Huraa,BoT,mmeonyesha njia.Nitakalo kusema hata hivyo ni kwamba, tatizo hili haliko BoT tu,limezagaa nchi nzima.Na ni kubwa kiasi cha kutisha.Sasa serikali kwa makusudi kubisa itoe vihiyo wote walioko ndani ya serikali yenyewe, mashirika ya umma na binafsi.Kila cheti kihakikiwe upya, ni rahisi.Naamini kwamba utendaji mbovu uliokithiri katika serikali yetu na mashirika ya umma na binafsi, unaletwa kwa kiasi fulani na vihiyo hawa.Ninaamini pia kwamba ni rahisi zaidi kumhonga kihiyo kuliko msomi aliye bobea.Ni swala la 'mindset'.Mtu mwenye akili nzuri,si rahisi kuwa fisadi.Fisadi ni mtu mwenye matatizo ya akili.Amefirisika kiakili.Kwa hiyo tukitoa vihiyo tutapunguza ufisadi kwa kiasi fulani.