Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Mmh kuna Mpya tena?
Inaitwa The bible itaonyeshwa Leo NBC
Hii Thread Ina Chafuka Sio Mda.
Inaoneshwa time gani kwa ET?
Saa 3 usiku,kwa Tz alfajili
huyo ni BRIAN DECON mzaliwa wa uingereza mwenye asili ya uyadi.
Aliweza kupita ktk mchujo wa watu elfu moja waliopita ktk mchujo wa nani atakae kuwa nyota ktk filamu hiyo.
Aliweza kuisoma Biblia mara nyingi zaidi ili kumjua yesu kiundani.
Mwisho wa siku bwana huyu alikuja kuokoka.
Ukumbukwe kwamba filamu ya yesu ndio filamu ilietafsiriwa ktk lugha nyingi zaidi duniani na ni filamu iliyotazamwa kwa muda mrefu.
Ni filamu yenye mafunzo mengi na isiyobagua umri wa mtazamaji.
Kuna uzi humu ulishawahi kumzungumzia huyu jamaa kwa upana zaidi
ni The Passion of the Christ. Mel Gibson hajaigiza hapo, ni mwongozaji!
Hazisujudiwi ila uwepo wake unakumbusha tu uwepo tu wa kitu cha namna hiyo. Ni kama unavyoweza kuchora picha yako its not real ila ukiiona unajikumbuka. Lakini cha zaidi ni kuna hata wapagani ambao wanaabudu miti na mawe na hawana shida na mtu yoyote. Pa kuanzia kuna dini ambazo ni kitovu cha fujo na ughaidi hizi ndizo zinahitaji kufanyiwa overhaul.
Jibu makini sana...bahati mbaya walio wa mwovu hawawezi anzia fikra hapo.. Kwani shehe anapominya sauti na kuitetemesha anaposoma q'uran anamuigiza nani? Muhammad, swahaba la kiarabu, Jibril au mungu? .
View attachment 247773
Si nia yangu kujadili katika mlengo huu, bali kujifunza na kuielewa dunia ilikotoka na iendako, katika machapisho mengi ya kiroho hasa ya kikristu hutumia picha ya Brian Robert Deacon inayofahamika kuwa ni ya Yesu Kristu wa Nazareti, lakini upembuzi wangu umebaini kuwa Anaitwa Brian Deacon, amezaliwa 13 February 1949 Huko Oxford Uingereza, Baba yake anaitwa Robert Thomas Deacon ambae aitaalamu alikuwa faundi magari, Mama yake anaitwa Eileen Mary ambaye alikuwa Nesi, Brian Deacon ni Mtoto wa pili kuzaliwa katika familia yao, Brian Deacon alioa mke wa kwanza mwaka 1977 aitwae Rula Lenska ambae amezaa nae mtoto mmoja aitwae Lara Brian Deacon, Lakini Mwaka 1982 mkewe alimtuhumu mumewe kutembea nje ya ndoa na ndoa yao kuvunjika, Alikaa miaka 16 na Hawara yake Cecy Redknap mpenzi wake wa muda mrefu, Mwaka 1998 alioa kke mwingine aitwaye Natalie Block ambaye mpaka leo wako pamoja,
Msanii Brian Deacon alipata tenda ya kuigiza katika Filamu kama YESU, Filamu alizowahi kushiriki ni A - Zed & Two Nought Mwaka 1985, Feather Seapent Mwaka 1976, Lillie Mwaka 1978 Na nk, Wakristo Sura Deacona huyu Msanii wanaitumia katika maombi yao mbele za Mungu kama sura ya YESU Mnazareti, Pia katika Makanisani Wameweka sura yake ikiwakilisha uwepo wa Yesu.
Yupo "Yesu mwingine" anaitwa Meil Gibson alicheza picha ya The Passion of Jesus Christ!
Meil Gibson anafanana sana na Yesu wa Nazareti. Mwaka jana alikuja Bongo na kila alipokwenda alifuatwa na makundi ya makubwa ya watu wakimuita na kumfananisha na Yesu wa Nazareti.
Baada ya kumaliza kucheza The Passion of Jesus Christ, Meil Gibson aliokoka na sasa anasambaza neno la Mungu.
Wakati wanacheza picha ya the Passion of Jesus Christ huko Israel/Palestine, kuna wakati waigizaji waligoma. Basi Director wa movie akamwambia Meil Gibson, Wewe Yesu hebu kaongee na wafuasi wako wamegoma. "Yesu" baada ya kuongea na wafuasi wake wakaacha mgomo na kuendelea ku act hiyo picha.