WA MAMNDENII
JF-Expert Member
- Jun 5, 2010
- 344
- 57
kwa siku tatu mfululizo nimekuwa nakwenda kupata huduma kwenye benki ya akiba kariakoo , nimeudhika na huduma ya mhudumu ambaye anakuwa teller number 4 anavyohudumia kwa muda mrefu mteja mmoja, leo nimeshuhudia mteja mmoja anadeposit hela yake kasimama zaidi ya robo saa anahudumiwa. mi mwenyewe juzi nimetumia dakika kumi kudeposit fedha kwa huyo mwanadada. anaweza kuhesabu fedha kwenye machine halafu tena anahesabu kwa mkono kisha tena mashine halafu anakagua moja baada ya nyigine yaani anakera na kuchefua. ni kweli umakini unahitajika kwenye maswala ya hela ila uendane na speed kwenye karne hii ya sayansi na teknolojia. nawashauri viongozi wa hilo tawi wajali muda wa wateja sio waturudishe zile enzi za benki ya posta kuweka fedha inakuchukua saa karibu tatu na ukitaka kutoa mshiko ndo utasahau muda uliokuja. kwa maana hiyo huyo mwanadada hafai kukaa kaunta apangiwe kazi nyingine mara moja.