Mwiba
JF-Expert Member
- Oct 23, 2007
- 7,607
- 1,744
Kama ulikuwa bado unaburuzwa na vyama vingine visivyo na msimamo basi hujachelewa ,Hapa Tanzania kipo Chama kimoja tu ambacho ndicho Chama ambacho kila Mtanzania anatakiwa ajiunge nacho na kuendeleza upinzani wa kweli dhidi ya serikali iliyopo madarakani ,ukweli huu umeonekana huko Pemba na karibu utajitokeza na Unguja ,kuweza kufikia kuzuia uandikishaji wa wapiga kura hewa ,umoja uliopatikana Pemba ndio umoja unaoogopwa na utawala wa CCM kutokea hapa Tanzania,kiasi cha kuifanya serikali ya Kikwete isijue inafanya nini ,ilianza na kupeleka mapolisi kibao ,ikafuatiwa na kupelekwa majeshi na vifaa vya kivita ,kumbuka chaguzi zilizopita walionekana majeshi wakiwa na marocket launcher ,leo mambo yamezidi wameongezea na vifaru ,fikiria hiyo ni Pemba tu peke yake inauhangaisha utawala wa CCM ,je ikiwa upinzani uliopo Pemba utaenea Tanzania nzima ?
WaTanzania ninawaeleza kuwa hakuna na hatuna haja ya kuwa na misusuru mirefu ya vyama vya upinzani ,ni lazima tuelewe kuwa misururu hii inaletwa na huyu Sultani CCM ili kuwagawa wananchi katika makundi makundi na hivyo kusababisha kuzigawa kura za wananchi walio wengi.
Ndugu waTanzania ni lazima tuone ukweli na tuukubali kuwa Chama cha kweli cha Upinzani Tanzania ni CUF ,mbinu zinazofanywa na Chama tawala kukidhoofisha Chama hiki ni kubwa sana na CCM inatumia mabilioni ya fedha katika kuhakikisha kuwa kinafanikiwa lakini msimamo ambao unatokana na idadi ndogo ya WaTanzania unasababisha kushindwa kwa mbinu za CCM katika kuimaliza CUF ,msimamo huu bado unahitajia WaTanzania wengine kujiunga nao katika kuelekea safari ya kujikomboa kutoka kwa utawala wa Sultani CCM.
Tusikubali maneno yanayosemwa kuwa CUF kina nguvu zaidi Pemba,hilo halina ukweli ndani yake ni kutaka kuzidisha hila za kuwafanya WaTanzania waamini kuwa CUF ni chama cha upande mmoja au ni Chama cha watu fulani tu ,waPemba ,kauli hizo ni nonesense na kila Mtanzania mwenye akili timamu inafaa azitupilie mbali.
Ni Mtanzania gani ambae ana akili timamu utamuaminisha kuwa CUF haikupata mbunge hata mmoja katika uchaguzi mkuu uliopita hapa Tanzania ? Hila na njama ambazo ziliwagusa viongozi wakuu wa vyama vingine ambao walipiga kura na kujipigia kura ,hawakuziona hata ile kura ya mtu na mkewe zilipokwendea ,na hivyo ndivyo ilivyofanyiwa CUF kwa ujumla ni jambo ambalo lipo wazi kabisa ,kuwa mbinu za CCM ni kubwa sana juu ya kuona CUF haipati mbunge hata mmoja na wale wengine wanaopata huwa ni kama ruzuku inayotolewa ili kuwaziba macho wananchi. Ukweli ni kuwa matokeo ya uchaguzi mzima ni ya kupanga. Na kule ambako wananchi wamesimama kidete upangaji haukuwezekana.
Nani anaweza kuamini kuwa Lipumba alishinda uchaguzi Mkuu uliopita hapa Tanzania ? Inakuwa ni vigumu ndivyo ilivyofanywa iwe na ionekane hivyo kuwa hakushinda na chama chake hakikupata hata mbunge mmoja hapa Tanzania Bara ,ni hujuma nzito sana iliyofanywa ambayo inaweza kuiweka nchi matatani kwa siku zijazo ,maana watu wakiwa na msimamo kama uliopo Pemba wa kupinga kudhulumiwa haki yao na kuburuzwa ,inakuwa ni hatari sana.
Hivi sasa kuna mambo yanakuwa twisted ,kuna mambo ya muungano sijui mambo ya mafuta ,tunaona malumbano kati ya viongozi wa CCM bara na wenzao wa CCM visiwani ,hapa hamna lolote ni mchezo wanawachezea waTanzania ,ni lazima mulielewe hilo ,hawa watu kuwepo madarakani wanategemeana kwa asilimia mia moja ,hivyo hawawezi kuwa wapumbavu wagombanie au wagombane kwa mafuta au mambo ya Muungano ,hayo hayawezi kutokea na kutekelezeka ndani ya Chama kimoja cha CCM ni ulaghai mkubwa usiowahi kufanywa na kufanyiwa wananchi ,kwa lugha nyingine panafanywa usanii.
Matokeo yake ni WaTanzania bara kuona WaZanzibari wanauchoyo na WaZanzibari kuona wajamaa wanataka kutumeza ,hapa hakuna kitu ila ni game played by CCM ,ukiangalia utaona CCM wanajipandisha chati kwa kujionyesha kuwa wataulinda muungano na pia mafuta na gesi yapo chini ya Muungano na serikali ya Mapinduzi haina ubavu sijui na hili na lile ,wakati wale wa zanzibari nao wanatingisha kuwa mali ya Zanzibar ni kwa Wazanzibari ,maigizo yote hayo bado Mtanzania unaona kweli sasa sio mchezo WaZanzibari hawatuchezei na wale wenzangu mie kule Zenji nao wanaona na kuambiana unasikia umeona Waziri alivyosema wabara hawayajui Mapinduizi waache watuchezee tu, jamii nzima inapindishwa na kuwekwa katika makundi mawili ambayo yote ni CCM ,hivi unategemea nini ?
Ni lazima tuamke ili kuepuka siasa hizi anazotupeleka Sultani CCM ni lazima tuiunge mkono CUF ili turithi mapambano yalioanzshwa na WaPemba ,mapambano ambayo yanatakiwa kuungwa mkono na WaTanzania wote chini ya bendera moja ya CUF na si vinginevyo.
Pemba kwa walipofikia ni pakupigiwa mfano na wamefanikiwa kutoa tension kwa maTaifa ya nje na hata kufikia kwa EAC kusema inaweza kuifukuza Tanzania katika umoja huo ikiwa itaonekana inavunja haki na misingi ya demokrasia na inaangaliwa namna mambo yanavyotokea Pemba ,kwa vyovyote vile naweza kusema Jakaya Mrisho Kikwete yupo matatani na huo ndio ukweli.
Itakuwaje ikiwa WaTanzania wote watakuwa na msimamo kama waliokuwa nao watu wa Pemba ? Pemba mambo ni makubwa kulivyo yanavyoripotiwa tulisikia kuwa waandikishaji wa wapiga kura wameondoka kutokana na fujo ukweli ni kuwa WaPemba wamesusia kwenda kuandikisha baada ya kuona hila zinazofanywa ni mbaya na hazina mshiko zaidi ya ubabaishaji wa CCM,imebidi kambi za kuandikisha zifungwe na weshasema haendi kuandikisha mtu kama kila aliefikia umri wa kupiga kura amekubaliwa kuandikwa bila ya kipingamizi chochote kile.
WaTanzania ninawaeleza kuwa hakuna na hatuna haja ya kuwa na misusuru mirefu ya vyama vya upinzani ,ni lazima tuelewe kuwa misururu hii inaletwa na huyu Sultani CCM ili kuwagawa wananchi katika makundi makundi na hivyo kusababisha kuzigawa kura za wananchi walio wengi.
Ndugu waTanzania ni lazima tuone ukweli na tuukubali kuwa Chama cha kweli cha Upinzani Tanzania ni CUF ,mbinu zinazofanywa na Chama tawala kukidhoofisha Chama hiki ni kubwa sana na CCM inatumia mabilioni ya fedha katika kuhakikisha kuwa kinafanikiwa lakini msimamo ambao unatokana na idadi ndogo ya WaTanzania unasababisha kushindwa kwa mbinu za CCM katika kuimaliza CUF ,msimamo huu bado unahitajia WaTanzania wengine kujiunga nao katika kuelekea safari ya kujikomboa kutoka kwa utawala wa Sultani CCM.
Tusikubali maneno yanayosemwa kuwa CUF kina nguvu zaidi Pemba,hilo halina ukweli ndani yake ni kutaka kuzidisha hila za kuwafanya WaTanzania waamini kuwa CUF ni chama cha upande mmoja au ni Chama cha watu fulani tu ,waPemba ,kauli hizo ni nonesense na kila Mtanzania mwenye akili timamu inafaa azitupilie mbali.
Ni Mtanzania gani ambae ana akili timamu utamuaminisha kuwa CUF haikupata mbunge hata mmoja katika uchaguzi mkuu uliopita hapa Tanzania ? Hila na njama ambazo ziliwagusa viongozi wakuu wa vyama vingine ambao walipiga kura na kujipigia kura ,hawakuziona hata ile kura ya mtu na mkewe zilipokwendea ,na hivyo ndivyo ilivyofanyiwa CUF kwa ujumla ni jambo ambalo lipo wazi kabisa ,kuwa mbinu za CCM ni kubwa sana juu ya kuona CUF haipati mbunge hata mmoja na wale wengine wanaopata huwa ni kama ruzuku inayotolewa ili kuwaziba macho wananchi. Ukweli ni kuwa matokeo ya uchaguzi mzima ni ya kupanga. Na kule ambako wananchi wamesimama kidete upangaji haukuwezekana.
Nani anaweza kuamini kuwa Lipumba alishinda uchaguzi Mkuu uliopita hapa Tanzania ? Inakuwa ni vigumu ndivyo ilivyofanywa iwe na ionekane hivyo kuwa hakushinda na chama chake hakikupata hata mbunge mmoja hapa Tanzania Bara ,ni hujuma nzito sana iliyofanywa ambayo inaweza kuiweka nchi matatani kwa siku zijazo ,maana watu wakiwa na msimamo kama uliopo Pemba wa kupinga kudhulumiwa haki yao na kuburuzwa ,inakuwa ni hatari sana.
Hivi sasa kuna mambo yanakuwa twisted ,kuna mambo ya muungano sijui mambo ya mafuta ,tunaona malumbano kati ya viongozi wa CCM bara na wenzao wa CCM visiwani ,hapa hamna lolote ni mchezo wanawachezea waTanzania ,ni lazima mulielewe hilo ,hawa watu kuwepo madarakani wanategemeana kwa asilimia mia moja ,hivyo hawawezi kuwa wapumbavu wagombanie au wagombane kwa mafuta au mambo ya Muungano ,hayo hayawezi kutokea na kutekelezeka ndani ya Chama kimoja cha CCM ni ulaghai mkubwa usiowahi kufanywa na kufanyiwa wananchi ,kwa lugha nyingine panafanywa usanii.
Matokeo yake ni WaTanzania bara kuona WaZanzibari wanauchoyo na WaZanzibari kuona wajamaa wanataka kutumeza ,hapa hakuna kitu ila ni game played by CCM ,ukiangalia utaona CCM wanajipandisha chati kwa kujionyesha kuwa wataulinda muungano na pia mafuta na gesi yapo chini ya Muungano na serikali ya Mapinduzi haina ubavu sijui na hili na lile ,wakati wale wa zanzibari nao wanatingisha kuwa mali ya Zanzibar ni kwa Wazanzibari ,maigizo yote hayo bado Mtanzania unaona kweli sasa sio mchezo WaZanzibari hawatuchezei na wale wenzangu mie kule Zenji nao wanaona na kuambiana unasikia umeona Waziri alivyosema wabara hawayajui Mapinduizi waache watuchezee tu, jamii nzima inapindishwa na kuwekwa katika makundi mawili ambayo yote ni CCM ,hivi unategemea nini ?
Ni lazima tuamke ili kuepuka siasa hizi anazotupeleka Sultani CCM ni lazima tuiunge mkono CUF ili turithi mapambano yalioanzshwa na WaPemba ,mapambano ambayo yanatakiwa kuungwa mkono na WaTanzania wote chini ya bendera moja ya CUF na si vinginevyo.
Pemba kwa walipofikia ni pakupigiwa mfano na wamefanikiwa kutoa tension kwa maTaifa ya nje na hata kufikia kwa EAC kusema inaweza kuifukuza Tanzania katika umoja huo ikiwa itaonekana inavunja haki na misingi ya demokrasia na inaangaliwa namna mambo yanavyotokea Pemba ,kwa vyovyote vile naweza kusema Jakaya Mrisho Kikwete yupo matatani na huo ndio ukweli.
Itakuwaje ikiwa WaTanzania wote watakuwa na msimamo kama waliokuwa nao watu wa Pemba ? Pemba mambo ni makubwa kulivyo yanavyoripotiwa tulisikia kuwa waandikishaji wa wapiga kura wameondoka kutokana na fujo ukweli ni kuwa WaPemba wamesusia kwenda kuandikisha baada ya kuona hila zinazofanywa ni mbaya na hazina mshiko zaidi ya ubabaishaji wa CCM,imebidi kambi za kuandikisha zifungwe na weshasema haendi kuandikisha mtu kama kila aliefikia umri wa kupiga kura amekubaliwa kuandikwa bila ya kipingamizi chochote kile.