Huu ni uzalendo au unyama?

Jun 16, 2009
64
0
Ndugu wana Jamii forum. Kwa masikitiko makubwa napenda kuwaeleza kwa uchache tu ufisaadi mwingine uliojitokeza hivi karibuni baada ya muheshimiwa DR Sheni kuchaguliwa kuwa rais wa Zanzibar na kufanya ziara rasmi ya kiserkali nchini Ungereza. Muheshimiwa huyo kwa mujibu wa nusa nusa yangu niliyoipata kutoka kwa affisa mmoja wa ubalozi wa Tanzania Bond Stree/ Statford avenu central London alikuwa na ujumbe wa watu 33 na wote walipangiwa makazi yao ya muda kwenye hoteli ya kifahari. Gharama za chakula, vinywaji na malazi kwa kila mtu mmoa ilikuwa ni sterling pound(£3000) kwa siku. Hii ni sawa na na Tsh 7500000 kwa siku moja kwa kila mtu. Kwa watu wote 33 ni sawa na Sh 247500000 na walikaa jijini Londoni kwa muda wa wiki moja. Kwa hivyo walitumia jumla ya Tsh 1732500000. Pesa hizi hazihusishi malipo ya posh(allowance per day). Je tujiulize kwa nafasi yake mheshimiwa DR SHENI watu 33 wote hao wa nini na alikwenda london kufanya nini? HIVI LINI WAAFRIKA TUTAACHA KASUMBA HII YA UBINAFIS NA KUFIKIRIA MAENDELEO YA NCHI ZETU? WATU 5 TU WANGELITOSHA KUFATANA NAYE NA SIO WANAKIJIJI WOTE WA KWAO MTAMBWE.
 
Zanzibar siku hizi kuna hiyo ndoa ya ccm na cuf kwahiyo msafara wowote wa kiongozi wa serikali ni lazima uwe na wajumbe wa vyama vyote viwili na ndio maana misafara ya wazanzibari viongozi inakuwa na wajumbe wengi na gharama zao ni lazima zitakuwa za kutisha;hasa wanapokwenda ughaibuni. Hizo ndizo faida za ndoa ya ccm na cuf wa wanavisiwani!
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom