SHABIKI maarufu wa Yanga, Steven Mwamwala, ambaye alianika hisia zake za kutaka kuonana na msanii maarufu wa filamu hapa nchini, Wema Sepetu, leo wanatarajiwa kukutana ana kwa ana.
Mwamwala, ni shabiki aliyejipambanua kwa wapenzi na mashabiki wa soka ndani na nje ya nchi, baada ya kumwaga machozi uwanjani timu yake ya Yanga ilipokubali kipigo cha mabao 5-0 kutoka kwa watani zao Simba.
Shabiki huyo, Julai 28, mwaka jana, siku ya fainali ya Kombe la Kagame, ambapo Yanga waliibuka mabingwa kwa kuwafunga Azam FC, mabao 2-0, alivua jezi yake na kubaki na fulana iliyoandikwa ‘I Love Wema Sepetu Ubingwa huu ni kwa ajili yako', na kuwaacha hoi wadau na mashabiki waliokuwepo Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam siku hiyo.
Shabiki huyo, alibainisha kuwa anamzimia msanii huyo wa mitindo kutokana na kazi zake, hivyo anatamani siku moja aweze kumuona ana kwa ana tofauti na sasa anamshuhudia kwa njia ya runinga.
Akizungumza na Tanzania Daima, Wema alisema, amepata taarifa za shabiki huyo siku nyingi, ila hakuzipa uzito kwa kuwa hakuamini, kwani aliona ni kama shabiki wake tu anayekubali kazi zake.
"Niliambiwa na watu kitu kama hicho, sawa siwezi jua anataka kuonana na mimi aniambie nini, basi kesho nitaonana naye ofisini kwangu," alisema Wema.
Kwa upande wake, shabiki huyo alishukuru kuwezeshwa kukutana na Wema, angalau aongee naye kidog
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.