Huyu ndiye Nicholas Mgaya - Katibu Mkuu TUCTA

Kwa nchi inayotawaliwa na USALAMA WA TAIFA usitegemee kutokea wazalendo wa kweli kwani wanazimwa kabla ya kufikia huo mlima wa uzalendo.

Dawa ni Moja tu. Tujitolee kutoa elimu kwa kizazi chetu ili wakifika zama zao wasiwe kama sisi wenye hekima na heshima za uoga. Tuhesabu kwamba kizazi hiki hakina jipya kwa future ya Tanzania ila kizazi kijacho ndicho tukipe majukumu ya kusimamia nchi vyema. Tumeuzwa live lakini hatujauzwa milele, tumedanganywa live but hatujadanganywa milele. tutakufa na machungu yetu moyoni but tupande mioyo ya faraja, matarajio, misimamo thabiti na jitihada kwa kizazi kijacho.

Kama hatutafanya hivyo naapa watanzania wataendelea kuchagua viongozi bomu kila ahsubuhi na kujutia jioni.

katika Yoote nayaona mabadiliko ya Umma, nawafeel Watanzania wanavyobadilika, waache kizazi cha Kikwete na kina Lowassa kife, kije kizazi cha nuclear, kwa vitisho hivyo wazalendo hawataogopa kama walivyo kizazi hiki cha kina Mgaya.
Mgaya kulinganisha na kizazi cha nyuma yeye ni shujaa.
yeye ameweza kusema maneno yaliyomkwaza Rais bila Woga, miaka kumi nyuma kwa maneno kama hayo kina Mtikila walilazwa ndani kwa kuitwa wachochezi..
hii inafanya baadhiya vijana leo kuanza kuzoea utamaduni wakuambiana makavu.....
 
I really wonder...These incompetent Interlopers like Jk doesnt know that one day they will bite Dust just like Amar Yuar'dua
 
Anfaal unafanya makosa katika hayo mahesabu yako. Kabla ya TUCTA kudai kiwango cha 315,000/= walifanya utafiti wa hali ya maisha na mfumuko wa bei na kufikia kiwango hicho. Hebu jiulize katika hali ya sasa mfanyakazi mwenye kaya ya watu wanne hizo 315,000/= zinaweza kumwezesha kulisha familia yake kutokea tarehe 1 hadi 30 kwa mwezi? Je ni nani mwenye wajibu wa kumhakikshia huyu mfanyakazi "maisha bora"? Na nani alimuahidi mfanayakazi huu "maisha bora".

Tazama ripoti ya mdhibiti na mkaugizi mkuu, kila mwaka serikali inapoteza mabilini ya shilingi kwa misamaha ya kodi isiyostahili, wizi, ubadhirifu n.k. Je unafikiri ni nani anapaswa kuhakikisha hizi fedha za umma zinalindwa na kutumika vizuri, sio rais wa nchi?

Serikali ya awamu ya nne inajiendesha kwa gharama kubwa sana ambazo zingeweza kupunguzwa na fedha hizo kutumika kuwalipa wafanyakazi. Mathalani Barza la Mawaziri lina mawaziri na mabaibu 60; serikali zilizopita zilikuwa na baraza lenye mawaziri kati ya 30 na 40 tu. Wote hawa wanafanya kazi yenye tija kwa wananchi?

Kumbuka kuwa mwenye wajibu wa kwanza kudhibiti mfumuko wa bei ni rasi, je unaonaje sasa mfumuko wa bei?

Ni vyema ukatafakari kwanza kabla ya kutoa lawama ka TUCTA
 
Ben.
Mmh.

They really sucks sometimes...

Jamaa hawezi kupunguza mzururo wake nchi za nje lakini anakuja kurushia watu wafanyakazi vijembe?Kuongoza nchi kiholela tu

Angepunguza hizo anasa zake za kushinda angani kuliko muda aliotumia ardhini tungeweza kuongea story tofauti by now,tusingekuwa tunajadili mgomo tena
 
Mgaya umenena tena kwa ustaarabu, tumekusikia endelea hivo kwa kutokuwa na jazba, fanya kazi yako ya kutetea wanaonyonywa na mafisadi, historia itakukumbuka, nasisi tupo nyuma yako. Mungu akulinde, akupe nguvu na ujasiri wa kufanikisha hayo.

Ulivo mjibu JK, imedhihirisha wewe ni mtu makini, Masikini sijui aufiche wapi uso wake!
 
Mgaya umenena tena kwa ustaarabu, tumekusikia endelea hivo kwa kutokuwa na jazba, fanya kazi yako ya kutetea wanaonyonywa na mafisadi, historia itakukumbuka, nasisi tupo nyuma yako. Mungu akulinde, akupe nguvu na ujasiri wa kufanikisha hayo.

Ulivo mjibu JK, imedhihirisha wewe ni mtu makini, Masikini sijui aufiche wapi uso wake!

Jakaya ameaibika sana sana! sijui atatoka vipi hapo jamaa wamejibu kwa busara na hekima ila wamemng'ong'a kiakili
 
Jakaya ameaibika sana sana! sijui atatoka vipi hapo jamaa wamejibu kwa busara na hekima ila wamemng'ong'a kiakili

wamemuonesha ni kwa namna gani hana nidhamu , adabu wala staha, kweli mimi namuhurumiaga sana, najiuliza anataka miaka mingine mitano ya nini ?
 
Naikubali TUCTA chini ya kiogozi shujaa Mgaya sasa kuliko miezi michache nyuma......................

Hii walioitumia TUCTA ni safi sana maana hata kama wangeng'ang'ania mgomo wangepata turn up ndogo sana kutokana na vitisho vya Rais siku mbili kabla ya Mgomo, sasa at least wamewapa nafasi wafanyakazi kudigest na kutambua kipi ni cha ukweli na kipi ni cha Uongo. Nadhani kutokana na Uongo wa Serikali kuwekwa wazi Wafanyakazi watakuwa na Imani zaidi na TUCTA
 
Hii walioitumia TUCTA ni safi sana maana hata kama wangeng'ang'ania mgomo wangepata turn up ndogo sana kutokana na vitisho vya Rais siku mbili kabla ya Mgomo, sasa at least wamewapa nafasi wafanyakazi kudigest na kutambua kipi ni cha ukweli na kipi ni cha Uongo. Nadhani kutokana na Uongo wa Serikali kuwekwa wazi Wafanyakazi watakuwa na Imani zaidi na TUCTA

Probably
 
Inaonekana wachangiaji wengi mko wepesi wa kusahau matokio! Kwenye vurugu za uchaguzi Mkuu Kenya vyama vya upinzani viilitisha maandamano kupinga kile kilicho kuwa kikiendelea huko kwa ndg zetu wakenya,upande wa Chadema nakumbuka mwenyekiti Mbowe alikuwa nje ya nchi hivyo chama kilikuwa mikononi mwa marehemu Chacha Wange .Kwa masikio yangu polisi wakayapiga marufuku maandamano yale,Chacha wange siku hiyo akatoa taarifa kupitia moja ya redio za hapa nchini akisisitiza kufanyika kwa maandamano yale.Binafsi nilikuwa nikimuamini sana marehemu Zakayo hasa ktk suala la msimamo,hivyo sikujiuliza zaidi ya mara moja kuhusu kushiriki maandamano hayo,nikawahi mapema mida ya saa 2 asubuhi tayari kwa lolote! Ndg zangu nilichokikuta pale hadi waleo sijawahi kusahau ndo maana hata leo nimeona nilidhishe nafsi yangu walau kwa kuwasimlia wanaharakati wenzengu mjue kazi iliyopo mbele yetu na ugumu wake.
Pamoja na watu wengi kuitikia maandamano yale hakuna hata kiongozi mmoja wa chama cha siasa aliyejitokeza achilia mbali kuendelea na taratibu za mgomo bali hata kuchapisha vikaratasi na kuvibadika kwenye nguzo za umeme kutueleza kinacho endelea! bahati mbaya Chacha Wangwe aliishatangulia mbele ya haki ila kimsingi alikuwa na swali la kujibu.Nikwanini alikuwa akipinga asicho kiweza? Mgaya bado yupo ,anaswali la kujibu kabla na yeye hatujaanza ooh labda angekuwepo.Tanzania hatuwezi kufanikiwa kwa kuwa na viongozi wenye kutaka sifa pasipo kuzifanyia kazi,nimesoma makala moja ya Happiness Katabazi kwenye Tanzania daima ya leo ndiyo imenizindua kuwa kumbe tulikuwepo wengi waliochukizwa na udhaifu wa TUCTA.Swali ni je kwa nini nasisi tunakubaliana nao? tulisitahili kufanya mgomo wetu usihusiana na TUCTA tofauti na hapo tukubali kwamba nasisi ni sehemu ya tatizo.
 
Mimi ngoja niwaonyeshe jinsi mimi nakubaliana Na TUCTA ya Mgaya pamoja na kina Dokta Slaaa Kuhusu Kima cha 315,000. Kwa kifupi Hata hiki Chenyewe baadoo!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!.
Tufanye Hesabu ndogo tu ya haraka;
Chukua Familia Ya Mume na Mke Mmoja na watoto wawili tu
Chukulia mtu anapanda gari mbili kila siku ambao kwa kweli ndio wastani
Nauli ya wazazi ya siku (Daladala) sh 1000 X 2 = 2000
Watoto (Daladala Mbili Kwasiku Mara mbili X Watoto wa 2)= (100x2x2) 400
Mlo wa mchana (1500x5) 7,500
Mlo wa usiku (1500x5) 7,500
Jumla ndogo 17,400

(17,400 X 30) = 516,000
Tambua kwamba Hapo sijaweka yafuatayo;
· Kodi ya Nyumba
· Bili ya umeme
· Mshahara wa hausi girl na hausi boy kama yupo
· Bili ya maji

HEBU NIAMBIENI WAPENDWA TUCTA WANA KOSA GANI HAPO.ZAIDI SANA WAMEONA HURUMA KUTAJA KIASI HICHO!
 
Mimi ngoja niwaonyeshe jinsi mimi nakubaliana Na TUCTA ya Mgaya pamoja na kina Dokta Slaaa Kuhusu Kima cha 315,000. Kwa kifupi Hata hiki Chenyewe baadoo!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!.
Tufanye Hesabu ndogo tu ya haraka;
Chukua Familia Ya Mume na Mke Mmoja na watoto wawili tu
Chukulia mtu anapanda gari mbili kila siku ambao kwa kweli ndio wastani
Nauli ya wazazi ya siku (Daladala) sh 1000 X 2 = 2000
Watoto (Daladala Mbili Kwasiku Mara mbili X Watoto wa 2)= (100x2x2) 400
Mlo wa mchana (1500x5) 7,500
Mlo wa usiku (1500x5) 7,500
Jumla ndogo 17,400

(17,400 X 30) = 516,000
Tambua kwamba Hapo sijaweka yafuatayo;
· Kodi ya Nyumba
· Bili ya umeme
· Mshahara wa hausi girl na hausi boy kama yupo
· Bili ya maji

HEBU NIAMBIENI WAPENDWA TUCTA WANA KOSA GANI HAPO.ZAIDI SANA WAMEONA HURUMA KUTAJA KIASI HICHO!

Mkuu umesema kweli kabisa..Na hata hayo mahesabu yenyewe uliyopiga kuna vitu vingi vya muhumi umeviacha..Wengi wetu tuko pamoja na TUCTA Mkuu...
 
Back
Top Bottom