Rev. Mtikila ameiambia BBC kwamba usiku kucha leo hakulala kwa kutofahamu ni hatua gani atachukua endapo hukumu ya Mahakama ya rufaa itamwangusha. Mimi namshauri tu kwamba wakati wa kuwa na mgombea binafsi hasa kwenye ngazi ya URAIS bado. Aachane kwa sasa na mradi huu ambao nia yake ni nzuri tu kwa hapo baadae. Kwa sasa hatuna chaguzi huru, hatuna tume huru ya uchaguzi, miundombinu ya uchaguzi bado ni duni sana, elimu ya uraia ni ya kiwango cha chini sana kwa wapiga kura wetu, umasikini wa watu wetu unatisha, vyombo vya dola bado ni vya chama kilekile,.....
Tuna mengi ya kushughulikia kwa sasa kabla ya hili la mgombea huru.
Mkuu ninakubaliana na hoja zako kwamba kuna mambo mengi sana ya kutatua, lakini kila kitu kina mwanzo wake. Tukisema tukae tusubiri serikali ya CCM ifanye kazi hiyo, hawawezi maana mazingira yaliyopo yanawapa nafasi ya kushinda kirahisi kwenye chaguzi. Iwapo tutafanikiwa kubadilisha kitu kimoja kimoja, tutafika mahali pazuri. Mtoto huwa haanzi kwa kukimbia, lazima atambae, asimame then anapiga hatua moja na kudondoka na finally anaweza kutembea na kukimbia.
Ninakubaliana na idea yako kuhusu nafasi ya mgombea urais kutogombewa na wagombea binafsi, lakini kwenye Ubunge sioni ubaya wake. Vyama vya siasa vimekuwa vikiminya demokrasia kwenye nominations, na hasa CCM. Ndio maana final list huwa inatolewa two or three days kabla Tume ya Uchaguzi (NEC) haijafunga kupokea fomu za wagombea. CCM wanafanya hivyo ili mtu akinyimwa haki asiweze kukatiza kwenda chama kingine, lakini kama kuna opportunity ya mgombea binafsi ni rahisi kuamua kujaza fomu na kuzipeleka NEC as independent candidate.
Kwa hayo yanayofanywa na CCM ni kuwabana na kuwaondoa diplomatically wale wote ambao wanaweza kuonekana wanakwenda against maslahi ya chama. Subiri nominations za mwaka huu ndio watu wataelewa kwanini serikali imekuwa ikipiga dana dana swala la mgombea binafsi, maana muathirika mkubwa ni CCM na ndio maana wanakwepa sana swala hilo.