MAMMAMIA
JF-Expert Member
- Feb 26, 2008
- 3,811
- 1,603
New generation ya Wahispania, ndoa kwa maana ya "kufunga ndoa", sio issue kwani sheria zao zinawapa haki ya kukubalika kama wana ndoa kwa kuishi pamoja miaka miwili. Labda utafautishe baina ya divorce na separation. Kwao, divorce ni suala gumu sana kiasi kwamba "wanahofu ya kuoana kwa kuogopa urasimu na gharama kubwa za divorce". Kwa hiyo upo right unaposema wanaweza kukaa pamoja kwa miaka mingi kabla ya kuamua kufunga ndoa, lakini hata ikifikia hatua hiyo, kunakuwa na uhakika wa kuwa ndoa hiyo itadumu. Kwa hili sioni ubaya wowote kwani "sababu kubwa ya divorce katika jamii zetu ni kukimbilia kuoana", baada ya hiyo miaka 5 uliyosema au kasoro, mnagundua kuwa picha haziendi na mnaachana. Na kwa kuwa "at first instance" unaogopa commitment, hii ni faida kwako. Hata hivyo ninakushauri uwe na uamuzi thabiti kwani kukataa kwako commitment kunaweza kupelekea "kumsaliti huyu binti", na kwa kuwa umeshaonja uchungu wa kusalitiwa, usije ukawa msaliti wewe.Bellerina kumpenda nampenda, inapokuja kwenye tamaduni za mahusiano wenzetu hawa tuko tofauti nao ktk at least vitu viliwi, kwenye uhusiano wako straight na ni waaminifu zaidi yetu, kwenye swala la ndoa huwaga naona kama wanaweza kutoka muda wowote wakiboreka, divorce si ishu kwao. Katika hili la divorce I'm still old fashined, mimi naamini ndoa ni kufa na kuzikana. Kuwa na mke mzungu sijawahi fikiria huko nyuma ila nimeanza kulifikiria. Huyu bibie nadhani anafikiria ndoa ila si unajua kwao haiendagi fasta kivile, anaweza kutaka mkae pamoja hata five years kabla ya kuingia kwenye ndoa!
Kuhusu tafauti za kiutamaduni, ni suala la kila mmoja kujifunza mema ya utamaduni wa mwenzake, kuvumilia unayoyahisi ni mabaya kwako, na zaidi kulegeza kamba katika misimamo yetu.
Ikiwa huyu msichana kakubali kurudi Bongo, ni ishara tosha ya kuwa nakupenda kweli kwani tatizo au kikwazo kikubwa kwa Wahispania (hasa wasichana) ni kuhama kwao.
Mkuu, ikiwa unampenda, usisubiri sana na chukua uamuzi haraka.