Huu ubishi, nipeni maoni yenu.

Judgement

JF-Expert Member
Nov 13, 2011
10,327
4,779
Ninasibishe misemo hii miwili na ninachokisemea hapa.
"Tembea uyaone" na
"Hujafa hujaumbika"
Hii ni kauli iliyobeba malalamiko lukuki kutoka kwa Baba (mzazi) kwenda kwa kijana wake wa kiume :-

"Huyu mtoto nimemsomesha kwa gharama zangu , nikijinyima mambo kadha wa kadha , nikijua nawekeza kwa mwanangu.
Matarajio ni aje kunilea pale mie nitakapofikia kuchoka.

Umefika wakati sasa nimechoka nahitaji nipate mafao yalionifanya niwekeze kwake hali imekua kinyume na matarajio.
Mwanangu ana kazi nzuri ni Boss Pale TRA , lakini sina faida nae! .
Wanaonufaika na pesa zake ni wanawake malaya na wenye ma'Bar, yeye ni pombe , pombe na yeye.

Hivi majuzi tumetoleana nae maneno , tumebishana sana akiwa kalewa ananiambia mimi sikumsomesha, bali kasomeshwa na walimu shuleni, namnukuu "kwani pesa zako ulizokua unalipa bila walimu ningesoma?" mwisho nukuu.

Wadau ubishi wa nani kamsomesha kijana baina ya Baba na Mwalimu tuusemeeje ?
Kijana ndiyo yuko sahihi au Baba?
Kwa maana ya kusema kila mmoja kati yao apaswa aishi kivyakevyake?
Nawasilisha.
 
kijana yuko sahihi walimu ndio waliosomesha baba kalipa ada
 
Na bila Baba kulipa fees, hapo TRA angekuwepo?

Kijana hana adabu, haikuwa busara kumjibu hivyo baba yake..........Ndio mwalimu alimpa maarifa lakini kusomesha ni zaidi ya mwalimu kunahitajika jitihada ya mzazi kuhakikisha mwanafunzi amekwenda shule, amepata chakula, sare, na maneno ya kumtia moyo mwanafunzi.......isingekuwa haya angeweza kumsikiliza mwalimu?
 
Judgement,are you serious? How dare you?
Ambao hamjazaa,inshalah mola awajalie uoe,mzae,mlee na kisha ndo mrudi uzi huu.
Kuzaa na kulea ni jukumu kubwa sana,omba Mungu akupe mzazi mwenzio mlee pamoja.
 
Judgement,are you serious? How dare you?
Ambao hamjazaa,inshalah mola awajalie uoe,mzae,mlee na kisha ndo mrudi uzi huu.
Kuzaa na kulea ni jukumu kubwa sana,omba Mungu akupe mzazi mwenzio mlee pamoja.

Hee! Mukubwa hujalala mpaka mida hizi ? Pamoja na mapilika yako ya majukwaani mchana kutwa!
Nway nasaha zako zina mashiko.
 
Kijana hana adabu, haikuwa busara kumjibu hivyo baba yake..........Ndio mwalimu alimpa maarifa lakini kusomesha ni zaidi ya mwalimu kunahitajika jitihada ya mzazi kuhakikisha mwanafunzi amekwenda shule, amepata chakula, sare, na maneno ya kumtia moyo mwanafunzi.......isingekuwa haya angeweza kumsikiliza mwalimu?

Uyasemayo yana sense.
 
Hichi ndicho kizaz cha karne 21.

Kiongozi , hebu tufanye research isijekua hawa Kuku na Mayai ya broiler, Chips zikaangwazo kwa mafuta ya Transfoma, Industries food products , generally vikawa vinachangia kuharibu mentality ya vijana wa 21 century ?
Si inasemwa tusiangalie tulipoangukia tuangalie kilichocoz anguko!
 
Ninasibishe misemo hii miwili na ninachokisemea hapa.
"Tembea uyaone" na
"Hujafa hujaumbika"
Hii ni kauli iliyobeba malalamiko lukuki kutoka kwa Baba (mzazi) kwenda kwa kijana wake wa kiume :-

"Huyu mtoto nimemsomesha kwa gharama zangu , nikijinyima mambo kadha wa kadha , nikijua nawekeza kwa mwanangu.
Matarajio ni aje kunilea pale mie nitakapofikia kuchoka.

Umefika wakati sasa nimechoka nahitaji nipate mafao yalionifanya niwekeze kwake hali imekua kinyume na matarajio.
Mwanangu ana kazi nzuri ni Boss Pale TRA , lakini sina faida nae! .
Wanaonufaika na pesa zake ni wanawake malaya na wenye ma'Bar, yeye ni pombe , pombe na yeye.

Hivi majuzi tumetoleana nae maneno , tumebishana sana akiwa kalewa ananiambia mimi sikumsomesha, bali kasomeshwa na walimu shuleni, namnukuu "kwani pesa zako ulizokua unalipa bila walimu ningesoma?" mwisho nukuu.

Wadau ubishi wa nani kamsomesha kijana baina ya Baba na Mwalimu tuusemeeje ?
Kijana ndiyo yuko sahihi au Baba?
Kwa maana ya kusema kila mmoja kati yao apaswa aishi kivyakevyake?
Nawasilisha.

Katika mabishano yao nadhani wote huenda hawakutendeana sawa, naamini katika mazungumzo staha ya maneno inapaswa kutumiwa na rika zote iwe wazee au vijana, baba au mwana ili kuweka utangamano au uelewano wa kile wanacholiongea na wanachokusudia kukiongea na kieleweke.
Pili ningependa Wazazi tuelewe na tubadilike, kumsomesha mtoto ni wajibu wetu. Haya mawazo ya kumsomesha mtoto kwa minajili ya kuwekeza ili baadae aje akutunze nadhani hatuko sahihi. Cha msingi tusomeshe na tuwajengee misingi ya kuweza kusimama wao kama wao na kuendesha maisha yao kwa namna tunavotaka wawe.
Hii habari ya kuwekeza kwa watoto ili baadae waje watufae kiuchumi kwa maoni yangu wengi hatuko sahihi. Tuna wajibu wa kuwawezesha ili waje wawe na maisha mazuri, na pia tusijisahau kuwekeza sehemu stahiki kwa ajili ya mafao yetu sisi wenyewe kama wazazi.

Itokee tu mtoto aamue kukuongezea nguvu kiuchumi, lakini isiwe lazima. HAYA NI MAWAZO YANGU.
 
Ninasibishe misemo hii miwili na ninachokisemea hapa.
"Tembea uyaone" na
"Hujafa hujaumbika"
Hii ni kauli iliyobeba malalamiko lukuki kutoka kwa Baba (mzazi) kwenda kwa kijana wake wa kiume :-

"Huyu mtoto nimemsomesha kwa gharama zangu , nikijinyima mambo kadha wa kadha , nikijua nawekeza kwa mwanangu.
Matarajio ni aje kunilea pale mie nitakapofikia kuchoka.

Umefika wakati sasa nimechoka nahitaji nipate mafao yalionifanya niwekeze kwake hali imekua kinyume na matarajio.
Mwanangu ana kazi nzuri ni Boss Pale TRA , lakini sina faida nae! .
Wanaonufaika na pesa zake ni wanawake malaya na wenye ma'Bar, yeye ni pombe , pombe na yeye.

Hivi majuzi tumetoleana nae maneno , tumebishana sana akiwa kalewa ananiambia mimi sikumsomesha, bali kasomeshwa na walimu shuleni, namnukuu "kwani pesa zako ulizokua unalipa bila walimu ningesoma?" mwisho nukuu.
pole kwa mahasibu, ila epuka kubishana na mtu aliyelewa hamtapata muafaka. Ongea nae akiwa sober na uone atajibu nini.

Wadau ubishi wa nani kamsomesha kijana baina ya Baba na Mwalimu tuusemeeje ?
Kijana ndiyo yuko sahihi au Baba?
Kwa maana ya kusema kila mmoja kati yao apaswa aishi kivyakevyake?
Nawasilisha.
nini kilianza: yai vs kuku
kipi bora: pesa vs elimu
nani zaidi: ndugu vs rafiki nk
epuka argument kama hizi, hazina tija
 
hivi bila mzazi kujinyima na kutafuta shule, plus kulipa ada, hao walimu huyo kijana angewaonea wapi?
 
Roho inauma kwakweli, ukiona kichanga kikiumwa wazazi wanavyopata stress na hata kushindwa kula. Majamaa, spend time zenu na wamama wanaolea vichanga, inasaidia kurudisha heshima kwa wazazi wako. You know what am I saying...
 
Liliwahi kutokea katika familia inayonihusu kabisa,
hali iliendelea baba akaugua kwa kuwa hakuwa na nyumba nzuri ilibidi augulie kwenye zizi la ng'ombe
japo kijana alishajenga nyumba pembeni (akiwa anafunga milango kuacha mlinzi kwenda zake town kazini)
baba akatwaliwa (RIP Mzee S).

Baada ya muda mfupi sana toka atwaliwe baba yake, kila yule kijana akirudi zake wikiend akifungua mlango anamkuta baba yake kakaa sebuleni kwake, baada ya hapo alihangaika sana kwa kuwa ana imani za kishirikina, ila hata sasa bado siyo swari.

Hapo mnaweza kupata majibu nyie wenyewe kuwa mzazi ni nani.

Kijana ni chizi........! sema tu hajafikia hatua ya kupelekwa mirembe
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom