Huitaji nyundo kurekebisha Ndoa yako

Pdidy

JF-Expert Member
Nov 22, 2007
50,956
22,148
Mengi yanarekebika!

Huhitaji nyundo kubwa kiasi hiki!Mahusiano ni kazi kwani zaidi ya kupendana wakati mwingine migogoro hujitokeza, msongo wa mawazo huja, furaha huota mabawa.

Jambo kubwa zaidi ni kwamba watu hutofautiana jinsi ya kutatua matatizo yanapotokea, desturi hutofautiana hata matarajio hutofautiana hata hivyo ukweli ni kwamba wengi bado tunahangaika kujua na kufahamu ni namna gani tunaweza kuishi vizuri na wengine hasa wale tunaowapenda kwani wakati mwingine yale tulitarajia imekuwa tofauti.

Unapokuwa umempata Yule unayempenda, Yule ambaye umeamua maisha yako yote duniani utaishi naye iwe katika shida au raha, iwe katika umaskini au utajiri au katika hali yoyote kazi kubwa ni kujenga mahusiano endelevu mwaka hadi mwaka.
Wengi kujenga huu uhusiano ni kukutana na milima na mabonde kwani inawezewekana upendo wa kweli kuzaliwa au kinyume chake .

Wanandoa wengu huachana kwa matatizo ambayo yanaweza kurekebishwa (fixable problems). Matatizo ambayo yanaweza kurekebika ni matatizo ambayo huhusisha watu wawili (mke na mume) ambao walianza kwa kupendana na upendo kuanza kuchuja na wao kutofanya chochote ili kurejesha upya penzi lao kwenye mstari kama kawaida.

Kila jambo huwa na msingi wake na msingi ukitikiswa na kufanya nyufa ambazo huendelea kuongezeka ni kweli jingo la mahusiano haliwezi kufika popote.

Wengi wanaoachana hukiri kwamba “Sikutegemea kama ingetokea kwangu” ni kweli hakuna ambaye huingia kwenye mahusiano akiwa amejiandaa au akijua kwamba ipo siku wataachana kama wapo basi ni wachache sana na lazima akili zao zina matatizo.

Hata hivyo mambo ya ndoa au mahusiano yana mambo mengi sana ambayo ni udanganyifu na watu wengi wanaamini udanganyifu badala ya ukweli na matokeo yake wameangamia.
Je ni udanganyifu gani ambao wengi wanaamini ni ukweli?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom