Huduma za afya nchini: Mkapa vs Kikwete.

Hacha uongo kumtetea mhuza sura CT scaner zilikuwepo toka 2004 pale BUGANDO, KCMC,na MHUHIMBIL mie nimetibiwa pale BUgando kwa 2004 zilikuwepo

Weka ushahidi wa ripoti yako ya CT scanner (i scan) uiweke hapa. Wewe umefanyiwa cardiograph unasema CT scan.
 
Porojo zinazosaidia ni njema sana kuliko porojo zisizo saidia.

Utawala wa kabla ya Kikwete ulikuwa wapi? usiwe wa mwanzo? mpaka anakuja Kikwete ku rescue bado ni mbaya? au UNFPA ilikuwa haipo? fikiri.

zomba, unajua kitu kinaitwa UNDAF? Au unafikiri wengine wanafanya mambo kwa mtindo wa zima moto kama serikali ya CCM inayoongozwa na matukio?
 
zomba, unajua kitu kinaitwa UNDAF? Au unafikiri wengine wanafanya mambo kwa mtindo wa zima moto kama serikali ya CCM inayoongozwa na matukio?

Wewe utaishia kuuliza maswali tu kwa sababu huna explanation ambayo ni plausible.
 
Lipi ambalo limeisha au limepungua? Tatizo la njaa na umeme lipo pale pale, na pengine limeongezeka. Juzi tumetangaziwa TANESCO imefilisika. Ujambazi umebadilika tu, kutoka ule wa kutumia silaha mpaka ule wa kwenye mtandao! TUWE WAKWELI.

Tatizo la njaa halijauwa mtu toka Kikwete ashike madaraka, leo hii tuna chakula cha akiba.

Tatizo la umeme, sijui kama unaelewa miradi inayoendelea kuanzia wakati wa Kikwete tu ili kutatua hili tatizo, au unataka vielelezo?

Ujambazi alioukuta Kikwete unatisha, watu walikuwa wanafunga mitaa na barabara. Ukitoka Dar kwenda Singida tu, ukitoka Dodoma tu ilikuwa lazima uende na escort ya polisi wenye silaha, hakuna malori yalikuwa yanatembea usiku na hiyo ilikuwa ni kila siku kwa muda wote wa utawala wa Mkapa. Nenda leo ukaone.

Ma escorst ya polisi wenye silaha yamepunguwa kutoka kila pembe za Tanzania, au hilo hulijui? leo unasikia Mtoni kumefungwa mtaa watu wanapora? umesikia Kariakoo kumefungwa mtaa watu wanapora? hayo yalikuwa ni mambo ya kawaida wakati wa Mkapa.

Leo unasikia EPA, unasikia Radar, unasikia Kiwira, unasikia BOT. Unajuwa uhalifu huo ulifanyika wakati upi? Kikwete anayaibua na anayatibu hayo maradhi (waulize madaktari kama haujumuwa na kuugunduwa ugonjwa utatibu nini?).

Life span ya Mtanzania ni miaka 57.4 kwa miaka 7 tu ya Kikwete, niambie kabla ya Kikwete ilikuwepo hiyo?
 
hii ya MRI na CT scan ni sawa na mtu kulinganisha uwepo wa androids kipindi cha mkapa

na pia kutokana na mfumo wa afya.... na hasa in our developing countries kipimo kikubwa cha afya ni basics health care package na sio 4th generation interventions kama mleta mada anavyotumia vigezo

tunatakiwa tuangalia minimum health care packages at all levels, service delivery success nk

nina wasiwasi na watu wanotumia na JK kumtetea... nivi hana hata epidemiologists wawili wamuandalie a good document kuliko hawa wawili anaowatumia humu??
 
zomba, unajua kitu kinaitwa UNDAF? Au unafikiri wengine wanafanya mambo kwa mtindo wa zima moto kama serikali ya CCM inayoongozwa na matukio?

Mimi sikijuwi hicho kitu wala sina haja ya kukijuwa, nikifikia kutaka kukijuwa ntakijuwa bila ya kukuuliza wewe.

Huko juu Nilisema Maisha ya Mtanzania yamepanda kwa miaka 5 kwa miaka saba tu ya Kikwete, nimeambiwa hiyo data ilikuwa ya miaka 5 ya mwanzo wa uongozi wa Kikwete na kwa sasa ni miaka 57.4 ikimaanisha kuwa imepanda kwa miaka 9 kwa miaka 7 ya uongozi wa Kikwete (hii ni rikodi ya dunia) Unalijuwa hilo? Ushahidi huu hapa:


Google Public Data Explorer 57.4 years - 2010
Source: World Bank

5N8M81ujtYgAAAABJRU5ErkJggg==
 
hii ya MRI na CT scan ni sawa na mtu kulinganisha uwepo wa androids kipindi cha mkapa

na pia kutokana na mfumo wa afya.... na hasa in our developing countries kipimo kikubwa cha afya ni basics health care package na sio 4th generation interventions kama mleta mada anavyotumia vigezo

tunatakiwa tuangalia minimum health care packages at all levels, service delivery success nk

nina wasiwasi na watu wanotumia na JK kumtetea... nivi hana hata epidemiologists wawili wamuandalie a good document kuliko hawa wawili anaowatumia humu??

Hivi katika mgomo unaoendelea hivi sasa umesikia kuna daktari anayezungumzia minimum healthcare package? Sote tumesikia CT scanner na MRI zikitajwa kuwa ni miongoni mwa vitu muhimu vinavyokosekana, ndio tukajiuliza, kwani hizo zimeanza kuja lini Tanzania? Jibu liko kwenye thread...
 
Kama vifaa hivyo vimenunuliwa wakati huo ni kwa sababu alikuta kuna reserve ya fedha za kutosha. Leo inabidi wakope kwa mabenki kwa shughuli za serikali!
 
Nimesikia kuanzia Sasa Ruhusa ya Kutoka Bungeni au Kutohudhuria vikao atakuwa anatoa Spika pekee... hali naona imekuwa Tete...

Spika you can lie People but you cant lie your self and You can fool people sometimes but not all the times... Tafakari zingatia Nchi ni yetu na sio Yako au Yenu
 
Nimesikia kuanzia Sasa Ruhusa ya Kutoka Bungeni au Kutohudhuria vikao atakuwa anatoa Spika pekee... hali naona imekuwa Tete...

Spika you can lie People but you cant lie your self and You can fool people sometimes but not all the times... Tafakari zingatia Nchi ni yetu na sio Yako au Yenu

Duduwasha, hii taarifa mpya sana!
 
kwa mara ya kwanza mtu apasuliwa kichwa badala ya mguu?????

Kwa mara ya kwanza mawaziri wa afya mfululizo wakosa mashiko na kuachia ngazi

kwa mara ya kwanza madakitari waendesha migomo mfululizo kwa kuzorotata secta ya afya

Kwa mara ya kwanza viongozi kwa asilimia kubwa kutibiwa pia kucheki afya zao ng'ambo ya inchi

kwa mara ya kwanza dawa feki/bandia zimeenea inchi nzima

Kwa mara ya kwanza ............. wagonjwa hawana wakuwatetea.........mara ya kwanza....serikali yaishi maisha ya propaganada secta ya afya ........mara ya kwanza............

1. huduma za afya kwa ujulma wake zimezolota kupita wakati wowote ule wa maisha yangu.
2. Rushwa katika wizara ya afya imepita aibu na mipaka, kama mnasilikiza BBC swahili asubuhi utaona idara ya afya ilivyooza na kupoteza njia.
3. Madawa hakuna wala vitendea kazi, hili halihitaji data, ushahidi, wala maelezo yoyote vinginevyo unatibiwa hospitali binafsi. (BBC swahili inasaidia sana kutoa utata huu maana wanawahoji raia moja kwa moja na kuepuka porojo na uongo wa serikali)

Tatizo ninaloliona Serkali na wapiga debe wake ni wahuni wa kupika data, kuwakilisha data fake na kuuhadaa uma wa watanzania. Haiwezekani reseach data zivary inversely proportional ukizipeleka kwenye uhalisia.

Nirahisa sana kujidanganya mhusika, kwa dunia ya leo si lahisi kuwahadaa watanganyika na walimwengu kwa ujumla wake.
 
Wote (Fisadi Mkapa na DHAIFU) ni sifuri tu hakuna hata aliyekuwa na afadhali.
 
Sote tunashuhudia jinsi madaktari wanavyomshambulia Rais Kikwete kwa shutuma za kutozipa kipaumbele huduma za afya nchini. Kumbukumbu zangu zinaonyesha kuwa kipindi cha Mkapa hakukuwa na shutuma kali kiasi hiki. Nimejaribu kuchimbachimba ili kujua kwa nini shutuma hizi zimekuwa kali zaidi kipindi hiki nikagundua kuwa:

1. CT scanner ya kwanza Tanzania ilianza kutumia mwaka 2007 katika hospitali ya Muhimbili. Hii ni baada ya Rais Kikwete kuingia madarakani. Sote tunajua kuwa madaktari mara nyingi hutumia mfano wa kipimo hichi kuwa ni miongoni mwa vitu muhimu vinavyokosekana kwenye utoaji huduma bora za afya. Rais Mkapa hakununua CT scanner hivyo kuwaacha madaktari wasijue nini wanachokosa, na hivyo wakatulia tuliii. "Kimbelembele" cha Kikwete kutaka kuleta technologia ya kisasa nchini inamgharimu. Sasa madaktari washaijua CT scanner na wanataka zaidi na zaidi.

2. Magnetic Resonance Imaging machine ya kwanza Tanzania imeanza kutumika mwaka 2009 baada ya Rais Kikwete kuingia madarakani. Mkapa alijua kuwa akileta hivi vitu, wataalam na wananchi watataka zaidi na matokeo yake "watamuona mbaya". Mkapa aliwafanya watanzania waamini kuwa vitu hivi kwa Tanzania haviwezekani kabisa, Kikwete amejaribu kuonyesha kuwa tunaweza kwa kiasi fulani - wananchi na wataalam baada ya kuona tunaweza kwa kiasi fulani sasa wanataka tuweze "to the fullest".

3. Kituo cha upasuaji wa moyo nchini kimeanzishwa baada ya rais Kikwete kuingia madarakani. Mkapa alijua kuwa ukishaleta mambo ya upasuaji wa moyo watanzania watataka zaidi, akayaacha. Sasa madaktari wanalalamika kwa nini kituo hicho hakina wataalam na vifaa vya kutosha.

4. Huduma ya kusafisha damu kwa figo la mashine, dialysis, imeanza kutolewa nchini baada ya Rais Kikwete kuingia madarakani. Madaktari vijana wamepewa fursa za kwenda nchi mbalimbali kujifunza juu ya huduma hii. Baadhi yao wamesharudi nchini na wanatoa huduma hiyo. Miongoni mwa vijana hao ni viongozi wa mgomo wa kutaka huduma bora za afya na maslahi zaidi. Iwapo Kikwete angefanya kama Mkapa na kuacha huduma hii isipatikane nchini pengine madaktari wangeendelea kuamini kuwa hilo haliwezekani Tanzania na kuwa watulivu.

5. Baada ya kuona kuwa kuna vijiji havipati kabisa huduma ya usafiri wa wagonjwa, serikali ya Kikwete imebuni utaratibu wa kutumia Bajaj ili kila kijiji nchini kiwe na aina fulani ya huduma ya kwanza ya usafiri wa kuwafikisha wagonjwa sehemu ambayo watapata aidha usafiri bora zaidi au huduma bora ya afya. Jambo hili limefanya serikali ya Kikwete ishambuliwe sana, huku watu wakisahahu kuwa Mkapa aliona bora awaache wanakijiji hap bila huduma yoyote. Kwa vile Mkapa alikaa kimya kabisa kuhusu hili, hakulaumiwa. Kimbelembele cha Kikwete kutafuta utatuzi wa matatizo ya watu wa vijijini umemponza, sasa analaumiwa kwa kubuni njia ya kwasaidia watanzania.

6. Hivi sasa Kikwete anajiandalia tena "bomu" lingine kwa sababu serikali yake imeshaanza kutuma madaktari vijana wakajifunze Afrika Kusini na Ulaya jinsi ya kufanya operesheni kwa kutumia kamera (laparoscopic operations), vijana hawa wakirudi watafunguliwa vituo vya kufanya operesheni hizo ambapo mtu anaweza kufanyiwa operesheni ya tumbo na kurudi nyumbani siku hiyohiyo bila kovu! Ninapata hisia kuwa vijana hawa nao wataanzisha mgomo wa kutaka huduma iwe ya kiwango cha juu kama kule walikotoka kujifunza na kumtupia lawama muasisi wa utamaduni wa kuheshimu taaluma ya udaktari kwa kuwapa madaktari wa Tanzania exposure.

Nyongeza: Utamaduni huu wa Rais Kikwete kuleta maendeleo ya kweli umemgharimu pia katika sekta ya elimu ambapo alihamasisha kuwepo kwa shule za kata na kuwapa fursa watoto ambao wangekosa kabisa elimu kupata angalau fursa fulani ya kuelimika kwa kiwango fulani. Hivi sasa shule za kata ndio zimekuwa kigezo cha kulaani jitihada za serikali kwa kuwa wanafunzi "wanafeli". Kikwete angewaacha waishie darasa la saba kama ilivyokuwa kipindi cha Mkapa na marais wengine, wasingekuwa shule, hata kufeli wasingefeli na Kikwete asingelaumiwa kwa matokeo mabaya.

Hofu: Kwa mafunzo haya yanayotolewa na wananchi kwa Kikwete, Rais ajaye atatakiwa kuchagua mtindo wa Mkapa au Kikwete! Mpaka hapa tulipo inaonekana kuwa mtindo aliotumia Mkapa una manufaa zaidi kwake na chama chake kisiasa, lakini je vipi kuhusu maisha halisi ya watu wetu?

Nini kifanyike: wataalam, wanaharakati na wananchi ni wajibu wao kudai huduma bora na kuishinikiza serikali ifanye kila liwezekanalo kutoa kilicho bora zaidi kwa watu wake. Hata hivyo makundi haya yanawajibika kutambua, kuheshimu na kutamka hadharani jitihada za viongozi wanaojitoa kimasomaso kuzisaka huduma bora kwa watanzania ili kuwatia moyo waendelee kufanya hivyo. Tukilalamika zaidi kuliko kuonyesha moyo wa shukurani tutaishia kuambiana "LIWALO NA LIWE".
Nyerere alishajua Safari za Nje Ni Tamu so alifanya Jitihada Kikwete asiingie Madarakani akimjua Fika Jamaa anavyopenda Kusafiri kwani alijua Kikwete akianza kusafiri basi atazidi na kuzidi... ni hili Yunaliona...


Nasikitikia Vijana wenzangu Wabunge wa CCM kwa kumsifia Raisi kwa kuteua Wakuu wa Wilaya...!!!! wakai hiyo ni kazi yake!
Itafikia Siku watamsifia Raisi kwa Kunywa Maji!...By Sugu MB..


Huduma ya Afya Haijafikia kama tunavyohitaji Raisi bado anakazi Nzito kulingana na Muda wake Madarakani... Na Hii tabia ya kusikiliza Vilaza badala ya Wananchi itamcost katika Historia...
 
Sote tunashuhudia jinsi madaktari wanavyomshambulia Rais Kikwete kwa shutuma za kutozipa kipaumbele huduma za afya nchini. Kumbukumbu zangu zinaonyesha kuwa kipindi cha Mkapa hakukuwa na shutuma kali kiasi hiki. Nimejaribu kuchimbachimba ili kujua kwa nini shutuma hizi zimekuwa kali zaidi kipindi hiki nikagundua kuwa:

1. CT scanner ya kwanza Tanzania ilianza kutumia mwaka 2007 katika hospitali ya Muhimbili. Hii ni baada ya Rais Kikwete kuingia madarakani. Sote tunajua kuwa madaktari mara nyingi hutumia mfano wa kipimo hichi kuwa ni miongoni mwa vitu muhimu vinavyokosekana kwenye utoaji huduma bora za afya. Rais Mkapa hakununua CT scanner hivyo kuwaacha madaktari wasijue nini wanachokosa, na hivyo wakatulia tuliii. "Kimbelembele" cha Kikwete kutaka kuleta technologia ya kisasa nchini inamgharimu. Sasa madaktari washaijua CT scanner na wanataka zaidi na zaidi.

2. Magnetic Resonance Imaging machine ya kwanza Tanzania imeanza kutumika mwaka 2009 baada ya Rais Kikwete kuingia madarakani. Mkapa alijua kuwa akileta hivi vitu, wataalam na wananchi watataka zaidi na matokeo yake "watamuona mbaya". Mkapa aliwafanya watanzania waamini kuwa vitu hivi kwa Tanzania haviwezekani kabisa, Kikwete amejaribu kuonyesha kuwa tunaweza kwa kiasi fulani - wananchi na wataalam baada ya kuona tunaweza kwa kiasi fulani sasa wanataka tuweze "to the fullest".

3. Kituo cha upasuaji wa moyo nchini kimeanzishwa baada ya rais Kikwete kuingia madarakani. Mkapa alijua kuwa ukishaleta mambo ya upasuaji wa moyo watanzania watataka zaidi, akayaacha. Sasa madaktari wanalalamika kwa nini kituo hicho hakina wataalam na vifaa vya kutosha.

4. Huduma ya kusafisha damu kwa figo la mashine, dialysis, imeanza kutolewa nchini baada ya Rais Kikwete kuingia madarakani. Madaktari vijana wamepewa fursa za kwenda nchi mbalimbali kujifunza juu ya huduma hii. Baadhi yao wamesharudi nchini na wanatoa huduma hiyo. Miongoni mwa vijana hao ni viongozi wa mgomo wa kutaka huduma bora za afya na maslahi zaidi. Iwapo Kikwete angefanya kama Mkapa na kuacha huduma hii isipatikane nchini pengine madaktari wangeendelea kuamini kuwa hilo haliwezekani Tanzania na kuwa watulivu.

5. Baada ya kuona kuwa kuna vijiji havipati kabisa huduma ya usafiri wa wagonjwa, serikali ya Kikwete imebuni utaratibu wa kutumia Bajaj ili kila kijiji nchini kiwe na aina fulani ya huduma ya kwanza ya usafiri wa kuwafikisha wagonjwa sehemu ambayo watapata aidha usafiri bora zaidi au huduma bora ya afya. Jambo hili limefanya serikali ya Kikwete ishambuliwe sana, huku watu wakisahahu kuwa Mkapa aliona bora awaache wanakijiji hap bila huduma yoyote. Kwa vile Mkapa alikaa kimya kabisa kuhusu hili, hakulaumiwa. Kimbelembele cha Kikwete kutafuta utatuzi wa matatizo ya watu wa vijijini umemponza, sasa analaumiwa kwa kubuni njia ya kwasaidia watanzania.

6. Hivi sasa Kikwete anajiandalia tena "bomu" lingine kwa sababu serikali yake imeshaanza kutuma madaktari vijana wakajifunze Afrika Kusini na Ulaya jinsi ya kufanya operesheni kwa kutumia kamera (laparoscopic operations), vijana hawa wakirudi watafunguliwa vituo vya kufanya operesheni hizo ambapo mtu anaweza kufanyiwa operesheni ya tumbo na kurudi nyumbani siku hiyohiyo bila kovu! Ninapata hisia kuwa vijana hawa nao wataanzisha mgomo wa kutaka huduma iwe ya kiwango cha juu kama kule walikotoka kujifunza na kumtupia lawama muasisi wa utamaduni wa kuheshimu taaluma ya udaktari kwa kuwapa madaktari wa Tanzania exposure.

Nyongeza: Utamaduni huu wa Rais Kikwete kuleta maendeleo ya kweli umemgharimu pia katika sekta ya elimu ambapo alihamasisha kuwepo kwa shule za kata na kuwapa fursa watoto ambao wangekosa kabisa elimu kupata angalau fursa fulani ya kuelimika kwa kiwango fulani. Hivi sasa shule za kata ndio zimekuwa kigezo cha kulaani jitihada za serikali kwa kuwa wanafunzi "wanafeli". Kikwete angewaacha waishie darasa la saba kama ilivyokuwa kipindi cha Mkapa na marais wengine, wasingekuwa shule, hata kufeli wasingefeli na Kikwete asingelaumiwa kwa matokeo mabaya.

Hofu: Kwa mafunzo haya yanayotolewa na wananchi kwa Kikwete, Rais ajaye atatakiwa kuchagua mtindo wa Mkapa au Kikwete! Mpaka hapa tulipo inaonekana kuwa mtindo aliotumia Mkapa una manufaa zaidi kwake na chama chake kisiasa, lakini je vipi kuhusu maisha halisi ya watu wetu?

Nini kifanyike: wataalam, wanaharakati na wananchi ni wajibu wao kudai huduma bora na kuishinikiza serikali ifanye kila liwezekanalo kutoa kilicho bora zaidi kwa watu wake. Hata hivyo makundi haya yanawajibika kutambua, kuheshimu na kutamka hadharani jitihada za viongozi wanaojitoa kimasomaso kuzisaka huduma bora kwa watanzania ili kuwatia moyo waendelee kufanya hivyo. Tukilalamika zaidi kuliko kuonyesha moyo wa shukurani tutaishia kuambiana "LIWALO NA LIWE".
hakuna lolote! mwaka 2005 mwishoni mwa kipindi cha Mkapa kulikuwa na mgomo mkubwa sana wa Madaktari hapa TAnzania, hii pia ilileta changamoto kubwa sana kwa serikali ya CCM kuwa makini zaidi na sekta ya afya, wakapanisha mishahara na kuanzanza kuboresha sehemu kadhaa za skta hio. Tatizo ni kwamba uboreshaji wao ni duni mnooo! kama umeamua kununua CT scan, nunua za kutosha nchi nzima! mbona mashangingi huwa yananunuliwa ya kutosheleza viongozi wote kuanzia ngazi za wilayani? Tusifanye watanzania kuwa ni vipofu, tunatupiwa kamfupa kamoja basi turidhike, ati kwa kuwa aliyepita hakututupia hata kamfupa kamoja! kwa kifupi, MKAPA na KIKWETE wanaweza kutofautiana katika jinsi walivyoijenga secta ya afya, LAKINI MKAPA WALA KIKWETE KIUJUMLA HAWAJAIJENGA SECTA HIYO KABISAAA SERIOUSLY SPEAKING! ni kama wanapaka rangi nyumba ili ipendeze kwa nje, waweze kuipiga picha na kuitoa magazetini na kuwaambia watanzania jinsi gani wao ni wazuri, lakini ndani hakuna nyumba!
 
Hao wanaosema huduma zilikuwa bora kipindi cha Mkapa ni wataalam?
Kama ni wataalam maana yake ni kwamba hiyo mitambo na wataalam alioleta Kikwete sio muhimu. Na kama sio muhimu kwanini tunataka viongezwe wakati tunaona vilipokosekana mambo yalikuwa poa zaidi?
AAAAAAAAA ZEMARKOPOLO!!!!!!!! karibu katika uwanja wa JF na nia zako zijulikanazo DR IMANI KONDO MPONDA!
 
Kipindi cha Kikwete tumeona "life span" imepanda kwa miaka zaidi ya miaka 5 kwa miaka 7 tu. Haijwahi kutokea kabla yake, wakati Nyerere anamuachia Mwinyi madaraka "life span" ya Mtanzania ilikuwa miaka 48 tu. Kipindi cha Mwinyi na Mkapa ikapanda miaka 2 (imagine kwa miaka 20 imepanda kutokea 48 na kufika 50), kipindi cha Kikwete imepanda na kufika 55, ni miaka 7 kwa miaka saba tu. Halafu huyo huyo anaonekana mbaya kwenye afya.

Life span aliyoacha Nyerere 48 years - Miaka 24 ya kutawala
Life span waliyoacha Mwinyi na Mkapa 50 years - Miaka 20 ya kutawala
Life span iliyopo wa huu wa Kikwete 57.4 years - Miaka 7 ya kutawala. (rikodi ya dunia).

Source: World Development Indicators and Global Development Finance - Google Public Data Explorer

Afya haipatikani hospitali pekee, ni kuanzia kwenye lishe, namna ya kukinga maradhi, huduma za mwanzo (vituo vya afya).

Hakuna aliyemfikia Kikwete kwa hayo yote. Vituo vya Afya na zahanati ni vingi zaidi kuliko wakati wowote, huduma ya mwanzo ni kubwa zaidi kuliko wakati wowote (vibajaji ni mfano mzuri), Kuzuwia maradhi (vyandarua ni mfano mmoja wapo).

Rais Kikwete alipoingia madarakani tu alikutana na matatizo sugu na makubwa matatu aliyoyarithi kutoka kwa Mkapa nayo ni; Njaa, Umeme na Ujambazi (nani asiyekumbuka?). Na akayashughulikia hayo ipasavyo. Bado tu ni mbaya?

Urgument za kitoto peleka kwenye NEC ya magamba, aliyekwambia lifespan inaongezeka kutokana na vibajaji nani?
Umefikiria suala la usahihi wa takwimu (reliability) hizo, vifo vingapi vinavyotokea vijijini haviripotiwi?? Mara ngapi takwimu zimechakachuliwa kufurahisha wakubwa??

Wakati unafanya inference ya lifespan inatokana na uongozi wa JK impact ya ongezeko la wasomi ambao wanajua umuhimu wa balanced diet na mazoezi uliiexclude vipi??
 
machine zilizoibiwa na kina Mahita kupelekwa Morogoro kwao watu wamekaa kimya? vifaa vimenunuliwa na serikali ya JK pia ila wasiseme hakukuwa na vifaa alipongia Mkapa au JK, labda vimeharibika au vimeibiwa au vinahitajika vifaa zaidi
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom