Mbaneingoma Zom
JF-Expert Member
- Feb 23, 2011
- 201
- 14
Ndugu zangu wadau wa JF na watanzania kwa ujumla wake naomba tujadili jambo hili nyeti ambalo mimi mdau mwenzenu nimeligundua na nikaona si vema kulikalia kimya.
Wakati bado watu wanalipigia kelele jambo la kufeli kwa kiwango kikubwa kwa wahitimu wa kidato cha nne, hata wengi kuomba vijana hao warudie mitihani yao Baraza la mitihani Tanzania limeonekana kupingana na dhana hiyo waziwazi.
Ndugu wana JF ikumbukwe kwamba kimbilio la mwisho la vijana hao na wengine wengi walioadhiriwa na mfumo mbovu wa elimu wa hapa nchi ni kurudia mitihani yao kwa gharama kubwa!!
Watoto wengi ni wale wanaotokea katika familia masikini ambazo hata mkate wa kila siku ni matatizo makubwa. Lakini cha kushangaza watoto hawa wasukumizwa mbali na mifumo ya Elimu kana kwamba wao si sehemu ya jamii yetu hii!! Nasema haya kwa uchungu mkubwa kwa sababu, Kila mwaka Baraza la mitihani limekuwa likikusanya pesa nyingi kutoka kwa watoto au watu wazima wanaotaka kurudia mitihani yao.
Wengi wa watahiniwa hao ni hao watoto wa shule za kata ambao kwa wao kufaulu inategemea sana kudra za Mwenyezi Mungu kwa kuwa mfumo umewatenga! Kwani mazingira yao ya kujifunzia hayawapi uhakika wa kufaulu. Kufuatia hali hii hawa watoto wamekuwa wakitegea hii mitihani ya kurudia au utahiniwa wa kujitegemea. Kutokana na hali mbaya kiuchumi ya hawa watoto na hata watu wazima wanaorudia mitihani yao huhitaji muda wakutosha kujiandaa ili kuweza kumudu kulipia gharama za kurudia mitihani.
Pia watahiniwa hao watarajiwa huhitaji huruma kutoka kwa mtu yeye ya kuwapunguzia gharama ili suala lao la kufanya mitihani lisiwe gumu kiasi cha kuwaganya washidwe kufanya hivyo, hasa kukizingatia nchi yetu licha ya kuwa na raslimali nyingi ina hitaji wasomi watakao wenzesha matumizi bora ya rasilimali za nchi kwa manufaa y watanzania.
Lakini cha kushangaza kila kukicha hali ndo inazidi kuwawia vigumu watu hawa. Kwanza muda wa kujiandikisha kufanya mitihani umepungua tangu mie miezi mitatu hadi miwili, hili peke yake linawafungia wengine milango ya kufanya mitihani! Ikiwa huyu motto wa masikini atakuwa hana pesa ndani ya kipindi hicho basi system itakuwa imeshamtema mpaka mwaka mwingine.
Miaka yote watahiniwa hupewa muda mzuri wa kujiandaa kutoka siku ambayo mwezi wa pili hasi mwezi wa nne mwishoni! Mwaka huu ambopo sisi tulitarajia serikali ingetoa fursa (muda) ya kutosha kwa hawa watoto ambao kwa makusudi wamefelishwa lakini imebana muda wa watu kujiandi andikisa kutoka muda wa miezi mitatu hadi miezi miwili.
Pia tulitegemea Serikali ingepunguza hata gharama ili watu hawa wamudu kujaribu bahati yao, lakini mambo ni kinyume kabisa na hivyo ndo kwanza gharama zimeongezeka!! Wameongeza kipengele cha kujiandikisha kwa kuumia mtandao. Kwa hapa Arusha unatakiwa kulipa sh, 3500 ili uweze kujiandikisha kwa njia hiyo lakini gharama za kulipia ule mtihani zinakuwa ziko palepale. Pia katika kufanya hivo hawaakupi kufanya usajili mwenyewe hata kama una uelewa wa kutumia mtandao. Watakufichia neno la siri ili usiweze kufanya hivyo mwenyewe. sasa mimi najiuliza ikiwa watahiniwa hao wanalipa sh. 50, 00 pesa hiyo haitoshi kuwasaidia kusajili mpaka watake tena pesa zingine kutoka kwa hawa watu?
Na kama suala la kuwasaidia kuandikisha ni gumu kwa nini mtu asiruhusiwe kujiandiishwa mwenyewe? Mimi naona serikali yetu imekusudia kabisa kuwaacha hawa watoto wawe nje ya mfumo! Jambo lingine ni vituo vya kufanyia mitihani vituo hivyo vimekuwa vikiopanga bei zao wenyewe bila mtu yeyote kuwadhibiti. Kituo kunamgharimu kijana huyu kati ya dh. 25,000 hadi 50,000 Je serikali hailioni hili? Au au tuamini hivyo kwamba wao kushidwa kwa vijana hawa ndio lengo lao? Ebu tuangalie Jeduali hapo chini tuone ni kwa kiasi gani inakuwa ngumu kawa vijana hawa kuendelea na masomo yao.
Kitu kinacholipiwa
Picha
Gharama za kutuma pesa
Kituo
Gharama za mitihani
Jumla ya kwanza
Kwa maisha ya watanzani wengi hasa waishio vijijini inaonekana kabisa hawatakiwi kuendelea na masomo yao! Kwani kipato cha wazazi wao ni kidogo sana! unapofupisha muda wa kujiandikisha, unapoongeza gharama za kujiandikisha, unapolazimisha wajiandikishe kwa mtandao kwa gharama zingine kuacha ile pesa anayolipa Baraza la mitihani, na unapoacha vituo vya mitihani vijipangie bei vyenyewe ni kwamba unawazuia hawa wa.
Wana JF Naomba michango yenu ya kimawazo.
Wakati bado watu wanalipigia kelele jambo la kufeli kwa kiwango kikubwa kwa wahitimu wa kidato cha nne, hata wengi kuomba vijana hao warudie mitihani yao Baraza la mitihani Tanzania limeonekana kupingana na dhana hiyo waziwazi.
Ndugu wana JF ikumbukwe kwamba kimbilio la mwisho la vijana hao na wengine wengi walioadhiriwa na mfumo mbovu wa elimu wa hapa nchi ni kurudia mitihani yao kwa gharama kubwa!!
Watoto wengi ni wale wanaotokea katika familia masikini ambazo hata mkate wa kila siku ni matatizo makubwa. Lakini cha kushangaza watoto hawa wasukumizwa mbali na mifumo ya Elimu kana kwamba wao si sehemu ya jamii yetu hii!! Nasema haya kwa uchungu mkubwa kwa sababu, Kila mwaka Baraza la mitihani limekuwa likikusanya pesa nyingi kutoka kwa watoto au watu wazima wanaotaka kurudia mitihani yao.
Wengi wa watahiniwa hao ni hao watoto wa shule za kata ambao kwa wao kufaulu inategemea sana kudra za Mwenyezi Mungu kwa kuwa mfumo umewatenga! Kwani mazingira yao ya kujifunzia hayawapi uhakika wa kufaulu. Kufuatia hali hii hawa watoto wamekuwa wakitegea hii mitihani ya kurudia au utahiniwa wa kujitegemea. Kutokana na hali mbaya kiuchumi ya hawa watoto na hata watu wazima wanaorudia mitihani yao huhitaji muda wakutosha kujiandaa ili kuweza kumudu kulipia gharama za kurudia mitihani.
Pia watahiniwa hao watarajiwa huhitaji huruma kutoka kwa mtu yeye ya kuwapunguzia gharama ili suala lao la kufanya mitihani lisiwe gumu kiasi cha kuwaganya washidwe kufanya hivyo, hasa kukizingatia nchi yetu licha ya kuwa na raslimali nyingi ina hitaji wasomi watakao wenzesha matumizi bora ya rasilimali za nchi kwa manufaa y watanzania.
Lakini cha kushangaza kila kukicha hali ndo inazidi kuwawia vigumu watu hawa. Kwanza muda wa kujiandikisha kufanya mitihani umepungua tangu mie miezi mitatu hadi miwili, hili peke yake linawafungia wengine milango ya kufanya mitihani! Ikiwa huyu motto wa masikini atakuwa hana pesa ndani ya kipindi hicho basi system itakuwa imeshamtema mpaka mwaka mwingine.
Miaka yote watahiniwa hupewa muda mzuri wa kujiandaa kutoka siku ambayo mwezi wa pili hasi mwezi wa nne mwishoni! Mwaka huu ambopo sisi tulitarajia serikali ingetoa fursa (muda) ya kutosha kwa hawa watoto ambao kwa makusudi wamefelishwa lakini imebana muda wa watu kujiandi andikisa kutoka muda wa miezi mitatu hadi miezi miwili.
Pia tulitegemea Serikali ingepunguza hata gharama ili watu hawa wamudu kujaribu bahati yao, lakini mambo ni kinyume kabisa na hivyo ndo kwanza gharama zimeongezeka!! Wameongeza kipengele cha kujiandikisha kwa kuumia mtandao. Kwa hapa Arusha unatakiwa kulipa sh, 3500 ili uweze kujiandikisha kwa njia hiyo lakini gharama za kulipia ule mtihani zinakuwa ziko palepale. Pia katika kufanya hivo hawaakupi kufanya usajili mwenyewe hata kama una uelewa wa kutumia mtandao. Watakufichia neno la siri ili usiweze kufanya hivyo mwenyewe. sasa mimi najiuliza ikiwa watahiniwa hao wanalipa sh. 50, 00 pesa hiyo haitoshi kuwasaidia kusajili mpaka watake tena pesa zingine kutoka kwa hawa watu?
Na kama suala la kuwasaidia kuandikisha ni gumu kwa nini mtu asiruhusiwe kujiandiishwa mwenyewe? Mimi naona serikali yetu imekusudia kabisa kuwaacha hawa watoto wawe nje ya mfumo! Jambo lingine ni vituo vya kufanyia mitihani vituo hivyo vimekuwa vikiopanga bei zao wenyewe bila mtu yeyote kuwadhibiti. Kituo kunamgharimu kijana huyu kati ya dh. 25,000 hadi 50,000 Je serikali hailioni hili? Au au tuamini hivyo kwamba wao kushidwa kwa vijana hawa ndio lengo lao? Ebu tuangalie Jeduali hapo chini tuone ni kwa kiasi gani inakuwa ngumu kawa vijana hawa kuendelea na masomo yao.
Kitu kinacholipiwa
Gharama yake
3,000
5,500
2,5000 – 40,000
35,00 – 50,0000
68,500
98,500
Kwa maisha ya watanzani wengi hasa waishio vijijini inaonekana kabisa hawatakiwi kuendelea na masomo yao! Kwani kipato cha wazazi wao ni kidogo sana! unapofupisha muda wa kujiandikisha, unapoongeza gharama za kujiandikisha, unapolazimisha wajiandikishe kwa mtandao kwa gharama zingine kuacha ile pesa anayolipa Baraza la mitihani, na unapoacha vituo vya mitihani vijipangie bei vyenyewe ni kwamba unawazuia hawa wa.
Wana JF Naomba michango yenu ya kimawazo.