Huu wizi wa vodacom wa vocha za tsh450 watanzania wanauziwa tsh500 serikali iko wapi?

Tanzaniaone

Member
Apr 21, 2012
28
25
Ninapenda kuchukua fursa hii kuwauliza baadhi ya watu wenye dhamana kama akina January Makamaba na baadhi ya wabunge waliomo humu kwenye jamii Forum kuwa kwa nini wanaiacha nchi inaenda pabaya na wao wakiona ,Watanzania maskini wanaibiwa hadharani na makampuni ya simu ,maanake imekuwa siyo kificho tena mawakala wa makampuni ya simu wametengeneza vocha zenye thamani ya Tsh 450 na watanzania wa hali ya chini wanauziwa kwa Tsh 500 ,huu wizi utaendelea mpaka lini,hamuoni kama watanzania wa hali ya chini ndiyo wanaoibiwa?NO,wanadhurumiwa? mbona mnakuwa siyo wazalendo kwa nchi yenu na watu wenu ambao ndiyo wapiga kura wenu na walipa kodi? mbona mnasahau kuwa mtu wa chini analipa kodi pia?tena analipa kodi bila kumuibia mtu wala kuiibia nchi yake tofauti na hao wawekezaji ambao wanalipa kodi kwa kuiibia nchi na kuwadhurumu wananchi?tangu lini kitu cha Tsh 450 mtu akauziwa Tsh 500? Tunahitaji tamko la serikali katika suala hili na ikiwezakana uchapishwaji wa vocha za namana hiyo upigwe marufuku huo ni wizi na dhuruma kubwa kwa nini wasiweke Tsh 400? kwani watu walishindwa au kulalamika kuwa hawataki vocha za Tsh 500? Ninategemea hilo suala kama ni wazalendo mnaweza kuliangalia kwa makini na kulitafutia ufumbuzi,kwani wanaoibiwa na kudhurumiwa ni wananchi wa kipato cha chini na ndiyo wengi,ni muda wa kutafakali na kuchukua hatua
 
Back
Top Bottom