Hussein Tuwa vs Eric Shigongo (Riwaya)

Ulishahi kusoma hadithi za Musiba, kama sanda ya jambazi, kikomo no 1 na no 2 na vingine vingi alivokua akitunga kabla ya kuzuiwa na serikali, ama wewe ni kizazi kipya?

kizazi cha kipya
 
Wewe kujiita "TIGGA MUMBA" tayari inaonyesha nani unamkubali.

Wamfahamu JADU MFAUME? Nimekukumbusha ee?

Aisee ni nzur mnoo
Nilikua mpaka nalala kitabu kipo mkononi ...nafanya shughuli zangu fasta tena najifungia kimyaa utadhan nachek muvi
 
Namshukuru Tuwa, amenifanya niache kusoma stori za udaku. Shigongo uongo umezid af uhalisia amnaa kwenye mengi
 
Hussein tuwa nimeshamsoma kwenye mkimbizi na mtuhumiwa jamaa ana kipaji,huyu shigongo n msanii 2 hadithi zake za kutunga kma script y bongo movie uwongo mwingi ukimsoma tuwa unaelewa riwaya zake kwa mtiririko murua
 
Ulishahi kusoma hadithi za Musiba, kama sanda ya jambazi, kikomo no 1 na no 2 na vingine vingi alivokua akitunga kabla ya kuzuiwa na serikali, ama wewe ni kizazi kipya?
Kwa nini alizuiwa?
 
Tuwa buana. Nimejibia kabisa kitabu chake cha Mfadhili form six yangu. Ghkaaa!!! Mzee wa koma hata hamuingii tuwa. Shigongo s kitu now days
 
Unakosea sana kusema Tuwa alibahatisha,hii inatokana na kuwa labda hujafuatilia sana riwaya zake.

Jamaa sio mmiliki wa gazeti lolote so huwa anatoa kwenye gazeti la kiu kwa kupokezana either na Beka Mfaume au Amri Bhawji.

Mfano wa riwaya ambazo nimezisoma za Tuwa ni
1.Mkimbizi
2.Mtuhumiwa
3.Utata wa 9/12
4.Mdunguaji
5.Bondia
6.Mfadhili (tena hiki kitabu kilichukua hadi tuzo ya MacMillan na kikawa kinatumika mashuleni kwa wale wa wanaosoma Kiswahili advance)

Nimesoma hadithi za Shigongo nyiingi saana ila uwezo wa Hussein Issa Tuwa upo juu sana.Tafuta kitabu chake hata kimoja nakuhakikishia hutojuta na nnauhakika utajiunga katika chama cha Tuwa ktk riwaya

Ahsante.

Mm hapa shahidi wako, mfadhili nimejibia mtihani wangu wa kidato cha sita 2012
 
Na Mtuhumiwa kitabu kimetoka jana..

Kwa wanaotaka wawasiliane na "0766 000 663" na "0655428 085"
 
Tuwa ni kiboko yao hadi msakwa anapokuwa msaka ndan ya mkimbiz ilikuwa balaa
 
Daa ile mkimbiz ilikuwa balaa, nilikuwa mteja wa kiu bila kupenda. Kaandika riwaya chache ila mkali Hana mfanowe hapa tz
 
Na Mtuhumiwa kitabu kimetoka jana..

Kwa wanaotaka wawasiliane na "0766 000 663" na "0655428 085"
Hivi hii mtuhumiwa ya sasa 2015 ina tofauti na mtuhumiwa aliyokua ametoa miaka ya nyuma?
Maana mi mwenyeww nimeshangaa kua mtuhumiwa imetoka wakati kitabu hiki kilikuwepo?
Naomba nijibu plZ maana kesho nataka nikachukue copy yangu fa6 pale biafra..

Tuwa ni tsunami ktk liwaya za kibongo
 
Shigongo ni sio muandishi bali ni mkalimani anayecopy kazi za watu na kutafsiri kwa kiswahili kisha huweka jina lake kama yeye ndo kaandika riwaya hiyo.

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums

Mkuu unaweza kuthibitisha hilo au chuki tu izo?
 
Hussein tuwa ni best aisee
bahati mbaya sana sijazisoma hizi unazozisemea za mtuhumiwa na mkimbizi ila mwaka 2004-2005 nilisoma hadithi zake mbili znaitwa
utata wa 9/12
na mdunguaji

yaani nashindwa hata kuzielezea ni balaa shigongo hamna kitu

Utata 9/12 hatari sana na JADU MFAUME
 
Hivi hii mtuhumiwa ya sasa 2015 ina tofauti na mtuhumiwa aliyokua ametoa miaka ya nyuma?
Maana mi mwenyeww nimeshangaa kua mtuhumiwa imetoka wakati kitabu hiki kilikuwepo?
Naomba nijibu plZ maana kesho nataka nikachukue copy yangu fa6 pale biafra..

Tuwa ni tsunami ktk liwaya za kibongo

KWA maelezo yake ni kuwa mtuhumiwa cha sasa kakifanyia marekebisho kidogo sana lakini ndio anakitoa kwa Mara ya kwanza kwenye kitabu na ndio RIWAYA yake ya kwanza kuiandika lakini ndio RIWAYA yake ya mwisho kutoa kitabu.
sijui kama utakuwa umenisoma hapo kuna sababu nyingi sana zilizokuwa nje ya uwezo wake ndio zilisababisha.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom