nao katika kujenga uchumi wa kijamaa!??



 
In short, namkubali sana Prof Babu kutokana na yale machache sana ninayoyafahamu kuhusu yeye! Nahisi, umeniubulia kiu ya kutaka kumfahamu kwa undani zaidi mzee huyu. Hata hivyo, kuna sehemu umenichanganya pale unaposema Prof Babu alikuwa mjamaa na bado alikuwa hakubaliani na sera za ujamaa za Mwalimu ambazo aliziiga kutoka China! Aidha, umeshaeleza kwamba Babu alikuwa na mafungamano na mataifa ya kijama hususani China na Cuba!!! So, ina maana Babu alikuwa anaikubali China kwa lipi ikiwa alikuwa hakubaliani nao katika kujenga uchumi wa kijamaa!??

Katika kitabu cha Prof.Babu kiitwacho African Socialism or Socialist Africa? ndicho pengine kinaonyesha Babu alikuwa na mrengo gani.Kifupi ni kwamba ni kweli Prof.Babu alikuwa mjamaa.Tofauti na Mwalimu Nyerere ilikuwa ni namna ya kutekeleza sera za ujamaa.Prof.Babu alikuwa anataka Scientific Socialism,ujamaa unaotokana na mazingira ya nchi za kiafrika,kuliko kuiga kila kitu kutoka mataifa ya ujamaa kama vile Uchina.Maana inasemekana Mwalimu Nyerere alichukua sera za ujamaa kutoka China (hasa sera ya vijiji) ambayo baadae wote tunajua nini kilichotokea.
 
Babu was great akiwa uhamishoni tu, lakini akiwa Kiongozi wa Taifa hakuwa na nia njema rohoni mwake na hili taifa na Mwalimu alimjua mapema sana. - William

Inawezekana unayoyasema ni kweli.Lakini ninachojua ni kwamba Prof.Babu hakuweza kupata nafasi ya kutumia uwezo wake katika nafasi za uongozi alizokuwa amepewa.Pia tunatakiwa kujua kwamba alipewa nafasi hizo si kwa sababu ya uwezo wake,bali ilikuwa ni sehemu ya kumpoteza katika siasa za Zanzibar.Aidha inawezekana alikuwa na nia mbaya rohoni mwake (kitu ambacho si rahisi kudhibitisha),lakini ni vizuri utuambie kile ambacho hatukijui kuhusu Babu,maana historia ni pana sana,na mambo mengine yanajificha sana.
 
Mimi ni mmoja ya watu wanaomheshimu sana marehemu Prof. Haroub Othman! Huyu alikuwa msomi mahiri, aliyependa kuuhubiri ukweli bila kuchuja au kuuma uma maneno. Rip Prof! Ni moja ya wasomi ninao wa miss sana in our times.

Nakubaliana na wewe rafiki yangu.Prof.Haroub alikuwa msomi wa aina yake katika taifa letu.Tofauti na wasomi wengi,yeye hakupenda makuu,mtu asiyependa kujikweza,aliwaheshimu watu wote bila kujali elimu zao,mnyenyekevu,mwenye busara,mpole,mshauri,msema kweli,muungwana,hakuwa mchoyo n.k.Lakini kifo ni mipango ya Mungu,wakati mwingine unaweza kukufuru,kwamba kwanini asiwachukue hawa makuwadi wa soko huria?Lakini Mungu anabaki kuwa Mungu.Kila nafsi itaonja mauti.Lihimidiwe jina la bwana.
 
Hata JK naye kashindwa kuishi na waliotofautiana naye kimawazo:
1. Wapinzani wanafunguliwa mashtaka kwa kigezo feki cha tishio la Al Shabaab!
2. Mzee Babu Seya anaozea gerezani kwa kula "chakula cha mzee!"
3....
Kwa kifupi, nyuma ya tabasamu la Bwana Mkubwa kuna visasi kibao!

Kila mtu ana tafsiri yake.Na kila mtu ana haki ya kujieleza.Lengo la kuuliza jinsi Mwalimu Nyerere kushindwa kuishi na aliokuwa anatofautiana nao kimawazo na kiitikadi ilikuwa inalenga sisi wa kizazi hiki kujisaili.Kama ambavyo Mwalimu Nyerere alivyowahi kusema kwamba tatizo letu tunachukua mambo mabaya na kuacha mambo mazuri yaliyofanywa na utawala wake.Utofauti wa mawazo ndio unaweza kutusaidia katika harakati za maendeleo kama tofauti hizo tutachukulia positively.Lakini watu wengi hatupendi kutofautiana,tunapenda ndio mzee.Kutoka Ikulu,serikali za mitaa na hata kwenye familia.Boss ofisini anataka ndizo mzee,Baba nyumbani anapenda Ndio Mzee.Viongozi wa vyama vya siasa wanapenda Ndio Mzee.Hivi ndivyo tulivyozoea kuishi,kutofautiana kimawazo tumeweka ni uadui.Tunatakiwa tubadilike.
 
Mwankuga Babu alitaka sana kuitawala Zanzibar na kila nafasi aliyopewa alijaribu kuitumia kutengeneza njia ya kushika Urais wa Zanzibar. Yeye ndiye aliyepeleka wanafunzi 10 wa Ukomandoo Cuba wakiwemo Salim na Mahafudhi, well naomba niishie hapa. - William
 
Siasa za wakati ule wa cold war, zilijaa utata mtupu. Ilikuwa rahisi kuzika watu wazima na bila kuulizwa kwanini unafanya hivyo. Victims wa siasa zile wapo ila sina hakika kama Babu was one of them for any good or bad reasons!
 
Mwankuga Babu alitaka sana kuitawala Zanzibar na kila nafasi aliyopewa alijaribu kuitumia kutengeneza njia ya kushika Urais wa Zanzibar. Yeye ndiye aliyepeleka wanafunzi 10 wa Ukomandoo Cuba wakiwemo Salim na Mahafudhi, well naomba niishie hapa. - William

Kwa hilo nakubaliana na wewe.Lakini ni dhambi kwa Babu kuutaka Urais wa Zanzibar?Vinginevyo tuko pamoja.
 
Hivi Abdularahman Mohamed Babu aliwahi kuwa Profesa? Sikumbuki. Nikumbusheni.
 
Back
Top Bottom