Huduma ya Kangaroo

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Feb 3, 2009
42,268
33,040
Huduma ya Kangaroo



Mama amemshikilia mtoto wake ambaye amezaliwa kabla ya muda wa ujazito kukamilika katika kituo cha hospitali cha Kapiolani Medical Center NICU, Honolulu, Hawaii​




Huduma ya Kangaroo ni huduma inayofanyiwa watoto wachanga, ambao huzaliwa kabla ya muda wa ujauzito kukamilika, watoto huguzishwa moja kwa moja na ngozi ya mtu mzima. Huduma ya Kangaroo kwa watoto ambaohuzaliwa kabla ya muda wa ujauzito kukamilika inaweza kufanywa saa chache kwa kila siku, lakini kama wako sawa kiafya muda huo unaweza kuongewzwa. Baadhi ya wazazi wanaweza kupakata watoto wao kwa saa nyingi kwa siku. Huduma ya Kangaroo, ambayo inatokana na jinsi baadhi ya {0wanyama wa marsupia{/0} wanavyobeba vikembe vyao, nilianzishwa awali kuhudumia watoto wachanga wanaozaliwa kabla ya muda wa ujauzito kukamilika katika maeneo ambayo hayana inikiubeta ama si za kutegemewa.​




Huduma ya Kangaroo hunuia kurejesha hali ya kumfungia mtoto na mama ama baba kwa kumweka moja kwa moja karibu na ngozi ya mmoja wao. Hali hii humhakikishia mtoto joto la mwili na kuhusiana kisaikolojia. Mlalo wa Kangaroo humpa nafasi ya kunawiri. Kiwango imara cha joto la mzazi husaidia katika kudhibiti joto la mtoto mchanga kwa urahisi kuliko inikiubeta, na hurahisisha kunyonyesha.
Ingawa njia hii ya kuhudumia mtoto mchanga ni tofauti na ile ya Utaratibu wa Ulaya ya NICU NICU iliyoelezwa hapa, njia zote mbili si za kipekee, na inakadiriwa kuwa zaidi ya vitengo 200 vya Vyumba vya watoto mahututi hutumia huduma ya Kangaroo siku hizi. Utafiti mmoja wa hivi karibuni uligundua kwamba asilimia 82 ya vitengo vya huduma ya watoto mahututi hutumia huduma ya kangaroo siku hizi huko Marekani.

Historia

Si maeneo yote duniani yaliyo na nyenzo za kutoa huduma za kiufundi na wafanyakazi wa huduma za afya kwa watoto wanaozaliwa kabla ya muda wa ujauzito kuisha au walio chini ya uzani. Mwaka 1978, kutokana na kuongezeka kwa maradhi na viwango vya vifo katika Taasisi ya Materno Infantil NICU huko Bogotá, Colombia, Dkt. Edgar Rey Sanabria, Profesa wa Taaluma ya magonjwa ya watoto wachanga katika Idara ya Huduma za watoto - Chuo Kikuu cha Nacional cha Colombia, ilianzisha utaratibu wa kuondoa uhaba wa watoa huduma za ulezi na ukosefu wa nyenzo. Alipendekeza kwamba wamama wawe na mguso WA moja kwa moja na ngozi ya watoto na watoto wao wanaozaliwa wakiwa chini ya uzani wa kawaida ili kuwapa joto na kwanyonyesha kwa njia ya pekee kama walivyohitaji. Hii ilipunguza msongamano katika nafasia za inikiubeta na walezi.
Kipengele kingine cha huduma ya Kangaroo ilikuwa ni kutolewa mapema kwa mtoto katika mlalo wa kangaroo licha ya kwamba mtoto hajakomaa. Imethibitishwa kuwa na mafanikio katika kuongeza uwekano wa mtoto ambaye huzaliwa kabla ya kukomaa ama mwenye uzani mdogo kunusurika na kupungua hatari ya maambukizi ya hospitali, magonjwa hatari, na ugonjwa wa kupumua (Conde-Agudelo, Diaz-Rossello, & Belizan, 2003). Aidha, iliongeza unyonyeshaji wa pekee kwa muda mrefu na kuboresha kuboresha kuridhika kwa mzazi na kujiamini.

Vigezo vinvyostahiki

Awali watoto ambao walistahiki huduma ya kangaroo ni pamoja na watoto waliozaliwa kabla ya muda wa ujauzito kukamilika au wenye uzani wa chini ya gramu 1500, waliopumua wenyewe. Ufuatiliaji wa hali ya mapafu na moyo, oksimetri, oksijeni ya ziada au pua (shinikizo la mpito wa hewa) uingizaji hewa, uingizaji kwenye mishipa, na hali zingine za ukaguzi hazizuii huduma ya kangaroo. Kwa hakika, watoto walio katika huduma ya kangaroo huelekea kutoathiriwa na apnea kuwa chini ya kukabiliwa na apnea na bradikadia na huwa na mahitaji ya oksijeni yasiyobadilika.
Mwanzoni mwa miaka ya 1990, dhana hiyo ilitetewa Amerika ya Kaskazini kwa watoto ambao hawakuwa wametosheleza kipindi cha ujauzito katika NICU na baadaye kwa watoto wazima. Utafiti umefanywa katika mataifa yaliyoendelea lakini kuna kusitishwa katika kutekelezwa kwa huduma ya kangaroo kutokana na upatikanaji wa inikiubeta na teknolojia kwa urahisi.

Mbinu
Katika huduma ya kangaroo kawaida mtoto huvaa mbeleko peke yake na hufungwa kwa mlalo wa kichwa juu katika kifua wazi cha mama na ugwe wa nguo kwa namna ambayo kichwa na shingo ya mtoto huzuia apnea. Mama huvaa shati au gauni ya hospitali iliyofunguliwa mbele. Nguo huzungushwa karibu na chini ya mtoto ili kuleta mkunjo.
Kukumbatia kwa nguvu kunatosha kwa mama kupumua na kifua kusonga ili kuchochea mtoto kupumua. Kwa sababu ya kukaribiana sana kutokana na kufungwa kwa kifua cha mama, mtoto huwa katika mazingira ya kiwango cha juu cha gesi ya kaboni dayoksaidi ambayo pia huchochea kupumua.

Akina baba wanaweza pia kutumia njia ya kugusana moja kwa moja na ngozi ya mtoto.
Inaelekea kwamba kuanzisha huduma ya kangaroo saa mbili za mwanzo za kuzaliwa kwa mtoto ndiyo wakati mwafaka ili kufaulu katika kunyonyesha. Watetezi wengi wa njia za kawaida za kujifungua huhimiza mguso wa moja kwa moja wa ngozi punde tu mtoto anapozaliwa

baina ya mama na mtoto bila usumbufu wowote. Watoto lazima wawe na joto na bila unyevunyevu. Njia hii inaweza kutumika kila wakati ama kwa muda wa kipindi kifupi kila siku hatua kwa hatua huku ikiongezwa kadri mtoto anavyozidi kuizoea kwa wale watoto ambao wameathirika

na matatizo makubwa ya kiafya. Inaweza kuanzishwa wakati mtoto amezaliwa au baada ya saa, siku, au majuma baada ya kuzaliwa. Wanaounga mkono huduma ya Kangaroo wanasisitiza njia ya mguso wa moja kwa moja wa ngozi kwa muda wa takriban majuma sita ili mtoto na mama waweze kuimarika katika unyonyeshaji na na wawe wamepona kutokana na matatizo ya ya kiafya yanayotokana na kujifungu

Ingawa huduma ya kangaroo ni sawa, kwa namna fulani, na kumvaa mtoto, njia hizo mbili zina tofauti zao. Mara nyingi huduma ya Kangaroo hufanyiwa watoto ambao hawajakomaa kwa kutumia vifaa rahisi na angalau baadhi ya usimamizi wa daktari. Kumvaa mtoto kunaweza kufanywa kwa aina mbalimbali za mbeleko na ugwe, mara nyingi hufanyiwa watoto waliozaliwa tu kadhalika wanaotambaa.

Faida
Kwa Wazazi

Huduma ya Kangaroo ina manufaa kwa wazazi kwa sababu inakuza kuunganika na kuhusiana kwa karibu, inaboresha kujiamini kwa mzazi, na husaidia katika kuongezeka kwa uzalishaji wa maziwa na mafanikio ya kunyonyesha

Kwa watoto wanaozaliwa kabla ya kipindi cha ujauzito kukamilika na walio chini ya uzani

Inaaminika kuwa huduma ya kangaroo huwafaidi zaidi watoto wanaozaliwa kabla ya kipindi cha ujauzito kukamilika na watoto wenye uzani mdogo, ambao hupata joto la kawaida, mpigo wa moyo, na kasi ya kupumua , kupata uzani zaidi, visa vichache vya maambukizi ya

hospitali na kupungua kwa matukio ya ugonjwa wa njia ya kupumua Zaidi ya hayo, utafiti unaonyesha kwamba watoto ambao huzaliwa kabla ya muda wa ujauzito kukamilika ambao hupata huduma ya kangaroo na huboresha uwezo wao wa kiakili, kiwango cha chini c ha msongo, kutohisi maumivu kwa urahisi, ukuaji ulio mzuri, na mabadiliko mazuri katika ukuaji wa hisi. Aidha, huduma ya kangaroo husaidia

kukuza ruwaza za watoto kulala na huenda ikawa suluhisho kwa riahi ya watoto.Kuruhusiwa kutoka hospitali mapema pia ni unaweza
kutokea matokeo Mwisho, huduma ya kangaroo husaidia kukuza unyonyeshaji wa mara kwa mara, na inaweza kuboresha kuunganika baina ya mtoto na mama.

Kwa taasisi

Aghalabu huduma ya kangaroo hupunguza muda wa kukaa hospitali, hupunguza haja ya teknolojia ya matibabu, huongeza kushirikishwa kwa mzazi na nafasi za mafunzo na matumizi mazuri ya fedha za matibabu.
Kwa jamii

Kwa ujumla, huduma ya kangaroo inasaidia kupunguza magonjwa na vifo katika nchi zinazoendelea, hutoa nafasi kwa ajili ya kufundisha wakati wa ziara ya baada ya mtoto kuzaliwa hupunguza gharama za hospitali.
 
Ahsante MziziMkavu....umenifurahisha na hii post. Actually kesho kutwa (Thursday) naenda kuco-direct a 10 minutes documentary on 'Kangaroo Mother Care (KMC)' kwa zahanati za wilaya ya Temeke. Surprisingly, si waTanzania wengi wanafahamu kuhusu njia hii ya kumpa na kutunza joto la mtoto hasa njiti na waliozaliwa na uzito pungufu ambao wako kwenye hatari kubwa ya kufa kutokana na matatizo ya joto pungufu mwilini. Its so unfortunate sehemu wanapozaliwa watoto hawa (vijijini) hakuna incubators za kuwapa joto, na hii ni njia muhimu au naweza sema njia pekee ya kupunguza hatari ya kifo kwao!
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom