HUKU JK akiuza sura, Kibaki kujenga reli mpya Nairobi na bandari Lamu!

Phillemon Mikael

Platinum Member
Nov 5, 2006
10,533
8,619
Kenya wamezindua mradi mkubwa wa ujenzi wa mtandao wa reli ya umeme kuunganisha nairobi na vitongoji vya karibu na uwanja wa ndege ,mradi huu unakadiriwa kukamilika mwaka 2011.

Sambamba na hilo wametumia pesa walizopata kwa kuuza hoteli yao ya kifahari ya GRAND REGENY kwa serikali ya Libya kuanzishia ujenzi wa bandari mpya ya LAMU,hii inatarajiwa kuwa kubwa kuliko ya mombasa na tarari pesa za kumalizia mradi huu zimepatikana,MELI YA KWANZA ITATIA NANGA LAMU MWAAKA 2012.

Mradi wa bandari ya lamu unalenga soko la sudani kusini na sehemu ya kusini ya ethiopia...na pia reli zitajngwa kwenda huko sambamba.

Tanzania chini ya jk wameshindwa kuendeleza bandari ya kusini ya mtwara kulenga soko kubwa la kusini na ile ya TANGA kulenda soko la uganda na kaskazini ya tanzania kupitia musoma....pia pesa walizopata kwenye EPA au wanazodai kupata wameshindwa kuzitumia kwenye miradi inayopimika ...badala yake wanadai kuzitumia kwenye mradi wa kufikirika wa mbolea ambao wala hatutaweza kuupima wanananchi wa kawaida....ingekuwa busara kama wangejengea vitu vya kuonekana kama wenzao walivyofanya....
 
Huyo Kibaki miaka mitano ya kwanza alifanya nini?..
Yawezekana kabisa haya yote yametokana na serikali ya mseto.. Sisi je tumejiandaa vipi?
 
wewe mbona una wasi wasi?
sisi tuna mradi wa reli kwenda RWANDA itajengwa karibuni...

tuna mradi wa kujenga INTERNATIONAL airport kule BAGAMOYO itajengwa karibuni

tuna mradi wa refinery mpya itajengwa KARIBUNI

Tuna mradi wa bomba la mafuta toka TANGA-RWANDA-BURUNDI..itajengwa karibuni inshaalah

Tuna mradi wa kuvuna MVUA toka THAILAND inshaalah nayo itafanikiwa tuu

Tuna mradi wa MJI MPYA kule mbele sijui kunaitwaje..wasomali tayari wako site

Tuna mradi wa kujenga bandari BRAND NEW kule Bagamoyo itafanikiwa tuu ni uhai tuu mkulu

mwisho zaidi tuna mradi wa kuziba ule mtaro mbele ya HAIDERY PLAZA ambao unatoa harufu na maji machafu tangu mwaka jana ...isipokuwa taarifa ni kuwa meya wa ILALA na KIMBISA bado wanafanya feasibility study kujua lile shimo litazibwaje

at least for once you should be grateful kuwa nia TUNAYO,UWEZO TUNAO isipokuwa hatujajaaliwa tuu
 
Hivi mradi wa mvua ya Thailand bado umo vitabuni? Mimi nilidhani ulienda na Lowassa.
 


Sambamba na hilo wametumia pesa walizopata kwa kuuza hoteli yao ya kifahari ya GRAND REGENY kwa serikali ya Libya kuanzishia ujenzi wa bandari mpya ya LAMU,hii inatarajiwa kuwa kubwa kuliko ya mombasa na tarari pesa za kumalizia mradi huu zimepatikana,MELI YA KWANZA ITATIA NANGA LAMU MWAAKA 2012.

....

Nimehamasika! Watanzania labda wauze mbuzi zao wajenge reli. Daraja la kigamboni tumeweka tenda ya wafanyabiashara binafsi! Kaka JK iga basi haya mazuri mazuri!
 
Kenya wamezindua mradi mkubwa wa ujenzi wa mtandao wa reli ya umeme kuunganisha nairobi na vitongoji vya karibu na uwanja wa ndege ,mradi huu unakadiriwa kukamilika mwaka 2011.

Sambamba na hilo wametumia pesa walizopata kwa kuuza hoteli yao ya kifahari ya GRAND REGENY kwa serikali ya Libya kuanzishia ujenzi wa bandari mpya ya LAMU,hii inatarajiwa kuwa kubwa kuliko ya mombasa na tarari pesa za kumalizia mradi huu zimepatikana,MELI YA KWANZA ITATIA NANGA LAMU MWAAKA 2012.

Mradi wa bandari ya lamu unalenga soko la sudani kusini na sehemu ya kusini ya ethiopia...na pia reli zitajngwa kwenda huko sambamba.

Tanzania chini ya jk wameshindwa kuendeleza bandari ya kusini ya mtwara kulenga soko kubwa la kusini na ile ya TANGA kulenda soko la uganda na kaskazini ya tanzania kupitia musoma....pia pesa walizopata kwenye EPA au wanazodai kupata wameshindwa kuzitumia kwenye miradi inayopimika ...badala yake wanadai kuzitumia kwenye mradi wa kufikirika wa mbolea ambao wala hatutaweza kuupima wanananchi wa kawaida....ingekuwa busara kama wangejengea vitu vya kuonekana kama wenzao walivyofanya....

Kijana umechambua sana, lakini mbona mahospital makubwa mapya hayajengwi na ya kisasa? Au ndo hizo za zamani zinatosha mfano Bugando ,muhimbili na kcmc tu! Watu wameongezeka mabadiliko yawepo.
 
Miradi ambayo inaweza kupimwa utekelezaji wake ama kuhojiwa na wananchi sio jambo la kipaumbele kwa viongozi wa Tanzania, wao wanachotaka ni miradi ya majukwaani na fedha zinzazotengwa zihamishiwe kwenye mambo yao binafsi, ukiuliza sana utaambiwa hilo/hayo hayamo kwenye ilani ya chama tawala!. "MUNGU IBARIKI TANGANYIKA"
 
wewe mbona una wasi wasi?
sisi tuna mradi wa reli kwenda RWANDA itajengwa karibuni...

tuna mradi wa kujenga INTERNATIONAL airport kule BAGAMOYO itajengwa karibuni

tuna mradi wa refinery mpya itajengwa KARIBUNI

Tuna mradi wa bomba la mafuta toka TANGA-RWANDA-BURUNDI..itajengwa karibuni inshaalah

Tuna mradi wa kuvuna MVUA toka THAILAND inshaalah nayo itafanikiwa tuu

Tuna mradi wa MJI MPYA kule mbele sijui kunaitwaje..wasomali tayari wako site

Tuna mradi wa kujenga bandari BRAND NEW kule Bagamoyo itafanikiwa tuu ni uhai tuu mkulu

mwisho zaidi tuna mradi wa kuziba ule mtaro mbele ya HAIDERY PLAZA ambao unatoa harufu na maji machafu tangu mwaka jana ...isipokuwa taarifa ni kuwa meya wa ILALA na KIMBISA bado wanafanya feasibility study kujua lile shimo litazibwaje

at least for once you should be grateful kuwa nia TUNAYO,UWEZO TUNAO isipokuwa hatujajaaliwa tuu

duh.. tuna miradi mingi!
 
wewe mbona una wasi wasi?
sisi tuna mradi wa reli kwenda RWANDA itajengwa karibuni...

tuna mradi wa kujenga INTERNATIONAL airport kule BAGAMOYO itajengwa karibuni

tuna mradi wa refinery mpya itajengwa KARIBUNI

Tuna mradi wa bomba la mafuta toka TANGA-RWANDA-BURUNDI..itajengwa karibuni inshaalah

Tuna mradi wa kuvuna MVUA toka THAILAND inshaalah nayo itafanikiwa tuu

Tuna mradi wa MJI MPYA kule mbele sijui kunaitwaje..wasomali tayari wako site

Tuna mradi wa kujenga bandari BRAND NEW kule Bagamoyo itafanikiwa tuu ni uhai tuu mkulu

mwisho zaidi tuna mradi wa kuziba ule mtaro mbele ya HAIDERY PLAZA ambao unatoa harufu na maji machafu tangu mwaka jana ...isipokuwa taarifa ni kuwa meya wa ILALA na KIMBISA bado wanafanya feasibility study kujua lile shimo litazibwaje

at least for once you should be grateful kuwa nia TUNAYO,UWEZO TUNAO isipokuwa hatujajaaliwa tuu
mkuuu...

kuna miradi ya kugawia watu fedha yaani MABILIONI YA JK (KIBAKI AIGE AFE!!!)

Utaratibu wetu ni wa pekee na wa kupigiwa mfano kwa wasiopenda kusonga mbele...
 
wewe mbona una wasi wasi?
sisi tuna mradi wa reli kwenda RWANDA itajengwa karibuni...

tuna mradi wa kujenga INTERNATIONAL airport kule BAGAMOYO itajengwa karibuni

tuna mradi wa refinery mpya itajengwa KARIBUNI

Tuna mradi wa bomba la mafuta toka TANGA-RWANDA-BURUNDI..itajengwa karibuni inshaalah

Tuna mradi wa kuvuna MVUA toka THAILAND inshaalah nayo itafanikiwa tuu

Tuna mradi wa MJI MPYA kule mbele sijui kunaitwaje..wasomali tayari wako site

Tuna mradi wa kujenga bandari BRAND NEW kule Bagamoyo itafanikiwa tuu ni uhai tuu mkulu

mwisho zaidi tuna mradi wa kuziba ule mtaro mbele ya HAIDERY PLAZA ambao unatoa harufu na maji machafu tangu mwaka jana ...isipokuwa taarifa ni kuwa meya wa ILALA na KIMBISA bado wanafanya feasibility study kujua lile shimo litazibwaje

at least for once you should be grateful kuwa nia TUNAYO,UWEZO TUNAO isipokuwa hatujajaaliwa tuu

Pia mmesahau mradi wa kupanda na kuvuna wa DECI!!!!!!!!!!!
 
Kijana umechambua sana, lakini mbona mahospital makubwa mapya hayajengwi na ya kisasa? Au ndo hizo za zamani zinatosha mfano Bugando ,muhimbili na kcmc tu! Watu wameongezeka mabadiliko yawepo.

Mbili za hizo tatu zina wenyewe. Bugando ni msaada wa Roma kwa Marehemu Cardinal Rugambwa wakati KCMC ni nguvu ya waLuteri. Bila ya hawa wawili tusingekuwa na hospitali ya rufaa yenye jina nchini.
 
Mbili za hizo tatu zina wenyewe. Bugando ni msaada wa Roma kwa Marehemu Cardinal Rugambwa wakati KCMC ni nguvu ya waLuteri. Bila ya hawa wawili tusingekuwa na hospitali ya rufaa yenye jina nchini.

Aacha bwana eeh, mimi nilijua tumejengewa na serikali yetu, kumbe loh ,kweli tuna matatizo sana ndio maana hata viongozi wanatibiwa nje, napata shaka pia na hawa madactari wetu na vyuo wanavyosomea.
 
Phillemon ahsante sana tunashukuru ila kuna kitu unaoneaka unakiovalUku, sisi miradi yetu ni safari nje kwa sana. Mpaka sasa tumevunja record na tutaendelea kuivunja mpaka ikome si unaona saa hizi tuko Saudia kwa raha zetu?!?

The game unapoint sana lazima uwe genius kwa kweli umenivunja mbavu. Ila miradi ya harufu ni mingi, mingine hukuitaja, kuna ubungo karibu na urafiki na maeneo ya magomeni/jangwani. Pia kuna miradi ya mifereji ya maji machafu kama maeneo ya May Fair na shoppers plaza. Sina hakika kama Kimbisa na mwenzie watakuwa wamemaliza feasibility study kama Yesu hajarudi.

ILA TANZANIA NAKUPENDA LAKINI PIA NAKUONEA HURUMA SANA KWA KUKOSA UONGOZI TAIFANI MPAKA MTAANI KAMA SIO HADI NGAZI YA FAMILIA.
 
Hapa naona kila mtu anajaribu kuomyesha namna jk na serikali yetu tukufu inavyoshindwa kutekeleza majukumu yake jambo ambalo si la kweli ata kidogo.Utendaji wa serikali ya JK hauwezi kupimwa kwa vile Kibaki kajenga reli basi na sisi tujenge reli....ni ujinga kwa kweli.Kwa faida ya wasomaji wa hapa pengine niseme machache sana yaliofanywa na serikali ya Jk ili watu wote tuweze kuyapima.....kwanza ni ujenzi na upanuzi wa chuo kikuu cha dodoma....wanafunzi elfu alobaini wataingia hapo.....pili ni walter sector program inayotekelezwa kwa sasa ambapo kila mji utanufaika kwa maji safi kwa kiwango cha asilimia 94....kwa sasa tayari kigoma wameenza utekelezaji wa kuvuta maji toka mto malagalasina kusambazwa kigoma...wakazi wa maeeneo ya dar wanaona ujenzi wa mabomba mapya ya maji hususani maeneo ya tabata nimeshuhudia mwenyewe...ujenzi wa vyumba vya madarasa tayari kwawanafunzi wapya kuingia umefanyika nchi nzima...nani aliwapofusha mpaka yote haya hamuyaoni?
 
wewe mbona una wasi wasi?
sisi tuna mradi wa reli kwenda RWANDA itajengwa karibuni...

tuna mradi wa kujenga INTERNATIONAL airport kule BAGAMOYO itajengwa karibuni

tuna mradi wa refinery mpya itajengwa KARIBUNI

Tuna mradi wa bomba la mafuta toka TANGA-RWANDA-BURUNDI..itajengwa karibuni inshaalah

Tuna mradi wa kuvuna MVUA toka THAILAND inshaalah nayo itafanikiwa tuu

Tuna mradi wa MJI MPYA kule mbele sijui kunaitwaje..wasomali tayari wako site

Tuna mradi wa kujenga bandari BRAND NEW kule Bagamoyo itafanikiwa tuu ni uhai tuu mkulu

mwisho zaidi tuna mradi wa kuziba ule mtaro mbele ya HAIDERY PLAZA ambao unatoa harufu na maji machafu tangu mwaka jana ...isipokuwa taarifa ni kuwa meya wa ILALA na KIMBISA bado wanafanya feasibility study kujua lile shimo litazibwaje

at least for once you should be grateful kuwa nia TUNAYO,UWEZO TUNAO isipokuwa hatujajaaliwa tuu


--- Mradi wa kupanua New Bagamoyo Road bado uko vitabuni tangu early 2000s, feasibility study bado inafanyika, hata jana watu wenye vijizibao vya kung'ara walikuwepo mabarabarani wakihoji wananchi. Utamalizika KARIBUNI.

--- Dar Rapid Transport (DART) umeandikwa weee tangu ukiwa chini ya kina Sykes, mwongo mmoja sasa unapita. Utamalizika KARIBUNI.

--- Mradi wa vitambulisho UTAMALIZIKA 2010 baada ya uchaguzi kufanyika, utakuwa umetekelezeka kwa jimbo moja tu la Dar. Kisha feasibility study nyingine itaibuka kujua kama tuendelee nao au tuutose na ku-revert to alternative paper based ID, hivyo kuweza kumalizika miaka michache baada ya hapo KARIBUNI.

--- Dar Ring Road utamalizika KARIBUNI.

--- Daraja la Kigamboni (hatimaye litamalizika karibuni)

--- Kesi zote za wahujumu uchumi zitamalizika KARIBUNI!

Inasikitisha. Iwapo nchi ikiwa katika amani kama ilivyo yetu inashindwa kuwa na maendeleo ya chapchap; M.Mungu atuepushe nayo - itakuwaje pale machafuko yatakapotokea? Hamna namna nyingine ya kuelezea hii situation tuliyo nayo sisi. Siasa zetu under CCM zina incubate machafuko ya kisiasa, kwani paka huyu anayegandamizwa kwenye kona kila kukicha kwa kutumia kivuli cha utulivu na amani ipo siku atageuka chui. Dua zetu zinatofautiana, wengine wanaomba isitokee kabisa, wengine wanaomba itokee KARIBUNI.
 
Hapa naona kila mtu anajaribu kuomyesha namna jk na serikali yetu tukufu inavyoshindwa kutekeleza majukumu yake jambo ambalo si la kweli ata kidogo.Utendaji wa serikali ya JK hauwezi kupimwa kwa vile Kibaki kajenga reli basi na sisi tujenge reli....ni ujinga kwa kweli.Kwa faida ya wasomaji wa hapa pengine niseme machache sana yaliofanywa na serikali ya Jk ili watu wote tuweze kuyapima.....kwanza ni ujenzi na upanuzi wa chuo kikuu cha dodoma....wanafunzi elfu alobaini wataingia hapo.....pili ni walter sector program inayotekelezwa kwa sasa ambapo kila mji utanufaika kwa maji safi kwa kiwango cha asilimia 94....kwa sasa tayari kigoma wameenza utekelezaji wa kuvuta maji toka mto malagalasina kusambazwa kigoma...wakazi wa maeeneo ya dar wanaona ujenzi wa mabomba mapya ya maji hususani maeneo ya tabata nimeshuhudia mwenyewe...ujenzi wa vyumba vya madarasa tayari kwawanafunzi wapya kuingia umefanyika nchi nzima...nani aliwapofusha mpaka yote haya hamuyaoni?

hii ndo tz,"hata baba akimpeleka mwanae shule anataka ashukuriwe"
 
Yaguju ,feza ya kukwiba wataipata wapi wakianzisha hisia za kujenga mambo hayo ,ikiwa tuna reli ya kati miaka zaidi ya 90 ,tumeshindwa kuiendeleza reli ambayo ilitakiwa iwe ya kisasa kabisa kuvuna feza za wanyarwanda na Waburundi na kule Tazara ,yaani wezi hawa wanakwiba benki kuu halafu unawaletea mawazo mchovu ya kuwavunja moyo ,wacha watafune ,ndio maana wanakula chao hawali cha nchi nyengine ,endeleeni kukwiba shamba la babu wa Taifa kwani hawa wezi ukiwapima miaka yao ni wajukuu wa Nyerere tu ,so shamba la babu wa Taifa.
 
Kwa ahadi tu, Kibaki hampati Kikwete hata chembe!..
Pamoja na yote haya wakuu zangu hivi kweli sisi wananchi tunaoongozwa pia wazima au?..
 
Back
Top Bottom