Mfahamu Hussein Shekilango, aliyepewa jina la barabara jijini Dar (kuanzia Bamaga - Urafiki)

JokaKuu

Platinum Member
Jul 31, 2006
30,442
54,993
image.jpeg

Hivi kuna yeyote amewahi kujiuliza Shekilango ni nani mpaka barabara kubwa jijini DSM ikapewa jina lake?

Naomba mwenye historia na wasifu wa Shekilango atuwekee. Naamini siko peke yangu ambaye hatuna taarifa zake.

=====

Michango ya wadau...

Kaka Joka Kuu,
Mzee Hussein Shekilango aliwahi kuwa Mbunge wa Korogwe na Baadaye alikuwa waziri Wa Nchi Ofisi Ya Waziri Mkuu anayeshughulikia mambo ya Utawala (Nafikiri utakuwa unawafahamu watumishi wa namna hii). Mzee Shekilango alikuwa mtu wa karibu sana na Rais Nyerere (RIP) na Waziri Mkuu wa wakati huo Mh.Edward Sokoine (RIP).

Ilikuwa mwezi May/1980 Mzee Shekilango pamoja na watumishi wengine wa serikali na Wanajeshi wa Jeshi la Ulinzi walipata ajali ya ndege huko Arusha na kufariki. Mzee Shekilango na ujumbe wake walikuwa wanasafiri kwa ndege ndogo kutoka Arusha kwenda Entebbe. Ikumbukwe kuwa kipindi hicho tulikuwa katika vita na Utawala wa Amin,na inasemekana Mzee Shekilango alikuwa ametumwa na Rais kwa kazi maalumu huko Uganda.

Sina Ufahamu ni nani alipendekeza Jina la Barabara ile ya Shekilango (Mwenge/sinza) lakini Shekilango anahesabiwa kama shujaa,kwa sababu alikufa kazini na katika shughuli za Vita vya Kagera. Mtoto wa Kiume wa Marehemu Shekilango alikuwa mmojawapo ya wanachama wa CCM 19 walioomba Ubunge wa Korogwe -Magharibi katika Uchaguzi Mkuu wa 2005.

View attachment 448709
JE WAJUA?

HUSSEIN RAMADHANI SHEKILANGO, SHUJAA ALIYEKUFA AKIIJENGA UGANDA

Jijini Dar es salaam kuna Barabara Mashuhuri kama 'Shekilango Road', ikianzia maungio ya Barabara ya Morogoro eneo la Nyumba za NHC mkabala na Kiwanda cha Urafiki, ikipitia Mitaa yote ya Sinza na kuishia Maungio ya Barabara ya Ali Hassan Mwinyi kituo cha Bamaga.

Ni watanzania wachache wajuao kuwa Barabara hiyo ya Shekilango imepewa jina Maalum kwaajili ya heshima ya Ndugu Hussein Ramadhani Shekilango, aliyekuwa Waziri wa Nchi katika Ofisi ya Waziri Mkuu, akishughulika zaidi na mambo ya Utawala, wakati wa Uongozi wa Rais Julius Nyerere na Makamo wake Aboud Jumbe Mwinyi.

Hussein Shekilango alichaguliwa na Wananchi wa kwao kuwa Mbunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wa Jimbo la Korogwe Mjini, Mkoani Tanga katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 1975, akiachia nafasi yake ya Zamani ya Meneja Mkuu wa Shirika la Usagishaji Nchini (NATIONAL MILLING CORPORATION).

Mwaka huo huo akachaguliwa na Rais Julius Nyerere kuwa Waziri wa Nchi katika Ofisi ya Waziri Mkuu (Utawala) akiwa chini ya Makamu wa Pili wa Rais na Waziri Mkuu, ndugu Rashid Mfaume Kawawa.

Mwaka 1977 yalifanyika Mabadiliko makubwa ya Baraza la Mawaziri Nchini, aliyekuwa Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kulinda Taifa, Ndugu Edward Moringe Sokoine aliteuliwa kuwa Waziri Mkuu akichukua nafasi ya Kawawa, Shekilango akabakishwa katika nafasi yake lakini akiwa na bosi mpya.

MATATIZO YA UGANDA

Mara baada ya Mapambano ya Vita vya Kagera, Mwanzoni mwa mwaka 1979 Vikosi vya Jeshi la Wananchi wa Tanzania vilifanikiwa kumng'oa Madarakani Dikteta Amin wa Uganda na kumpachika Ndugu Yusufu Lule kama Rais wa Muda wa Taifa hilo Jirani. Lule hakudumu sana madarakani kwa kuwa mwezi Juni, 1979 naye aling'olewa madarakani kwa kutofautiana na Baraza la Ushauri la Taifa la Nchi hiyo juu ya uteuzi wa nafasi za Mawaziri, na nafasi yake kuchukuliwa na Ngudu Godfrey Binaisa.

Miezi kadhaa baada ya kuchukua madaraka kwa Binaisa katika Serikali ya Uganda bado mambo ya kuendesha nchi hiyo hayakuonekana kwenda vizuri, Changamoto za kujenga upya nchi hiyo iliyoharibiwa na vita zilikuwa kubwa, huku Jeshi jipya la nchi hiyo likiwa na kashfa ya kufanya ukatili kwa wananchi na pia kushiriki kwenye uhalifu na uporaji. Ili kuimarisha mambo ya Kiutawala ya Nchi hiyo ilimbidi Rais Nyerere ambaye bado vikosi vya Jeshi lake vilikuwa havijaondoka Uganda, ampeleke Waziri Hussein Ramadhani Shekilango kwenda kusaidia mambo ya Kiutawala ya Nchi hiyo.

Mwezi Mei, 1980 ilizuka sintofahamu kubwa katika Utawala wa Uganda, Rais Godfrey Binaisa alimuondoa Jeshini Mnadhimu Mkuu wa Jeshi la Nchi hiyo (zamani akiitwa Chief of Staff) Ndugu David Oyite Ojok na kumteua kuwa Balozi wa Uganda Nchini Algeria, sababu kubwa ikitajwa kuwa ni nidhamu mbaya ya Jeshi la nchi hiyo hasa kwenye masuala ya Ukatili kwa wananchi na Uporaji.

Uamuzi huo wa Rais Binaisa haukumfurahisha Kiongozi huyo Namba 2 wa Jeshi la Nchi hiyo, hivyo alikataa Uteuzi mpya, na wanajeshi waliokuwa Watiifu kwake wakatangaza kumuondoa Madarakani Rais Binaisa aliyekuwa akilindwa na Jeshi la Wananchi wa Tanzania katika Hekalu la Rais la Entebbe. Misururu mirefu ya Magari ikaonekana katika Jiji la Kamapala, ambapo Wanajeshi watiifu kwa David Ojok walikuwa wakiyapekuwa magari yote yaliyokuwa yakitoka na kuingia ndani ya jiji hilo ili kuhakikisha hakuna silaha, huku pia wakikiteka Kituo cha Redio cha Taifa cha Nchi hiyo.

Wanajeshi wafuasi wa Ojok waliweka vizuizi katika barabara zote za Jiji la Kampala na kuamua kuyalinda majengo yote nyeti ya Serikali likiwemo Jengo la Nile Mansion Hotel ambalo ndilo lililokuwa na Ofisi nyingi za Wizara nyeti za Serikali ya Nchi hiyo.

Kung'olewa kwa Binaisa kulifanywa na Tume maalum ya Watu sita, ambayo ilikuwa ni sehemu ya Baraza la Ushauri la Taifa lililomng'oa Rais Lule, huku matendo ya Tume hiyo pamoja na Ojok kwenye wiki hiyo yakihusishwa zaidi na Rais Milton Obote aliyekuwa ughaibuni, ambaye aling'olewa Madarakani na Amin mwaka 1971. Obote alikanusha kuhusika na matendo hayo ya Ojok yaliyokuwa yakiteteresha hali ya ustawi wa nchi hiyo japo haikubadili ukweli kuwa marafiki hao lao lilikuwa moja.

katika hali ya matatizo yote hayo, Waziri Hussein Ramadhani Shekilango pamoja na Balozi Kilumanga waliamua kupanda Ndege kwenda kumpa habari za namna hali halisi ya mambo ilivyo nchini humo Rais Nyerere ambaye alikuwa kwenye Ziara ya Kiserikali Mkoani Arusha. Safari hiyo ndiyo ikawa mwisho wa maisha yao.

Ilikuwa siku ya huzuni mno kwa kumpoteza Waziri huyo damu changa, Tarehe 11 Mei, 1980, ndege ya Kijeshi iliyowachukua Shekilango, Balozi Kilumanga pamoja na Wanajeshi wanne wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania ilianguka katika vilima vya Jiji la Arusha na Abiria wote kupoteza Maisha, wakiacha huzuni na majonzi mazito kwa Watanzania.

Msafara wa Rais ukakatisha ziara na shughuli ya Mapokezi ya Miili ya Mashujaa wetu hao ndiyo ikawa Ratiba rasmi, huku Rais Nyerere akionyesha kwa dhati namna alivyohuzunishwa kwa kumpoteza Waziri huyo Mchapa Kazi kwa Taifa. Majonzi zaidi yakiwa kwa Wanakorogwe waliopoteza Kijana wao Msomi wa Makerere aliyejitolea kuwatumikia kwa dhati.

Shekilango alizikwa Kijijini kwao Jitengeni, Korogwe, Mkoani Tanga, huku akisindikizwa na umati mkubwa wa watu, mpaka leo akibaki Mbunge kipenzi cha watu wa Korogwe na akisifika Serikalini kwa hatua yake ya kurudisha Madaraka Mikoani. Kwa kumuenzi kuna Shule yenye jina lake Jimboni Korogwe.

Mamlaka za Uongozi wa Jiji la Dar es salaam kwa kutambua mchango wa Shekilango kwa Taifa, ikaamua kuipa Barabara mpya iliyokuwa inajengwa wakati huo jina la Shekilango ili kumuenzi shujaa huyu.

Mola amlaze Pema Shujaa Hussein Ramadhani Shekilango

Pichani ni Ndugu Hussein Ramadhani Shekilango, Picha ni kwa Hisani ya Familia ya Shekilango, Ukurasa wa Watanzania Mashuhuri unatoa shukrani za dhati kwa Bi Ikupa Shekilango kwa Msaa wake kwa Ukurasa.

marehemu shekilango alifariki 19 may, 1979, nikiwa darasa la tano, one of our relative luteni peter mallya died in that accident, ndege iligonga vilima fulani huko arusha kutokana na hali mbaya ya hewa.

luteni mallya, our relative was the only son to his parents.

siku hiyo gazeti la uhuru liliandika shekilango na wengine sita wafariki

JE WAJUA?

HUSSEIN RAMADHANI SHEKILANGO, SHUJAA ALIYEKUFA AKIIJENGA UGANDA

Jijini Dar es salaam kuna Barabara Mashuhuri kama 'Shekilango Road', ikianzia maungio ya Barabara ya Morogoro eneo la Nyumba za NHC mkabala na Kiwanda cha Urafiki, ikipitia Mitaa yote ya Sinza na kuishia Maungio ya Barabara ya Ali Hassan Mwinyi kituo cha Bamaga.

Ni watanzania wachache wajuao kuwa Barabara hiyo ya Shekilango imepewa jina Maalum kwaajili ya heshima ya Ndugu Hussein Ramadhani Shekilango, aliyekuwa Waziri wa Nchi katika Ofisi ya Waziri Mkuu, akishughulika zaidi na mambo ya Utawala, wakati wa Uongozi wa Rais Julius Nyerere na Makamo wake Aboud Jumbe Mwinyi.

Hussein Shekilango alichaguliwa na Wananchi wa kwao kuwa Mbunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wa Jimbo la Korogwe Mjini, Mkoani Tanga katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 1975, akiachia nafasi yake ya Zamani ya Meneja Mkuu wa Shirika la Usagishaji Nchini (NATIONAL MILLING CORPORATION).

Mwaka huo huo akachaguliwa na Rais Julius Nyerere kuwa Waziri wa Nchi katika Ofisi ya Waziri Mkuu (Utawala) akiwa chini ya Makamu wa Pili wa Rais na Waziri Mkuu, ndugu Rashid Mfaume Kawawa.

Mwaka 1977 yalifanyika Mabadiliko makubwa ya Baraza la Mawaziri Nchini, aliyekuwa Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kulinda Taifa, Ndugu Edward Moringe Sokoine aliteuliwa kuwa Waziri Mkuu akichukua nafasi ya Kawawa, Shekilango akabakishwa katika nafasi yake lakini akiwa na bosi mpya.

MATATIZO YA UGANDA

Mara baada ya Mapambano ya Vita vya Kagera, Mwanzoni mwa mwaka 1979 Vikosi vya Jeshi la Wananchi wa Tanzania vilifanikiwa kumng'oa Madarakani Dikteta Amin wa Uganda na kumpachika Ndugu Yusufu Lule kama Rais wa Muda wa Taifa hilo Jirani. Lule hakudumu sana madarakani kwa kuwa mwezi Juni, 1979 naye aling'olewa madarakani kwa kutofautiana na Baraza la Ushauri la Taifa la Nchi hiyo juu ya uteuzi wa nafasi za Mawaziri, na nafasi yake kuchukuliwa na Ngudu Godfrey Binaisa.

Miezi kadhaa baada ya kuchukua madaraka kwa Binaisa katika Serikali ya Uganda bado mambo ya kuendesha nchi hiyo hayakuonekana kwenda vizuri, Changamoto za kujenga upya nchi hiyo iliyoharibiwa na vita zilikuwa kubwa, huku Jeshi jipya la nchi hiyo likiwa na kashfa ya kufanya ukatili kwa wananchi na pia kushiriki kwenye uhalifu na uporaji. Ili kuimarisha mambo ya Kiutawala ya Nchi hiyo ilimbidi Rais Nyerere ambaye bado vikosi vya Jeshi lake vilikuwa havijaondoka Uganda, ampeleke Waziri Hussein Ramadhani Shekilango kwenda kusaidia mambo ya Kiutawala ya Nchi hiyo.

Mwezi Mei, 1980 ilizuka sintofahamu kubwa katika Utawala wa Uganda, Rais Godfrey Binaisa alimuondoa Jeshini Mnadhimu Mkuu wa Jeshi la Nchi hiyo (zamani akiitwa Chief of Staff) Ndugu David Oyite Ojok na kumteua kuwa Balozi wa Uganda Nchini Algeria, sababu kubwa ikitajwa kuwa ni nidhamu mbaya ya Jeshi la nchi hiyo hasa kwenye masuala ya Ukatili kwa wananchi na Uporaji.

Uamuzi huo wa Rais Binaisa haukumfurahisha Kiongozi huyo Namba 2 wa Jeshi la Nchi hiyo, hivyo alikataa Uteuzi mpya, na wanajeshi waliokuwa Watiifu kwake wakatangaza kumuondoa Madarakani Rais Binaisa aliyekuwa akilindwa na Jeshi la Wananchi wa Tanzania katika Hekalu la Rais la Entebbe. Misururu mirefu ya Magari ikaonekana katika Jiji la Kamapala, ambapo Wanajeshi watiifu kwa David Ojok walikuwa wakiyapekuwa magari yote yaliyokuwa yakitoka na kuingia ndani ya jiji hilo ili kuhakikisha hakuna silaha, huku pia wakikiteka Kituo cha Redio cha Taifa cha Nchi hiyo.

Wanajeshi wafuasi wa Ojok waliweka vizuizi katika barabara zote za Jiji la Kampala na kuamua kuyalinda majengo yote nyeti ya Serikali likiwemo Jengo la Nile Mansion Hotel ambalo ndilo lililokuwa na Ofisi nyingi za Wizara nyeti za Serikali ya Nchi hiyo.

Kung'olewa kwa Binaisa kulifanywa na Tume maalum ya Watu sita, ambayo ilikuwa ni sehemu ya Baraza la Ushauri la Taifa lililomng'oa Rais Lule, huku matendo ya Tume hiyo pamoja na Ojok kwenye wiki hiyo yakihusishwa zaidi na Rais Milton Obote aliyekuwa ughaibuni, ambaye aling'olewa Madarakani na Amin mwaka 1971. Obote alikanusha kuhusika na matendo hayo ya Ojok yaliyokuwa yakiteteresha hali ya ustawi wa nchi hiyo japo haikubadili ukweli kuwa marafiki hao lao lilikuwa moja.

katika hali ya matatizo yote hayo, Waziri Hussein Ramadhani Shekilango pamoja na Balozi Kilumanga waliamua kupanda Ndege kwenda kumpa habari za namna hali halisi ya mambo ilivyo nchini humo Rais Nyerere ambaye alikuwa kwenye Ziara ya Kiserikali Mkoani Arusha. Safari hiyo ndiyo ikawa mwisho wa maisha yao.

Ilikuwa siku ya huzuni mno kwa kumpoteza Waziri huyo damu changa, Tarehe 11 Mei, 1980, ndege ya Kijeshi iliyowachukua Shekilango, Balozi Kilumanga pamoja na Wanajeshi wanne wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania ilianguka katika vilima vya Jiji la Arusha na Abiria wote kupoteza Maisha, wakiacha huzuni na majonzi mazito kwa Watanzania.

Msafara wa Rais ukakatisha ziara na shughuli ya Mapokezi ya Miili ya Mashujaa wetu hao ndiyo ikawa Ratiba rasmi, huku Rais Nyerere akionyesha kwa dhati namna alivyohuzunishwa kwa kumpoteza Waziri huyo Mchapa Kazi kwa Taifa. Majonzi zaidi yakiwa kwa Wanakorogwe waliopoteza Kijana wao Msomi wa Makerere aliyejitolea kuwatumikia kwa dhati.

Shekilango alizikwa Kijijini kwao Jitengeni, Korogwe, Mkoani Tanga, huku akisindikizwa na umati mkubwa wa watu, mpaka leo akibaki Mbunge kipenzi cha watu wa Korogwe na akisifika Serikalini kwa hatua yake ya kurudisha Madaraka Mikoani. Kwa kumuenzi kuna Shule yenye jina lake Jimboni Korogwe.

Mamlaka za Uongozi wa Jiji la Dar es salaam kwa kutambua mchango wa Shekilango kwa Taifa, ikaamua kuipa Barabara mpya iliyokuwa inajengwa wakati huo jina la Shekilango ili kumuenzi shujaa huyu.

Mola amlaze Pema Hussein Ramadhani Shekilango

View attachment 316648


JINA SHEKILANGO


Jijini Dar es salaam kuna Barabara Mashuhuri kama 'Shekilango Road', ikianzia maungio ya Barabara ya Morogoro eneo la Nyumba za NHC mkabala na Kiwanda cha Urafiki, ikipitia Mitaa yote ya Sinza na kuishia Maungio ya Barabara ya Ali Hassan Mwinyi kituo cha Bamaga.

Ni watanzania wachache wajuao kuwa Barabara hiyo ya Shekilango imepewa jina Maalum kwaajili ya heshima ya Ndugu Hussein Ramadhani Shekilango, aliyekuwa Waziri wa Nchi katika Ofisi ya Waziri Mkuu, akishughulika zaidi na mambo ya Utawala, wakati wa Uongozi wa Rais Julius Nyerere na Makamo wake Aboud Jumbe Mwinyi.

Hussein Shekilango alichaguliwa na Wananchi wa kwao kuwa Mbunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wa Jimbo la Korogwe Mjini, Mkoani Tanga katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 1975, akiachia nafasi yake ya Zamani ya Meneja Mkuu wa Shirika la Usagishaji Nchini (NATIONAL MILLING CORPORATION).

Mwaka huo huo akachaguliwa na Rais Julius Nyerere kuwa Waziri wa Nchi katika Ofisi ya Waziri Mkuu (Utawala) akiwa chini ya Makamu wa Pili wa Rais na Waziri Mkuu, ndugu Rashid Mfaume Kawawa.

Mwaka 1977 yalifanyika Mabadiliko makubwa ya Baraza la Mawaziri Nchini, aliyekuwa Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kulinda Taifa, Ndugu Edward Moringe Sokoine aliteuliwa kuwa Waziri Mkuu akichukua nafasi ya Kawawa, Shekilango akabakishwa katika nafasi yake lakini akiwa na bosi mpya.

MATATIZO YA UGANDA
Mara baada ya Mapambano ya Vita vya Kagera, Mwanzoni mwa mwaka 1979 Vikosi vya Jeshi la Wananchi wa Tanzania vilifanikiwa kumng'oa Madarakani Dikteta Amin wa Uganda na kumpachika Ndugu Yusufu Lule kama Rais wa Muda wa Taifa hilo Jirani. Lule hakudumu sana madarakani kwa kuwa mwezi Juni, 1979 naye aling'olewa madarakani kwa kutofautiana na Baraza la Ushauri la Taifa la Nchi hiyo juu ya uteuzi wa nafasi za Mawaziri, na nafasi yake kuchukuliwa na Ngudu Godfrey Binaisa.

Miezi kadhaa baada ya kuchukua madaraka kwa Binaisa katika Serikali ya Uganda bado mambo ya kuendesha nchi hiyo hayakuonekana kwenda vizuri, Changamoto za kujenga upya nchi hiyo iliyoharibiwa na vita zilikuwa kubwa, huku Jeshi jipya la nchi hiyo likiwa na kashfa ya kufanya ukatili kwa wananchi na pia kushiriki kwenye uhalifu na uporaji. Ili kuimarisha mambo ya Kiutawala ya Nchi hiyo ilimbidi Rais Nyerere ambaye bado vikosi vya Jeshi lake vilikuwa havijaondoka Uganda, ampeleke Waziri Hussein Ramadhani Shekilango kwenda kusaidia mambo ya Kiutawala ya Nchi hiyo.

Mwezi Mei, 1980 ilizuka sintofahamu kubwa katika Utawala wa Uganda, Rais Godfrey Binaisa alimuondoa Jeshini Mnadhimu Mkuu wa Jeshi la Nchi hiyo (zamani akiitwa Chief of Staff) Ndugu David Oyite Ojok na kumteua kuwa Balozi wa Uganda Nchini Algeria, sababu kubwa ikitajwa kuwa ni nidhamu mbaya ya Jeshi la nchi hiyo hasa kwenye masuala ya Ukatili kwa wananchi na Uporaji.

Uamuzi huo wa Rais Binaisa haukumfurahisha Kiongozi huyo Namba 2 wa Jeshi la Nchi hiyo, hivyo alikataa Uteuzi mpya, na wanajeshi waliokuwa Watiifu kwake wakatangaza kumuondoa Madarakani Rais Binaisa aliyekuwa akilindwa na Jeshi la Wananchi wa Tanzania katika Hekalu la Rais la Entebbe.

Misururu mirefu ya Magari ikaonekana katika Jiji la Kamapala, ambapo Wanajeshi watiifu kwa David Ojok walikuwa wakiyapekuwa magari yote yaliyokuwa yakitoka na kuingia ndani ya jiji hilo ili kuhakikisha hakuna silaha, huku pia wakikiteka Kituo cha Redio cha Taifa cha Nchi hiyo.

Wanajeshi wafuasi wa Ojok waliweka vizuizi katika barabara zote za Jiji la Kampala na kuamua kuyalinda majengo yote nyeti ya Serikali likiwemo Jengo la Nile Mansion Hotel ambalo ndilo lililokuwa na Ofisi nyingi za Wizara nyeti za Serikali ya Nchi hiyo.

Kung'olewa kwa Binaisa kulifanywa na Tume maalum ya Watu sita, ambayo ilikuwa ni sehemu ya Baraza la Ushauri la Taifa lililomng'oa Rais Lule, huku matendo ya Tume hiyo pamoja na Ojok kwenye wiki hiyo yakihusishwa zaidi na Rais Milton Obote aliyekuwa ughaibuni, ambaye aling'olewa Madarakani na Amin mwaka 1971. Obote alikanusha kuhusika na matendo hayo ya Ojok yaliyokuwa yakiteteresha hali ya ustawi wa nchi hiyo japo haikubadili ukweli kuwa marafiki hao lao lilikuwa moja.

katika hali ya matatizo yote hayo, Waziri Hussein Ramadhani Shekilango pamoja na Balozi Kilumanga waliamua kupanda Ndege kwenda kumpa habari za namna hali halisi ya mambo ilivyo nchini humo Rais Nyerere ambaye alikuwa kwenye Ziara ya Kiserikali Mkoani Arusha. Safari hiyo ndiyo ikawa mwisho wa maisha yao.

Ilikuwa siku ya huzuni mno kwa kumpoteza Waziri huyo damu changa, Tarehe 11 Mei, 1980, ndege ya Kijeshi iliyowachukua Shekilango, Balozi Kilumanga pamoja na Wanajeshi wanne wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania ilianguka katika vilima vya Jiji la Arusha na Abiria wote kupoteza Maisha, wakiacha huzuni na majonzi mazito kwa Watanzania.

Msafara wa Rais ukakatisha ziara na shughuli ya Mapokezi ya Miili ya Mashujaa wetu hao ndiyo ikawa Ratiba rasmi, huku Rais Nyerere akionyesha kwa dhati namna alivyohuzunishwa kwa kumpoteza Waziri huyo Mchapa Kazi kwa Taifa. Majonzi zaidi yakiwa kwa Wanakorogwe waliopoteza Kijana wao Msomi wa Makerere aliyejitolea kuwatumikia kwa dhati.

Shekilango alizikwa Kijijini kwao Jitengeni, Korogwe, Mkoani Tanga, huku akisindikizwa na umati mkubwa wa watu, mpaka leo akibaki Mbunge kipenzi cha watu wa Korogwe na akisifika Serikalini kwa hatua yake ya kurudisha Madaraka Mikoani. Kwa kumuenzi kuna Shule yenye jina lake Jimboni Korogwe.

Mamlaka za Uongozi wa Jiji la Dar es salaam kwa kutambua mchango wa Shekilango kwa Taifa, ikaamua kuipa Barabara mpya iliyokuwa inajengwa wakati huo jina la Shekilango ili kumuenzi shujaa huyu.

Mola amlaze Pema Hussein Ramadhani Shekilango
 
Ninachokumbuka alikuwa waziri na alikufa akiwa njiani toka Uganda kwenye ajali ya helkopta, hivyo alikufa akiwa kazini enzi za mwalimu, baada ya vita vya kumuondoa Nduli Iddi Amini.
 
Halafu haya majina ya Shekilango na Shemhando ni hayo hayo ya Kilango na Mhando

wasambaa zamani walikuwa wanafikiri mtu kuitwa sheikh ni title ya ujiko
so wakaanza kuongeza sheikh kwenye majina yao.

Yaani mhando ikawa sheik mhando
kilango ikawa shekilango
lukindo ikawa shelukindo n.k

sasa ndo imekuwa hivyo.
 
Alikuwa Waziri wa nchi ofisi ya waziri mkuu na alifariki 1980 akitokea Entebbe Uganda, na ndege iliangukia Arusha, unaweza kusearch Hussein Shekilango nafikiri unaweza kupata data zaidi.
 
..hivi kuna yeyote amewahi kujiuliza Shekilango ni nani mpaka barabara kubwa jijini DSM ikapewa jina lake?

..naomba mwenye historia na wasifu wa Shekilango atuwekee. naamini siko peke yangu ambaye hatuna taarifa zake.


Kaka Joka Kuu,

Mzee Hussein Shekilango aliwahi kuwa Mbunge wa Korogwe na Baadaye alikuwa waziri Wa Nchi Ofisi Ya Waziri Mkuu anayeshughulikia mambo ya Utawala (Nafikiri utakuwa unawafahamu watumishi wa namna hii).Mzee Shekilango alikuwa mtu wa karibu sana na Rais Nyerere (RIP) na Waziri Mkuu wa wakati huo Mh.Edward Sokoine (RIP).

Ilikuwa mwezi May/1980 Mzee Shekilango pamoja na watumishi wengine wa serikali na Wanajeshi wa Jeshi la Ulinzi walipata ajali ya ndege huko Arusha na kufariki.Mzee Shekilango na ujumbe wake walikuwa wanasafiri kwa ndege ndogo kutoka Arusha kwenda Entebbe.Ikumbukwe kuwa kipindi hicho tulikuwa katika vita na Utawala wa Amin,na inasemekana Mzee Shekilango alikuwa ametumwa na Rais kwa kazi maalumu huko Uganda.

Sina Ufahamu ni nani alipendekeza Jina la Barabara ile ya Shekilango (Mwenge/sinza) lakini Shekilango anahesabiwa kama shujaa,kwa sababu alikufa kazini na katika shughuli za Vita vya Kagera.Mtoto wa Kiume wa Marehemu Shekilango alikuwa mmojawapo ya wanachama wa CCM 19 walioomba Ubunge wa Korogwe -Magharibi katika Uchaguzi Mkuu wa 2005.
 
Wow this is interesting i never though ile barabara ya shekilango imewekwa kutoka na umaarufu wa mtu. Nimefurahi kujua hii
Bravo aliyeleta hii mada!
 
Ukitaka kujua zaidi nenda Sea View, mama Shekilango yupo huko.
 
The Boss,

Hey The Boss,
My mom is msambaa and my daddy is half Irish half dutch.

Taarifa yako sio ya kweli.
Wako watu wanaitwa Lukindo mpaka leo, and what I can remember is that, Lukindo is called Ukindo in Kisambaa
Wako watu wanaoitwa Kilango mpaka leo.

She in kisambaa is [ a son of ]

See this, Maukindo
A daughter of Ukindo.
 
Halafu haya majina ya shekilango na shemhando ni hayo hayo ya kilango na mhando

wasambaa zamani walikuwa wanafikiri mtu kuitwa sheikh ni title ya ujiko
so wakaanza kuongeza sheikh kwenye majina yao.

Yaani mhando ikawa sheik mhando
kilango ikawa shekilango
lukindo ikawa shelukindo n.k

sasa ndo imekuwa hivyo.

Mkuu Wasambaa tulikua tuna weka "she" siyo "sheikh". Na huko kuweka "She" ni kwa mtu ambae anaoa msambaa. So Mhando akimuoa msamba inawekwa "she" anakua Shemhando.
 
Mie hapa nashangaa kumbe kila kitu kina maana yake. Na Mandela Road, Samora zina maana gani?
 
Mh bibie hata hizi nazo?

Hizo nimeuliza kwa nini ziliitwa hivo

Hiyo Mandela ni rais wa SA alikuja TZ wakaita barabara Mandera Or

Na Samora - Ni Sababu Ya samora wa Msumbiji or kuna maana nyingine

aulizae ataka kujua ??:)nijibu basi kimei mie niko huku Bariadi village kwa kina Kanumba
 
Hizo nimeuliza kwa nini ziliitwa hivo

Hiyo Mandela ni rais wa SA alikuja TZ wakaita barabara Mandera Or

Na Samora - Ni Sababu Ya samora wa Msumbiji or kuna maana nyingine

aulizae ataka kujua ??:)nijibu basi kimei mie niko huku Bariadi village kwa kina Kanumba
Hizo zote ni Heshima Waliopewa hao wa asisi wa mataifa ni kuwaenzi wapigania Uhuru ndo maana hata ukienda Zimbabwe, Namibia, kuna nyerere road huko! by the way Bariadi village hakuna salooni inayoweza kutengeneza unywele huo bibie! teh teh
 
Hizo zote ni Heshima Waliopewa hao wa asisi wa mataifa ni kuwaenzi wapigania Uhuru ndo maana hata ukienda Zimbabwe, Namibia, kuna nyerere road huko! by the way Bariadi village hakuna salooni inayoweza kutengeneza unywele huo bibie! teh teh

Thanks u make ma Nyerere Day
 

Mkuu Wasambaa tulikua tuna weka "she" siyo "sheikh". Na huko kuweka "She" ni kwa mtu ambae anaoa msambaa. So Mhando akimuoa msamba inawekwa "she" anakua Shemhando.

Mhando
Kilango au kisambaa chenyewe( Kiango)

Na hii yote ilitokea wakati huo wa enzi za mababu kwamba mtoto wa Kiango anaweza kuitwa Shekiango
Au hata kuoa tena, mwanaume akioa anaweza kuchukua title ya mke wake.

Kama mwanamke ni Mzingwa basi mwanaume atakayemuoa anaweza kua akachagua jila la Shemzigwa.
As my mom said, She = son of or mume wa...

Kama Yugoslavia wanavyoitana Milosovic, Ibrahimovic.

Wanaojua kisambaa zaidi wafafanue, kwani mimi haya nilifundishwa na mama labda kuna Ufafanuzi zaidi
 
Marehemu shekilango alifariki 19 may, 1979, nikiwa darasa la tano, one of our relative luteni peter mallya died in that accident, ndege iligonga vilima fulani huko arusha kutokana na hali mbaya ya hewa.

Luteni Mallya, our relative was the only son to his parents.

Siku hiyo gazeti la Uhuru liliandika shekilango na wengine sita wafariki
 
duh! nimeiona hii leo, historia ya shekilango niliwahi kuambiawa kuwa, enzi hizo huyo mzee shekilango alikuwa anaishi sinza, kwahiyo wasambaa wakiwa wanasafiri kuja dar walikuwa wanasema kwa kisambaa ''TITAITA KWA SHEKIANGO'' yaani tunakwenda kwa mzee shekilango, so ikawa kila mtu anasema anakwenda kwa shekilango na ndio ikawa mwanzo wa shekilango na hatimaye hiyo barabara ikapewa hilo jina.
 
Back
Top Bottom