Mtumishi Wetu
JF-Expert Member
- Oct 12, 2010
- 5,712
- 1,906
Za hasubuhi wanajamii, waasalamu Alyekumu!
Sijaelewa hawa jamaa wa SISIEMU Vijana (UVCCM) wanaelekea wapi na wanapeleka wapi umoja wao?
Sasa inaonyesha wazi SISIEM hawana nia ya kukemea ufisadi, kwenye gazeti la Rai Mwema la jumatano, kijana mmoja kwa jina la Mrisho mwenye machungu na nchi hii ya Tanzania alitoa malalamiko kuwa EL na RA ndio watu waliokipotezea mvuto chama cha SISIEM. Akaonyesha wazi kabisa kuhusu kashfa za Richmond, Dowans na zingine nyingi kuwa wahusika wakuu ni hao viongozi waandamizi wa chama. Lakini cha ajabu akasimama huyo Bwn Bashe na kupinga kitu kilicho wazi na kusema waliokihujumu chama ni Mzee Six na Bwn Pombe Makufuli, mmoja akikemea ufisadi na mwingine akitekeleza majukumu ya bomoa bomoa.Kwa msimamo huo kikao chote kikaunga mkono huo upuuzi, huyo Bwana Bashe akajitambulisha kuwa yeye ni mwajiliwa wa Kampuni za RA. Wajumbe wote wakamkumbatia huyo Bwn Bashe na kumpa uwenyekiti wa kamati ya kuimalisha umoja wao.
Wakasahau maovu ya hao mafisadi na kukumbatia vibaraka wao. Sasa Ndg zangu wameibuka vijana ambao ni maajenti wa mafisadi. Hawana uchungu na dhiki za nchi hii, wanatetea wale walio watuma!
Sasa kwa njia hiyo SISIEMU watajinyumbua kama walivyosema na kuvaa gamba jipya?
SISIEMU hawana nia kabisa ya kupiga vita ufisadi bali hicho chama imekuwa ngome ya mafisadi wanaofilisi nchi yetu hii ya Tanzania!
Tufanyeje kujikomboa?
Nawasilisha
Sijaelewa hawa jamaa wa SISIEMU Vijana (UVCCM) wanaelekea wapi na wanapeleka wapi umoja wao?
Sasa inaonyesha wazi SISIEM hawana nia ya kukemea ufisadi, kwenye gazeti la Rai Mwema la jumatano, kijana mmoja kwa jina la Mrisho mwenye machungu na nchi hii ya Tanzania alitoa malalamiko kuwa EL na RA ndio watu waliokipotezea mvuto chama cha SISIEM. Akaonyesha wazi kabisa kuhusu kashfa za Richmond, Dowans na zingine nyingi kuwa wahusika wakuu ni hao viongozi waandamizi wa chama. Lakini cha ajabu akasimama huyo Bwn Bashe na kupinga kitu kilicho wazi na kusema waliokihujumu chama ni Mzee Six na Bwn Pombe Makufuli, mmoja akikemea ufisadi na mwingine akitekeleza majukumu ya bomoa bomoa.Kwa msimamo huo kikao chote kikaunga mkono huo upuuzi, huyo Bwana Bashe akajitambulisha kuwa yeye ni mwajiliwa wa Kampuni za RA. Wajumbe wote wakamkumbatia huyo Bwn Bashe na kumpa uwenyekiti wa kamati ya kuimalisha umoja wao.
Wakasahau maovu ya hao mafisadi na kukumbatia vibaraka wao. Sasa Ndg zangu wameibuka vijana ambao ni maajenti wa mafisadi. Hawana uchungu na dhiki za nchi hii, wanatetea wale walio watuma!
Sasa kwa njia hiyo SISIEMU watajinyumbua kama walivyosema na kuvaa gamba jipya?
SISIEMU hawana nia kabisa ya kupiga vita ufisadi bali hicho chama imekuwa ngome ya mafisadi wanaofilisi nchi yetu hii ya Tanzania!
Tufanyeje kujikomboa?
Nawasilisha