Huwezi Amini! Huu ni UJUHA

Mfumwa

JF-Expert Member
Aug 29, 2008
1,456
42
Aliyemlawiti mwanawe atupwa jela miaka 60
Martha Mtangoo, Dodoma
Daily News; Monday,December 29, 2008 @21:15

Mkazi wa Msalato, Augustino Letema Slau (45), amehukumiwa kwenda jela miaka 60 baada ya kupatikana na hatia ya kumbaka na kumlawiti mwanawe wa kumzaa mwenye umri wa miaka 10.

Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Wilaya mkoani hapa, Groly Mwakihaba alidai mahakamani hapo jana kuwa mtuhumiwa huyo alitenda kosa hilo kati ya Septemba na Novemba mwaka jana, ambako katika muda usiojulikana, alimwingilia mwanawe kinyume cha maumbile na kumbaka.

Hakimu huyo alisema katika eneo la Msalato katika Manispaa ya Dodoma, mtuhumiwa huyo alimbaka mwanawe na kumlawiti ambapo baada ya kufanya kitendo hicho, alimtishia mtoto huyo kuwa iwapo atasema atamnyonga hadi afe.
Mwakihaba alisema wakati Sau akimwingilia mwanawe, alikuwa akimpaka mlenda katika sehemu zake zote za siri jambo ambalo lilimsababishia maumivu makali.

Alisema mtoto huyo aliyekuwa akilala na shangazi yake baada ya mama yake mzazi kufariki, alikuwa akichukuliwa na baba yake huyo na kumpeleka chumbani kwake muda ambao walikuwa peke yao na kumvua nguo zake na kuanza kumfanyia vitendo hivyo huku akimwonya kuwa asimweleze mtu yeyote.

Ilidaiwa mahakamani hapo kuwa baadaye walimu wa mtoto huyo walimwona akiwa anatembea vibaya huku akiwa mnyonge, kitendo kilichowalazimu kumhoji, ndipo alipowaeleza kuwa baba yake amekuwa akimlazimisha kumbaka na kumlawiti.

Alisema baada ya walimu hao kupata maelezo hayo, walimchukua mtoto huyo na kumpeleka Hospitali ya Serikali ya Mirembe ambako mtoto huyo alifanyiwa uchunguzi wa kina na kubainika kuwa alikuwa amefanyiwa vitendo hivyo.

Hakimu Mwakihaba alisema taarifa ya daktari ilibainisha kuwa mtoto huyo alikutwa ameharibika katika sehemu yake ya uke huku sehemu yake ya nyuma ikiwa imeongezeka ukubwa na kuingia vidole viwili tofauti na ilivyo kawaida, jambo ambalo lilionyesha kuwa mtoto huyo ameingiliwa mara nyingi.

Alisema kutokana na ushahidi uliotolewa na mashahidi ikiwamo mtoto huyo, unamtia hatiani mtuhumiwa na kuhukumiwa miaka 30 kwa kila kosa; la kwanza likiwa ni kufanya mapenzi na mtoto wake na kosa la pili likiwa ni kumlawiti, vitendo ambavyo ni kinyume cha sheria na adhabu hiyo ataitumikia kwa pamoja.

Awali, Mwendesha Mashitaka Mrakibu Msaidizi wa Polisi, Christina Mkonongo aliiomba mahakama kutoa adhabu kali kwa mtuhumiwa huyo kutokana na vitendo hivyo kukithiri katika jamii ili iwe fundisho kwa watu wengine wenye tabia hiyo. Naye mtuhumiwa huyo alipopewa nafasi ya kujitetea kabla ya kuhukumiwa aliiomba mahakama isimtie hatiani kwa kuwa hakufanya vitendo hivyo na kuwa hayo ni majungu tu ambayo yamefanywa kwa ajili ya kutaka kumwangamiza.

Source: Habari Leo
 
Safi sana. Nadhani litakuwa ni fundisho kwa wote wenye tabia ya kuwasarandia watoto wao.
 
Hiviiiii binadamu wengine wana akili kweli? mimi huwa nashindwa hata kuelewa- afadhali sikuwa rais wa nchi - ah
 
Na huyo shangazi mtu aliyekuwa akilala na huyo mtoto naye alitakiwa aonje joto ya jiwe kidogo haiwezekani siku zote hizo mtoto anafanyiwa unyama aina maana alikuwa hajui? au walikula deal na huyo hayawani...
 
God forbid! Hii dunia inaelekea kuisha! Mibaba mingine bwana! Nadhani miaka sitini haitoshi na haitoi fundisho madhubuti kwa mafilauni wengine kama huyu. Wako wapi wanaotaka adhabu ya kunyongwa ifutwe? Its too sad for the kid.
 
Mahakama ya Kadhi iletwe..hii haitoshi wajameni..

Bila kuhusisha na Dini ya Kiislam huoni raha. na lau angekuwa na jina la kiislam tungekukoma. hujasikia muislam akizungumzia imani ya mkosaji. hapa ni suala la Jamii na sio dini.

Wacha chuki zako mbaya dhidi ya Uislam wewe na mwenzio Max.
 
Bila kuhusisha na Dini ya Kiislam huoni raha. na lau angekuwa na jina la kiislam tungekukoma. hujasikia muislam akizungumzia imani ya mkosaji. hapa ni suala la Jamii na sio dini.

Wacha chuki zako mbaya dhidi ya Uislam wewe na mwenzio Max.

Wewe ni nani mpaka unizuie kutoa maoni yangu? Unaposikia neno mahakama ya kadhi tayari unajihisi kutukanwa! Wallahi kuna kitu unanitafuta si bure..Ktk neno 'mahakama ya kadhi' kunani? Mbona mi naliona ni suala la kheri tu ndg? Tena nilishaomba tu ikianzishwa mnijulishe, nitakuwa radhi kugawa hamzat 50 au 80 kwa wazinzi..Au hilo nalo ni tusi pia..Mwe..
 
Wewe ni nani mpaka unizuie kutoa maoni yangu? Unaposikia neno mahakama ya kadhi tayari unajihisi kutukanwa! Wallahi kuna kitu unanitafuta si bure..Ktk neno 'mahakama ya kadhi' kunani? Mbona mi naliona ni suala la kheri tu ndg? Tena nilishaomba tu ikianzishwa mnijulishe, nitakuwa radhi kugawa hamzat 50 au 80 kwa wazinzi..Au hilo nalo ni tusi pia..Mwe..

Pole ndugu yangu unazidi kujidhihirisha, hakuna mtu kasema umetukana, nilichokisema hiki hapa chini

"Bila kuhusisha na Dini ya Kiislam huoni raha. na lau angekuwa na jina la kiislam tungekukoma. hujasikia muislam akizungumzia imani ya mkosaji. hapa ni suala la Jamii na sio dini.

Wacha chuki zako mbaya dhidi ya Uislam wewe na mwenzio Max."
 
pole ndugu yangu unazidi kujidhihirisha, hakuna mtu kasema umetukana, nilichokisema hiki hapa chini

"bila kuhusisha na dini ya kiislam huoni raha. Na lau angekuwa na jina la kiislam tungekukoma. Hujasikia muislam akizungumzia imani ya mkosaji. Hapa ni suala la jamii na sio dini.

Wacha chuki zako mbaya dhidi ya uislam wewe na mwenzio max."

wewe ni nani mpaka unizuie kuuhusisha uislamu na posts zangu?
 
Huyo Agustino kwanza wangempeleka katika mental institution wakamtazama na kumtibu asije akawafanyia kitendo kama hicho wafungwa wenzake huko gerezani.
 
wewe ni nani mpaka unizuie kuuhusisha uislamu na posts zangu?

mimi ni Mahmoud Qaasim, sijakuzuia, wala siajwahi kufikiria jambo kama la kukuzuia, na siwezi kukuzuia kutoa maoni yoyote yale.

ninachosema wacha chuki, toa maoni bila chuki ilitupate kufaidika na maoni yako. maana kila kunapotokea hoja ya kijamii hoja ambayo inaudhalilishaji ndani yake hata kama aliyelifanya ni mtu binafsi basi fikra zako huja ni kuhusisha udhalilishaji huo na uislam. hilo ndilo linalonifanya nikwambie usiendeshwe na fikra za chuki. jaribu kuwa na staha katika fikra japo kidogo. Uislam sio m-baya kama unavyofikiri na ulivyofundishwa, jifunze toka pande zote halafu upime ndipo utoe maoni. Hakika mimi nathamini sana mafunzo mengi unayoyatoa kule kwenye Jukwaa letu la dini na wala sina chuki binafsi dhidi yako.
Kama nimekukwaza kwa namna yoyote ile basi pole sana, na nakutakia kheri katika Mwaka wa 2009. Allah aweze kukufunulia zaidi uweze kuuona ukweli na uongofu na uweze kuufuata. (ieleweke kuwa "ukweli na uongofu" sijamaanisha kuwa lazima iwe ni uislam, bali ni ule Ambao Muumba wetu anataka wanaadamu tuufuate, na si vinginevyo.)
 
Hivi kisheria Mtu akifungwa miaka 60 ni kweli atatumikia?au ile ya adhabu kwenda pamoja,mahakama ya kadhi si sababu kwani kuna sheria za kiislamu zinatumika mahakamani,wanasheria mtusaidie.
 
Halafu jamaa bila aibu anajitetea,bila kusema hata kumtaja huyo anaye pika majungu kwa lengo la kumuangamiza;dah!Imekaa vibaya sana hii,actually ni tukio la kusikitisha.Ila mahakama nayo imeniacha kidogo "Alisema kutokana na ushahidi uliotolewa na mashahidi ikiwamo mtoto huyo, unamtia hatiani mtuhumiwa na kuhukumiwa miaka 30 kwa kila kosa; la kwanza likiwa ni kufanya mapenzi na mtoto wake na kosa la pili likiwa ni kumlawiti, vitendo ambavyo ni kinyume cha sheria na adhabu hiyo ataitumikia kwa pamoja. "
Sasa inamaana kama angekuwa siyo mwanae na adhabu ingepungua?Wanasheria naombeni mwongozo hapo.
 
Huyu jamaa hana tofauti na mnyama yeye anaweza akampanda dadaake,mama ake n.k kuna watu wengine ubongo wao ni kama wa wanyama kama ng'ombe,mbuzi n.k
 
Watu kama hawa wanastahili hukumu ya kunyongwa mpaka afe, maana bila woga hata aibu kenda kujipinda kwa mtoto wake wa miaka 10 hata kama angekuwa si mtoto wake huyu ni wa kunyonga tu...:(:(
 
Bila kuhusisha na Dini ya Kiislam huoni raha. na lau angekuwa na jina la kiislam tungekukoma. hujasikia muislam akizungumzia imani ya mkosaji. hapa ni suala la Jamii na sio dini.

Wacha chuki zako mbaya dhidi ya Uislam wewe na mwenzio Max.


I abhorrence ISLAM, you are very correct, iter-alia, I repugnance it, ad infinitum.
 

I abhorrence ISLAM, you are very correct, iter-alia, I repugnance it, ad infinitum.


Hivi huyu Mahamudu Kasimu kwanini lazima akuseme Max na Mtindiowaubongo?

Dhambi wafanye Waislam, chuki wapewe MaxShimba na Mtindiowaubongo!!!!! Kwenye thread hii aliyefanya kituko wala si Muisilamu, kulikoni!

Kaaazi kweli kweli.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom