Hukumu ya Zombe: Aachiwa!

Kwa mtizamo wa haraka, mauaji ya vijana hawa yangetokea leo isingeundwa tumeya rais wala kusikia tamko lolote kutoka kinywani mwake na akina Zombe na wenzake wangepewa pongezi nyingi mno kutoka kwa watawala wetu. Kuundwa kwa Tume ya Mhe Kipenka na kukamatwa kwa akina Zombe ilitokana na upya/ugeni wa madaraka/ofisi kwa watawala waliokuwepo wakati huo kuanzia Rais na wale wa chini yake. Kwa siku za karibuni mauaji mengi ya kiholela yamefanywa na askari ama raia lakini hakuna hatua zozote zilizochukuliwa. Mauaji ya albino, polisi walioua Tunduma, Arusha Dar (Kimara) Kyela na kwingineko ni mifano michache ya matukio ya kutisha ambayo yanatokea ndani ya utawala wa sasa pasipo hatua zozote kuchukuliwa.

Mungu zirehemu roho za wale wote waliofikwa na mauti kwa njia hii ya kishetani na mkono wa Mungu uwaelemee wahusika wote popote pale walipo.
 
ni pigo kubwa kwa wapenda amani na haki wa Tanzania kuna kila sababu ya kuhoji maamuzi ya jaji massati kweli tunapoelekea nathubutu kusema Tanzania inaelekea mwisho wake , wananchi wanapoteza imani na vyombo vyao kama mahakama na polisi, hivi kweli miongoni mwa watuhumiwa kuna waliokiri mahakamani kuelewa nani alitoa amri ya mauaji na walikuwepo ni ushahidi gani massati alihitaji kuelewa hilo?
nachoweza kukiri ni kuwa MUNGU yupo na atawapigania wanyonge watanzania i remain to be living ila watuhumiwa hao wote waliohusika ikwa ni pamoja na jaji aliyetoa hukumu hawana muda mrefu wa kuishi mungu atawaaadhibu tu na uovu wao utaoneshwa.poleni sana familia za mahenge na wapenda haki wa tanzania.
li nchi hili na viongozi wake wametuchosha kweli nimeshikwa na simanzi sanaa.im real down with the way mambo yanaenda bongo,,,
 
Kama utawara wa sheria ndio huu basi hata wakina Chenge, Luwassa, kalamagi, Msabaha,hosea,mwanyika,Mlamba, Yona, Mgonja, waachane nao kwa maana wataigalagaza serikali na kuishia kuwalipa vijisenti vya wananchi walipa kodi. Ukijumlisha na mapesa waliyokwisha kwapua sasa mtawafanya wakwasi. mahakama haina uwezo wa kuadhibu wahalifu hivyo visheria havifai ,na vimepitwa na wakati .Tutaishia kutiana machungu basi.
 
Kama Mahakama imemuachia huru kwa kutokukamilika kwa ushahidi, anaeona ana ushahidi wa kutosha auhukumu kisa watajuana kwa Mwenyezi Mungu.
 
Sheria bwana ni kitu cha ajabu sana!
Lakini kila jambo linalotokea lina maana yake...!
Na malipo yote hufanyika hapahapa duniani...!
Sheria ishafanya kazi yake na kashaonekana hana hatia,hata tukilalamika haitasaidia kitu,kilichobaki kikubwa tusubiri tuone kama serikali itakata rufaa au la!
Na kingine tulisubiri jeshi la polisi lifanye huo uchunguzi lilete hao waliohusika na mauaji...!!!
Kazi kubwa sasa ipo kwa serikali na hilo jeshi la polisi!Kazi kwao...!!!
 
mmh nilimuona mamamwenye nyumba wa zombe mahali akisema waliodhani atafulia sababu mumewe kawekwa ndani walie tu,hafulii na mungu anamjalia afya na yuko na yeye siku zote nikajua huyu tayari atakua kaongea na mumewe na kampa uhakika kama kesi hamna kitu anarudi uraiani,sasa naamini hisia zangu yaani hiyo nchi ni kuzimu hakyanani duuu.


Naamini atakuwa bi mdogo Fatuma, maana ni mpayukaji mzuri sana. Hajatulia na sijui Zombe atalipiza kisasi kwa akina nanihino!!!! Akina nanihino wa Keko magereza, tahadhari!!!!
 
Jaji ameshindwa kutetea damu za marehemu. Hivyo basi, mikono yake naye imejaa damu za marehemu. Mpaka wakati wake ukifika akumbuke hilo

let us base our arguments on facts sio ushabiki..i agree kuwa waendesha mashtaka wetu ni mbumbumbu..Zombe alisema toka mwanzo kuwa hakuna kesi pale
 
Yote anajua mwenyezi mungu wao waseme na vyeo vyao, pesa zao, kujuana kwao maana nchi ni yao si yetu lakini ipo siku moja tu yote yatakua na mwisho kwani binadamu wote tunaamini kuwa no longer at ease kwa maana hiyo basi wamewatanguliza wenzao ila na wao hivyohivyo ni njia nawo pia wataipitia, mauti ni ya kila binadamu kwa hiyo bado hawajashinda kama ni mtihani basi final bado pua zote zimetizama chini hakuna iliyoenda juu hata moja na kama ipo basi inamatatizo uchungu waupatao wanandugu basi ipo siku wataulipa iyo wakae wakilijua.

Nasikia uchungu kupita kiasi utadhani aliyeuwawa baba yangu yani wana JF tumuombeni mola sana
 
Kama Mahakama imemuachia huru kwa kutokukamilika kwa ushahidi, anaeona ana ushahidi wa kutosha auhukumu kisa watajuana kwa Mwenyezi Mungu.


My God !!!!!!!! We are going to die all of us kwani sasa naona huu ndio mwisho wa dunia kwani itafikia kipindi hii selikali yetui ukiwa anajua kitu basi wanatumwa tu ua huyu ukionekana maisha umeyapatia utaitwa jambazi na amri inatoka tu ua rijambazi hilo sasa kama si mwisho wa dunia nini ? jamani jamani jamani we tired for this rearly !!!!!!!!!!!!!
 
Dakika chache baada ya Jaji Salum Masati kuwaachia huru washitakiwa hao baada ushahidi uliowasilishwa na upande wa mashtaka, kushindwa kuwatia hatiani, mayowe yalisikika mahakamani hapo yakitaja jina la zombe, zombe zombe kama ishara ya kufurahiswa na hukumu hiyo.

Hata hivyo, sambamba na washangilia ushindi huo, baadhi ya wananchi waliokuwepo mahakamani hapo walionesha hisia za kupinga wazi wazi uamuzi huo wa mahakama kwa kuzomea na kupiga mawe magari ya polisi yaliyokuwa mahakamani hapo. Awali, akisoma hukumu, Jaji Masati alisema kuwa, vielelezo vilivyowasilishwa mahakamani hapo na upande wa mashtaka ni vya kimazingira na hafifu na kwamba vimeshindwa kubainisha pasipo shaka kuwa, washtakiwa hao walitenda kosa hilo.

Sakata zima la kesi hii ya Zombe mwanzo mwisho (A-Z) linatiririka kama hivi: Januari 14, 2006 (mauaji) Oysterbay wawatia mbaroni wafanya biashara hao. Askari kutoka katika vituo vya polisi Chuo Kikuu, Urafiki na kuwatia mbaroni wafanyabiashara hao eneo la Sinza Palestina wakiwatuhumu kuhusika na uporaji wa pesa za Kampuni ya Bidco katika Barabara ya Sam Nujoma.

Januari 15, 2006: Zombe atamba kuua majambazi sugu. Januari 16/ 17 2006: Utata waibuka waliojitambulisha kuwa ni ndugu wa waliouawa wafika kwenye vyombo vya habari na kudai kuwa waliouawa ni ndugu zao na kwamba hawakuwa majambazi bali walikuwa ni wafanyabiashara wa madini kutoka Wilaya ya Mahenge mkoani Morogoro. Vyombo mbalimbali vilifanya utafiti dhidi ya utata huo lakini Kamanda Zombe alisisitiza kuwa ni majambazi, alidai wao ni wataalamu ndiyo wanaojua majambazi na wafanyabiashara .

Vyombo vya habari vyajikita kufanya uchunguzi eneo la Sinza kwenye Ukuta wa Posta alikosema Zombe kuwa ndiko walikouliwa wafanyabiashara hao baada ya kurushiana risasi na polisi, wananchi wa eneo husika wakana kusikia milio ya risasi katika eneo hilo kwa siku iliyotajwa. Baadhi ya vyombo vya habari vilienda katika kampuni ya Bidco kuthibitisha madai ya kuporwa pesa. Bidco walikiri kuporwa pesa lakini walikana kuwa alizozionyesha Zombe siyo zao na kwamba za kwao zilikuwa hazikufungwa.

Vyombo vya habari vyamuuliza Kamanda Zombe kuhusu utata huo, lakini Zombe alishikilia msimamo wake na kufoka kuwa asifundishwe kazi. Januri 23, 2006: Rais Jakaya Kikwete aunda Tume ya Jaji Kipenka kuchunguza ukweli wa mauaji hayo. Januari 24. 2006: Tume yaapishwa na kupewa siku ishirini na moja za kufanya kazi siku hiyo hiyo ilianza kazi kwa kuweka sawa mikakati.

Januari 25, 2006: Tume yatoa matangazo kwenye vyombo vya habari kuwataka watu wote wenye taarifa zozote kuhusu mauaji hayo wajitokeze kutoa ushahidi mbele ya tume hiyo. Januri 26, 2006: Tume yaanza kuwahoji mashahidi katika Ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam, ilianza na askari waliohusika na wananchi wa kawaida, yahoji watu zaidi ya 90 Dar es Salaam, Arusha na Mahenge Morogoro. Mbali na kuandika yatumia vinasa sauti 36 kuhifadhi kumbukumbu za mahojiano.

Tume ilikabidhi ripoti kwa Rais Februari 17, 2006 Februari 20, 2006 mwanzo wa kesi askari kumi na moja bila Zombe walipandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kwa tuhuma za mauaji ya wafanyabiashara hao na kusomewa mashtaka ya kuua kwa kukusudia. Juni 9, 2006: Zombe apandishwa kizimbani na kusomewa mashtaka ya mauaji peke yake mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi Addy Lyamuya.

Juni 15, 2006: Zombe afutiwa shitaka la mauaji ya wafanyabiashara hao lililokuwa likimkabili peke yake na kuunganishwa na washtakiwa wenzake kumi na moja mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi Mfawidhi Sivangilwa Mwengesi na kuwa mshtakiwa wa kwanza katika kesi hiyo.

Septemba 28, 2006 Washtakiwa wote walipandishwa kizimbani katika Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Dar es Salaam kwa mara ya kwanza mbele ya Jaji Laurean Kalegea . Mei 2008: Kesi yaanza kusikilizwa chini ya Jaji Kiongozi Salum Massati sehemu hiyo ya kwanza ilisikizwa kwa awamu tatu.

Mei 26, 2008: Mahakama yaanza rasmi kusikiliza ushahidi kutoka upande wa mashtaka. Mei 30, 2008: Zombe awawakia waendesha mashitaka awatuhumu kuwa wanachelekewesha kesi kwa makusudi kwa kuandaa mashahidi wachache ili waendelee kupata posho kubwa kutokana na kuendesha kesi hiyo.

Juni 9, 2008: Mashahidi wadai wao ndiyo majambazi ni shahidi wa ishirini na tano upande wa mashtaka (PW 25 Shabani Sain Manyanya) na PW 26 Ramadhan Said Tupa wadai wao ndio walipora pesa za Bidco ambazo washtakiwa walidai ziliporwa na marehemu (wafanyabiashara). Waliwaacha midomo wazi wananchi waliokuwa wakifuatilia kesi hiyo mahakamani. Juni 12, 2008: mwisho wa awamu ya kwanza ya sehemu ya kwanza jumla ya mashahidi 29 watoa ushahidi.

Septemba 1, 2008, awamu ya pili (sehemu ya kwanza) shahidi afichua siri ya mauaji ni PW 30 Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora Emson Mmari alikuwa mjumbe kwenye timu iliyoundwa na Mkuu wa Jeshi la Polisi ‘IGP’ Said Mwema kuchunguza chanzo na ukweli wa mauaji hayo na alikuwa akifanya kazi Makao Makuu ya Jeshi la Polisi, alielezea mahakama kuwa wafanyabiashara hao waliuliwa katika Msitu wa Pande ulioko Mbezi Luis, alidai kuwa walikuwa wakirushwa kwenye gari mmoja mmoja na kulazwa chini na kupigwa risasi.

Septemba 2, 2008: Mahakama yazuru eneo la mauaji.
Mahakama ilianzia Sinza walikokamatwa wafanyabiashara kabla ya kuuawa kisha ikaenda Barabara ya Sam Nujoma lilikodaiwa gari la Kampuni ya Bidco lilikoporwa pesa, halafu Sinza Ukuta wa Posta yalikodaiwa kutokea mapambano baina ya polisi na wafanyabaishara waliouawa kisha mahakama ikaenda Msitu wa Pande. PW 30 alionyesha mahakama mahali wafanyabiashara walikolazwa na kupigwa risasi.

Yamaliza Bunju kulikodaiwa kuwa mshtakiwa wa pili alilazimisha baadhi ya washtakiwa wafyatue risasi hewani ionekane silaha zilitumika kwenye mapambano, wananchi waliwazomea akina Zombe.

Zombe, Koplo Lema wazozana Zombe na aliyekuwa mshtakiwa wa kumi na moja Rashid Lema wazozana chini kwa chini baada ya Zombe kuonyesha kushangaa msitu huo na kudai hajawahi kufika katika eneo hilo.

Septemba 7, 2008 Mwisho wa awamu ya pili sehemu ya kwanza jumla ya washahidi watatu tu ndiyo walioweza kupata nafasi walitoa ushahidi na kufanya mashahidi kufikia 32. Septemba 26, 2008 . Upande wa mashtaka wafunga ushahidi katika awamu ya tatu ya sehemu ya kwanza iliyoanza Septemba 22.

Februari 3, 2009. Sehemu ya pili – utetezi Februari 4, 2009 Hoja ya utetezi. Mawakili upande wa utetezi wawasilisha hoja zao wakijaribu kupangua ushahidi uliotolewa mahakamani na upande wa mashtaka wadai wateja wao (washtakiwa) hawana kesi ya kujibu kwa kuwa upande wa mashtaka umeshindwa kuthibitisha mashtaka juu yao. Waiomba mahakama iwaachie huru . Febuari 5, 2009. Hoja upande wa mashtaka: Waendesha mashataka (PP) wajibu hoja za utetezi huku wakirejea ushahidi walioutoa wadai washtakiwa wote wanahatia.

Februari 9, 2009: Uamuzi wa Jaji Massati kuwaachia huru washtakiwa watatu PC Noel Leonard (4) Koplo Moris Nyengelela (6) na Koplo Felix Cedric (8) asema hawana kesi ya kujibu Zombe na wengine tisa wabanwa jaji asema wanakesi ya kujibu Zombe ataka aanza kujitetea siku hiyo . Februari 10. 2009: Zombe ajitetea apanda kizimbani na muongozo wa utetezi wa Jeshi la Polisi General Order (PGO). Ajitetea kwa saa tatu kesi yaahirishwa bila kumalizika.

Februari 12, 2009: Bageni naye kizimbani. Zombe amalizia utetezi wake na kueleza kilichomsikitisha ni kitendo cha kubambikiwa kesi na aliyekuwa Mkurugenzi wa Mashtaka wa zamani (DPP) Godfrey Shahid ambaye kwa sasa ni Jaji wa Mahakama Kuu.

Atumia saa nane kujitetea; mshtakiwa wa pili SP Christopher Bageni, Mkuu wa Upelelezi naye asononeka kizimbani ajitetea lakini naye aeleza kuwa anamlilia dada yake baada ya kusikia amekamatwa (Bageni) Februari 15, 2009 Makere alia na Zombe ni mshatakiwa wa tatu ASP Ahmad Makele Mkuu wa Upelelezi Kituo cha Urafiki akili kuwakamata marehemu wakiwa hai lakini awatupia mpira askari wa Chuo kikuu kuwa wao ndiyo walioondoka nao na kusema Zombe alimbambikia.

Febuari 19, 2009, Koplo Lema bado hoi ashindwa kufika mahakamani kujitetea. Zamu yake mshtakiwa wa kumi na mbili Koplo Rajab Bakari, naye akwama kujitetea akidai kuwa kuna maneno ambayo ni lazima Koplo Lema aseme kwanza kwa mdomo wake ndipo na yeye aweze kujitetea.

Machi 2, 2009 Koplo Lema alazwa. Hali yake yabadilika na kupelekwa katika Hospitali ya Wilaya ya Temeke kwa matibabu.

Machi 3, 2009: Ahamishiwa Hospitali ya Muhimbili Mchi 19, 2009: Ahamishiwa katika Taasisi ya Saratani Ocean Road Aprili 3, 2009, Aaga dunia saa kumi alfajiri katika Hospitali Bingwa ya magonjwa ya saratani Ocean Road jijini Dar es Salaam.

Aprili 21, 2009: Wakili wa Zombe Moses Mailla alifariki dunia saa tano na adhuhuri kwa ugonjwa figo katika Hospitali ya Bentab Memorial Houston Texas nchini Marekani alikokuwa amekwenda kwa ajili ya matibabu.

April 28, 2009. Mahakama yafuta mashtaka rasmi dhidi ya Koplo Lema . Koplo Rajabu Bakari atoboa siri ya mauaji ajitetea kwa saa tano na dakika kadhaa akili kushuhudia mauaji na kuelezea ilivyokuwa hatua kwa hatua na kudai tukio hilo lilikuwa kubwa kwake hajawahi kuona aeleza viongozi wake kuficha ukweli wa tukio hilo huku wakitishiwa kuwa atakayetoa siri atabebshwa msalaba mwenyewe.

Aprili 29 na 30, 2009 Kesi yaahirishwa mara mbili baada ya wakili wa mshatakiwa wa kumi na mbili Denis Msafiri augua na kushindwa kuhudhuria mahakamani.

Mei 4, 2009: Zombe aomba kujiteta upya shahidi amwacha Zombe njia panda pia alidai kuwa washtakiwa hao walikamatwa na simu mahabusu vocha na pesa walizokuwa wanazitumia kuwasiliana na DPP na kwamba mkuu huyo wa Gereza la Ukonga ni shahidi wake.

Mei 5, 2009 Jaji Massati amgomea, adai sababu zake si za msingi. Asema hatua hiyo itaathiri mwenendo mzima wa kesi, Mawakili wa mshtakiwa wengine nao wamwekea ngumu. Mei 6, 2009: Mahakama yafunga rasmi ushahidi wa utetezi. Na kutaja tarehe nyingine ya mahakama.

Mei 7, 2009: Mawakili wa utetezi watupa karata yao ya mwisho kuwanasua wateja wao walia maelezo ya Koplo Lema wakiisihi mahakama isiyatumie katika mwenendo wa kesi hiyo. Juni 25 2009 upande wa mashtaka wajibu hoja ya utetezi wadai waweza kuthibitisha juu ya washtakiwa wote na kwamba wote wanahatia wamchambua mshtakiwa mmoja mmoja na kueleza jinsi walivyothibitisha mashtaka dhidi yake.

Juni 26, 2009: Majumuisho. Maoni ya wazee wa Baraza wamtakasa Zombe wadai hana hatia kwamba upande wa mashtaka umeshindwa kuthibitisha mashtaka dhidi yake kwa kuwa katika mashahidi wake 37 hakuna hata mmoja aliyeweza kuthibitisha Zombe kuhusika na mauji hayo moja kwa moja.

Agosti 17, 2009: Hukumu!!! Washtakiwa wengine waliobaki katika kesi hiyo baada ya wengine kuachiwa huru na mwingine kufariki Dunia ni pamoja na ACP Abdallah Zombe SP Christopher Bageni, ASP Ahmes Makele WP 4595 Jeni Andrew Koplo Emmanuel Mabula PC Michael Sonza CPL Ebeneth Salo C/CPL Rajab Bakari na D Koplo Festus Gwabisabi.

Wakati huo huo, jana majira ya saa 11 jioni, Uwazi liliongea na Mbunge wa Ulanga Mashariki, wanakotoka wafanyabiashara hao waliouawa, Mhe. Celine Ompeshi Kombani (CCM), ambaye alikiri kuwa marehemu walikuwa ni wapigakura wake na kusema kwamba hana cha kuchangia kwenye maamuzi yaliyotolewa na mahakama ila kama imeamua kuna watuhumiwa waliohusika na mauaji hayo wachukuliwe hatua stahili.

“Nikweli marehemu walikuwa ni wapiga kura wangu ila kama mahakama imeamua sina cha kusema, kwani hayo ni masuala ya sheria, lakini kama pia imesema kuwa kuna watuhumiwa ambao walihusika basi watafutwe na sheria ichukue mkondo wake,” alisema mbunge huyo kwa njia ya simu kutoka Morogoro alikokuwa kikazi.
 
Jamani jamani wana JF wenzangu tunapaswa kufikiri kwa umakini huyu mwandishi wa habari anamakosa gani ikiwa tume yenyewe iliyoagizwa na mkuu wa nchi mwenyewe walithibitisha kuwa zombe ni mtuhumiwa leo iweje kwa mwandishi jamani yani mi roho inaniuma sana natamani huyo zombe aje aniue tu na mimi yani wametengeneza mazingira wana JF wenzangu muda si mrefu utasikia zombe anaidai fidia selikali kwa kumuita muuaji lakini lile fungu ataenda kugawana na hao hao mi papa pamoja na huyo mkuu wao wa nchi yani mi namchukia kodi zetu zinafanywa ni mtaji wao yani mwenzenu roho inananiuma sana mshaharara wangu unavyopanguliwa kodi kubwa inaniuma sana sasa muuaji kaachiwa wezi wa epa kuna nini tena sijui tujikwamue vipi nashindwa hata kuendelea kuandika mikono inatetemeka kwa hasira
 
Mkuu ulitaka Jaji afanyeje, awe nje ya sheria? Maamuzi ya sheria hayaendani na utashi wa wananchi wanataka maamuzi yawe vipi.

Ukiniambia kwamba waendesha mashitaka wa serikali ndio wamechemka hapo tutakuwa pamoja lakini sio Jaji.

Kuntakinte uko sawa kabisa,waendesha mashtaka waliandaa mashtaka kwa kukurupuka au yawezekana pia tulikuwa tunapigwa changa la macho.

kilichopo tugange yajayo hiyo ndo imeshatoka hivyo.
 
Kuntakinte uko sawa kabisa,waendesha mashtaka waliandaa mashtaka kwa kukurupuka au yawezekana pia tulikuwa tunapigwa changa la macho.

kilichopo tugange yajayo hiyo ndo imeshatoka hivyo.

Hii ndio bongo bwana!! Mimi nakubaliana na wewe 1 kwa 1!! kwamba lilikuwa changa la macho!! Mahakamani hatufuati haki bali sheria! hawa wanasheria wa serikali walijua toka mwanzo mashitaka hayana nguvu ya kisheria. Hakuna la ajabu, mambo ya mahakama hakuna mtu asiyeyajua, kesi zinaamuliwa usiku kwenye vikao maalum, mchana pale kortini ni danganya toto!! Subiri jamaa aingie mtaani, wabaya wake wote watamtambua!!
 
let us base our arguments on facts sio ushabiki..i agree kuwa waendesha mashtaka wetu ni mbumbumbu..Zombe alisema toka mwanzo kuwa hakuna kesi pale

Lakini pia kusema ni mbumbumbu, mie siamini! They know exactly what they planned to do and they have done it!
 
Tuache ku-interpret sheria kama a linguistic trash.Ushahidi kwenye kesi ya Zombe uwezekano ni mkubwa kwamba ule ushahidi haukuwa water-tight.
Mnataka sheria itafsiriwe kwa ushahidi kisa kila mtu alikuwa anataka Zombe ahukumiwe?
Hata kama ameua yeye,the prosecuting side did not do the needful to make sure Zombe was convicted of the crime he was alleged to have committed.
Tusisahau kwamba KAtiba ya Muungano ina assume presumption of innocence.
Tuache kujifanya mahakimu wakati hatujui sheria
 
Kwa mtizamo wa haraka, mauaji ya vijana hawa yangetokea leo isingeundwa tumeya rais wala kusikia tamko lolote kutoka kinywani mwake na akina Zombe na wenzake wangepewa pongezi nyingi mno kutoka kwa watawala wetu. Kuundwa kwa Tume ya Mhe Kipenka na kukamatwa kwa akina Zombe ilitokana na upya/ugeni wa madaraka/ofisi kwa watawala waliokuwepo wakati huo kuanzia Rais na wale wa chini yake. Kwa siku za karibuni mauaji mengi ya kiholela yamefanywa na askari ama raia lakini hakuna hatua zozote zilizochukuliwa. Mauaji ya albino, polisi walioua Tunduma, Arusha Dar (Kimara) Kyela na kwingineko ni mifano michache ya matukio ya kutisha ambayo yanatokea ndani ya utawala wa sasa pasipo hatua zozote kuchukuliwa.

Mungu zirehemu roho za wale wote waliofikwa na mauti kwa njia hii ya kishetani na mkono wa Mungu uwaelemee wahusika wote popote pale walipo.
Nilikuwa napita tu hapa.........
 
Nilikuwa napita tu hapa.........

Kwa mtizamo wa haraka, mauaji ya vijana hawa yangetokea leo isingeundwa tumeya rais wala kusikia tamko lolote kutoka kinywani mwake na akina Zombe na wenzake wangepewa pongezi nyingi mno kutoka kwa watawala wetu. Kuundwa kwa Tume ya Mhe Kipenka na kukamatwa kwa akina Zombe ilitokana na upya/ugeni wa madaraka/ofisi kwa watawala waliokuwepo wakati huo kuanzia Rais na wale wa chini yake. Kwa siku za karibuni mauaji mengi ya kiholela yamefanywa na askari ama raia lakini hakuna hatua zozote zilizochukuliwa. Mauaji ya albino, polisi walioua Tunduma, Arusha Dar (Kimara) Kyela na kwingineko ni mifano michache ya matukio ya kutisha ambayo yanatokea ndani ya utawala wa sasa pasipo hatua zozote kuchukuliwa
Usipite tu mkuu, angalia na kutafakari pia,
 
Tuache ku-interpret sheria kama a linguistic trash.Ushahidi kwenye kesi ya Zombe uwezekano ni mkubwa kwamba ule ushahidi haukuwa water-tight.
Mnataka sheria itafsiriwe kwa ushahidi kisa kila mtu alikuwa anataka Zombe ahukumiwe?
Hata kama ameua yeye,the prosecuting side did not do the needful to make sure Zombe was convicted of the crime he was alleged to have committed.
Tusisahau kwamba KAtiba ya Muungano ina assume presumption of innocence.
Tuache kujifanya mahakimu wakati hatujui sheria


Mkuu haya Mapungufu mara nyingi hufanywa makusudi na mfumo kupitia ofisi ya Mwendesha Mashikata.(DPP).


Ebu cheki kipande cha hukumu ya Jaji.
At the beginning of this judgment I started by declaring that the victims were brutally killed. This has remained

so todate. The only question was, whether it was these accuseds who actually did so? After going through the
evidence on record, I have come to the conclusion that it is not so. There is no direct or circumstantial evidence
to show that any of them killed the victims. The nearest evidence was that some of them i.e. the 2nd, 3rd and
the 12th accused were present at the scene of the killings and witnessed them, but they did not kill in person.
The closest offences the 2nd and 3rd and 12th accuseds could have been convicted of, is for their role as aiders
and abettors; but in the absence in court, of the actual perpetrators the case against them is not made up but

remains that of strong suspicion, which is not sufficient to found a conviction. In the
228
absence of the actual perpetrators it is difficult to establish common intention among the accused persons.

As Mr. Magafu learned counsel, has rightly observed throughout the trial and it cannot be gainsaid that this
case was hastily investigated and taken to court. Although the Commission of Inquiry had recommended the
prosecution of 15 suspects (excluding the 1st accused) only 12 of them thus listed were charged, leaving out

some crucial parties. In so doing, the prosecution, according to PW30 and PW36 depended heavily on the

statements of the 11th and 12th accuseds. But as BARTH C.J. of Kenya said in R V KAMAU (1924) 10 KLR. 8
"Shortcuts are usually inexpedient, and every effort should be made to prove the case alleged against an
accused without a reliance on a confession which can as easily be retracted as made. The police should not be
satisfied that a confession having been obtained, a case is completed".
Applying that observation in MANUBHAI HIRA v. THE CROWN (1945) 7 ZLR,4 the Eastern African Court of
Appeal remarked:
229
"The learned Chief Justice in R v KAMAU was in that case dealing with a confession, but what he then said
applies with equal force to other statements made to the police by accused persons in custody. Such statements
are as easily denied or retracted as made and the police should not be satisfied that their investigation is
complete unless and until they have, apart from anything the accused person may have said, obtained the best
and fullest evidence to support the charge."
This was clearly demonstrated in the present case, as we have observed on the evidence on record. Apart from
the 11th and 12th accuseds' statements, the only other independent medical and ballistic and circumstantial
evidence was inconclusive and could not prove the case against the accused persons beyond reasonable.
With these few concluding remarks, I now proceed to declare that the prosecution has failed to prove their case
against the accused persons beyond reasonable doubts. I therefore find all the accuseds not guilty and acquit
them of all the counts.
230
I order that they be released immediately from prison, unless otherwise lawfuly held. I also order the police
force to intensity their efforts in tracking down the actual perpetrators of these offences and bring them to
book.
It is so ordered.
S.A.Massati
JAJI KIONGOZI.(rtd)
17.8.2006
Assessors thanked and discharged.
S.A.Massati
JAJI KIONGOZI. (rtd)
17.8.2009
 
Back
Top Bottom