Hussein Bashe aongea na vyombo vya habari

Mkuu,

Jamaa wanaonekana wanaamini wana ushawishi mkubwa, kama hujashawishiwa wewe basi huenda kuna mamilioni ya watanzania wamefanikiwa kuwashawishi kama wanavyoainisha hapo juu.

Najaribu kushawishika pia lol

Tatizo la nchi hii ni kwamba kila kitu kinapangwa kwa mtazamo wa Dar es Salaam. Hata shule za sekondari za kutwa zilianza kwa mtazamo wa Dar ambako kuna mabasi. Umeme ukikosekana Dar inakuwa kama ni tatizo la wote hata watu wa Lindi ambao hawapo kwenye grid. Dar inakuwa kila kitu.

Mimi naishi na kutembelea vijiji mbalimbali naongea na vijana wakada mbalimbali, nashangaa sana kuambiwa eti jamaa wanakubalika. Kuna mahali ukienda wanashangaa kusikia eti kuna UVCCM. Wengi wanajua kuna CCM kwa sababu wakati wakampeni huwagawia kanga na fulana za kijani baada ya hapo mambo huishia na kupewa pombe za kienyeji au pilau.

Labda urudi mpango wa enzi ya TANU YOUTH LEAGUE ambapo vijana wa shule walishurutisha kujiunga na baadaye ndani ya CCM wanafunzi wa vidato vya tano na sita walilazimishwa kujiunga na CCM kama tiketi ya kwenda chuo kikuu. La si hivyo UVCCM itabakia kuwa ni ya vijana walio barikiwa na vipato au watoto wawenye madaraka na biashara kubwakubwa waishio mijini.

Na ndio maana matamko yote yanatolewa mijini na vijana wa mijini na sio vijijini kama Nanguruwe au Igawisenga. Na watoaji utawasikia ni akina Hussen Bashe, Nape na Ridhiwan. Hao ndio wenye chama, wengine wote ni wadandiaji.
 
Heshima mbele mkuu, heading ya hii thread haiendani na content yake, Inv kaandika "H. Bashe aongea na vyombo vya habari" wakati jamaa hata kwenye kiti alikuwa hajakaa, angesubiri apate content then aanzishe thread.

kiswahili kinakusumbua, typing pia kwenye red, ufahamu wa mambo, ubishi usokuwa na tija.
 
Mkuu unatupoteza, hizi updates weka kule juu mkuu.

Watatumia, HAKI ELIMU, TGNP, TWAWEZA, AGENDA PARTICIPATION etc
Inategemea pia vision ya hizo asasi.

Kila mtu anatakakuitisha mkutano na waadishi wa habari,sasa hii imekuwa ni fujo sio taarifa tena.
Basi hata mimi nitakuwa na mkutano na waandishi wa jamiiforum hapo kesho kuanzia saa nne 4:00am.
Tafadhali waandishi wote wa Jamiiforum msikose kuna mjadala mkubwa sana utafanyika kesho hapa hapa JAMIIFORUM.
Karibuni wote wenye itikadi na wasio na itikadi za kisiasa au za kidini,za kielimu au za kimachinga.Wote tuko sawa

Wanajaribu kufaidika na hili wimbi la Uchaguzi wa Bavicha...Hao ni opportunists.Wanajaribu kuonyesha Ajenda tulizo nazo hata wao wanazo.Ni kwa nini kaamua kufanya Press conference kipindi hiki?Wanatafuta kunufaika kimtindo na hii ride ya BAVICHA.

Bashe kasema umefika wakati CCM lazima ikubali kufanya siasa nje ya chama! Mtu ndani ya UVCCM akipata kuhudhuria mojawapo ya mikutano ya BAVICHA na akaona hoja inayoongelewa ni ya msingi na manufaa kwa nchi basi isiachwe kisa ni kutoka upinzani.

Ofcourse tunataka tushindane na chama strong,tataizo watachukua ajenda zetu na hawataweza kuzitekeleza.Hadi sasa kaiba ajenda ngapi za wagombea wa BAVICHA?Anajaribu kuzitumia kujijenga yeye na kundi lake,hillarious! Ni lini UVCCM waliwahi kuwa na uchungu na wamachinga?

Watakoma kuwanyima vijana wa Tanzania baraza huru la Taifa,BAVICHA itaziba ombwe hilo.Matumaini ya vijana wa Tanzania leo hii hayawezi kuwa ndani ya UVCCM tena.Hata hivyo,wafanye homework yao vizuri na wajiandae kukutana na storm ya BAVICHA mpya,hata Sekretarieti yao ikae chonjo


wezi tu hawa....tunawapa muda na pumzi zetu badala ya kuwatoa! kila siku tunaimba nao na kucheza nao ngoma!

