canaan
Member
- Mar 1, 2008
- 46
- 6
Majuzi CRD Bank wameanzisha huduma ya Tembo card master card. Huduma hii
ilizinduliwa kwa mbwembwe na majigambo ya aina yake. Kama kawaida ya
watanzania tunapenda sana sifa ya kwamba sisi ndio kwanza kutoa kitu
fulani, lakini huduma zinazoendana na kuwa wa kwanza is virtually
zero.
Baada ya kusikia majigambo yao, na ukizingatia hii huduma nilikuwa
naitaka sana ili niweze kufanya online transactions; nilichangamkia
kuchukua Mastercard ya Tembo na kuweka vijisenti kadhaa ili niweze
kununua vitu mbalimbali hasa Amazon. Nilishangaa kwamba kadi yangu
ilikuwa haitambuliwi.
Nikachukua jukumu la kwenda kwenye tawi langu ili kujua kulikoni;
nilipofika mapokezi nikamkata dada mmoja na kumwambia tatizo langu na
kumuonyesha kadi yangu. Baadae akaniambia siwezi kufanya transaction
mpaka nijaze fomu ambayo nitailipia shilingi 1000 kwa mwezi; nikasema
sawa na akanipa fomu nikajaza, Baadae akaipeleka kwa boss wake na kuja
na jibu kwamba Tembo Mastercard haifanyi online transaction bali ni
Visa Card.
Nikashangaa sana vitu viwili:
1. Kwa ufahamu wangu, mtu anayekaa/handle Inquiries lazima awe
knowledgeable na huduma zinatolewa na benki, na sio mtu wa ku-
mislead wateja na kuwapotezea muda wao. Hapo sio mahali pa kumuweka
staff aliyepo orientation
2. CRDB msipende sifa za kuwa kwanza kutoa huduma fulani wakati hakuna
kinachoendelea. Benki makini inayoendeshwa na watu makini inajipanga
na kuhakikisha kwamba inapoanzisha huduma fulani panakuwa hakuna
porojo tena - only for the customer to see results and enjoy the
product - vinginevyo utawala wa benki unaonekana kama una walakini.
ilizinduliwa kwa mbwembwe na majigambo ya aina yake. Kama kawaida ya
watanzania tunapenda sana sifa ya kwamba sisi ndio kwanza kutoa kitu
fulani, lakini huduma zinazoendana na kuwa wa kwanza is virtually
zero.
Baada ya kusikia majigambo yao, na ukizingatia hii huduma nilikuwa
naitaka sana ili niweze kufanya online transactions; nilichangamkia
kuchukua Mastercard ya Tembo na kuweka vijisenti kadhaa ili niweze
kununua vitu mbalimbali hasa Amazon. Nilishangaa kwamba kadi yangu
ilikuwa haitambuliwi.
Nikachukua jukumu la kwenda kwenye tawi langu ili kujua kulikoni;
nilipofika mapokezi nikamkata dada mmoja na kumwambia tatizo langu na
kumuonyesha kadi yangu. Baadae akaniambia siwezi kufanya transaction
mpaka nijaze fomu ambayo nitailipia shilingi 1000 kwa mwezi; nikasema
sawa na akanipa fomu nikajaza, Baadae akaipeleka kwa boss wake na kuja
na jibu kwamba Tembo Mastercard haifanyi online transaction bali ni
Visa Card.
Nikashangaa sana vitu viwili:
1. Kwa ufahamu wangu, mtu anayekaa/handle Inquiries lazima awe
knowledgeable na huduma zinatolewa na benki, na sio mtu wa ku-
mislead wateja na kuwapotezea muda wao. Hapo sio mahali pa kumuweka
staff aliyepo orientation
2. CRDB msipende sifa za kuwa kwanza kutoa huduma fulani wakati hakuna
kinachoendelea. Benki makini inayoendeshwa na watu makini inajipanga
na kuhakikisha kwamba inapoanzisha huduma fulani panakuwa hakuna
porojo tena - only for the customer to see results and enjoy the
product - vinginevyo utawala wa benki unaonekana kama una walakini.