Huku Ndio Kusherehekea Muungano??

BabaDesi

JF-Expert Member
Jun 30, 2007
6,032
3,944
Ninaangalia maadhimisho ya sherehe za Muungano yanayoonyeshwa moja kwa moja na kituo cha televisheni cha ITV. Mvua inanyesha. Watoto waliokuwa wakionyesha michezo ya halaiki wamemaliza michezo yao na badala ya kutolewa kiwanjani, wamekalishwa chini kwenye uwanja uliojaa maji huku mvua ikiendelea kunyesha, waheshimiwa wakiwa wamekaa jukwaani wakiangalia ngoma. umri wa wengi wa watoto hawa ni chini ya miaka 16. Hivi hakuna kiongozi yoyote mwenye busara anayeweza kutoa amri watoto wale wanyanyuliwe pale walipo na wakajibanze banze sehemu nyingine badala ya kukaa chini ambapo pameloa chapa chapa?? Huku ndio kuwajali watoto wetu?? Huku ndio kusherehekea Muungano?? Imeniuma sana.
 
Ukiuliza utaambiwa wale ni wanajesshi wamejiandaa kwa hali yeyote mvua na jua....kwanza hawana sehemu ya kukaa maana wako 1000...na uwanja umeshajaa pomoni...
 
BabaDesi heshima mbele mkuu, hiyo ndiyo hulka ya viongozi wetu kujifikiria interests zao kwanza halafu watu wengine baadae; hata wakiwa watoto!!
 
Last edited:
Ukiuliza utaambiwa wale ni wanajesshi wamejiandaa kwa hali yeyote mvua na jua....kwanza hawana sehemu ya kukaa maana wako 1000...na uwanja umeshajaa pomoni...

...Inawezekana, Skills. lakini angalau basi wangeambiwa wasimame tu kuliko kukaa chini kwenye uwanja uliojaa maji. ama angalau basi wangeambiwa tu watawanyike maana shughuli yao iliishakwisha. Naamini wengi wangekimbilia nyuma ya jukwaa la kijani ambalo sijui siku hizi linaitwa nini!!
 
Hata mimi kile kitendo kilinichukiza, nikafikiri labda ni mimi tu.
Zaidi ya hapo uwanja ulikuwa umejaa wageni waalikwa kutoka kila kona ya dunia, sasa sijui tumejenga picha gani pale.
 
kwa nini kila siku sherehe kubwa za Muungano zinafanywa DAR?

No wonder wenyewe kule ZANZIBAR hawautaki huu muungano
 
"Hata mimi kile kitendo kilinichukiza, nikafikiri labda ni mimi tu.
Zaidi ya hapo uwanja ulikuwa umejaa wageni waalikwa kutoka kila kona ya dunia, sasa sijui tumejenga picha gani pale."
__________________

Kang:

Mvua ilipozidi kuendelea huku watoto wamekaa chini, kwa kwa nini JK, kama Amiri Jeshi Mkuu asitoe agizo la kusitisha shughuli ile iliyobakia (ile ya ngoma) ili kuwanusuru watoto? Hivi kweli mtu huyu ana huruma ya viumbe hawa? Inavyoonekana huruma yake kubwa huionyesha kwa mafisadi tu siyo kwa binadamu wengine.
 
Baba Desi,

Muungano ndio huo kama ulikuwa haujui! Lakini cha msingi siyo watoto kulowa maji au kutokulowa maji, cha msingi ni Je, wanauthamini Muungano wenyewe?Wanaufahamu au tunawapeleka puta bila kuwaeleza umuhimu na thamani ya Muungano.

Ahsante kwa kujali watoto wa Kitanzania.
 
Mvua ilipozidi kuendelea huku watoto wamekaa chini, kwa kwa nini JK, kama Amiri Jeshi Mkuu asitoe agizo la kusitisha shughuli ile iliyobakia (ile ya ngoma) ili kuwanusuru watoto? Hivi kweli mtu huyu ana huruma ya viumbe hawa? Inavyoonekana huruma yake kubwa huionyesha kwa mafisadi tu siyo kwa binadamu wengine.

Kweli bongo kazi ipo!, ufisadi ukipigiwa kelele wanalalamika unaharibu sifa ya Tanzania ulimwenguni. Sasa hao watoto waliokalishwa kwenye mvua hicho kitendo hakiharibu sifa ya Tanzania kwa hao viongozi waliokuja kushiriki. Very sad.
 
Kwani waandahaji wa hilo tamasha, hawakujuwa kuwa kutakuwa na mvua?

Sasa hao watoto maskini ya Mungu wakipata ugonjwa wa Pneumonia, litakuwa jukumu la nani kama si mzazi!?

Si kazi vitoto vingine hapo vina matatizo ya ugonjwa wa Ngiri tayari (
Hernia).

sidhani hata hao walio waandaa/kuwataarisha kama watawasaidia kwa hilo.
 
Last edited:

Similar Discussions

Back
Top Bottom