Mujumba
JF-Expert Member
- Jan 20, 2011
- 853
- 306
nilishtuka sana niliposikia mbunge wa moshi mjini mzee Ndesamburo almaharufu kama ndesapesa kamwaga milion 20 kuchangia chama chake cha CDM! KWANINI NILISHTUKA? mzee ndesamburo kupitia kampuni yake ya utalii amekuwa akiwatumikisha vijana wengi wa moshi mjini kupandisha watalii mlima kwa ujira mchache sana,wengi wao hawana mikataba ya kazi na hivyo kushundwa kwenda pa kudai maslahi, vibarua hao wamekuwa wakiranda randa katika hotel ya mzee huyo iitwayo KEYS HOTEL kufatilia ujira wao ambao umekuwa ukicheleshwa bila sababu ya msingi! sasa huyu babu anawezaje kumwaga mamilion kwa chama ilhali vijana wanaoumuingizia mamilion hayo wakiishi katika dimbwi la umaskini? HUU NI UNAFIKI