Huwa najiuliza ni kwanini viongozi wa nchi za Kiarabu pamoja na Mataifa makubwa kama China hupenda kutumia Lugha zao hata wanapoalikwa kwenye mikutano mikubwa ya Kimataifa, huwa kuna mkalimani anatafsiri, sisi watanzania tuna lugha yetu ya kiswahili na ninaamini kwamba viongozi wetu wengi hata wananchi ni wepesi sana kwa hii lugha kuliko lugha za kigeni. Kwa mfano kiongozi akikosea uandishi wa lugha ya kigeni huzarauliwa sana ingawa mara nyingi ujumbe unaeleweka je huu sio utumwa wa kifikra? kuna tatizo gani kiongozi akiandaa hotuba yake kwa lugha ya kiswahili alafu mkalimani akatafsiri kama ilivyo kwa viongozi wa nchi za kiarabu na baadhi ya nchi zilizoendelea? Sijawahi kumsikia Ghadafi akiongea kiingereza hata kama amefanya ziara katika mataifa makubwa. Tafakari.