Zinduna
JF-Expert Member
- Nov 6, 2011
- 2,378
- 3,379
Leo naomba kueleza lililo moyoni mwangu, wallahi sitanii, maana najua hapa watu watakuja na vijineno vya kukatisha tamaa~~~~Mabibi na Mabwana naomba saaana jambo hili msilifanyie dhihaka.
Ni hivi, kuna kijana mmoja kahamia huku visiwani Zenji mwaka jana mwishoni. Huyu kijana anaishi mtaa wa pili kutoka hapa nyumbani. Mara nyingi akienda kupunga upepo ufukweni huwa anapita hapa kwetu na hapiti bila kutusalimu, kwani kijana mwenyewe ana heshima kweli na aonekana kuwa amefunzwa huko kwao. Hivi karibuni nilipokuwa huko Dar, kula mwaka mpya alikumpa rafiki yangu kadi aniletee ya kunitakia heri ya mwaka mpya na niporudi na kupewa kadi hiyo nilimpa ahsante wakati anapita hapa kwetu. alifurahi sana.
Sasa juzi nimekutana naye Hoteli moja ya ufukweni nikiwa na dada yangu na tulipata wasaa wa kuzungumza kidogo na hapo ndipo aliposema yaliyo moyoni mwake kuwa ananipenda na angependa tuwe wapenzi. Nimemwahidi nitamjibu. Kusema ukweli ni kijana mzuri kwa sura na nimtanashati hasa na mwenye heshma kwa wakubwa na wadogo. Lakini kuna tatizo. Tatizo lenyewe ni kwamba, huyu bwana ni mfupi mno, yaani tukisimama ananifika kiunoni (Mie ni mwembamba na mrefu kiasi)~~~~~ Mwenzenu mie na wanaume wafupi~~~ akha! Hilo kwa kweli limeniwia gumu kukubali ombi lake, maana hata kutembea naye barabarani mwenzenu sitaweza.....
Sasa naomba msaada mwenzenu, nitumie msamiati gani kumkatalia, maana sipendi nimuumize moyo wake.
Ni hivi, kuna kijana mmoja kahamia huku visiwani Zenji mwaka jana mwishoni. Huyu kijana anaishi mtaa wa pili kutoka hapa nyumbani. Mara nyingi akienda kupunga upepo ufukweni huwa anapita hapa kwetu na hapiti bila kutusalimu, kwani kijana mwenyewe ana heshima kweli na aonekana kuwa amefunzwa huko kwao. Hivi karibuni nilipokuwa huko Dar, kula mwaka mpya alikumpa rafiki yangu kadi aniletee ya kunitakia heri ya mwaka mpya na niporudi na kupewa kadi hiyo nilimpa ahsante wakati anapita hapa kwetu. alifurahi sana.
Sasa juzi nimekutana naye Hoteli moja ya ufukweni nikiwa na dada yangu na tulipata wasaa wa kuzungumza kidogo na hapo ndipo aliposema yaliyo moyoni mwake kuwa ananipenda na angependa tuwe wapenzi. Nimemwahidi nitamjibu. Kusema ukweli ni kijana mzuri kwa sura na nimtanashati hasa na mwenye heshma kwa wakubwa na wadogo. Lakini kuna tatizo. Tatizo lenyewe ni kwamba, huyu bwana ni mfupi mno, yaani tukisimama ananifika kiunoni (Mie ni mwembamba na mrefu kiasi)~~~~~ Mwenzenu mie na wanaume wafupi~~~ akha! Hilo kwa kweli limeniwia gumu kukubali ombi lake, maana hata kutembea naye barabarani mwenzenu sitaweza.....
Sasa naomba msaada mwenzenu, nitumie msamiati gani kumkatalia, maana sipendi nimuumize moyo wake.