Huyu naye katumwa na nani kuchakachua haki za wanavyuo

lifeofmshaba

JF-Expert Member
Feb 19, 2011
867
219
Serikali izuie midahalo ya siasa shuleni, vyuoni'

TAASISI ya Utawala Bora na Maendeleo Tanzania (CEGODETA) imeishauri Serikali kupiga marufuku midahalo inayochangia kukosekana nidhamu na kusababisha uvunjifu wa amani shuleni na vyuoni.

Mkurugenzi Mtendaji wa taasisi hiyo, Thomas Ngawaiya aliliambia gazeti hili ofisini kwake kwamba vipo baadhi ya vyama vya siasa vimekuwa vikiingiza siasa mashuleni, hali inayosababisha wanafunzi kuchanganya mambo mawili kwa wakati mmoja na kuchangia kiwango cha elimu kushika.

Alisema midahalo ya siasa ambayo imekuwa ikifanyika vyuoni, demokrasia imekuwa ikitumika vibaya kutokana baadhi ya wachangiaji mada na wasikilizaji kutoa kauli zisizostahili kwa viongozi wa nchi.

"Wanafunzi wengi wamekuwa wakichanganywa na siasa ambayo imekuwa ikiingizwa mashuleni na baadhi ya vyama, mwanafunzi anatakiwa apate elimu na shule sio sehemu ya siasa, hali hii imechangia hata kiwango cha ufaulishaji kushuka," alisema Ngawaiya.

Ngawaiya ambaye pia ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi wa CCM Mkoa wa Kilimanjaro, alisema pia demokrasia imekuwa ikitumika vibaya, jambo alilodai kuwa nchi za Magharibi zimekuwa zikitumia fursa hiyo kuhakikisha nchi zenye amani zinaingia katika machafuko.

Kauli ya Ngawaiya ililenga kongamano la kujadili katiba lililoandaliwa na Jumuiya ya Wanataaluma wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDASA) wiki iliyopita kujadili Katiba ambapo alisema baadhi ya wachangiaji walitumia vibaya demokrasia.

source habari leo


MY TAKE:huyo thomas ngawayi kalipwa kiasi gani kusema uongo wa wazi namna hii? nani kamwambie elimu ya juu inashushwa na siasa kama sio upungufu wa walimu na na vifaa vya mafunzo kwa vitendo? kwanza hakuna takwimu kwamba elimu ya juu imeshuka nadhani anaongelea shule za kata? na hao wamewai kushiriki midahalo kweli? au ni shule na kata za jk? thomas kama unamuogopa kikwete au wamekutuma basi unaishushia hadhi hiyo taasisi yanu nadhani wakufukuze kazi huna fikra, au kwa sababu ccm walizomewa wanataka midahalo ifanyike manzese
 
Kwa taarifa ni kwamba Ngawaiya kitaaluma hata darasa la saba hakumaliza.
Hivyo alivyosema ni sawa kulingana na upeo wake wa kufikiri.
 
Yaleyale ya mama S. Simba na nchi za magharibi! Atakapoombwa atoe ushahidi atasema sijasema! Kuna wakati alishaomba ujumbe wa NEC CCM kwa ahadi ya kumwondoa Ndesamburo na kuiangamiza CDM mkoa wa kilimanjaro!
 
Hivi ni chama gani kinacho peleka siasa mashuleni na vyuoni zaidi kama sio ccm?
Tuanze na chipukizi wa ccm,hawa ni watoto wa primary,...kiongozi wao ni mtoto wa kikwete.
...
Huyu kichaa tu,amekosa la kuongea na watakufa wengi sana kwa presha
 
Sijaona source ya hii habari! taja gazeti gani limenukuu akisema uliyoandika ndo uchangiaji uwe makini kwani ulichoandika kina mashiko na kinajadilika
 
Sijaona source ya hii habari! taja gazeti gani limenukuu akisema uliyoandika ndo uchangiaji uwe makini kwani ulichoandika kina mashiko na kinajadilika

ni mwananchi mkuu nilipotoka hapo
 
kweli kabisa mkuu
Yaleyale ya mama S. Simba na nchi za magharibi! Atakapoombwa atoe ushahidi atasema sijasema! Kuna wakati alishaomba ujumbe wa NEC CCM kwa ahadi ya kumwondoa Ndesamburo na kuiangamiza CDM mkoa wa kilimanjaro!
 
Serikali izuie midahalo ya siasa shuleni, vyuoni’

TAASISI ya Utawala Bora na Maendeleo Tanzania (CEGODETA) imeishauri Serikali kupiga marufuku midahalo inayochangia kukosekana nidhamu na kusababisha uvunjifu wa amani shuleni na vyuoni.

Mkurugenzi Mtendaji wa taasisi hiyo, Thomas Ngawaiya aliliambia gazeti hili ofisini kwake kwamba vipo baadhi ya vyama vya siasa vimekuwa vikiingiza siasa mashuleni, hali inayosababisha wanafunzi kuchanganya mambo mawili kwa wakati mmoja na kuchangia kiwango cha elimu kushika.

Alisema midahalo ya siasa ambayo imekuwa ikifanyika vyuoni, demokrasia imekuwa ikitumika vibaya kutokana baadhi ya wachangiaji mada na wasikilizaji kutoa kauli zisizostahili kwa viongozi wa nchi.

“Wanafunzi wengi wamekuwa wakichanganywa na siasa ambayo imekuwa ikiingizwa mashuleni na baadhi ya vyama, mwanafunzi anatakiwa apate elimu na shule sio sehemu ya siasa, hali hii imechangia hata kiwango cha ufaulishaji kushuka,” alisema Ngawaiya.

Ngawaiya ambaye pia ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi wa CCM Mkoa wa Kilimanjaro, alisema pia demokrasia imekuwa ikitumika vibaya, jambo alilodai kuwa nchi za Magharibi zimekuwa zikitumia fursa hiyo kuhakikisha nchi zenye amani zinaingia katika machafuko.

Kauli ya Ngawaiya ililenga kongamano la kujadili katiba lililoandaliwa na Jumuiya ya Wanataaluma wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDASA) wiki iliyopita kujadili Katiba ambapo alisema baadhi ya wachangiaji walitumia vibaya demokrasia.

source habari leo


MY TAKE:huyo thomas ngawayi kalipwa kiasi gani kusema uongo wa wazi namna hii? nani kamwambie elimu ya juu inashushwa na siasa kama sio upungufu wa walimu na na vifaa vya mafunzo kwa vitendo? kwanza hakuna takwimu kwamba elimu ya juu imeshuka nadhani anaongelea shule za kata? na hao wamewai kushiriki midahalo kweli? au ni shule na kata za jk? thomas kama unamuogopa kikwete au wamekutuma basi unaishushia hadhi hiyo taasisi yanu nadhani wakufukuze kazi huna fikra, au kwa sababu ccm walizomewa wanataka midahalo ifanyike manzese

Kama ni kweli amesema atuambie kama mwanae Joachim aliharibiwa na siasa gani katika chuo gani? Akiendelea tutamwaga data hapa. Ebo! Tumechoshwa na uropokaji sasa
 
Jamani tumsamehe huyu jamaa..

  1. Hajui mchango wa vyuo na taasisi za elimu
  2. Sidhani kama ni mtu wa level ya kuwakosoa wasomi...sisi tutamsikiliza mtu kama Prof Baregu,Dr Lweitama nk
  3. Anatafuta pakutokea baada ya kupotezwa kwenye siasa na CCM...
 
Huyo ni tahira kabisa. Vyo ViKuu na ma shule ndie yenyewe. Wasomi wenzetu songeni mbele na mpikanie haki zetu na zenu zote. Kama CCM were good leaders we would not have been where we are today. CCM have messed up na wakubali mabadiliko. Asie kubali kushindwa sio mshindani. CCM = CHAMA CHA MAOCHAFU.
 
Nadhani antafuta pa kutokea coz hanajipya so ameona bora aropokwe ili watu wajue kama yupo..anatia hata huruma...ooh poor ngawaiya ...!!
 
Na kweli huyo nae Mama Simba ni Mayai kabisa. Yale yale tunapeana ma Sweet Malaya wa zamani. Uso kama mikati pua kama keneza Ooooh ana mume kweli ? Sidani kama mwanaume mwenye macho mazuri can take such a woman as a wife. She is UGLY extremely UGLY
 
asante mkuu sikujua kiwango chake cha shule hapo sasa nimeelewa anajaribu kusukuma train la mizigo peke yake
Yaleyale ya mama S. Simba na nchi za magharibi! Atakapoombwa atoe ushahidi atasema sijasema! Kuna wakati alishaomba ujumbe wa NEC CCM kwa ahadi ya kumwondoa Ndesamburo na kuiangamiza CDM mkoa wa kilimanjaro!
 
Huyo ni tahira kabisa. Vyo ViKuu na ma shule ndie yenyewe. Wasomi wenzetu songeni mbele na mpikanie haki zetu na zenu zote. Kama CCM were good leaders we would not have been where we are today. CCM have messed up na wakubali mabadiliko. Asie kubali kushindwa sio mshindani. CCM = CHAMA CHA MAOCHAFU.

Poor ngawaiya. Wakati tunaanza kuona mchango wa wasomi ktk jamii yeye anapiga tu domo. Hajui kwamba Hakuna nchi iliyoendelea bila wasomi.
 
Back
Top Bottom