Ufunguo
JF-Expert Member
- Aug 18, 2012
- 330
- 231
Hivi karibuni niliagiza gari ndogo (980 CC) kutoka Japan kutokana na unafuu wake (mafuta na bei) ili kukidhi mahitaji mbalimbali kulingana na mwenendo wa maisha ya sasa. Pamoja na kwamba serikali iliongeza kodi ya uchakavu kwenye magari yaliyotengenezwa zaidi ya miaka 8 iliyopita, nilijikamua na kulipia gharama zote za ushuru.
Cha kushangaza pendekezo hilo kwa sasa limekataliwa na bunge na sijajua utaratibu unakuwaje kwa watanzania ambao wamekumbwa na tatizo hilo la kulipia ushuru ambao haukuwa umepata baraka za bunge. Anyway, tatizo langu la msingi hapa ni kwamba baada ya gari kufika bandarini na kukaa kama wiki moja kabla ya kutolewa, gari ilikutwa imeibiwa control box na power-window.
Baada ya kuhoji sana nikapewa document na bandari inayoonesha eti gari ilipokelewa bila control box na power-window wakati vitu vyote hivyo vilikuwepo wakati gari inasafirishwa hadi inafika bandarini Dar. Baada ya kuzama kwa undani zaidi nikagundua kumbe kuna mtandao kamili. Mkaguzi wa bandari anaweza kusema kitu X hakipo katika fomu ya ukaguzi wakati siyo kweli halafu baadae anawaambia vijana wake wakavyofoe vitu hivyo katika gari husika nafikiri kwa ushurikiano na agent.
Kibaya zaidi ni kwamba wanafanya unyama huo huku mmiliki wa gari tayari ameshalipia gharama zote za storage ikiwa ni pamoja na faini ya siku zilizozidi. Naamini tatizo hili si langu tu bali watanzania wengi limeshawapata, sasa tufanyeje wadau?. Je watanzania wakianza kupitishia mizigo yao bandari za nchi za jirani kama Kenya walaumiwe?.
Cha kushangaza pendekezo hilo kwa sasa limekataliwa na bunge na sijajua utaratibu unakuwaje kwa watanzania ambao wamekumbwa na tatizo hilo la kulipia ushuru ambao haukuwa umepata baraka za bunge. Anyway, tatizo langu la msingi hapa ni kwamba baada ya gari kufika bandarini na kukaa kama wiki moja kabla ya kutolewa, gari ilikutwa imeibiwa control box na power-window.
Baada ya kuhoji sana nikapewa document na bandari inayoonesha eti gari ilipokelewa bila control box na power-window wakati vitu vyote hivyo vilikuwepo wakati gari inasafirishwa hadi inafika bandarini Dar. Baada ya kuzama kwa undani zaidi nikagundua kumbe kuna mtandao kamili. Mkaguzi wa bandari anaweza kusema kitu X hakipo katika fomu ya ukaguzi wakati siyo kweli halafu baadae anawaambia vijana wake wakavyofoe vitu hivyo katika gari husika nafikiri kwa ushurikiano na agent.
Kibaya zaidi ni kwamba wanafanya unyama huo huku mmiliki wa gari tayari ameshalipia gharama zote za storage ikiwa ni pamoja na faini ya siku zilizozidi. Naamini tatizo hili si langu tu bali watanzania wengi limeshawapata, sasa tufanyeje wadau?. Je watanzania wakianza kupitishia mizigo yao bandari za nchi za jirani kama Kenya walaumiwe?.