ZeMarcopolo
Platinum Member
- May 11, 2008
- 14,017
- 7,220
Sote tunashuhudia jinsi madaktari wanavyomshambulia Rais Kikwete kwa shutuma za kutozipa kipaumbele huduma za afya nchini. Kumbukumbu zangu zinaonyesha kuwa kipindi cha Mkapa hakukuwa na shutuma kali kiasi hiki. Nimejaribu kuchimbachimba ili kujua kwa nini shutuma hizi zimekuwa kali zaidi kipindi hiki nikagundua kuwa:
1. CT scanner ya kwanza Tanzania ilianza kutumia mwaka 2007 katika hospitali ya Muhimbili. Hii ni baada ya Rais Kikwete kuingia madarakani. Sote tunajua kuwa madaktari mara nyingi hutumia mfano wa kipimo hichi kuwa ni miongoni mwa vitu muhimu vinavyokosekana kwenye utoaji huduma bora za afya. Rais Mkapa hakununua CT scanner hivyo kuwaacha madaktari wasijue nini wanachokosa, na hivyo wakatulia tuliii. "Kimbelembele" cha Kikwete kutaka kuleta technologia ya kisasa nchini inamgharimu. Sasa madaktari washaijua CT scanner na wanataka zaidi na zaidi.
2. Magnetic Resonance Imaging machine ya kwanza Tanzania imeanza kutumika mwaka 2009 baada ya Rais Kikwete kuingia madarakani. Mkapa alijua kuwa akileta hivi vitu, wataalam na wananchi watataka zaidi na matokeo yake "watamuona mbaya". Mkapa aliwafanya watanzania waamini kuwa vitu hivi kwa Tanzania haviwezekani kabisa, Kikwete amejaribu kuonyesha kuwa tunaweza kwa kiasi fulani - wananchi na wataalam baada ya kuona tunaweza kwa kiasi fulani sasa wanataka tuweze "to the fullest".
3. Kituo cha upasuaji wa moyo nchini kimeanzishwa baada ya rais Kikwete kuingia madarakani. Mkapa alijua kuwa ukishaleta mambo ya upasuaji wa moyo watanzania watataka zaidi, akayaacha. Sasa madaktari wanalalamika kwa nini kituo hicho hakina wataalam na vifaa vya kutosha.
4. Huduma ya kusafisha damu kwa figo la mashine, dialysis, imeanza kutolewa nchini baada ya Rais Kikwete kuingia madarakani. Madaktari vijana wamepewa fursa za kwenda nchi mbalimbali kujifunza juu ya huduma hii. Baadhi yao wamesharudi nchini na wanatoa huduma hiyo. Miongoni mwa vijana hao ni viongozi wa mgomo wa kutaka huduma bora za afya na maslahi zaidi. Iwapo Kikwete angefanya kama Mkapa na kuacha huduma hii isipatikane nchini pengine madaktari wangeendelea kuamini kuwa hilo haliwezekani Tanzania na kuwa watulivu.
5. Baada ya kuona kuwa kuna vijiji havipati kabisa huduma ya usafiri wa wagonjwa, serikali ya Kikwete imebuni utaratibu wa kutumia Bajaj ili kila kijiji nchini kiwe na aina fulani ya huduma ya kwanza ya usafiri wa kuwafikisha wagonjwa sehemu ambayo watapata aidha usafiri bora zaidi au huduma bora ya afya. Jambo hili limefanya serikali ya Kikwete ishambuliwe sana, huku watu wakisahahu kuwa Mkapa aliona bora awaache wanakijiji hap bila huduma yoyote. Kwa vile Mkapa alikaa kimya kabisa kuhusu hili, hakulaumiwa. Kimbelembele cha Kikwete kutafuta utatuzi wa matatizo ya watu wa vijijini umemponza, sasa analaumiwa kwa kubuni njia ya kwasaidia watanzania.
6. Hivi sasa Kikwete anajiandalia tena "bomu" lingine kwa sababu serikali yake imeshaanza kutuma madaktari vijana wakajifunze Afrika Kusini na Ulaya jinsi ya kufanya operesheni kwa kutumia kamera (laparoscopic operations), vijana hawa wakirudi watafunguliwa vituo vya kufanya operesheni hizo ambapo mtu anaweza kufanyiwa operesheni ya tumbo na kurudi nyumbani siku hiyohiyo bila kovu! Ninapata hisia kuwa vijana hawa nao wataanzisha mgomo wa kutaka huduma iwe ya kiwango cha juu kama kule walikotoka kujifunza na kumtupia lawama muasisi wa utamaduni wa kuheshimu taaluma ya udaktari kwa kuwapa madaktari wa Tanzania exposure.
Nyongeza: Utamaduni huu wa Rais Kikwete kuleta maendeleo ya kweli umemgharimu pia katika sekta ya elimu ambapo alihamasisha kuwepo kwa shule za kata na kuwapa fursa watoto ambao wangekosa kabisa elimu kupata angalau fursa fulani ya kuelimika kwa kiwango fulani. Hivi sasa shule za kata ndio zimekuwa kigezo cha kulaani jitihada za serikali kwa kuwa wanafunzi "wanafeli". Kikwete angewaacha waishie darasa la saba kama ilivyokuwa kipindi cha Mkapa na marais wengine, wasingekuwa shule, hata kufeli wasingefeli na Kikwete asingelaumiwa kwa matokeo mabaya.
Hofu: Kwa mafunzo haya yanayotolewa na wananchi kwa Kikwete, Rais ajaye atatakiwa kuchagua mtindo wa Mkapa au Kikwete! Mpaka hapa tulipo inaonekana kuwa mtindo aliotumia Mkapa una manufaa zaidi kwake na chama chake kisiasa, lakini je vipi kuhusu maisha halisi ya watu wetu?
Nini kifanyike: wataalam, wanaharakati na wananchi ni wajibu wao kudai huduma bora na kuishinikiza serikali ifanye kila liwezekanalo kutoa kilicho bora zaidi kwa watu wake. Hata hivyo makundi haya yanawajibika kutambua, kuheshimu na kutamka hadharani jitihada za viongozi wanaojitoa kimasomaso kuzisaka huduma bora kwa watanzania ili kuwatia moyo waendelee kufanya hivyo. Tukilalamika zaidi kuliko kuonyesha moyo wa shukurani tutaishia kuambiana "LIWALO NA LIWE".
1. CT scanner ya kwanza Tanzania ilianza kutumia mwaka 2007 katika hospitali ya Muhimbili. Hii ni baada ya Rais Kikwete kuingia madarakani. Sote tunajua kuwa madaktari mara nyingi hutumia mfano wa kipimo hichi kuwa ni miongoni mwa vitu muhimu vinavyokosekana kwenye utoaji huduma bora za afya. Rais Mkapa hakununua CT scanner hivyo kuwaacha madaktari wasijue nini wanachokosa, na hivyo wakatulia tuliii. "Kimbelembele" cha Kikwete kutaka kuleta technologia ya kisasa nchini inamgharimu. Sasa madaktari washaijua CT scanner na wanataka zaidi na zaidi.
2. Magnetic Resonance Imaging machine ya kwanza Tanzania imeanza kutumika mwaka 2009 baada ya Rais Kikwete kuingia madarakani. Mkapa alijua kuwa akileta hivi vitu, wataalam na wananchi watataka zaidi na matokeo yake "watamuona mbaya". Mkapa aliwafanya watanzania waamini kuwa vitu hivi kwa Tanzania haviwezekani kabisa, Kikwete amejaribu kuonyesha kuwa tunaweza kwa kiasi fulani - wananchi na wataalam baada ya kuona tunaweza kwa kiasi fulani sasa wanataka tuweze "to the fullest".
3. Kituo cha upasuaji wa moyo nchini kimeanzishwa baada ya rais Kikwete kuingia madarakani. Mkapa alijua kuwa ukishaleta mambo ya upasuaji wa moyo watanzania watataka zaidi, akayaacha. Sasa madaktari wanalalamika kwa nini kituo hicho hakina wataalam na vifaa vya kutosha.
4. Huduma ya kusafisha damu kwa figo la mashine, dialysis, imeanza kutolewa nchini baada ya Rais Kikwete kuingia madarakani. Madaktari vijana wamepewa fursa za kwenda nchi mbalimbali kujifunza juu ya huduma hii. Baadhi yao wamesharudi nchini na wanatoa huduma hiyo. Miongoni mwa vijana hao ni viongozi wa mgomo wa kutaka huduma bora za afya na maslahi zaidi. Iwapo Kikwete angefanya kama Mkapa na kuacha huduma hii isipatikane nchini pengine madaktari wangeendelea kuamini kuwa hilo haliwezekani Tanzania na kuwa watulivu.
5. Baada ya kuona kuwa kuna vijiji havipati kabisa huduma ya usafiri wa wagonjwa, serikali ya Kikwete imebuni utaratibu wa kutumia Bajaj ili kila kijiji nchini kiwe na aina fulani ya huduma ya kwanza ya usafiri wa kuwafikisha wagonjwa sehemu ambayo watapata aidha usafiri bora zaidi au huduma bora ya afya. Jambo hili limefanya serikali ya Kikwete ishambuliwe sana, huku watu wakisahahu kuwa Mkapa aliona bora awaache wanakijiji hap bila huduma yoyote. Kwa vile Mkapa alikaa kimya kabisa kuhusu hili, hakulaumiwa. Kimbelembele cha Kikwete kutafuta utatuzi wa matatizo ya watu wa vijijini umemponza, sasa analaumiwa kwa kubuni njia ya kwasaidia watanzania.
6. Hivi sasa Kikwete anajiandalia tena "bomu" lingine kwa sababu serikali yake imeshaanza kutuma madaktari vijana wakajifunze Afrika Kusini na Ulaya jinsi ya kufanya operesheni kwa kutumia kamera (laparoscopic operations), vijana hawa wakirudi watafunguliwa vituo vya kufanya operesheni hizo ambapo mtu anaweza kufanyiwa operesheni ya tumbo na kurudi nyumbani siku hiyohiyo bila kovu! Ninapata hisia kuwa vijana hawa nao wataanzisha mgomo wa kutaka huduma iwe ya kiwango cha juu kama kule walikotoka kujifunza na kumtupia lawama muasisi wa utamaduni wa kuheshimu taaluma ya udaktari kwa kuwapa madaktari wa Tanzania exposure.
Nyongeza: Utamaduni huu wa Rais Kikwete kuleta maendeleo ya kweli umemgharimu pia katika sekta ya elimu ambapo alihamasisha kuwepo kwa shule za kata na kuwapa fursa watoto ambao wangekosa kabisa elimu kupata angalau fursa fulani ya kuelimika kwa kiwango fulani. Hivi sasa shule za kata ndio zimekuwa kigezo cha kulaani jitihada za serikali kwa kuwa wanafunzi "wanafeli". Kikwete angewaacha waishie darasa la saba kama ilivyokuwa kipindi cha Mkapa na marais wengine, wasingekuwa shule, hata kufeli wasingefeli na Kikwete asingelaumiwa kwa matokeo mabaya.
Hofu: Kwa mafunzo haya yanayotolewa na wananchi kwa Kikwete, Rais ajaye atatakiwa kuchagua mtindo wa Mkapa au Kikwete! Mpaka hapa tulipo inaonekana kuwa mtindo aliotumia Mkapa una manufaa zaidi kwake na chama chake kisiasa, lakini je vipi kuhusu maisha halisi ya watu wetu?
Nini kifanyike: wataalam, wanaharakati na wananchi ni wajibu wao kudai huduma bora na kuishinikiza serikali ifanye kila liwezekanalo kutoa kilicho bora zaidi kwa watu wake. Hata hivyo makundi haya yanawajibika kutambua, kuheshimu na kutamka hadharani jitihada za viongozi wanaojitoa kimasomaso kuzisaka huduma bora kwa watanzania ili kuwatia moyo waendelee kufanya hivyo. Tukilalamika zaidi kuliko kuonyesha moyo wa shukurani tutaishia kuambiana "LIWALO NA LIWE".