Chapakazi,

Hawa Mwisho wao umefika,hawa wanaojifanya kuja na mkkati wa kuinusuru UVCCM wanatapatapa tu.Watumie Muda wao mwingi kunadi ideology ya chama na kuitafsiri katika utekelezaji ili kuteka nyoyo za watanzania.Tunataka tupambane na UVCCM/CCM iliyo imara ili ushindi wetu 2015 uwe mtamu.Waendelee kujiimarisha wakutane kimbunga chetu
 
We gamba jipya lishachoka tayari...we bado wasubiri kipindi cha michezo saa mbili kasorobo, sie twaangalia live kuanzia warm-up mpaka final whistle...:msela:
Kama huna habari kamili kwa nini unaanzisha thread mkuu...ungesubiri hadi uwe na hiyo habari..
 
kwani bashe ni nani na anawakilisha nini chenye maslahi ya nchi hii?
 
Kama huna habari kamili kwa nini unaanzisha thread mkuu...ungesubiri hadi uwe na hiyo habari..
Mkuu tumia upstairs kufikiri, Ameanzisha thread ili na wale waliopo waendelee kutoa kitu live,Ugeni wako usiwe shida kwetu,tulia jifunze na baadae utaielewa JF kwa undani.
 
Aulizwe wakati wa kampeni za uchaguzi 2010, katibu mkuu CCM alidharau tena kwa kejeli vyombo vya habari kwa kukataza wana CCM kuhudhuria midahalo, leo imekuaje siku hizi CCM ndiyo vinara wa kuita au kukimbilia vyombo vya habari?

Mimi nafikiri media zote ziwapuuze CCM hawana jipya wala utashi wa kumkomboa mtanzania.
 
Aisee, hii ndiyo Tanzania.

UVCCM wamegundua kwamba inapoteza mvuto mbele ya jamii, wana'reform' jumuiya yao sijui kama ndo watafanikiwa kurudisha mvuto maana naona kilichosababisha wapoteze mvuto bado ndo hicho wanakorogana mara hafukuzwi mtu mara oh vijana wanatumiwa.

Nasubiri kwa hamu sinema hii iishe ili tuendelee na mengine yaliyo ya muhimu kwa ustawi wa taifa letu kuliko kusikiliza upupu huu.
 
Ghafla Midahalo na public hearings zimekuwa means za kuwavutia vijana. Wangetekeleza ajenda za vijana ipasavyo na sera zenye maslahi kwa Taifa kusingekuwa na haja ya kutumia nguvu nyingi
 
Sasa naanza kukubali vua gamba ya CCM ni danganya toto.....i can see wanavosuka mpango wa kukwepa kuwatema magamba makuu matatu....lets wait and see..
 
Suala la uraia wa Bashe mbona halina utata? Huyu bwana ni wa kutoka ukoo wa Darood kutoka jimbo la Puntiland. Ni ukoo maarufu kwa uharamia na mimi nilifikiri wakati mzuri kuondoka ulikuwa ni pale Rais wa Serikali ya Mpito alipokuja kufanya ziara hapa.

Haya mambo ya kumwacha atambe tambe ndiyo baadae anakuwa kama Rostam halafu kumtoa inakuwa ni issue mpaka maandamano. Ni fisadi chipukizi ambaye anatakiwa kung'olewa.

Wana Jf naona Mbopo ameingia kazini kama wengi tuliokua katika press leo tulivotarajia, Bashe alipoulizwa juu ya mtu anaevuruga UVCCM alisema haya yafuatayo.

Kuna waziri muandamizi ambae hivi karibuni alifanya jitihada kubwa sana kutaka fedha tulizosamehewa na Kiongozi wa Libya ambazo zipo TIB apewe mfanya biashara mmoja wa kihindi ambae ni mbunge ikiwa ni mkakati wake wa kujipanga na waziri huyu ndie ambae alishindwa kufikisha nusu ya msaada waliopewa CCM na nchi mmoja katika uchaguzi uliopita, sasa waziri huyu ana watu wake JF na Bashe alitaja jina la Member anaitwa MBOPO na akasema hawa kwakua wanalipwa posho za dola walizoibiwa CCM na WAZIRI HUYO basi watafanya kazi yao.

Nimefanya uchunguzi Mbopo baada ya kuona mara ya kwanza umeongelea kabila la huyu mwana ccm ambae chama chake kiko hoi,kibila la huyu jamaa ni AL_ISHAKIA na sio Darood asili yake ni KASKAZINI eneo lililojitenga kutoka kusini,hawa jamaa asili yao ni wafugaji zaidi hoja ya mbopo kuwa huyu jamaa ni DAROOD si sahihi Darood ni watu wa kusini.

Kuhusu hawa darood kuwa ni pirates ni kweli lakini pirates wengi wanatoka KUSINI, lakini swala la kabila ama asili yake si hoja Mbona wewe unatoka KUSINI MWA AFRIKA ASILI YAKO NI MSUMBIJI, MBONA BOSI WAKO WAZIRI MEMBE ANATOKA KUSINI MWA AFRIKA, MBONA MKAPA ASILI YAKE MSUMBIJI, MBONA SHIVJI ASILI YAKE ASIA, hoja yako isiwe dhaifu namna hiyo wapo mafisadi hatari wenye rangi nyeusi ambao wanasumbua nchi hii kama bosi wako ambae ametaka kuiba fedha tulizosamehewa na GADIFI ambae alizuia sehemu ya fedha zilizoletwa kama msaada kwa ccm na ambazo anatumia sasa kukulipa wewe kwa kazi hii unayofanya sasa.

Tuangalie alichosema huyu jamaa kama kitawasaidia wao na chama chao sisi tunasubiri uchaguzi wa BAVICHA ili tupate viongozi tuanze KULIMA
 
Oh, bashe, tanzania ni nchi nzuri eeh?
kalete pirates wengine msaidiane kuitafuna shamba la bibi bongo.
 
Suala la uraia wa Bashe mbona halina utata? Huyu bwana ni wa kutoka ukoo wa Darood kutoka jimbo la Puntiland. Ni ukoo maarufu kwa uharamia na mimi nilifikiri wakati mzuri kuondoka ulikuwa ni pale Rais wa Serikali ya Mpito alipokuja kufanya ziara hapa.

Haya mambo ya kumwacha atambe tambe ndiyo baadae anakuwa kama Rostam halafu kumtoa inakuwa ni issue mpaka maandamano. Ni fisadi chipukizi ambaye anatakiwa kung'olewa.
Mbopo hii safi sana, vipi Membe kasafiri na bwana Mkubwa
 
May 3rd, 2011


Kamati Ndogo ya Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) imepongeza na kuunga mkono hatua zilizochukuliwa na Chama cha Mapinduzi na zinazoendelea kuchukuliwa katika kuleta mageuzi ndani ya CCM.

Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari leo hii iliyosainiwa na Mwenyekiti wake Hussein Bashe kamati hiyo ndogo ya UVCCM, ilisema imempongeza Mwenyekiti wa CCM Dr. Jakaya Mrisho Kikwete kwa namna alivyosimamia mageuzi ndani ya Chama.

Taarifa hiyo ilisema kuwa kamati hiyo ndogo aidha inawapongeza Sekretarieti mpya na Kamati Kuu mpya iliyochaguliwa.

Katika taarifa hiyo ilisema ni vizuri kufanya mageuzi sasa wakati ambapo bado UVCCM kinakubalika kwa sababu kina wanachama 2.7 Milioni, kimeshinda chaguzi zote, kimetimiza miaka 32.

Taarifa iliongeza kuwa ni wakati muafaka kwa UVCCM kufanya mageuzi ili kuiimarisha kiuchumi na kifedha na hivyo kuifanya UVCCM iwe na rasimali zake zitakazokifanya kujitegemea na hivyo kuacha utegemezi.

Katika taarifa yake kamati hiyo ndogo iliongeza imepitia Hadidu za rejea za maeneo inayotakiwa kuyafanyia mageuzi ambayo ni Muundo wa UVCCM uliopo una ngazi sita za uongozi kwa upande wa Tanzania Bara yaani, Ngazi ya Shina, Tawi, Kata, Wilaya, Mkoa na Taifa na kwa Upande wa Zanzibar una ngazi 7 yaani Shina, Tawi, Wadi, Jimbo, Wilaya, Mkoa na Taifa.

Kamati ilifafanua kwenye taarifa yake je muundo huu unakidhi haja? Kuna mapendekezo gani toka kwa Vijana juu ya muundo huu.

Taarifa hiyo ilinukuliwa ikisema kamati itakuwa na wajibu wa kubuni na kutoa mapendekezo kutokana na maoni ya wadau, utaratibu mzuri wa kuboresha vyanzo vya mapato na hivyo kuimarisha UVCCM kimapato.

“ili kutimiza malengo hayo hapo juu, kamati hii itafanya kazi na kukutana na makundi mbalimbali. Makundi hayo ni pamoja Viongozi na Wanachama wa CCM na UVCCM na Viongozi waastafu wa CCM na UVCCM, Makada mbalimbali kama vile wanamichezo, wasanii, wamachinga, wavuvi, wasomi, waandishi wa habari, makamanda wa UVCCM na asasi zisizo za kiraia zinazojishughulisha na vijana,” ilisema taarifa hiyo.

Kamati hiyo ndogo itayokusanya maoni na Kuandaa mapendekezo ya mageuzi ndani ya UVVCM iliundwa na Baraza kuu la UVCCM Taifa lililokutana Dodoma tarehe 19/03/2011.
 
Hii kamati mbona haifanyi kazi yake badala yake inataka kupokonya madaraka ya viongozi wa juu wa UVCCM yenyewe; Hivi ukitumwa kufanya kazi yoyote kama kamati Press conference ya nini?

Kesho utasikia Mwingine anaibuka kusema hawajamtuma hayo anayoongea, matamko kwenye vyombo vya habari ya nini?
 
Nimemwangalia Mwenyekiti wa kamati ya kujivua gamba ya UVCCM Hussein Bashe akizungumza na vyombo vya habari. Anasema lengo la kamati yake ni kuhakiksha UVCCM inaendelea kuaminiwa na vijana na kwamba ni vizuri kufanya marekebisho wakati Chama kikiwa madarakani. Je, Bashe anaamini anachokisema? Marekebisho yapi? Yatoke kwa nani? Kwa maslahi ya nani? Wananchi wana imani na porojo hizi?
 
Back
Top Bottom