Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,319
- 33,125
Undumilakuwili wa Afande Sele waanikwa
Undumilakuwili wa Afande Sele waanikwa
Msanii Suleiman Msindi Afande Sele, ameanikwa kwa tabia yake ya undumilakuwili.
Picha za video, zinazomuonesha Afande akiwatukana Clouds FM, zimeanikwa mtandaoni kuthibitisha jinsi msanii huyo alivyo ndumilakuwili.
Hivi karibuni, Afande alisaliti harakati za wasanii wanaopambana katika mradi wa Anti Virus na kwenda kuimba kwenye tamasha la Clouds, jambo ambalo limewaudhi wadau wengi.
Katika video hiyo, Afande anatoa matusi makali kuwa Clouds wanataka kumuua kimuziki, akasema kwamba badala ya kusikiliza Clouds watu wasikilize Magic FM.
Katika mashambulizi hayo, Afande aliponda pia kuwa watangazaji wengine wa Clouds walikuwa watoto wakati yeye anakuwa Mfalme wa Rhymes mwaka 2004, hivyo akasisitiza hawambabaishi.
Hata hivyo, juzikati Afande alitosa tamasha la Vinega, Ustawi wa Jamii na kwenda kwenye shoo ya Clouds aliokuwa anawatukana kwamba wanamuua kimuziki.
Mbali na kwenda kwenye shoo, Afande aliponda tamasha la Vinega lakini mwisho wa mchezo, Vinega waliibuka kidedea kwa kukusanya nyomi la hatari.
Hii ndio Bangi kwa wingi ? au ndio show ya muzik ya kibongo?
Undumilakuwili wa Afande Sele waanikwa
Msanii Suleiman Msindi Afande Sele, ameanikwa kwa tabia yake ya undumilakuwili.
Picha za video, zinazomuonesha Afande akiwatukana Clouds FM, zimeanikwa mtandaoni kuthibitisha jinsi msanii huyo alivyo ndumilakuwili.
Hivi karibuni, Afande alisaliti harakati za wasanii wanaopambana katika mradi wa Anti Virus na kwenda kuimba kwenye tamasha la Clouds, jambo ambalo limewaudhi wadau wengi.
Katika video hiyo, Afande anatoa matusi makali kuwa Clouds wanataka kumuua kimuziki, akasema kwamba badala ya kusikiliza Clouds watu wasikilize Magic FM.
Katika mashambulizi hayo, Afande aliponda pia kuwa watangazaji wengine wa Clouds walikuwa watoto wakati yeye anakuwa Mfalme wa Rhymes mwaka 2004, hivyo akasisitiza hawambabaishi.
Hata hivyo, juzikati Afande alitosa tamasha la Vinega, Ustawi wa Jamii na kwenda kwenye shoo ya Clouds aliokuwa anawatukana kwamba wanamuua kimuziki.
Mbali na kwenda kwenye shoo, Afande aliponda tamasha la Vinega lakini mwisho wa mchezo, Vinega waliibuka kidedea kwa kukusanya nyomi la hatari.
Hii ndio Bangi kwa wingi ? au ndio show ya muzik ya kibongo?