Officer2009
JF-Expert Member
- Dec 20, 2010
- 560
- 110
Wanajamii, mi nimelazwa hapa Marangu Hospital tangu jana usiku, ila cha kusikitisha ni kuwa sijapata huduma inayostahili hadi sasa! Usiku nilipewa pain killers na dawa ya usingizi. Asubuhi ilipofika nikamfuata dokta na kumwambia kuwa maumivu yameanza tena, nikitegemea kuwa huenda nikachukuliwa vipimo stahili na kupewa tiba, ila haikuwa hivyo, kwani nilirudishwa wadini na kuambiwa nisubiri kwani watakuja wadini. Daktari aliingia wadini saa nne na robo asubuhi na baada ya kunihoji na kunishikashika tumbo akamwambia nesi kuwa natakiwa kuchukuliwa vipimo. Mi nikaendele kuugulia maumivu hadi mambo yalipozidi nikamfuata nesi tena(baada ya nusu saa) na kumuuliza kulikoni, ndo akaniambia niende maabara nikapime. Hadi sasa hivi saa nane kasoro ninapoandika majibu ya maabara bado hayajatoka, na sijatibiwa wala kujua maradhi yangu, pamoja na kuwa nina maumivu makali mno. Hivi kweli hivi ndo wanavyopasa kuhudumiwa?